Saturday, September 2, 2023

WATANZANIA WAASWA KUENZI VILIVYOACHWA NA WAASISI WA TAIFA

Katibu wa Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ndugu Omary Abdull Punzi katika Mahafali ya 22 ya Shule ya msingi Kambarage wilaya Kibaha Mkoani Pwani amewambia wazazi,walimu wanafunzi na wageni waliohudhuria mahafali kulinda vitu vyao vikiwemo vilivyoachwa na waasisi wa Taifa letu.

Punzi amesema kuwa wananchi wanawajibu wa kulinda vya kwao na kufanya matendo yaliyo kuwa mema waliorithishwa na wazee pamoja na kuunga nuhudi za Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amesema kuwa wanapaswa kuwekeza katika idara ya Elimu na maeneo mingine sambamba na hilo aliwaeleza Falsafa mbili za kuwa mzalendo za TA TE TI TO TU na ile ya SA SE SI SO SU Falsafa hizi zinapendwa sana kuzungumzwa na Mheshimiwa Paul Petro Kimiti Mwenyekiti wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Taifa Mhe Kimiti alishika nafasi mbalimbali serikalini.

Katika Mahafali hiyo Mgeni Rasmi alikuwa Ndugu Festo Issingo Meneja wa benki ya NMB Mkoa wa Pwani alichangia madawati 100 baada ya kuambiwa kuna uhaba wa madawati.

Kwa Upande wa Mkuu wa shule ya Msingi KAMBARAGE alimshukuru Katibu wa Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani na Meneja wa benki ya NMB Mkoa wa Pwani. 

Kwa niaba ya wazazi na walimu walimpendekeza ndugu Omary Abdull Punzi Katibu wa Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuwa mlezi wa Shule ya Kambarage Nyerere kwa kuwasaidia mawazo ili kufanikisha malengo yao.

Friday, September 1, 2023

WADAU WAOMBWA KUCHANGIA UZIO KUNUSURU WANAFUNZI KUBAKWA

SHULE ya Msingi Mwendapole Wilayani Kibaha imeomba wadau kuisaidia upatikanaji wa fedha kiasi cha shilingi milioni 80 ili kujenga uzio kukabiliana na vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa wanafunzi ikiwemo kubakwa.

Aidha mtu mmoja alihukumiwa miaka 30 jela kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wa shule hiyo huku wengine wawili kesi zao zikiendelea mahakamani kutokana na tuhuma za kubaka wanafunzi wa shule hiyo.

Hayo yalisemwa na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Rajab Chalamila wakati wa mahafali ya darasa la saba ya shule hiyo ambapo wanahitaji kiasi hicho ili kufanikisha ujenzi wa ukuta wa shule.

Kwa upande wake Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) LTD Mantawela Hamis alitoa kiasi cha shilingi 100,000 ikiwa ni mchangao wa chama hicho.

Naye Mwenyekiti wa kamati ya shule Abdulrahman Likunda alisema kuwa wamekuwa wakiihamasisha jamii kuichangia shule hiyo ili kukabiliana na changamoto mbalimbali shuleni hapo.


Thursday, August 31, 2023

JAMII PWANI YATAKIWA KUWALINDA WATOTO ILI WAISHI KWENYE MAZINGIRA MAZURI

WADAU wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) Mkoani Pwani wameshauriwa jamii kuwalinda watoto ili kuepukana na vitendo vya ukatili.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa Anjita Child Development Foundation Janeth Malela wakati wa kikao cha maandalizi ya uzinduzi wa Programu hiyo kwa Mkoa wa Pwani.

Malela alisema kuwa programu hiyo itasaidia kuimarisha ukuaji na maendeleo ya mtoto kikamilifu kimwili, kiakili, kukuza lugha, mawasiliano kijamii na kihisia. 

"Programu inalenga kuimarisha utoaji huduma bora za Afya, Lishe, Malezi yenye Mwitikio, ujifunzaji wa Awali na Ulinzi na Usalama kwa watoto wa miaka 0 hadi 8 na kuimarisha ushirikiano wa wadau wa sekta mbalimbali katika huduma za MMMAM,"alisema Malela.

Aidha alisema kuwa lengo kuu ni kusaidia watoto kwenye masuala ya malezi,makuzi,ujifunzaji,ulinzi wa mtoto,afya ili wakue katika mazingira mazuri na kukua kutokana na sheria zilizopo.

Kwa upande wake ofisa maendeleo ya jamii mkoa wa Pwani Rachel Chuwa alisema kuwa moja ya changamoto wanazozipata watoto ni baadhi ya wazazi na walezi kutowahudumia watoto wao kwa wakati kutokana na kutafuta mahitaji ya nyumbani.

Chuwa alisema kuwa malezi na makuzi wazazi wanapaswa wawahudumie lakini kwa sasa wanalelewa na televisheni na mitandao na suala la lishe shuleni baadhi wanatoa chakuka lakini waengine hawatoi hivyo mpango huo utasaidia kuondoa changamoto zolizopo ili wapate huduma stahiki.

Naye mkurugenzi wa shirika la maendeleo kwa vijana (YPC) Israel Ilunde alisema kuwa mpango huo ni muhimu sana kwani vijana wanakumbana na changamoto za kimaadili kutokana na kutopata malezi bora kutokana na hali ya kimaisha.

Ilunde alisema kuwa mpango huo utasaidia sana katika kuwalea watoto na kuondoa vitendo viovu kutokana na malezi watakayoyapata hivyo rasilimali zitengwe ili kuwalea watoto katika misingi mizuri ya kimaadili.

Mikoa 10 ambayo imeshazindua programu hiyo ni Tabora, Arusha, Morogoro, Rukwa, Manyara, Mbeya, Dodoma, Dar es Salaam, Kagera na Lindi.

JAMII PWANI YATAKIWA KUWALINDA WATOTO ILI WAISHI KWENYE MAZINGIRA MAZURI





WADAU wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) Mkoani Pwani wameshauriwa jamii kuwalinda watoto ili kuepukana na vitendo vya ukatili.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa Anjita Child Development Foundation Janeth Malela wakati wa kikao cha maandalizi ya uzinduzi wa Programu hiyo kwa Mkoa wa Pwani.

Malela alisema kuwa programu hiyo itasaidia kuimarisha ukuaji na maendeleo ya mtoto kikamilifu kimwili, kiakili, kukuza lugha, mawasiliano kijamii na kihisia. 

"Programu inalenga kuimarisha utoaji huduma bora za Afya, Lishe, Malezi yenye Mwitikio, ujifunzaji wa Awali na Ulinzi na Usalama kwa watoto wa miaka 0 hadi 8 na kuimarisha ushirikiano wa wadau wa sekta mbalimbali katika huduma za MMMAM,"alisema Malela.

Aidha alisema kuwa lengo kuu ni kusaidia watoto kwenye masuala ya malezi,makuzi,ujifunzaji,ulinzi wa mtoto,afya ili wakue katika mazingira mazuri na kukua kutokana na sheria zilizopo.

Kwa upande wake ofisa maendeleo ya jamii mkoa wa Pwani Rachel Chuwa alisema kuwa moja ya changamoto wanazozipata watoto ni baadhi ya wazazi na walezi kutowahudumia watoto wao kwa wakati kutokana na kutafuta mahitaji ya nyumbani.

Chuwa alisema kuwa malezi na makuzi wazazi wanapaswa wawahudumie lakini kwa sasa wanalelewa na televisheni na mitandao na suala la lishe shuleni baadhi wanatoa chakuka lakini waengine hawatoi hivyo mpango huo utasaidia kuondoa changamoto zolizopo ili wapate huduma stahiki.

Naye mkurugenzi wa shirika la maendeleo kwa vijana (YPC) Israel Ilunde alisema kuwa mpango huo ni muhimu sana kwani vijana wanakumbana na changamoto za kimaadili kutokana na kutopata malezi bora kutokana na hali ya kimaisha.

Ilunde alisema kuwa mpango huo utasaidia sana katika kuwalea watoto na kuondoa vitendo viovu kutokana na malezi watakayoyapata hivyo rasilimali zitengwe ili kuwalea watoto katika misingi mizuri ya kimaadili.

Mikoa 10 ambayo imeshazindua programu hiyo ni Tabora, Arusha, Morogoro, Rukwa, Manyara, Mbeya, Dodoma, Dar es Salaam, Kagera na Lindi.

CORECU LTD YASAIDIA CHANGAMOTO SHULE YA MSINGI MWENDAPOLE

 




CHAMA Cha Ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) LTD kitagharamia gharama za huduma ya maji kwenye Shule ya Msingi Mwendapole ili kukabiliana na changamoto ya maji shuleni hapo.

Aidha chama hicho pia kitagharamia utengenezaji wa mashine ya kudurusu na kuchapishia na kompyuta mpakato ili kurahisisha kazi za uchapaji na kudurusu zifanyikie shuleni hapo badala ya kuzipeleka sehemu nyingine ambapo inaondoa usiri wa kazi za shule ikiwemo mitihani.

Hayo yamesemwa na Meneja wa CORECU LTD Mantawela Hamis wakati wa mahafali ya darasa la saba ya Shule ya Msingi Mwendapole yaliyofanyika leo shuleni hapo Wilayani Kibaha.

Pia amewataka wazazi kuwalea wanafunzi hao kwenye maadili mema mara wamalizapo elimu yao ya msingi ili wajiandae kuendelea na masomo ya elimu ya sekondari.

Awali mwalimu mkuu wa shule hiyo Rajabu Chalamila amesema kuwa mbali ya changamoto ya vifaa vya stationari na maji pia wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa uzio.

Chalamila amesema kutokana na shule hiyo kutokuwa na uzio wanafunzi wamekuwa wakitoroka na kufanyiwa vitendo vya kikatili.


DIWANI KUIPSTIA SHULE PHOTOCOPY MASHINE

DIWANI wa Kata ya Kibaha Goodluck Manyama amejitolea kuipatia Shule ya Msingi Jitegemee mashine ya kudurufu karatasi ili kuipunguzia mzigo shule hiyo gharama za uchapishaji mitihani.

Aidha katika kukabili changamoto ya maji kwenye shule hiyo Halmashauri itapeleka mradi wa kisima cha maji.

Akizungumza shuleni hapo wakati wa mahafali ya darasa la saba alisema kuwa atawanunulia mashine hiyo baada ya shule hiyo kutoa ombi hilo kwake.

Manyama alisema kuwa hiyo ni moja ya changamoto kubwa zinayoikabili shule hiyo hivyo ameona awapunguzie mzigo huo ili kupunguza gharama za kudurusu mitihani na kazi nyingine za shule.

"Nimeona nitoe msaada huu ili iwe chachu na kwa wadau wengine wajitokeze kusaidia changamoto za shule ili wanafunzi waweze kusoma katika mazingira mazuri,"alisema Manyama.

Alisema kuwa atashirikiana na wadau wengine pamoja na wanajamii kuhakikisha wanatatua changamoto za shule hiyo ili itoe elimu bora kwa wanafunzi.

"Tumepata wadau watatuchimbia kisima ili maji yawe ya uhakika na tayari mipango imekamilika na kisima kitachimbwa hivyo tuvute subira baada ya muda mfupi maji yatapatikana,"alisema Manyama.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo Stori Samatta alisema kuwa katika kuhakikisha wanakabili changamoto amekuwa akishirikisha wadau kuchangia elimu shuleni hapo.

Samatta alisema kuwa licha ya kuwa na changamoto kwani baadhi ya wanajamii kutokuwa na moyo wa kuchangia lakini anawapa elimu ya kuwa na moyo wa kuchangia ili iwe faida kwa watoto wao.

Naye mwanafunzi Eveline Samweli alisema kuwa wanakabiliwa na baadhi ya changamoto ikiwa ni pamoja na upungufu wa maji, matundu ya vyoo, kutokuwa na uzio na chumba cha kompyuta na kompyuta.

Samweli alisema kuwa changamoto nyingine ni shule kutokuwa na jengo la utawala ambapo jumla ya wahitimu kwa mwaka huu ni 126 ambapo shule hiyo ina wanafunzi 912 na ilianzishwa mwaka 2004 na ina walimu 24.

JAMII PWANI YATAKIWA KUWALINDA WATOTO ILI WAISHI KWENYE MAZINGIRA MAZURI




WADAU wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) Mkoani Pwani wameshauriwa jamii kuwalinda watoto ili kuepukana na vitendo vya ukatili.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa Anjita Child Development Foundation Janeth Malela wakati wa kikao cha maandalizi ya uzinduzi wa Programu hiyo kwa Mkoa wa Pwani.

Malela alisema kuwa programu hiyo itasaidia kuimarisha ukuaji na maendeleo ya mtoto kikamilifu kimwili, kiakili, kukuza lugha, mawasiliano kijamii na kihisia. 

"Programu hii ni kutoa huduma za Afya, Lishe, Malezi yenye Mwitikio, ujifunzaji wa Awali na Ulinzi na Usalama kwa watoto wa miaka 0 hadi 8 na kuimarisha ushirikiano wa wadau wa sekta mbalimbali katika huduma za MMMAM,"alisema Malela.

Aidha alisema kuwa lengo kuu ni kusaidia watoto kwenye masuala ya malezi,makuzi,ujifunzaji,ulinzi wa mtoto,afya ili wakue katika mazingira mazuri na kukua kutokana na sheria zilizopo.

Kwa upande wake ofisa maendeleo ya jamii mkoa wa Pwani Rachel Chuwa alisema kuwa moja ya changamoto wanazozipata watoto ni baadhi ya wazazi na walezi kutowahudumia watoto wao kwa wakati kutokana na kutafuta mahitaji ya nyumbani.

Chuwa alisema kuwa malezi na makuzi wazazi wanapaswa wawahudumie lakini kwa sasa wanalelewa na televisheni na mitandao na suala la lishe shuleni baadhi wanatoa chakuka lakini waengine hawatoi hivyo mpango huo utasaidia kuondoa changamoto zolizopo ili wapate huduma stahiki.

Naye mkurugenzi wa shirika la maendeleo kwa vijana (YPC) Israel Ilunde alisema kuwa mpango huo ni muhimu sana kwani vijana wanakumbana na changamoto za kimaadili kutokana na kutopata malezi bora kutokana na hali ya kimaisha.

Ilunde alisema kuwa mpango huo utasaidia sana katika kuwalea watoto na kuondoa vitendo viovu kutokana na malezi watakayoyapata hivyo rasilimali zitengwe ili kuwalea watoto katika misingi mizuri ya kimaadili.

Mikoa 10 ambayo imeshazindua programu hiyo ni Tabora, Arusha, Morogoro, Rukwa, Manyara, Mbeya, Dodoma, Dar es Salaam, Kagera na Lindi.