NAIBU Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete amezitaka Serikali za Vijiji kuorodhesha majina ya wawekezaji ambao wamehodhi ardhi bila kuiendeleza ili irudishwe kwa ajili ya matumizi mengine.
Thursday, February 23, 2023
WASIOENDELEZA ARDHI KUNYANGANYWA
TANESCO KUONGEZA UZALISHAJI UMEME
Na Mwandishi Wetu Dodoma
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) linatarajia kuzalisha megawati 5,000 kupitia miradi mbalimbali ifikapo kwa mwaka 2025 hivyo kuongeza uzalishaji umeme kupitia gridi ya Taifa.
Hayo yamesemwa na kaimu Mkurugezi wa huduma kwa wateja wa shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) Martin Mwambene wakati akielezea utekelezaji wa shughuli mbalimbali ya shirika hilo na uelekeo wake kwa mwaka wa 2023 .
Mwambene amesema kuwa kwa sasa shirika hilo lina uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 1,820 wakati mitambo iliyopo ina uwezo wa kuzalisha megawati 1,300 pekee.
Amesema kuwa TANESCO kwa kutambua matatizo ya umeme yaliyopo nchini imekuja na mradi wa Gridi Imara ambapo katika bajeti ya mwaka huu imetengewa shilingi bilioni 500 kwa ajili ya kuanza utekelezaji wake.
"Katika mradi wa Grid Imara utajumuisha ununuzi wa mashine umba 6000, mita 700,000 za umeme, nguzo 380,000 ununuzi na ufungaji wa nyaya zenye urefu wa km 40,000, ujenzi wa njia za kusafirisha umeme mkubwa takribani kilomita 948 na ujenzi wa vituo 14 vya kupooza umeme,"amesema Mwambene.
Aidha amezungumzia pia maendeleo ya ujenzi katika Bwawa la Mwalimu NYerere kuwa upo katika asilimia 88 na zoezi la uwekaji maji limefikia mita za ujazo 133 kutoka usawa wa bahari
TCU KUTHIBITI UBORA
Thursday, February 16, 2023
WAKULIMA WATAKIWA KUTUMIA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI
Na Mwandishi Wetu Dodoma
Wednesday, February 15, 2023
KAMATI ZA MAGONJWA YA MLIPUKO KUTOA ELIMU KWA JAMII
IMEELEZWA kuwa uanzishwaji wa kamati za magonjwa ya milipuko kutasaidia kuielimisha jamii kukabili magonjwa ili yasisambae kwa kasi na kutoleta athari.
TBA YAENDELEA NA MIPANGO YA UJENZI KWA NYUMBA WATUMISHI
Na Mwandishi Wetu Dodoma
WANANCHI WATAKIWA KUKOPA KWA MALENGO
Na Mwandishi Wetu Dodoma