Tuesday, October 15, 2024

MKUU WA MAJESHI AWAVISHANI NISHANI MAJENERALI, MAAFISA NA ASKARI WA JWTZ




Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Jacob John Mkunda kwa niaba ya Mhe Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt Samia Suluhu Hassan amewavisha nishani mbalimbali Majenerali, Maafisa na Askari wa JWTZ Jijini Mwanza tarehe 15 Oktoba 2024.

Nishani hizo ni Nishani ya Utumishi Uliotukuka, Nishani ya Utumishi Mrefu, Nishani ya Utumishi Mrefu na Tabia Njema, Nishani ya Miaka 60 ya Muungano pamoja na Nishani ya Miaka 60 ya JWTZ.

Aidha,Jenerali Mkunda amewavisha nishani ya Jumuiya ya SADC Maafisa na Askari walioshiriki Ulinzi wa Amani nchini Msumbiji chini ya mwavuli wa Jumuiya hiyo.



Sunday, October 13, 2024

SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU NYERERE YAINGIA MAKUBALIANO NA CHUO CHA RENMIN CHA CHINA

SHULE ya Uongozi  ya Mwalimu Nyerere imeingia makubaliano  ya ushirikiano na Chuo Kikuu cha Renmin katika nyanja mbalimbali zikiwemo za mafunzo utafiti na kubadilishana wataalamu.

Wakisaini makubaliano hayo kati ya Mkuu wa Shule ya Mwalimu Nyerere Profesa Marcellina Chijoriga na kiongozi mkuu wa Chama Tawala Cha China Cha (CPC) kwenye Renmin Zhang Donggang katika Shule hiyo iliyopo Kibaha Mkoani Pwani walifurahishwa na ushirikiano huo.

Chijoriga alisema kuwa makubaliano hayo yatakuwa ni kwa ajili ya kubadilishana wataalamu ambapo wao watakuja huku na wa Tanzania watakwenda kwao ikiwa ni sehemu ya kubadilishana uzoefu.

“Chuo hicho ni kikubwa sana na cha muda mrefu na kiko vizuri kwenye masuala ya utafiti wa uandishi wa vitabu na katika masuala ya uandishi wa vitabu ambapo ushirikiano huo utakuwa na manufaa makubwa sana kwa pande zote mbili,”alisema Chijoriga.

Alisema kuwa chuo hicho cha Renmin kinauwezo mkubwa wa kuwajengea uwezo viongozi wa chama na serikali kwani kiko vizuri sana katika ufundishaji masuala hayo na watatumia uzoefu ili kujifunza kupitia kwao kwani kimeanza muda mrefu.

“Faida hiyo ni kwa vyama sita vya ukombozi Kusini mwa Afrika ambapo China ni msaidizi mzuri kwani wamesaidia ujenzi wa shule hiyo ambavyo ni CCM, FRELIMO, SWAPO, ANC na ZANU-PF ambapo CPC .  

Aidha alisema kuwa chuo hicho kilichopo Beijeng China kilianza ushirikiano mwaka jana ambapo uongozi wa Shule walikwenda na katibu mkuu wa CCM wakati ule Chongolo na sasa imeanza safari mpya na kina uzoefu mkubwa nani cha zamani sana.

“Tunashukuru sana kwani wametuonyesha ushirikiano mkubwa na makubaliano ya kutengeneza ushirikiano huu ni sasa safari mpya imeanz na leo waametupa vitabu tunawashukuru kwani maktaba yetu sasa itakuwa na vitabu vingi na wasomaji wataweza kujifunza masuala mbalimbali ya nchi ya China,”alisema Chijoriga.

Naye alisema Dk Evaristo Haule Naibu Mkuu wa Chuo Mipango Fedha na Utawala Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere alisema kuwa China imefanikiwa na tumeona namna gani kutumia njia ili kuona wao wamefanyaje na kufikia hatua kubwa kiasi hicho kwenye maendeleo na CPC inavyotoa dira kuongoza nchi yao wanataka twende pamoja katika miradi yao mikubwa ya kidunia.

 Haule alisema kuwa ili kwenda pamoja hivi karibuni Rais Dk Samia Suluhu Hassan alienda China kwenye mkutano wa ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika wao wana dira  na kufanya kazi kwa bidii na kuwa na nidhamu ya kazi na watu wawe na uzalendo wa nchi watu wanaangalia changamoto badala ya kuangalia fursa zilizopo.

Naye Dk Theresia Dominick kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam alisema kuwa Watanzania wanatakiwa kujifunza kwa kuwa nadhifu na wanaangalia masuala ya ulaji na wawe watu wa kujishusha na kuachana na matumizi yasiyo ya lazima na wasiwe na tamaa.

Dominick alisema  kuwa badhi ya wafanyabiashara Watanzania wamekuwa wakienda China hivyo wanapaswa kujifunza tabia za Wachina za kufanya kazi kwa bidii na kuwa na nidhamu ya jambo wanalolifanya ni mfano wa kuigwa.

Naye kiongozi huyo Zhang Donggang alisema kuwa ushirikiano uliopo baina ya China na Tanzania nan chi nyingine ni katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo ambapo wao wanaangalia sana maslahi ya wananchi.

Donggang alisema kuwa nchi za Afrika na China zinapaswa kushikana mkono katika kuhakikisha zinapiga hatua katika masuala ya kimaendeleoili kudumisha umoja uliopo kwani umoja uliopo umeleta mafanikio makubwa.

Mwisho. 


BASHUNGWA ARDHISHWA UJENZI SEKONDARI MPYA YA MSANGANI


WAZIRI wa Ujenzi Innocent Bashungwa ametaka kukamilishwa kwa ujenziwa Shule mpya ya Sekondari iliyopo mtaa wa Msangani Kata ya Masangani Wilayani Kibaha Mkoani Pwani yenye thamani ya shilingi milioni 528 iliyojengwa kwa fedha zitokanazo na mradi wa Seqip.

Bashungwa ameyasema hayo alipoweka jiwe la msingi la ujenzi wa shule hiyo ambayo iko kwenye hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na upauaji wa baadhi ya majengo mengine yakiwa kwenye hatua ya linta.

Amesema wajenzi hao wahakikishe ujenzi huo unakamilika kwa wakati uliopangwa ambapo ni Novemba mwaka huu ili Januari mwakani wanafunzi waanze kusoma ili kuwapunguzia umbali wanaotembea kutoka nyumbani na kwenda shule.

Amebainisha kuwa huo ni mwéndelezo wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan wa kuwekeza kwenye sekta ya elimu ambapo hakuna kijiji wala kata ambayo haijajengwa shule na hilo ni jambo la kupongezwa
na anaonyesha jinsi gani anavyothamini na kulipa  umuhimu suala la elimu kwa watoto.

"Wakala wa Barabaraba Nchini (TANROADS) Mkoa wa Pwani hakikisheni manaandika barua wizarani
mkandarasi alipwe ili arudi kazini kukamilisha ujenziwa kipande cha lami kuja Msangani kilichobaki kinakamilka na barabaraba za Tarura nazo mziangalie kupitia mfuko wa barabara ili kuwaondole a kero wananchi,"a lisema Bashungwa.

Aidha amesema kuwa kuhusu barabara ya njia nane wako kwenye mchakato wa kupata wawekezaji ili kuondoa changamoto ya foleni Kibaha ambapo kwa sasa imekuwa kero kubwa kwa wasafiri lengo ni kurahisisha usafiri maeneo yote.

Katika hatua nyingine amesemna kuwa ataongea na Waziri wa Maji ili kufanikisha kujengwa kisima
kwenye shule hiyo ambayo bado haina miundombinu ya maji ili kukabiliana na changamoto ya jami kwani hata maji ya ujenzi yanatolewa mbali.

Kwa upande vwake mkuu wa mkoa wa Pwani
Abubakari Kunenge amesema kuwa katika kipindi cha miaka minne ya utawala wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan jumla ya Shule 10 za Sekondari na Shule 10 za Msingi zimejengwa Wilayani Kibaha.

Kunenge amesema kuwa anamshukuru Rais kwa kuupatia mkoa huo fedha za maendeleo kiasi cha
shilingi trilioni 1.3 kwa ajili ya miradi mbalimbali
ya maendeleo hali ambayo inafanya mkoa huo kupiga hatua kubwa ya maendeleo kwa kipindi hichi cha awamu ya sita.

Naye mwalimu mkuu wa shule hiyo Lilian Marandu amesema kuwa mradi huo ulitambulishwa mwezi
mmoja uliopita na unatarajiwa kukamilika Novemba ukiwa na awamu saba za ujenzi ambapo kwa sasa umefikia hatua mbalimbali zikiwemo kupaua, lita na msingi.

Marandu amesema kuwa mradi huo una majengo yakiwemo ya utawala, maabara za masomo ya
5 sayansi, madarasa manne, vyoo matundu 12 kichomea taka na mnara wa tanki la maji na ofisi mbili za walimu ambazo wanategemea kukamilika ndani ya muda uliopangwa.

WAHITIMU KIDATO CHA NNE WATUMIE RASILIMALI ZILIZOPO NCHINI

WAHITIMU wa kidato cha nne nchini wametakiwa kuacha mawazo ya kwenda nje ya nchi kutafuta maisha badala yake watumie rasilimali za nchi kuongeza pato la Taifa.

Hayo yalisemwa Jijini na Mkurugenzi Mtendaji wa (SUMA JKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata wakati wa mahafali ya 40 ya kidato cha nne ya Shule ya Sekondari Jitegemee JKT.

Ngata alisema baadhi ya vijana wamekuwa na mawazo ya kwenda nje ya nchi kutafuta maisha mazuri na kuacha rasilimali zilizopo ambazo matafa ya nje wanazifuata.

"Msitamani kwenda majuu kwani wa huko wanatamani kuja huku kutumia rasilimali zetu ambazo Mungu ametubariki kuwa nazo na hazipo kokote kule zaidi ya Tanzania hivyo tumieni maarifa mliyopata ili kuzitumia,"alisema Ngata.

Alisema kuwa moja ya rasilimali ambayo vijana wanaweza kuitumia ni ardhi ambayo ikitumika vizuri inaweza kuwainua vijana kupitia maarifa waliyoyapata shuleni ambapo wamefundishwa ujasiriamali pamoja na kilimo.

"Ardhi ni chanzo kikubwa cha shughuli ya kufanya lakini mbali ya kilimo kuna uvuvi, ufugaji na madini kazi siyo lazima kuajiriwa ofisini unaweza kujiajiri mwenyewe kupitia stadi mlizojifunza,"alisema Ngata.

Aidha alisema vijana wanapaswa kuchangamkia fursa zilizopo na kuacha kushiriki kwenye mambo maovu hasa yale yanayohamasishwa kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo siasa uchwara na kuwa na nidhamu nakutojiingiza kwenye masuala ya ngono.

Naye Mkuu wa Shule hiyo Kanali Robert Kesi alisema kuwa wamewaandaa vizuri wanafunzi kwa kufanya mitihani mingi ya majaribio yenye hadhi ya kitaifa kwa nadharia na vitendo na wameiva .

Kesi alisema kuwa watawafanyia wahitimu semina kwa ajili ya kujiamini kwani kwenye mtihani hakuna maajabu na wasijihusishe na njia za udanganyifu wamshirikishe Mungu kwa kila jambo na kuwa hawataki daraja la nne kwani mwaka jana hakukuwa na daraja sifuri. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya Shule Bregadia Mstaafu Lawrence Magere alisema kuwa wanategemea changamoto zilizopo shuleni hapo zitafanyiwa kazi na wanawapongeza walimu kwa maandalizi mazuri kwa wanafunzi hao.

Awali akisoma risala ya wahitimu Shekha Said alisema kuwa moja ya mafanikio waliyopata ni kujifunza elimu ya ujasirismali ambapo wanaweza kutengeneza sabuni, kilimo cha mbogamboga, kutengeneza balbu zilizoungua na kurudi kufanya kazi kama zamani.

Said alisema kuwa shule inakabiliwa na changamoto ya uchakavu wa miundombinu pia madarasa hayana dari hali inayofanya sauti kuingiliana kati ya darasa na darasa wakati wa masomo, jumla ya wahitimu 89 waliagwa shuleni hapo.

Mwisho.



Saturday, October 12, 2024

MILIONI 1.2 KUANDIKISHWA PWANI

WATU milioni 1.2 Mkoani Pwani wanatarajiwa kuandikishwa kwenye Daftari la wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu.

Akizungumza baada ya kuzindua zoezi hilo kwenye Mtaa wa Mkoani A uliopo Kata ya Tumbi Wilaya ya Kibaha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge alisema kuwa idadi hiyo inatokana na sensa iliyofayika ambapo alisema kuwa vijana wengi watakuwa wamefikisha miaka 18 hivyo kuwa na sifa za kujiandikisha kupiga kura.

Kunenge alisema kuwa mkoa una jumla ya vituo vya kuandikisha wapiga kura 2,374 na kuna Vijiji 417, vitongoji 2,028 na Mitaa 72 ambapo wananchi kwenye maeneo hayo wanapaswa kwenda kujiandikisha ili wapate fursa ya kupiga kura itakapofika wakati wa uchaguzi.

“Tumeweka vituo vingi vya kujiandikisha kupunguza msongamano ili kila mtu apate haki ya kujiandikisha ili aje apate fursa ya kupiga kura ambayo ni haki yako ya kikatiba kwa mujibu wa kanuni taratibu na sheria za nchi yetu hivyo wananchi mjitokeze kwa wingi,”alisema Kunenge.

Alisema kuwa viongozi wa kwanza ni wale wa ngazi za chini hivyo kuchagua viongozi hawa ni wa muhimu sana kwani wao wako na wananchi kuanzia chini kabisa hivyo wananchi wanapaswa kujitokeza kuwachagua lakini waanze kujiandikisha kwanza kwani kama mwananchi hajajiandikisha hatapata fursa ya kupiga kura.

“Viongozi tunaoanza nao ni wa ngazi za chini kwa ajili ya kutuletea maendeleo na ndipo msingi wa utawala bora unapoanzia na hawa watatusaidia kutuletea maendeleo hivyo tuhakikishe tunashiriki kwenye uchaguzi huu ni muhimu sana ili kuchagua viongozi wanaotufaa,”alisema Kunenge.

Aidha alisema kuwa wananchi wajipange kushiriki uchaguzi kwani hiyo ni haki ya kikatiba hivyo wale wote waliofikia umri kuanzia miaka 18 wahakikishe wanajitokeza kujiandikisha ili wapate fursa ya kuchagua viongozi wanaowapenda.

“Hii ni fursa nzuri ya kuchagua viongozi ambao watatuongoza kwa kipindi cha miaka mitano na tukichagua viongozi bora watatuletea maendeleo ndani ya maeneo yetu kuanzia ngazi ya chini kabisa hivyo hii ni fursa kwetu sote kwa maendeleo yetu,”alisema Kunenge.

Kwa upande wake mmoja ya watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha ambaye ni moja ya watu waliokwenda kujiandikisha Simon Mwaiteleke alisema kuwa hiyo ni nafasi yake ya kumfanya ili aweze kuja kupiga kura kwa viongozi kwenye mtaa wake.

Mwaiteleke alisema kuwa uchaguzi ni hatua ya kupata viongozi watakaowatumikia wananchi hivyo anawaomba watu kujitokeza kwa wingi ili kutumia fursa hiyo ambayo hujitokeza kila baada ya miaka mitano.

Naye Saumu Almasi alisema kuwa hiyo ni fursa kwao wananchi kuchagua viopngozi wa Mtaa kuanzia mwenyekiti na wajumbe wake hivyo anaona ni fursa ya kumchagua kiongozi ambaye ana sifa ya kuongoza mtaa anaotoka.

Almasi alisema kuwa wananchi watumie fursa hiyo kumpata kiongozi bora na wasibaki kulalamika wakati hawashiriki uchaguzi kwani kiongozi bora anapatikana kwa kupigiwa kura na siyo kukaa pembeni na kulalamika.


Thursday, September 12, 2024

*KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ELIMU, UTAMADUNI YAIFAGILIA KIBAHA MJI KWA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO*

Na Mwandishi Wetu, Kibaha

Kamati ya Kudumu ya Bunge inayosimamia Wizara ya Elimu na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imeridhika na utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Shimbo iliyopo Kata ya Mkuza,Halmashauri ya Mji Kibaha.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.Husna Sekiboko  amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan ndoto na maono yake ni kuhakikisha watoto wa Kitanzania wanapata Elimu bora  kwenye Mazingira rafiki ili kuandaa Wataalam kulitumikia Taifa lao na kwamba Kibaha Mji wamesimamia Ujenzi wa shule hiyo kwa viwango na thamani ya fedha inaonekana.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Leah Lwanji ameieleza Kamati kuwa Jumla ya Shilingi 528,998,425 kupitia Mradi wa SEQUIP zilipokelewa  ajili ya Ujenzi wa miundombinu  27  na tayari imekamilika  na tayari Wanafunzi 281 kati yake wavulana 149 na Wasichana 132 wameanza kunufaika kwa kuwapunguzia umbali mrefu wa zaidi ya kilometa 8 kuifuata shule Mama ya Nyumbu.

Mhe.Hamisi Shabani Taletale ameipongeza Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa Mradi na kushauri kujengwa kwa uzio ili kuwawekea utulivu wanafunzi wakati wa Masomo.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Husna Sekiboko ametoa maelekezo ya Kamati kama ifuatavyo;

Mosi, Shule zote nchini ziwe na utaratibu wa kukagua maudhui ya vitabu kama vinaendana na maadili ya Watanzania kuelekeza vitabu vihakikiwe na kugongwa mihuri wa kuridhia Matumizi na Kamishina wa Elimu nchini.

Pili,Serikali iangalie upya mgawanyo wa fedha zinazotolewa kwa ajili ya Miradi kwani yapo maeneo wanakamilisha Ujenzi na maeneo mengine hawakamilishi ama Kujenga chini ya Kiwango na kuathiri matarajio na malengo.Ameitaka Wizara ya Elimu kufanya tathmini ya kimaeneo ili fedha zinazotolewa zitosheleze ili kuongeza tija ya Miradi husika.

Waziri wa Elimu Prof.Adolf Mkenda ameishukuru Kamati kwa kazi nzuri na kupokea maelekezo yote  ya Kamati kwa ajili ya kufanyia kazi.

Aidha,Mwenyekiti wa Kamati Mhe.Sekiboko amempongeza sana Dkt.Rogers Jacob Shemwelekwa Mkurugenzi wa Mji Kibaha kwa usimamizi mzuri wa Miradi ya Maendeleo kwa kushirikiana na Baraza la Madiwani kuhakikisha Mabilioni ya fedha yanayotolewa na Dkt.Samia Suluhu Hassan yanafanyakazi zinazoonyesha matokeo kwa Watanzania.

Wednesday, September 11, 2024

MAKOCHA WA TIMU ZA SOKA ZA JESHI WAPATA MAFUNZO TOKA KWA WAKUFUNZI TOKA UHOLANZI

Mkuu wa Majeshi nchini Jenerali Jacob Mkunda kupitia uratibu wa Baraza la Michezo la Majeshi ya Ulinzi Dunia (Conseil International du Sports Military) imewaleta wakufunzi na wataalum kutoa mafunzo kwa makocha ikiwa na lengo ni kuwaaendeleza maafisa wa jeshi na aksari wenye taaluma ya  ukocha wa Mpira wa miguu kutokana mahusiano  mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na nchi ya Uholanzi.

Dhamira ya mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa Tanzania ni  kupata walimu wazuri watakao saidia timu za jeshi zinazoshiriki ligi mbalimbali na Taifa.

Wakizungumza kwa wakati tofauti makocha ambao ni maafisa wa jeshi na aksari wameshukuru mkuu wa majeshi kwa kuliona hilo ambapo mbali na wakufunzi hao TFFwamekuwa wakitoa mafunzo mbalimbali lakini walimu hawa wakigeni wanavifaa  hivyo wanatoa ahadi ya kufanya vizuri katika kuhakikisha timu za majeshi na Taifa zinafanya vizuri.

Mafunzo  haya ni ya wiki mbili na ijumaa jioni yatafungwa rasmi hii inatokana na mahusiano mazuri ya Chama Cha Mpira wa Miguu cha Majeshi .