DKT. MUSHI AMEWASISITIZA WATANZANIA KUJENGA UTAMADUNI WA KULA NYAMA
Na Wellu Mtaki, Dodoma
MSAJILI wa bodi ya nyama nchini Dkt Daniel Mushi amewasisitiza Watanzania kujenga utamaduni wa kula nyama ili kukabiliana na utapiamlo.
Aidha utafiti unaonyesha Mtanzania mmoja hula kilo 15 za nyama badala ya kilo 50 kama inavyotakiwa
Ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa habari maelezo .
Dkt Mushi amesema kwamba utafiti uliofanywa na bodi hiyo umebaini baadhi ya nchi za Ulaya na nyinginezo mtu mmoja anakula kilo hadi 100 kwa mwaka.
Amepinga kauli ya watu kuwa nyama nyekundu ni hatari bali mlaji anatakiwa kuandaa nyama vizuri kuanzia katika kuipika hadi kwenye ulaji.
Katika hatua nyingine ameeleza kuwa kwa sasa wana mipango thabiti ya kutafuta masoko ya uhakika kwani mahitaji ya nyama nje ya nchi ni makubwa lakini Tanzania inasafirisha nyama kwa kiwango kidogo.