Saturday, October 29, 2022

WATANZANIA WATAKIWA KULA NYAMA


DKT. MUSHI AMEWASISITIZA WATANZANIA KUJENGA UTAMADUNI WA KULA NYAMA

Na Wellu Mtaki, Dodoma

MSAJILI wa bodi ya nyama nchini Dkt Daniel Mushi amewasisitiza Watanzania kujenga utamaduni wa kula nyama ili kukabiliana na utapiamlo.

Aidha utafiti unaonyesha Mtanzania mmoja hula kilo 15 za nyama badala ya kilo 50 kama inavyotakiwa

Ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa habari maelezo .

Dkt Mushi amesema kwamba utafiti uliofanywa na bodi hiyo umebaini baadhi ya nchi za Ulaya na nyinginezo mtu mmoja anakula kilo hadi 100 kwa mwaka.

Amepinga kauli ya watu kuwa nyama nyekundu ni hatari bali mlaji anatakiwa kuandaa nyama vizuri kuanzia katika kuipika hadi kwenye ulaji.

Katika hatua nyingine ameeleza kuwa kwa sasa wana mipango thabiti ya kutafuta masoko ya uhakika kwani mahitaji ya nyama nje ya nchi ni makubwa lakini Tanzania inasafirisha nyama kwa kiwango kidogo.



MADAKTARI BINGWA KUSOMESHWA


WIZARA YA AFYA YAANDAA MPANGO WA KUSOMESHA MADAKTARI BINGWA NA WABOBEZI.

Na Wellu Mtaki, Dodoma 

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imetoa ufadhili wa shilingi bilioni nane kwa kuwasomesha madaktari bingwa na wabobezi ili kukabiliana na uhaba wa wataalamu hao.

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma alipokuwa akitoa taarifa kwa umma kupitia vyombo vya habari.

Waziri Ummy amesema mpango huo unaojulikana kama Samia Scholaship utasomesha madaktari ngazi za ubingwa 139 watasoma nje ya nchi na wengine 318 watasomea hapa nchini.

Mwalimu amesema kuwa mpango huo utakuwa ni kwa seti akitolea mfano daktari bingwa wa magonjwa ya figo atakwenda kusoma pamoja na muuguzi na mtaalamu wa dawa ya usingizi ambapo jumla watakuwa watatu katika ugonjwa mmoja.

Amefafanua kuwa katika mpango huo tayari Rais Samia Suluhu Hassan ameikabidhi Wizara ya afya kiasi cha shilingi bilioni nane ambazo zitatumika kama ada na posho nyingine watakapokuwa mafunzoni.

Ameongeza kuwa Serikali imeamua kufanya hivyo baada ya kuona nchi inakabiliwa na upungufu mkubwa wa huduma za kibingwa na ubobezi.




Friday, October 28, 2022

WAVAMIZI WAMACHINGA KUCHUKULIWA HATUA










WAVAMIZI WA SOKO LA WAMACHINGA COMPLEX DODOMA WATACHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA 

Na Wellu Mtaki,Dodoma. 

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule amewakata wale wasio na sifa za machinga wasiingie kwenye soko la Wamachinga Complex kwani soko hilo limejengwa kwa ajili ya wamachinga.

 Sinyamule ameyasema hayo Mjini Dodoma wakati wa kusikiliza kero za wamachinga Dodoma kuhusu changamoto zinazowakabili. 

Sinyamule amesema kuwa baadhi wamefanya maombi kwa kudanganya taarifa ili wapate nafasi ndani ya soko hilo na wakibainika hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao. 

"Jiji endeleeni kutatua kero zitakazojitokeza ili wafanyabiashara wadodo wadogo waendelee kufanya biashara kwa amani na endapo kama kutajitokeza upungufu wa vizimba watapangiwa maeneo mengine,"amesema Sinyamule. 

Aidha ametangaza kuwa tatehe rasmi ya Wamachinga kuingia kwenye soko hilo ni tarehe Oktoba 28 na 30 mwaka huu na kuwataka viongozi wa Halmashauri ya Jiji kukaa eneo hilo siku zote kwa ajili ya kusimamia zoezi hilo na kuwataka LATRA kuhakikisha Daladala zinapitika njia ya soko hilo ifikapo Novemba Mosi na kunakuwa na kituo cha kupitia na kushushia abiria.

"Wamachinga fedha za mikopo zipo bali changamoto ya mikopo ni kuwa baadhi ya watu wanaunda vikundi vya watu watano ambapo ndani ya kundi hilo hakuna machinga hivyo ni vigumu kupata mkopo huo hivyo nawataka Wamachinga kuwa waaminifu kwenye zoezi la kukopa na waunde vikundi kwani fedha za mikopo zipo,"amesema Sinyamule.

Kwa upande wake Katibu tawala Mkoa wa Dodoma Dkt. Fatuma Mganga amesema Kuwa kuna mifuko zaidi ya 69 inatoa mikopo kwa wafanyabiashara wadogo wadogo na kuna taasisi za fedha hivyo mikopo ipo kila mmoja atapata mkopo huo kwa kufuata taratibu. 

Mwisho

Thursday, October 27, 2022

WAVAMIZI SOKO WAMACHINGA KUCHUKULIWA HATUA KISHERIA HATUA

WAVAMIVI WA SOKO LA WAMACHINGA COMPLEX DODOMA WATACHUKULIWA HATUA YA KISHERIA Na Wellu Mtaki, Dodoma Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule amewakata wale wote ambao awana sifa za machinga wasiingie kwenye soko ilo kwani soko limejengwa KWa ajiiri ya wanachinga tu KWa yoyote atakayebainika ameingia bila sifa za umachinga hatua za kisheria zitachukuliwa. Pia amewataka wamachinga kuamia kwenye soko ilo KWa amani ,Uaminifu na uhadilifu pasipo kuibiana Pamoja na kuzingatia usafi wa Mazingira. Hayo yamesemwa na mkuu wa Mkoa huyo wakati wa kusikiliza kero za wamachinga jijini dodoma kuhusu changamoto zinazowakabili wamachinga dodoma. Sinyamule amesema Kuwa wapo ambao wamefanya maombi KWa kudanganya taarifa ili wapate nafasi ndani ya soko ilo, endapo wakibainika hatua za kisheria zitachukuliwa. Aidha amewataka halmashauri ya jiji kutatua kero zote zinazojitokeza na ambazo zitajitokeza hapo baadae " Jiji endeleeni kutatua kero hizi na zitakazojitokeza Ili kuhakikisha wafanyabiashara wadodo wadogo wanafanya biashara KWa amani na endapo kama kutajitokeza upungufu wa vizimba watapangwa maeneo mengine"Amesema Sinyamule. Pamoja hayo Sinyamule ametangaza rasmi tarehe 28 hadi 30 octpbar mwaka huu ndiyo siku ya kuaza kuingia wamachinga kwenye soko ilo uku akiwataka viongozi wa Halmashauri ya jiji kukaa eneo ilo siku zote KWa ajiiri ya kusimamia zoezi ilo pamoja na kuwataka LATRA kuhakikisha kuwa kufikia tarehe 1 November daladala zinapitika njia ya soko hilo na kunakuwa na kituo cha kupitia na kushushia abiria. Pia Sinyamule amewahakikishia Wamachinga fedha za mikopo zipo bali changamoto ya mikopo ni kuwa baadhi ya watu wanaunda vikundi vya watu watano ambapo ndani ya kundi ilo hakuna machinga hivyo ni vigumu kupata mkopo huo hivyo amewataka Wamachinga kuwa wahaminifu mwenye zoezi la kukopa na waunde vikundi fedha za mikopo zipo. Kwa upande wake Katibu tawala Mkoa wa dodoma Dkt. Fatuma Mganga amesema Kuwa kuna mifuko zaidi ya 69 inatoa mikopo kwa wafanyabiashara wadogo wadogo pia kuna taasisi za fedha hivyo mikopo ipo kila mmoja atapata mkopo huo kwa kufata taratibu zilizopo. Mwisho

BMH YATOA MATIBABU YA MOYO KWA WATOTO

Na Wellu Mtaki, Dodoma BMH IMEAZA KUTOA MATIBABU YA MOYO KWA WATOTO. HOSPITALI ya Benjamin Mkapa (BMH), imeanza kufanya upasuaji wa moyo kwa watoto waliobainika kuzaliwa na matatizo ya moyo ambapo tayari watoto 10 wameshahudumiwa. Pia Serikali imeokoa zaidi ya Shilingi bilioni 2.3 kutokana na huduma za upandikizaji wa figo kwa wagonjwa 31 ambao wametibiwa kwa gharama ya Shilingi milioni 25 ambapo wangeenda kutibiwa nje ya nchi ingegharimu milioni 100 kwa mtu mmoja. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Oktoba 26, 2022,Mganga mkuu wa BMH Dk. Alphonce Chandika wakati akitoa taarifa ya utekelezaji na vipaumbele vya hospitali hiyo kwa mwaka 2022/ 2023 amesema wamefanikiwa kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa kuwa na maabara maalum inayotumika katika kutoa matibabu ya moyo pasipo kufungua kifua. Dk. Chandika ameeleza kuwa kuna wagonjwa nane ambao mapigo yao ya moyo yanashuka sana, walihudumiwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kupandikizwa betri kwenye moyo na kupitia maabara hiyo wameweza kuhudumia watoto 14 waliozaliwa na matatizo ya moyo. Amesema wagonjwa 39 waliobainika kuwa na matatizo makubwa ya moyo wamehudumiwa kwa kuwekewa vipandikizi na kati ya 39, wagonjwa wawili kati yao walihudumiwa kwa dharura ambapo kama ingekuwa ni kusafirishwa kwenda kupatiwa matibabu Dar es Salaam wangepoteza maisha. Ameongeza kuwa hospitali BMH ni ya pili hapa nchini kutoa huduma hiyo na kwamba tangu mwaka 2019, na kwamba jumla ya wananchi 715 wamehudumiwa kwa kuchunguzwa. Daktari huyo amebainisha kuwa tangu mwaka 2020, Hospitali ilifanikiwa kuanzisha upasuaji wa nyonga na magoti kwa kuweka vipandikizi na tayari wagonjwa 56 wamewekewa vipandikizi hivyo kwa wastani wa gharama ya shilingi milioni 12 ambapo gharama za huduma hizo nchi za nje ni takriban milioni 35. Aidha ameongeza kuwa huduma hiyo imeshatolewa kwa wagonjwa 148 kwa gharama ya Shilingi milioni 1.2 kwa mgonjwa mmoja, kwa nje ya nchi gharama ni zaidi ya milioni 7 huku akieleza kwamba wagonjwa hao 148, Serikali imeokoa zaidi ya Shilingi milioni 850. Ikumbukwe kuwa jitihada za Serikali kuhakikisha inawaletea wananchi huduma za afya zilizo bora, ilidhamiria kuiwezesha Hospitali ya Benjamini Mkapa kuwa na vifaa tiba vya kisasa na vinavyotumia teknolojia ya kisasa ili iweze kukidhi adhma yake ya kuwahudumia wananchi hao kwa kuwapatia matibabu ya kiwango cha juu. Mwisho

HAZINA YAKUSANYA BILIONI 852.9

SERIKALI kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina katika mwaka wa fedha 2021/22 imekusanya 852.9 sawa na asilimia 109.5 ya lengo kutoka katika kampuni ambazo serikali inamiliki hisa. Imesema ongezeko hilo linatokana na uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan ambapo ni zaidi ya kiasi kilichokusanywa Juni 30 mwaka jana ambacho ni sh. bilioni 638.87. Hayo yalibainishwa jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Umma, Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH), Lightness Mauki, wakati akizungumza na wandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa majukumu na mwelekeo wa ofisi hiyo katika mwaka huu wa fedha. Alisema fedha hizo zimekusanywa katika mapato yasiyo na kodi ambayo yanajumuisha gawio, michango ya asilimia 15 ya mapato ghafi na mapato mengineyo kutoka katika taasisi 287 zilizo chini ya ofisi ya msajiri. “Kuongezeka kwa makusanyo hayo kunatokana na kuimarisha usimamizi,ufuatiliaji na tathmini ya uwekezaji wa mitaji ya umma pamoja na hatua ambazo zilichukuliwa katika kukuza mapato na kudhibiti matumzi. Aliongeza kuwa:"Hadi kufikia Juni 30 mwaka huu Ofisi ya Msajili wa hazina ilikuwa inasimamia mashirika ya umma 287 Kati ya mashirika hayo 237 serikali ina hisa zaidi ya asilimia 51, taasisi 40 serikali inahisa chache na 10 za nje ya Nchi ambazo serikali imeweka uwekezaji. Lightness alisema serikali imewekeza kwenye mashirika hayo fedha sh.trilioni 70. Alisema kuwa serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina imeendelea na juhudi za kusimamia utendaji wa kampuni ambazo serikali inaumiliki wa hisa chache. Pia, alisema serikali inafanya majadiliano na wabia wenza na kusimamia kwa ukaribu matumizi yasiyo ya lazima, hivyo kuchangia ongezeko la gawio. "Mathalani mafanikio ya jitihada hizo yamejidhihirisha katika utendaji wa Banki ya NBC ambayo imeongeza faida kabla ya kodi kutoka sh. bilioni 7 mwaka 2020 hadi sh. bilioni 60 mwaka jana, ikiwa ni ongezeko la asilimia 757, ukuaji huu wa faida umewezesha benki kutoa gawio kwa serikali sh. bilioni 4.5 kiasi ambacho hakijawahi kufikiwa,"alieleza. Akitaja mafaniko ya Ofisi hiyo Lightness alisema wameweza kufanya upanuzi wa kiwanda cha sukari cha Kilombero ambacho serikali inamiliki asilimia 25 ya hisa. Alisema kutokana na kukua kwa mahitaji ya sukari nchini kulikuwa na uhitajio wa kupanua kiwanda cha sukari hicho ili kutimiza mahitaji. “Bodi ya wakurugenzi baada ya kufanya upembuzi yakinifu iliwasilisha mapendekezo ya kupanua kiwanda hicho ambapo sh. bilioni 571.6 zilitumika, uwekezaji huo unatarajia kuongeza kiwango cha uzalishaji sukari hadi kufikia tani 271,000 kutoka tani 127,000 za sasa,” alisema. .

Friday, May 20, 2022

KEDA YATOA MSAADA WA MARUMARU ZA MAMILIONI KWENYE SHULE ZA SEKONDARI

KIWANDA cha kutengeneza Marumaru cha Keda (T) Ceramics Co. Ltd kilichopo Pingo Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kimetoa Marumaru zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20 kwa shule za Pera na Msata. Akizungumza mara baada ya kuzikabidhi shule hizo Ofisa Tawala wa kiwanda hicho George Lulandala alisema kuwa maramaru hizo ni kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri ya usomaji kwa wanafunzi. Lulandala alisema kuwa wametoa vifaa hivyo ikiwa ni sehemu ya kurudisha mchango wao kwa jamii ambapo wamekuwa wakishiriki shughuli za wananchi ili kuwaletea maendeleo. "Tumeamua kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan kwani ameonyesha kuwajali wananchi wakiwemo wanafunzi ambapo amefanya mambo mengi kwenye sekta ya elimu ikiwemo ujenzi wa madarasa na miundombinu,"alisema Lulandala. Alisema kuwa wameamua kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan za kuboresha mazingira ya elimu ili wanafunzi wasome katika mazingira mazuri ambayo yatawafanya wapate uelewa vizuri. "Sekondari ya Msata imepatiwa maboksi 203 huku Pera Sekondari wakipata maboksi 100 na bado tutaendelea kutoa misaada mbalimbali ili kuhakikisha kuboresha sekta mbalimbali,"alisema Lulandala. Aidha alisema kuwa kwa kipindi cha nyuma walisaidia kituo cha afya cha Pera na huduma mbalimbali kwa wananchi kwenye maeneo mbalimbali kwenye wilaya na mkoa. "Tunafanya jitihada mbalimbali kusaidia masuala ya jamii hivyo hata wadau wengine nao wanapaswa kuisaidia serikali ili iweze kuwahudumia wananchi wake,"alisema Lulandala. Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Iddi Ng'oka alisema kuwa wanashukuru kiwanda hicho kwa msaada walioutoa kwani bila ya kuweka Marumaru sakafu imekuwa ikiharibika mara kwa mara. Ng'oka alisema kuwa wanaomba wapewe tena maramaru kwani kuna baadhi ya madarasa hayana Marumaru pamoja na ofisi hivyo wakipatiwa nyingine itasaidia sana. Mwisho.