Saturday, December 29, 2012

JUMUIYA YA WAZAZI KUTUMIA MAWAKILI KUREJESHA MALI ZAKE PWANI

Na John Gagarini, Kibaha

JUMUIYA ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Pwani imesema kuwa imeandaa mawakili ili kuhakikisha mali zote za Jumuiya hiyo zilizouzwa au kuchukluliwa kinyume cha sheria zinarudi.
Hayo yalisemwa jana na mwenyekiti wa mkoa wa jumuiya hiyo Bw Jackson Josian wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua semina juu ya uajasiraiamali kwa viongozi wa Jumuiya Kibaha Mjini.
Alisema kuwa Jumuiya hiyo ina mali nyingi ambazo baadhi zimechukuliwa au kuuzwa kinyume cha sheria jambo ambalo linafanya washindwe kujitegemea licha ya kuwa na rasilimali na tayari wameshawapata mawakili ili kurejesha mali hizo kisheria.
“Tuna rasilimali nyingi ambazo tunatarajia kuzirejesha kwani nyingine zimeporwa lakini tutahakikisha kuwa mali zote zinarudi mikononi mwetu ili kujenga uchumi wa Wazazi na chama kwa ujumla,” alisema Bw Josian.
Alizitaja baadhi ya mali za Jumuiya kuwa ni pamoja na shule, viwanja na mashamba ambapo baadhi ya viongozi wa Jumuiya hiyo wamehusika kusababisha mali hizo kupotea katika mazingira ya kutatanisha.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Jumiya ya Wazazi Kibaha Mjini Dkt Athuman Mokiwa alisema kuwa moja ya lengo la semina hiyo ni kuwafundisha juu ya kulinda mali za Jumuiya.
Dkt Mokiwa alisema kuwa viongozi wengine wameshindwa kabisa namna ya kusimamia miradi ya Jumuiya hiyo na kuifanya mingine iyumbe ambapo ingesimamiwa vema ingekuwa mkombozi ndani ya chama.
Mwisho.         

CHENCHI DOLA KUKARIBISHA MWAKA MPYA


Na John Gagarini, Kibaha
BONDIA machachari anayechipukia wa Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani Zumba Nkukwe (Chenchi Dola) anatarajia kuzikipiga na bondia Maisha Samson wa Mbeya mwaka mpya Januari Mosi 2013.
Chenchi Dola alisema kuwa yuko sawasawa kwa ajili ya pambano hilo ambalo litapigwa wilaya ya Kyela mkoani Mbeya.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha jana alisema kuwa hana wasiwasi na bondi huyo kwani amefanya mazoezi ya kutosha chini ya mwalimu wake aitwaye Poti ambapo mazoezi yake amekuwa akiyafanya Jijini Dar es Salaam.
“Nimejiandaa vya kutosha na siogopi bondia yoyote kwani nimejiandaa ipasavyo na hata raundi ya tatu hatafika ijapokuwa yeye atakuwa yuko nyumbani mbele ya mashabiki wake,” alisema Chenchi Dola.
Alisema kuwa watu wa Kyela wanatakiwa wajipange sawa sawa kupata burudani ya nguvu siku ya kufungua mwaka wa 2013 na ndipo anapoanza safari yake ya kuapambana na mabingwa waliopo sasa.
“Malengo yangu ni kuja kupambana na mabondia wakubwa wanaotamba kwa sasa ili tuweze kwenda sawa kwani malengo yangu ni kuwa bingwa kwani nitajiweka sawa ili nije kupambana na bondia mmoja wapo maarufu,” alisema Chenchi Dola.
Kwa upande wake meneja wa bondia huyo Ibrahim Kame kutoka TPBO alisema kuwa lengo la pambano hilo ni kutafuta mshindi ambaye atashiriki kwenye mashindano mbalimbali ili kujiongezea uzoefu.
“Bondia Chenchi Dola ni mzuri na natarajia atafanya vizuri na kumshinda mpinzani wake na baadaye tutamtafutia mapambano mengi zaidi ili aweze kuonyesha kipaji chake,” alisema Kame.
Aliongeza kuwa katika pambano hilo mabondia wakongwe kama vile Rshid Matumla “Snake Boy” na Maneno Oswald “Mtambo wa Gongo” watakuwepo kuangalia vijana wanavyopambana.
Mwisho.

Friday, December 28, 2012

AJINYOFOA SEHEMU ZA SIRI KUKWEPA MADENI



 Na John Gagarini, Kibaha
WASWAHILI wanasema ukistaajabu ya Musa basi utaona ya Firauni yaliyomkuta Bw  Charles Malosha (44) mkulima wa Visiga Kati wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani yanasikitisha kwani amekumbwa na masahibu ambayo hataweza kuyasahau katika maisha yake yote na kila aliyesikia hakika anashikwa na simanzi kutokana na kuondolewa sehemu zake za siri katika mazingira ya kutatanisha.
Akizungumza jana kwenye kituo cha afya cha Mlandizi Bw Malosha mwenye watoto sita alisema kuwa alitokewa na tukio hilo la kikatili akiwa kwenye kituo cha polisi Visiga lakini cha kushangaza watu walivumisha kuwa amengofoa sehemu zake za siri na kuzitafuna jambo ambalo si la kweli.
Bw Malosha alisema kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 26 mwaka huu  majira ya mchana ambapo alichukuliwa na mgambo na kuambiwa kuwa anaitwa kituo cha polisi ambapo alikwenda na ndipo alipoambiwa kuwa kuna watu kadhaa wanamdai fedha ambazo walimpa kwa ajili ya kuwanunulia kwa ajili ya kujengea.
“Wakati niko polisi kwenye selo walifika walalamikaji wakiwa na polisi mmoja ambapo kati yao mmoja alikuwa na rungu ambalo alinipiga nalo kichwani na kupoteza fahamu na nilipozinduka sehemu zangu za siri (Korodani) zilikatwa na nikajikuta damu nyingi zinamwagika na ndipo nilipokimbizwa hospitali kupata matibabu,” alisema Bw Malosha.
Alisema kuwa kimsingi alikuwa akidaiwa milioni tatu na watu watatu ambao walimpa fedha kwa ajili awauzie maeneo lakini alishindwa kuwapatia maeneo hayo kwa wakati waliokuwa wakiyataka.
“Kweli walikuwa wakinidai na mimi nilikuwa najipanga aidha kuwarudishia fedha zao au kuwatafutia sehemu nyingine ambapo tangu tuanze kuwasiliana ni kama miezi minne imepita sasa,” alisema Bw Malosha.
Kwa upande wake mkewe Bi Martha Boni alisema kuwa siku ya tukio hilo alimwaga na kumwambia hata mwona tena hivyo alee watoto wake jambo ambalo lilimshangaza lakini hakuweza kumfafanulia kuwa alikuwa akimaanisha nini.
“Baada ya muda nilipigiwa simu na kuambiwa kuwa mume wangu yuko hoi hospitali na hawezi kuongea kwa kweli nilichanganyikiwa na kutaka kujua yaliyomsibu lakini nilijulishwa kuwa ameondolewa sehemu zake za siri jambo ambalo lilizidi kuniumiza na kushindwa kujua nini cha kufanya na kuanguka chini kasha kupoteza fahamu,” alisema Bi Boni.
Bi Boni alisema kuwa anashangaa kusikia watu hao wakisema kuwa wanamdai milioni 20 jambo ambalo si lakweli kwani wanamdai shilingi milioni sita tu na alichukua milioni mbili kwa kila mmoja kwa watu watatu ambao wanatokea Jijini Dar es Salaam.
Naye mganga wa kituo hicho cha afya cha Mlandizi Dkt Nicetus Matem alisema kuwa alimpokea mgonjwa huyo ambaye alifika hapo huku akiwa anatokwa na damu nyingi na kumhudumia hadi damu ilipoacha kutoka.
“Ni kweli sehemu zake hizo za kiwanda cha kuzalishia mbegu (Korodani) zimeondolewa kabisa lakini hazikuondolewa na kitu chenye ncha kali bali kwani zilondolewa kwa kitu kiischo na ncha kali na nilipomuuliza alisema kuwa amezinyofoa yeye mwenyewe,” alisema Dkt Matem.
Dkt Matem alisema kuwa alirudishia vizuri lakini cha kusikitisha ni kwamba Bw Malosha hataweza kuzaa tena lakini hali ya sehemu yake kuu ya siri itakuwa ikifanya kazi kama kawaida na hali yake inaendelea vizuri.
Naye kamanda wa polisi mkoa wa Pwani  Ulrich Matei alisema kuwa taarifa alilzozipata ni kuwa mtu huyo alijijeruhi mwenyewe na alikuwa akidaiwa na milioni 11.5 na watu wanne tofauti.
“Aliachiwa shamba na bibi mmoja ambapo alikuwa akikata maeneo na kuyauza na yule mmiliki alipofika alisema kuwa maeneo aliyoyauza ni ya kwake kwani hakumruhusu kuyauza hivyo atajuana na watu hao hivyo awalipe yeye mwenwe,” alisema Matei.
Kamanda Matei  alisema kuwa watu hao walianza kumdai na kusema kuwa aliwadanganya kuwa eneo hilo ni lake hivyo arejeshe fedha zao kutokana na kuchanganyikiwa alifikia hatua ya kutaka kujiua.
“Lengo lake kujidhuru alitaka kujiua na hakufanyiwa kitendo hicho na mtu bali alifanya yeye mwenye na kwamba alifanyiwa na mtu si kweli na kama kuna mtu kamfanyia na kama kuna mtu anaficha ukweli nitafutailia kujua na akipata nafuu tutamhoji kupata ukweli kwani hana nia ya kumlinda mtu yoyote kwani kila mtu ana haki zake za msingi,” alisema Matei.
Aliongeza kuwa mtu huyo aliamua kufanya hivyo baada ya kuona kuwa sasa hana njia na ana deni na kuona njia ni kujiua na haiwezekani afanyiwe kitendo hicho kwenye kituo cha polisi.
 Mwisho

ANYOFOA SEHEMU ZA SIRI KUKWEPA MADENI



 Na John Gagarini, Kibaha
WASWAHILI wanasema ukistaajabu ya Musa basi utaona ya Firauni yaliyomkuta Bw  Charles Malosha (44) mkulima wa Visiga Kati wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani yanasikitisha kwani amekumbwa na masahibu ambayo hataweza kuyasahau katika maisha yake yote na kila aliyesikia hakika anashikwa na simanzi kutokana na kuondolewa sehemu zake za siri katika mazingira ya kutatanisha.
Akizungumza jana kwenye kituo cha afya cha Mlandizi Bw Malosha mwenye watoto sita alisema kuwa alitokewa na tukio hilo la kikatili akiwa kwenye kituo cha polisi Visiga lakini cha kushangaza watu walivumisha kuwa amengofoa sehemu zake za siri na kuzitafuna jambo ambalo si la kweli.
Bw Malosha alisema kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 26 mwaka huu  majira ya mchana ambapo alichukuliwa na mgambo na kuambiwa kuwa anaitwa kituo cha polisi ambapo alikwenda na ndipo alipoambiwa kuwa kuna watu kadhaa wanamdai fedha ambazo walimpa kwa ajili ya kuwanunulia kwa ajili ya kujengea.
“Wakati niko polisi kwenye selo walifika walalamikaji wakiwa na polisi mmoja ambapo kati yao mmoja alikuwa na rungu ambalo alinipiga nalo kichwani na kupoteza fahamu na nilipozinduka sehemu zangu za siri (Korodani) zilikatwa na nikajikuta damu nyingi zinamwagika na ndipo nilipokimbizwa hospitali kupata matibabu,” alisema Bw Malosha.
Alisema kuwa kimsingi alikuwa akidaiwa milioni tatu na watu watatu ambao walimpa fedha kwa ajili awauzie maeneo lakini alishindwa kuwapatia maeneo hayo kwa wakati waliokuwa wakiyataka.
“Kweli walikuwa wakinidai na mimi nilikuwa najipanga aidha kuwarudishia fedha zao au kuwatafutia sehemu nyingine ambapo tangu tuanze kuwasiliana ni kama miezi minne imepita sasa,” alisema Bw Malosha.
Kwa upande wake mkewe Bi Martha Boni alisema kuwa siku ya tukio hilo alimwaga na kumwambia hata mwona tena hivyo alee watoto wake jambo ambalo lilimshangaza lakini hakuweza kumfafanulia kuwa alikuwa akimaanisha nini.
“Baada ya muda nilipigiwa simu na kuambiwa kuwa mume wangu yuko hoi hospitali na hawezi kuongea kwa kweli nilichanganyikiwa na kutaka kujua yaliyomsibu lakini nilijulishwa kuwa ameondolewa sehemu zake za siri jambo ambalo lilizidi kuniumiza na kushindwa kujua nini cha kufanya na kuanguka chini kasha kupoteza fahamu,” alisema Bi Boni.
Bi Boni alisema kuwa anashangaa kusikia watu hao wakisema kuwa wanamdai milioni 20 jambo ambalo si lakweli kwani wanamdai shilingi milioni sita tu na alichukua milioni mbili kwa kila mmoja kwa watu watatu ambao wanatokea Jijini Dar es Salaam.
Naye mganga wa kituo hicho cha afya cha Mlandizi Dkt Nicetus Matem alisema kuwa alimpokea mgonjwa huyo ambaye alifika hapo huku akiwa anatokwa na damu nyingi na kumhudumia hadi damu ilipoacha kutoka.
“Ni kweli sehemu zake hizo za kiwanda cha kuzalishia mbegu (Korodani) zimeondolewa kabisa lakini hazikuondolewa na kitu chenye ncha kali bali kwani zilondolewa kwa kitu kiischo na ncha kali na nilipomuuliza alisema kuwa amezinyofoa yeye mwenyewe,” alisema Dkt Matem.
Dkt Matem alisema kuwa alirudishia vizuri lakini cha kusikitisha ni kwamba Bw Malosha hataweza kuzaa tena lakini hali ya sehemu yake kuu ya siri itakuwa ikifanya kazi kama kawaida na hali yake inaendelea vizuri.
Naye kamanda wa polisi mkoa wa Pwani  Ulrich Matei alisema kuwa taarifa alilzozipata ni kuwa mtu huyo alijijeruhi mwenyewe na alikuwa akidaiwa na milioni 11.5 na watu wanne tofauti.
“Aliachiwa shamba na bibi mmoja ambapo alikuwa akikata maeneo na kuyauza na yule mmiliki alipofika alisema kuwa maeneo aliyoyauza ni ya kwake kwani hakumruhusu kuyauza hivyo atajuana na watu hao hivyo awalipe yeye mwenwe,” alisema Matei.
Kamanda Matei  alisema kuwa watu hao walianza kumdai na kusema kuwa aliwadanganya kuwa eneo hilo ni lake hivyo arejeshe fedha zao kutokana na kuchanganyikiwa alifikia hatua ya kutaka kujiua.
“Lengo lake kujidhuru alitaka kujiua na hakufanyiwa kitendo hicho na mtu bali alifanya yeye mwenye na kwamba alifanyiwa na mtu si kweli na kama kuna mtu kamfanyia na kama kuna mtu anaficha ukweli nitafutailia kujua na akipata nafuu tutamhoji kupata ukweli kwani hana nia ya kumlinda mtu yoyote kwani kila mtu ana haki zake za msingi,” alisema Matei.
Aliongeza kuwa mtu huyo aliamua kufanya hivyo baada ya kuona kuwa sasa hana njia na ana deni na kuona njia ni kujiua na haiwezekani afanyiwe kitendo hicho kwenye kituo cha polisi.
 Mwisho