Saturday, March 21, 2026

DA ARUL ARQAM LEARNING CENTRE (DAALC) KUJENGA HOSPITALI YA KISASA.

TAASISI ya DA ARUL ARQAM LEARNING CENTRE (DAALC) ya Kibaha Mkoani Pwani inatarajia kujenga kituo cha taasisi chenye huduma mbalimbali za kijamii kikiwa ni pamoja Hospitali ya kisasa kwa gharama za shilingi bilioni 5.5.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwalimu wa Taasisi hiyo Karume Amri Abeid amesema kuwa kituo hicho kitajengwa eneo la Boko Wilaya ya Kibaha.

Abeid amesema kuwa eneo hilo ndilo litakalokuwa makao makuu ya Taasisi ambalo lina ukubwa wa hekari 11 na tayari nyumba ya mlinzi tayari imejengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi.

"Eneo hilo pia kutajengwa ofisi, Msikiti, shule ya awali hadi elimu ya juu yaani kidato cha sita, chuo cha elimu ya dini Ibtidai mpaka Thanawi, kituo cha kuhifadhisha Quran kwa watoto kuanzia miaka 5 na kuendelea,"amesema Abeid.

Amesema kuwa njia watakayoitumia kupata fedha ni michango mbalimbali toka kwa wadau, waumini na kufanya harambee ambapo hadi sasa wamekusanya kiasi cha shilingi milioni 2.

"Huduma zikiwemo za afya zitatolewa kulingana na jinsi badala ya huduma kutolewa na jinsi tofauti na wanufaika kwenye sekta ya afya na ajira haitajali dini bali ni kwa dini zote kwani lengo ni kutoa huduma bora na za kisasa,"amesema Abeid.

Aidha amesema kuwa matarajio ni kuanza ujenzi Januari mwakani mara fedha zitakapopatikana na kikubwa wadau mbalimbali wajitokeze kuchangia fedha ili kufanikisha ujenzi huo kwani watu wajitoe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kujenga ahera yetu.

Akizungumzia kuhusu sikukuu ya Iddi amesema kuwa siyo kuvaa vizuri na kupendeza bali ni kwa yule mwenye kumuogopa Mwenyezi Mungu na kukumbuka siku ya hesabu (Kiyama) ndiyo maana ya Iddi.

Ameongeza kuwa watu wamwabudu Mwenyezi Mungu na kuacha kumkasirisha na waishi maisha haya na si wakati wa mfungo peke yake ili wasimkosee.

Thursday, March 12, 2026

KIVUKO MKOMBOZI WANAFUNZI SHULE YA MAMLAKA

 MTAA wa Machinjioni Kata ya Tangini umeishukuru Serikali kwa ujenzi wa kivuko kwenye barabara inayoelekea Shule ya Msingi Mamlaka kwa kuwaondolea adha ya wanafunzi kuvuka kwa kubebwa mgongoni.

Ujenzi wa kivuko hicho ambacho kimewekwa makalavati mawili kimeweza kuwaondolea adha wanafunzi wa shule hiyo ambapo kipindi cha mvua walishindwa kuvuka hadi wavushwe na watu wazima. 

Akizungumza na Mwenyekiti wa Mtaa huo Aidan Mchiwa amesema kuwa mbali ya changamoto iliyokuwepo kwa wanafunzi lakini pia iliwakumba wakazi wa maeneo karibu na shule hiyo.

Mchiwa amesema kuwa manufaa ya kivuko hicho yameonekana ambapo mvua kubwa zilizonyesha juzi wanafunzi na wananchi wanavuka bila ya shida yoyote tofauti na ilivyokuwa awali ikiwa ni wakati wa siku 100 za Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

"Eneo hilo ni mkondo wa maji hivyo mvua zinazonyesha maeneo mbalimbali maji yake yanapita hapo kwani ni eneo ambalo kuna bonde hivyo maji yanakuwa mengi na kusababisha adha kwa watu wanaopita kwenye barabara hiyo inayoelekea shuleni,"amesema Mchiwa.

Amesema kuwa serikali kupitia Halmashauri ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 9 na kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kujenga kivuko hicho ambapo hata magari na pikiiki yalikuwa yakipita kwa shida.

"Kuna maboresho kidogo yanatakiwa kufanyika ikiwa ni pamoja na mitaro na tukifanikiwa kupata fedha tutaichimba kwani bajeti tuliyopewa ya ujenzi wa kivuko hicho iliisha tutaomba kwa bajeti hii ili tuboreshe zaidi,"amesema Mchiwa.

Aidha amesema kuwa pia kwa kushirikiana na wananchi walifungua barabara tatu za Aidan, Nida na Kilima huku mbili zikiwa zimebakia za kwa Kapungu na kwa Landa.

KIVUKO MKOMBOZI WANAFUNZI SHULE YA MAMLAKA

MTAA wa Machinjioni Kata ya Tangini umeishukuru Serikali kwa ujenzi wa kivuko kwenye barabara inayoelekea Shule ya Msingi Mamlaka kwa kuwaondolea adha ya wanafunzi kuvuka kwa kubebwa mgongoni.

Ujenzi wa kivuko hicho ambacho kimewekwa makalavati mawili kimeweza kuwaondolea adha wanafunzi wa shule hiyo ambapo kipindi cha mvua walishindwa kuvuka hadi wavushwe na watu wazima. 

Akizungumza na Mwenyekiti wa Mtaa huo Aidan Mchiwa amesema kuwa mbali ya changamoto iliyokuwepo kwa wanafunzi lakini pia iliwakumba wakazi wa maeneo karibu na shule hiyo.

Mchiwa amesema kuwa manufaa ya kivuko hicho yameonekana ambapo mvua kubwa zilizonyesha juzi wanafunzi na wananchi wanavuka bila ya shida yoyote tofauti na ilivyokuwa awali ikiwa ni wakati wa siku 100 za Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

"Eneo hilo ni mkondo wa maji hivyo mvua zinazonyesha maeneo mbalimbali maji yake yanapita hapo kwani ni eneo ambalo kuna bonde hivyo maji yanakuwa mengi na kusababisha adha kwa watu wanaopita kwenye barabara hiyo inayoelekea shuleni,"amesema Mchiwa.

Amesema kuwa serikali kupitia Halmashauri ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 9 na kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kujenga kivuko hicho ambapo hata magari na pikiiki yalikuwa yakipita kwa shida.

"Kuna maboresho kidogo yanatakiwa kufanyika ikiwa ni pamoja na mitaro na tukifanikiwa kupata fedha tutaichimba kwani bajeti tuliyopewa ya ujenzi wa kivuko hicho iliisha tutaomba kwa bajeti hii ili tuboreshe zaidi,"amesema Mchiwa.

Aidha amesema kuwa pia kwa kushirikiana na wananchi walifungua barabara tatu za Aidan, Nida na Kilima huku mbili zikiwa zimebakia za kwa Kapungu na kwa Landa.

Wednesday, March 11, 2026

BIDHAA SOKO LA LOLIONDO BEI NZURI

BEI ya Vitunguu kwenye Soko la Loliondo Halmashauri ya Manispaa Kibaha iko juu kutoka shilingi 130,000 hadi 250,000 kwa gunia.

Aidha viazi mbatata ambavyo ni maarufu kwa ajili ya kukaangia chipsi vimeshuka bei kutoka shilingi 140,000 hadi 70,000 kwa gunia.

Akizungumza ofisini kwake Mjini Kibaha Naibu Katibu Mkuu wa soko hilo Alex Msimbe alisema kuwa kwa sasa bidhaa nyingi bei zake hazijapanda sana bali bei iko wastani.

Msimbe alisema kuwa bei hiyo ya vitungu imeongezeka sana kutokana na kipindi hichi ndiyo bei huwa inapanda sana lakini baadaye bei hiyo itashuka.

"Bei ya tenga la nyanya  imeshuka kutoka kati ya shilingi 85,000 na 70,000 hadi 35,000 huku mchele ukiuzwa kati ya shilingi 3,000, 2,500 hadi 2,700 kwa kilo na maharage yakiuzwa kati ya shilingi 2,700 hadi 3,000 kwa kilo.

Alisema kuwa bei ya unga wa sembe ni kati ya shilingi 1,400 na 1,500 kwa kilo na ngano ni shilingi 125,000 kwa kilo 50 huku sukari ikiuzwa shilingi 3,000 kwa kilo.

"Bei za bidhaa nyingi bei hazijapanda kwani kipindi hichi ni cha baadhi ya maeneo ni mavuno na mengine ndiyo wamepanda muda siyo mrefu hivyo kutoathiri sana bei,"alisema Msimbe.

Aidha alisema kuwa kwa sasa hakuna changamoto kwenye soko hilo kwani miundombinu ikiwemo ya maji, umeme na huduma muhimu kama za vyoo zote ziko vizuri kwani wanashirikiana vizuri na Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha ambao ndiyo wanaowasimamia.

"Kuhusu mitaji baadhi ya wafanyabiashara wananufaika na mikopo ya Halmashauri ile ya asilimia 10 na asilimia 7,"alisema Msimbe.

Tuesday, March 10, 2026

DED GAIRO APONGEZWA UJENZI WA SHULE YA AMALI

Hawa Wazee wangu ni Wawakilishi wa wana Kijiji cha Kwipipa kata ya Rubeho.

Walituma salam zao kupitia kwa Mhe. Diwani wiki mbili zilizopita kuwa wananiita. Na leo nimekutana nao kuwasilikiza, kumbe walitaka kunipa shukrani kwa ajili ya Mradi wa Shule ya AMALI iliyojengwa kwenye Kijiji cha Kwipipa. Wameshukuru kwa Usimamizi hadi Ukamilishaji wa shule na hatimae watoto wameanza masomo

Wazee wangu hawa tulianza nao wakati tunatafuta eneo na wakatoa eneo lote la Mradi. Wametoa salamu zao kwa Maandishi, kuongea na mwisho wakatoa mbuzi.


Saturday, March 7, 2026

KIKUNDI CHA LULU YA WAJANE WAISHUKURU MANISPAA YA KIBAHA KWA MKOPO WA MILIONI 46

KIKUNDI cha wanawake cha Lulu ya Wajane kilichopo  Kongowe, Manispaa ya Kibaha mkoani Pwani, kimeishukuru Manispaa ya Kibaha kwa kuwapatia mkopo wa shilingi milioni 46 uliowawezesha kuendesha na kukuza shughuli zao za kiuchumi.

Akizungumza kwa niaba ya wanakikundi, Mwenyekiti wa kikundi hicho Kanyenda Mweri amesema mkopo huo waliupata kupitia mpango wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri kwa makundi maalum, na wamefanikiwa kuurejesha ndani ya kipindi cha miezi 11.

Amesema kikundi chao kinajishughulisha na ufugaji wa kuku wa aina mbalimbali, ambapo huuza kuku hao kwa jumla na rejareja na hivyo kuwa chanzo kikuu cha kipato kwa wanachama wake.

Aidha, amesema baada ya mafanikio waliyoyapata, kwa sasa wanatarajia kuomba mkopo mwingine ambao utawawezesha kununua mashine ya kutotolea vifaranga ili kupanua zaidi shughuli zao za ufugaji na kuongeza uzalishaji.

Kikundi hicho kimebainisha kuwa mkopo huo umewasaidia kujikwamua kiuchumi na kuboresha maisha yao, sambamba na kutoa ajira kwa baadhi ya wananchi katika eneo lao.

PANGANI SEKONDARI WAPANDA MITI 344

SHULE ya Sekondari Pangani, Manispaa ya Kibaha imefanya zoezi la kupanda miti zaidi ya 344 katika mazingira ya shule hiyo ikiwa ni sehemu ya kutekeleza agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhimiza taasisi za elimu kuhifadhi mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Zoezi hilo limehusisha wanafunzi, walimu pamoja na viongozi wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Pangani kwa lengo la kuboresha mazingira ya shule hiyo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Tatu Mwambala amefafanua miti hiyo ni ya kivuli na mbao ambapo miti 220 imetolewa na kitalu cha Manispaa, miti 110 kutoka Wakala wa Misitu kupitia Shule ya Sekondari Msangani II na miti 14 ya matunda imenunuliwa na shule.

Amesema miti hiyo itasaidia kukuza stadi za utunzaji wa mazingira kwa wanafunzi pamoja na kuboresha mazingira ya shule.

Diwani wa Kata ya Pangani, John Katele amebainisha zoezi hilo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM pamoja na mikakati ya kupanda miti milioni 1.5 katika mkoa huo.

Kwa upande wake Ofisa Kilimo wa kata hiyo, Omary Ngulengule ameeleza kuwa, wanafunzi wamepata elimu ya vitendo kuhusu uchimbaji mashimo na upandaji sahihi wa miti ili wawe mabalozi wa utunzaji wa mazingira katika jamii.

Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule hiyo, Stanley Amos ameeleza elimu waliyoipata itawasaidia kuhamasisha familia na jamii kupanda miti na kutunza mazingira.