Monday, August 7, 2023

CWT KIBAHA WATAKA MABORESHO KIKOKOTOO

CHAMA Cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani kimeomba kanuni ya kikokotoo kuangaliwa upya au kirudishwe cha zamani ambacho kilikuwa ni asilimia 50 badala ya cha sasa ambacho ni asilimia 33.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa chama hicho Mwita Magige alipozungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake.

Magige amesema kuwa kanuni ya kugawa kikokotoo cha sasa iangaliwe upya ambapo mafao wanayoyapata baada ya kustaafu ni madogo tofauti na yale ya awali.

Amesema kuwa kanuni hiyo iangaliwe upya kwa kuboreshwa na ikiwezekana kirudishwe kikokotoo cha zamani ambacho ni kizuri kuliko cha sasa.

Aidha amesema kuwa kuboreshwa kikokotoo kutawafanya walimu wawe na morali ya kazi kwani watakuwa wanafuraha na malipo hayo mara baada ya kustaafu.


HALMASHAURI KUINUA VIPAJI VYA MICHEZO

HALMASHAURI ya Mji Kibaha imesema kuwa itaweka mazingira mazuri ya michezo ili kuinua vipaji vya vijana ili waweze kujiajiri kupitia michezo ambayo ni kama kiwanda.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Katibu Tawala wa Wilaya (DAS) Kibaha Moses Magogwa alipokuwa akikabidhi ubingwa kwa timu ya Umwelani iliposhindwa kwa kuifunga Wapolo kwa penati 3-1 kwenye michuano ya Micho Cup  kwenye uwanja wa Mwendapole ambapo ilijinyakulia kiasi cha shilingi milioni mbili.

Magogwa alisema kuwa michezo ni kiwanda cha ajira ambayo inaajiri vijana wengi ambapo inapaswa kuwekewa mazingira mazuri ili ajira hiyo iendelee kutoa ajira.

"Tutahakikisha halmashauri zote mbili ya Kibaha Mjini na Wilaya ya Kibaha zinaboresha masuala ya michezo kwani nimeona hamasa kubwa iliyopo kwenye michezo tumeona vijana walivyoshiriki michezo,"alisema Magogwa.

Aidha alise kuwa baada ya timu hiyo kushinda itafika ofisini kwa mkuu wa Wilaya kwa ajili ya kupongezwa kutokana na ushindi huo kwani Mkuu huyo wa Wilaya ndiye aliyepaswa kuwa mgeni rasmi lakini alipata dharura.

"Dc Nickson John anawapongeza kwa kutwaa ubingwa na amewakaribisha muende ofisini kwake akawapongeze kwani naye ni mdau wa michezo na anafurahi kuona vijana wakicheza michezo,"alisema Magogwa.

Aliongeza kuwa changamoto walizomweleza atazifanyia kazi kwani yeye ni mwenyekiti wa kamati ya michezo ya Wilaya atashirikiana na vyama vya michezo ili kuendeleza jitihada za michezo. 

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Wilaya ya Kibaha (KIBAFA) Robert Munis alisema kuwa mpango wa chama ni kuwa ni vituo nane vya kuendeleza soka la vijana.

Munis alisema wanapongeza waandaaji ya mashindano hayo kwani ni sehemu ya mpango wa chama kuwa na mashindano mara kwa mara ili kupata timu bora zitakazoshiriki kwenye ligi za Wilaya.

Kwa upande wa mratibu wa michuano hiyo ya Micho Cup Othamn Shija "Micho" alisema kuwa jumla ya timu 24 zilichuana kwenye awamu ya pili ya mashindano hayo.

Shija alisema kuwa changamoto kubwa ni kukosa wafadhili wa kudhamini mashindano hayo ambayo yana lengo la kuibua vipaji na kuwahamasisha vijana kushiriki michezo badala ya kujiingiza kwenye vitendo viovu pia kukuza soka la Kibaha.

UMWELANI WAKOMBA MILIONI 2 MICHO CUP

TIMU ya soka ya Umwelani imetwaa ubingwa wa Micho Cup baada ya kuifunga timu ya Wapolo kwa penati 3-1 baada ya kutoshana nguvu kwa kufungana 1-1 hadi dakika 90 zinamalizika.

Katika mchezo huo ambao ulipigwa kwenye uwanja wa Mwendapole hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimefungana magoli hayo.

Wapolo ndiyo waliokuwa wakwanza kuandika bao dakika ya 2 kupitia kwa Adolf Mpangule huku Umwelani wakisawazisha kupitia kwa Baraka Jafary dakika ya 26.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kukiwa na kosa kosa za hapa na pale lakini hadi dakika 90 hakuna mbabe aliyepatikana na kuingia hatua ya matuta.

Ambapo washindi walipata penati 3 huku Wapolo wakikosa penati zote na kupata 1 hivyo kutawazwa mabingwa na kujinyakulia kiasi cha shilingi milioni 2 taslimu.

Wapolo walijinyakulia seti mbili za jezi na mpira mmoja ambapo washindi walikabidhiwa zawadi na katibu tawala wa wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ambaye alimwakilisha mkuu wa wilaya ya Kibaha Nickson John.

Magogwa amesema kuwa serikali itashirikiana na wadau wa michezo ili kuendeleza michezo kwenye wilaya hiyo.

Naye mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Kibaha (KIBAFA) Robert Munis alisema kuwa mashindano hayo yamehamasisha mpira kwenye wilaya hiyo.

Kwa upande wake mratibu wa mashindano hayo Othaman Shija amesema kuwa changamoto kubwa ni kukosa wadhamini wa mashindano hayo na kuomba wadau kujitokeza kudhamini michuano hiyo inayofanyika kila mwaka ikiwa ni mwaka wake wa pili. 

Sunday, August 6, 2023

MAZINGIRA YA MICHEZO KUBORESHWA KUINUA SOKA KIBAHA

HALMASHAURI ya Mji Kibaha imesema kuwa itaweka mazingira mazuri ya michezo ili kuinua vipaji vya vijana ili waweze kujiajiri kupitia michezo ambayo ni kama kiwanda.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Katibu Tawala wa Wilaya (DAS) Kibaha Moses Magogwa alipokuwa akikabidhi ubingwa kwa timu ya Umwelani iliposhindwa kwa kuifunga Wapolo kwa penati 3-1 kwenye michuano ya Micho Cup  kwenye uwanja wa Mwendapole ambapo ilijinyakulia kiasi cha shilingi milioni mbili.

Magogwa alisema kuwa michezo ni kiwanda cha ajira ambayo inaajiri vijana wengi ambapo inapaswa kuwekewa mazingira mazuri ili ajira hiyo iendelee kutoa ajira.

"Tutahakikisha halmashauri zote mbili ya Kibaha Mjini na Wilaya ya Kibaha zinaboresha masuala ya michezo kwani nimeona hamasa kubwa iliyopo kwenye michezo tumeona vijana walivyoshiriki michezo,"alisema Magogwa.

Aidha alise kuwa baada ya timu hiyo kushinda itafika ofisini kwa mkuu wa Wilaya kwa ajili ya kupongezwa kutokana na ushindi huo kwani Mkuu huyo wa Wilaya ndiye aliyepaswa kuwa mgeni rasmi lakini alipata dharura.

"Dc Nickson John anawapongeza kwa kutwaa ubingwa na amewakaribisha muende ofisini kwake akawapongeze kwani naye ni mdau wa michezo na anafurahi kuona vijana wakicheza michezo,"alisema Magogwa.

Aliongeza kuwa changamoto walizomweleza atazifanyia kazi kwani yeye ni mwenyekiti wa kamati ya michezo ya Wilaya atashirikiana na vyama vya michezo ili kuendeleza jitihada za michezo. 

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Wilaya ya Kibaha (KIBAFA) Robert Munis alisema kuwa mpango wa chama ni kuwa ni vituo nane vya kuendeleza soka la vijana.

Munis alisema wanapongeza waandaaji ya mashindano hayo kwani ni sehemu ya mpango wa chama kuwa na mashindano mara kwa mara ili kupata timu bora zitakazoshiriki kwenye ligi za Wilaya.

Kwa upande wa mratibu wa michuano hiyo ya Micho Cup Othamn Shija "Micho" alisema kuwa jumla ya timu 24 zilichuana kwenye awamu ya pili ya mashindano hayo.

Shija alisema kuwa changamoto kubwa ni kukosa wafadhili wa kudhamini mashindano hayo ambayo yana lengo la kuibua vipaji na kuwahamasisha vijana kushiriki michezo badala ya kujiingiza kwenye vitendo viovu pia kukuza soka la Kibaha.

UMWELANI MABINGWA MICHO CUP

TIMU ya soka ya Umwelani imetwaa ubingwa wa Micho Cup baada ya kuifunga timu ya Wapolo kwa penati 3-1 baada ya kutoshana nguvu kwa kufungana 1-1 hadi dakika 90 zinamalizika.

Katika mchezo huo ambao ulipigwa kwenye uwanja wa Mwendapole hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimefungana magoli hayo.

Wapolo ndiyo waliokuwa wakwanza kuandika bao dakika ya 2 kupitia kwa Adolf Mpangule huku Umwelani wakisawazisha kupitia kwa Baraka Jafary dakika ya 26.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kukiwa na kosa kosa za hapa na pale lakini hadi dakika 90 hakuna mbabe aliyepatikana na kuingia hatua ya matuta.

Ambapo washindi walipata penati 3 huku Wapolo wakikosa penati zote na kupata 1 hivyo kutawazwa mabingwa na kujinyakulia kiasi cha shilingi milioni 2 taslimu.

Wapolo walijinyakulia seti mbili za jezi na mpira mmoja ambapo washindi walikabidhiwa zawadi na katibu tawala wa wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ambaye alimwakilisha mkuu wa wilaya ya Kibaha Nickson John.

Magogwa amesema kuwa serikali itashirikiana na wadau wa michezo ili kuendeleza michezo kwenye wilaya hiyo.

Naye mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Kibaha (KIBAFA) Robert Munis alisema kuwa mashindano hayo yamehamasisha mpira kwenye wilaya hiyo.

Kwa upande wake mratibu wa mashindano hayo Othaman Shija amesema kuwa changamoto kubwa ni kukosa wadhamini wa mashindano hayo na kuomba wadau kujitokeza kudhamini michuano hiyo inayofanyika kila mwaka ikiwa ni mwaka wake wa pili. 

UMWELANI WATWAA KOMBE MICHO CUP

TIMU ya soka ya Umwelani imetwaa ubingwa wa Micho Cup baada ya kuifunga timu ya Wapolo kwa penati 3-1 baada ya kutoshana nguvu kwa kufungana 1-1 hadi dakika 90 zinamalizika.

Katika mchezo huo ambao ulipigwa kwenye uwanja wa Mwendapole hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimefungana magoli hayo.

Wapolo ndiyo waliokuwa wakwanza kuandika bao dakika ya 2 kupitia kwa Adolf Mpangule huku Umwelani wakisawazisha kupitia kwa Baraka Jafary dakika ya 26.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kukiwa na kosa kosa za hapa na pale lakini hadi dakika 90 hakuna mbabe aliyepatikana na kuingia hatua ya matuta.

Ambapo washindi walipata penati 3 huku Wapolo wakikosa penati zote na kupata 1 hivyo kutawazwa mabingwa na kujinyakulia kiasi cha shilingi milioni 2 taslimu.

Wapolo walijinyakulia seti mbili za jezi na mpira mmoja ambapo washindi walikabidhiwa zawadi na katibu tawala wa wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ambaye alimwakilisha mkuu wa wilaya ya Kibaha Nickson John.

Magogwa amesema kuwa serikali itashirikiana na wadau wa michezo ili kuendeleza michezo kwenye wilaya hiyo.

Naye mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Kibaha (KIBAFA) Robert Munis alisema kuwa mashindano hayo yamehamasisha mpira kwenye wilaya hiyo.

Kwa upande wake mratibu wa mashindano hayo Othaman Shija amesema kuwa changamoto kubwa ni kukosa wadhamini wa mashindano hayo na kuomba wadau kujitokeza kudhamini michuano hiyo inayofanyika kila mwaka ikiwa ni mwaka wake wa pili. 

Saturday, August 5, 2023

WAKULIMA WATAKIWA KULIMA KILIMO CHA KIBIASHARA NA SIYO CHA KUJIKIMU

 

SEARIKALI imepanga kubadilisha kilimo kutoka kuwa cha kujikimu na kuwa kilimo cha biashara ambapo mabadiliko hayo yanafanyika kwa kuzingatia malengo ya kitaifa kama yalivyoainishwa kwenye dira ya taifa ya maendeleo 2025 na kuhakikisha kilimo ichangie ipasavyo Katika vita dhidi ya umasikini na kulenga kukuza sekta hiyo kufikia asilimia 10 ifikapo Mwaka 2030.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo  Mhe. Balozi Pindi Chana katika ufunguzi wa kongamano la zao la Mtama Jijini Dodoma kwenye maonesho ya nanenane.

Chana amesema kuwa mipango hiyo yote ya kitaifa imeweka mkazo kwenye mapinduzi ya viwanda na kubainisha sekta ya Kilimo kama mhimili imara utakaowezesha upatikanaji wa maligrafi za viwanda.

Amesema kuwa Mikoa ya kanda ya kati kama iliyo kwa Nchi na Dunia nzima inakabiliwa na mabadiliko ya tabia Nchi ambapo Mkoa wa Dodoma na Singida imeamua kwa dhati kuendeleza zao la Mtama ambalo limekuwa likistawi vizuri kwa hali ya hewa ya Mikoa hiyo.

Kanda ya kati imeamua kufanya uhamasishaji kupitia kongamano Hilo kuhusu matumizi ya teknolojia Bora Katika uzalishaji wa Zao la Mtama lengo likiwa ni kuunga mkono na kutekeleza kwa vitendo jitihada za Dkt. Mhe. Samia Suluhu Hassan Katika kuongeza Kasi ya ukuaji wa sekta ya Kilimo kutokana na kuhakikisha usalama wa chakula na kipato kwa wananchi.