Saturday, January 24, 2026

VIJANA WAPEWE MALEZI BORA KULINDA AMANI

MZJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) NEC Taifa kupitia Jumuiya ya Wazazi Hamoud Jumaa ameitaka Jumuiya hiyo kuwapa vijana malezi mazuri ili watunze amani.

Jumaa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini ameyasema hayo Mjini Kibaha wakati akifungua kikao cha Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani.

Amesema kazi ya Jumuiya hiyo ni kuhakikisha jamii hususani vijana wanakuwa na malezi bora ili kutojiingiza kwenye makundi ambayo hayana maadili mema.

"Tuwape elimu na malezi mazuri vijana wetu na tuzungumze nao juu ya amani kwani amani pia huleta afya njema na amani ndiyo kila jambo hivyo tuhubiri amani,"amesema Jumaa.  

Aidha amesema vijana nchini wanapaswa kudumisha amani na kutokubali kurubuniwa ili wasivunje amani iliyopo kwani bila amani hatutaweza kufanya mambo ya maendeleo.

"Vijana wanapaswa kulinda amani kwani ndiyo msingi wa Taifa la Tanzania na wasukubali kushawishiwa na watu kuharibu amani iliyopo kwani ikipotea ni gharama kuirudisha,"amesema Jumaa.

Amewataka viongozi wa Jumuiya  hiyo kuanza maandalizi ya uchaguzi wa Jumuiya utakaofanyika mwakani kwani uchaguzi ndani ya chama ni mgumu kuliko uchaguzi wa vyama.

"Muanze maandalizi na kama kuna kiongozi anaona anauwezo ajiandae kugombea kwenye chama wakati ukifika kwani Jumuiya hii ndiyo inayobeba jumuiya zote za chama,"amesema Jumaa.

Aliongeza kuwa viongozi wanapaswa kuacha alama kwa kuwa na miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kununua ardhi pamoja na ofisi za makatibu wa jumuiya kwa kila wilaya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Pwani Josiah Jackson amesema kuwa uchaguzi umekwisha kilichobaki ni kujenga jumuiya na chama.

Jackson amesema kuwa wanachama waache makandokando kwa kuwaacha waliochaguliwa wafanye kazi zao na kuwaunga mkono ambapo kwa mkoa walipata madiwani 17 kutoka jumuiya.

Naye katibu wa CCM Mkoa wa Pwani  Kitte Mfilinge amesema kuwa anaipongeza jumuiya kwa kufanya vizuri kwenye uchaguzi mkuu kwani mkoa umeshika nafasi tatu za juu hapa nchini.

Mfilinge amesema kuwa Jumuiya hiyo iko vizuri kwani ina mshikamano na imetulia hivyo kwa sasa wajiandae na uchaguzi wa jumuiya mwakani lengo ni kujenga chama ili kiwe imara.



Friday, January 23, 2026

AJIPATIA KIPATO KUPITIA PANYA WEUPE

VIJANA Mkoani Pwani wameshauriwa kuchangamkia mradi wa ufugaji panya weupe ambao ni chanzo cha mapato ambapo mmoja huuzwa kati ya shilingi 3,000 hadi 5,000 kwa panya mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Kibaha Mtaalamu wa Mifugo na Kilimo Rodney Mwasha amesema kuwa ufugaji wa panya hao hauna gharama kubwa.

Mwasha amesema kuwa panya hao ambao asili yao ni kutoka Japan wanatumika mashuleni kwa ajili ya mafunzo kwa wanafunzi mashuleni kwa somo la Bailojia.

"Panya hawa ni rahisi kuwafuga na hawana usumbufu na hata kuwahudumia ni rahisi kwani ni rafiki na siyo wakorofi na hawakufanyi kushindwa kufanya shughuli nyingine,"amesema Mwasha.

Amesema kuwa mradi huo ni mzuri na hautumii gharama kubwa za uzalishaji ambapo panya mmoja anauwezo wa kuzaa watoto nane hadi 10 kwa wakati mmoja na huzaa kila mwezi.

"Mimi nafuga kuku wa kienyeji, bata bukini, bata mzinga, nyuki na upande wa kilimo nalima mbogamboga na kuzalisha uyoga hivyo ufugaji wa panya nao ni sehemu ya kuongeza kipato,"amesema Mwasha.

Aidha amesema kuwa mahitaji ya panya kwa mashule ni kubwa sana hivyo vijana watumie fursa hiyo ili waweze kuongeza kipato chao na familia zao.

"Changamoto ya hawa panya ni nyoka ambao hupenda sana kula panya hivyo endapo hujaimarisha banda wanaweza kuliwa na changamoto nyingine ni maradhi,"amesema Mwasha.

Aliongeza kuwa panya hao chakula chao ni pumba, nafaka kama vile mahindi mtama na dagaa ambapo panya 300 gharama za kuwalisha ni kama 100,000 na faida ni kama milioni 1.5.

"Panya hawa wana uwezo wa kuishi miaka miwili na yeye alianza kwa kufuga panya wanne na sasa ana panya 300 hadi 400 ambapo soko lake huwa kipindi cha katikati ya mwaka,"amesema Mwasha.

Wednesday, January 21, 2026

FIDIA LAMI MAILI MOJA SHELI-MUHEZA ZAIVA

WANANCHI 65 wanaopitiwa na mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Barabara kuu ya Morogoro Bp Sheli hadi Muheza Kata ya Maili Moja Wilaya ya Kibaha wamefanyiwa tathmini kwa ajili ya kulipwa fidia.

Diwani wa Kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi amesema kuwa zoezi hilo ni muhimu kabla ya kuanza kutekelezwa kwa mradi huo Uboreshaji Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC) kwa Manispaa ya Kibaha.

Lutambi amesema kuwa barabara hiyo ni muhimu sana kwani itaufungua Mji wa Maili Moja pia itafungua uchumi wa wakazi wa Kata hiyo kuondoa changamoto ya ubovu wa barabara.

"Ninachowaomba wananchi kutoa ushirikiano ili ujenzi usiwe na changamoto kwani kwa sasa hichi ndiyo kipaumbele cha Kata yetu kwa mwaka huu lazima lami ijengwe ikiwa ni awamu ya kwanza,"amesema Lutambi.

Amesema ni mradi muhimu sana kwani utafungua fursa nyingi za kiuchumi na kurahisisha usafiri kuwa wa haraka na usafirishaji na Mji utajengeka na kuleta maendeleo kwenye Mitaa ya Uyaoni, Maili Moja Shule na Muheza.

Naye Salum Mizoka Mthamini wa mradi kutoka Kampuni ya Botek ambaye ni Mkandarasi mshauri kwa kushirikiana na Kampuni ya Uress amesema zoezi hilo linakwenda vizuri.

Mizoka amesema kuwa uthamini unaofanyika ni kujua kila mlengwa anadai na atalipwa nini na baada ya hapo malipo yatafanyika kwa wahusika ambao wameshatambuliwa kwenye barabara hiyo kwa awamu ya kwanza ikianza na kilometa 4.

Amesema kuwa lengo la kufanya tathmini ni kuhakikisha kila mtu anayepitiwa na mradi huo ambapo sehemu za nyumba au baraza zinataguswa watalipwa fidia.

"Tunataka kusiwe na migogoro wakati wa utekelezaji wa mradi ili ujenzi ufanyike bila ya manunguniko kwani walengwa watalipwa stahiki zao bila ya tatizo lolote,"amesema Mizoka.

Aidha amesema kuwa malipo hayo yanafanywa kulingana na hali ya soko kwa sasa na hadi wakati huu hakuna changamoto na zilizopo ni ndogo ndogo.

Tuesday, January 13, 2026

BAGAMOYO SUGAR YATWAA UBINGWA MKOA WA PWANI

TIMU ya soka ya Bagamoyo Sugar ya Wilayani Bagamoyo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Daraja la tatu Mkoa wa Pwani baada ya kuifunga Kiduli Fc ya Wilaya ya Kibaha kwa magoli 3-2 kwenye mchezo wa fainali.

Bagamoyo Sugar wametwaa ubingwa kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya fainali ya kwanza kushinda kwa kupata ushindi wa goli 1-0.

Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Wilaya ya Kibaha ulikuwa mkali na kuvutia mashabiki wengi wa Kibaha na Viunga vyake.

Kwa matokeo hayo timu ya Bagamoyo Sugar watawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya mabingwa wa mikoa.

Akikabidhi kombe kwa washindi mgeni rasmi wa mchezo huo huo Fidha Helmud (Tyson) ambaye ni Rais wa timu ya Barberian inayoshiriki ligi Daraja la Kwanza alizipongeza timu hizo kwa kuonyesha ufundi mkubwa wa kusakata kabumbu.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi amesema kuwa kufuatia kuwa mabingwa wa Mkoa huo watahakikisha wanaiunga mkono kwenye mashindano yanayofuata.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mabingwa wapya wa Mkoa wa Pwani Bagamoyo Sugar amesema kuwa kwa kushirikiana na Chama Cha Soka Wilaya ya Bagamoyo (BFA) Kelvin Mawata amesema kuwa lengo ni kuhakikisha timu hiyo inafika mbali kwa kufanya vizuri.

Mwenyekiti wa Kiduli Fc Ally Masimike amesema kuwa amekubaliana na matokeo hayo ambapo timu hiyo itarudi kambini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali.

BAGAMOYO SUGAR BINGWA PWANI

TIMU ya soka ya Bagamoyo Sugar ya Wilayani Bagamoyo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Daraja la tatu Mkoa wa Pwani baada ya kuifunga Kiduli Fc ya Wilaya ya Kibaha kwa magoli 3-2 kwenye mchezo wa fainali.

Bagamoyo Sugar wametwaa ubingwa kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya fainali ya kwanza kushinda kwa kupata ushindi wa goli 1-0.

Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Wilaya ya Kibaha ulikuwa mkali na kuvutia mashabiki wengi wa Kibaha na Viunga vyake.

Kwa matokeo hayo timu ya Bagamoyo Sugar watawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya mabingwa wa mikoa.

Akikabidhi kombe kwa washindi mgeni rasmi wa mchezo huo huo Fidha Helmud (Tyson) ambaye ni Rais wa timu ya Barberian inayoshiriki ligi Daraja la Kwanza alizipongeza timu hizo kwa kuonyesha ufundi mkubwa wa kusakata kabumbu.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi amesema kuwa kufuatia kuwa mabingwa wa Mkoa huo watahakikisha wanaiunga mkono kwenye mashindano yanayofuata.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mabingwa wapya wa Mkoa wa Pwani Bagamoyo Sugar amesema kuwa kwa kushirikiana na Chama Cha Soka Wilaya ya Bagamoyo (BFA) Kelvin Mawata amesema kuwa lengo ni kuhakikisha timu hiyo inafika mbali kwa kufanya vizuri.

Mwenyekiti wa Kiduli Fc Ally Masimike amesema kuwa amekubaliana na matokeo hayo ambapo timu hiyo itarudi kambini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali.

BINGWA

TIMU ya soka ya Bagamoyo Sugar ya Wilayani Bagamoyo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Daraja la tatu Mkoa wa Pwani baada ya kuifunga Kiduli Fc ya Wilaya ya Kibaha kwa magoli 3-2 kwenye mchezo wa fainali.

Bagamoyo Sugar wametwaa ubingwa kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya fainali ya kwanza kushinda kwa kupata ushindi wa goli 1-0.

Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Wilaya ya Kibaha ulikuwa mkali na kuvutia mashabiki wengi wa Kibaha na Viunga vyake.

Kwa matokeo hayo timu ya Bagamoyo Sugar watawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya mabingwa wa mikoa.

Akikabidhi kombe kwa washindi mgeni rasmi wa mchezo huo huo Fidha Helmud (Tyson) ambaye ni Rais wa timu ya Barberian inayoshiriki ligi Daraja la Kwanza alizipongeza timu hizo kwa kuonyesha ufundi mkubwa wa kusakata kabumbu.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi amesema kuwa kufuatia kuwa mabingwa wa Mkoa huo watahakikisha wanaiunga mkono kwenye mashindano yanayofuata.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mabingwa wapya wa Mkoa wa Pwani Bagamoyo Sugar amesema kuwa kwa kushirikiana na Chama Cha Soka Wilaya ya Bagamoyo (BFA) Kelvin Mawata amesema kuwa lengo ni kuhakikisha timu hiyo inafika mbali kwa kufanya vizuri.

Mwenyekiti wa Kiduli Fc Ally Masimike amesema kuwa amekubaliana na matokeo hayo ambapo timu hiyo itarudi kambini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali.

Monday, January 12, 2026

BAGAMOYO SUGAR MABINGWA DARAJA LA TATU MKOA WA PWANI

TIMU ya soka ya Bagamoyo Sugar ya Wilayani Bagamoyo imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Daraja la tatu Mkoa wa Pwani baada ya kuifunga Kiduli Fc ya Wilaya ya Kibaha kwa magoli 3-2 kwenye mchezo wa fainali.

Bagamoyo Sugar wametwaa ubingwa kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya fainali ya kwanza kushinda kwa kupata ushindi wa goli 1-0.

Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Wilaya ya Kibaha ulikuwa mkali na kuvutia mashabiki wengi wa Kibaha na Viunga vyake.

Kwa matokeo hayo timu ya Bagamoyo Sugar watawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya mabingwa wa mikoa.

Akikabidhi kombe kwa washindi mgeni rasmi wa mchezo huo huo Fidha Helmud (Tyson) ambaye ni Rais wa timu ya Barberian inayoshiriki ligi Daraja la Kwanza alizipongeza timu hizo kwa kuonyesha ufundi mkubwa wa kusakata kabumbu.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi amesema kuwa kufuatia kuwa mabingwa wa Mkoa huo watahakikisha wanaiunga mkono kwenye mashindano yanayofuata.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mabingwa wapya wa Mkoa wa Pwani Bagamoyo Sugar amesema kuwa kwa kushirikiana na Chama Cha Soka Wilaya ya Bagamoyo (BFA) Kelvin Mawata amesema kuwa lengo ni kuhakikisha timu hiyo inafika mbali kwa kufanya vizuri.

Mwenyekiti wa Kiduli Fc Ally Masimike amesema kuwa amekubaliana na matokeo hayo ambapo timu hiyo itarudi kambini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali.