Saturday, October 29, 2022

MATRILIONI YATENGWA MIRADI YA BARABARA NCHINI


TANROADS YATENGA TRILIONI 3.8 UTEKELEZAJI MIRADI YA BARABARA 

Na Wellu Mtaki, Dodoma

WAKALA wa Barabara Nchini (TANROADS) imetenga kiasi cha shilling trilioni 3.8 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya ujenzi wa barabara na madaraja makubwa nchi nzima.

Hayo yamesemwa leo na mtendaji mkuu wa Tanrods injinia Rogatus Mativila alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu shughuli mbalimbali zinazoendelea kufanywa na wakala.

Mativila amesema kuwa tayari wakala wa barabara imefanya usanifu wa miradi hiyo ambayo baadhi ni madaraja makubwa sita ikiwa ni pamoja na daraja la bwawa la Mtera Mkoani Dodoma , daraja la Jangwani Mkoani Dar - es- Salam, daraja la mkoa wa Simiyu, daraja la Mzinga, daraja la Mtoroni na makaravati sehemu mbalimbali nchini.

Amesema kuwa mradi mwingine mkubwa utakaotekelezwa ni ule wa ujenzi wa uwanja wa ndege wa Msalato ambapo Rais Samia Suluhu Hassan ataweka jiwe la msingi Oktoba 30 mwaka huu.

Ametoa wito kwa Watanzania hasa madereva wa magari kuitunza miradi hiyo kwa kuwa Serikali inatumia fedha nyingi kugharamia miradi hiyo.

No comments:

Post a Comment