Wednesday, September 11, 2024

MAKOCHA WA TIMU ZA SOKA ZA JESHI WAPATA MAFUNZO TOKA KWA WAKUFUNZI TOKA UHOLANZI

Mkuu wa Majeshi nchini Jenerali Jacob Mkunda kupitia uratibu wa Baraza la Michezo la Majeshi ya Ulinzi Dunia (Conseil International du Sports Military) imewaleta wakufunzi na wataalum kutoa mafunzo kwa makocha ikiwa na lengo ni kuwaaendeleza maafisa wa jeshi na aksari wenye taaluma ya  ukocha wa Mpira wa miguu kutokana mahusiano  mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na nchi ya Uholanzi.

Dhamira ya mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa Tanzania ni  kupata walimu wazuri watakao saidia timu za jeshi zinazoshiriki ligi mbalimbali na Taifa.

Wakizungumza kwa wakati tofauti makocha ambao ni maafisa wa jeshi na aksari wameshukuru mkuu wa majeshi kwa kuliona hilo ambapo mbali na wakufunzi hao TFFwamekuwa wakitoa mafunzo mbalimbali lakini walimu hawa wakigeni wanavifaa  hivyo wanatoa ahadi ya kufanya vizuri katika kuhakikisha timu za majeshi na Taifa zinafanya vizuri.

Mafunzo  haya ni ya wiki mbili na ijumaa jioni yatafungwa rasmi hii inatokana na mahusiano mazuri ya Chama Cha Mpira wa Miguu cha Majeshi .

No comments:

Post a Comment