Sunday, October 30, 2022

RAIS SAMIA KUZINDUA MATOKEO YA SENSA


RAIS SAMIA KUTANGAZA MATOKEO YA SENSA KESHO.

Na Wellu Mtaki, Dodoma.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa kutangaza matokeo ya Sensa ya watu na Makazi Oktoba 31 kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hamza Juma ameyasema hayo Jijini Dodoma alipokuwa akitoa taarifa kwenye kikao maalumu cha wajumbe wa kamati ya maandalizi ya uzinduzi wa tukio hilo.

Juma amesema kuwa maandalizi ya uzinduzi wa tukio la kutangazwa kwa matokeo ya sensa ya watu na anwani za makazi yamekamilika.

Ameeleza kuwa kazi kubwa ya kuratibu na kusimamia imefanywa na viongozi wa mkoa wa Dodoma na kilichobaki watakuwa wamekamilisha Oktoba 30.

Aidha amesema kuwa zoezi la sensa ya watu na makazi la mwaka huu limefanyika kisasa zaidi tofauti na miaka ya nyuma na litaisaidia Serikali katika kupanga mipango yake ya kiuchumi,kijamii na maendeleo. Zoezi la sensa ya watu na makazi lilifanyika hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment