Friday, October 28, 2022

WAVAMIZI WAMACHINGA KUCHUKULIWA HATUA










WAVAMIZI WA SOKO LA WAMACHINGA COMPLEX DODOMA WATACHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA 

Na Wellu Mtaki,Dodoma. 

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule amewakata wale wasio na sifa za machinga wasiingie kwenye soko la Wamachinga Complex kwani soko hilo limejengwa kwa ajili ya wamachinga.

 Sinyamule ameyasema hayo Mjini Dodoma wakati wa kusikiliza kero za wamachinga Dodoma kuhusu changamoto zinazowakabili. 

Sinyamule amesema kuwa baadhi wamefanya maombi kwa kudanganya taarifa ili wapate nafasi ndani ya soko hilo na wakibainika hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao. 

"Jiji endeleeni kutatua kero zitakazojitokeza ili wafanyabiashara wadodo wadogo waendelee kufanya biashara kwa amani na endapo kama kutajitokeza upungufu wa vizimba watapangiwa maeneo mengine,"amesema Sinyamule. 

Aidha ametangaza kuwa tatehe rasmi ya Wamachinga kuingia kwenye soko hilo ni tarehe Oktoba 28 na 30 mwaka huu na kuwataka viongozi wa Halmashauri ya Jiji kukaa eneo hilo siku zote kwa ajili ya kusimamia zoezi hilo na kuwataka LATRA kuhakikisha Daladala zinapitika njia ya soko hilo ifikapo Novemba Mosi na kunakuwa na kituo cha kupitia na kushushia abiria.

"Wamachinga fedha za mikopo zipo bali changamoto ya mikopo ni kuwa baadhi ya watu wanaunda vikundi vya watu watano ambapo ndani ya kundi hilo hakuna machinga hivyo ni vigumu kupata mkopo huo hivyo nawataka Wamachinga kuwa waaminifu kwenye zoezi la kukopa na waunde vikundi kwani fedha za mikopo zipo,"amesema Sinyamule.

Kwa upande wake Katibu tawala Mkoa wa Dodoma Dkt. Fatuma Mganga amesema Kuwa kuna mifuko zaidi ya 69 inatoa mikopo kwa wafanyabiashara wadogo wadogo na kuna taasisi za fedha hivyo mikopo ipo kila mmoja atapata mkopo huo kwa kufuata taratibu. 

Mwisho

No comments:

Post a Comment