VIONGOZI WATAKIWA KUHESHIMU VIAPO VYAO.
Tuesday, January 31, 2023
HESHIMUNI VIAPO VYENU
Sunday, January 29, 2023
SHULE BORA KUINUA KIWANGO CHA UBORA WA ELIMU AWALI NA MSINGI
Na Wellu Mtaki, Dodoma
WANAOFANYA VITENDO VYA UKATILI WATAKIWA KUACHA MARA MOJA
Na Elizaberth Paulo,Dodoma
MKUU wa mkoa wa Dodoma Mheshimiwa Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wanaume pamoja na wale wote wanaotenda vitendo vya kikatili kuacha mara moja kwani kundi kubwa linaloathirika na vitendo hivyo ni watoto na wanawake.
Aidha amesema mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa mikoa ambayo kuna vitendo vya ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto.
Senyamule ametoa wito huo katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma (General Hospital) alipokua akizindua kituo jumuishi cha utoaji wa huduma kwa manusura wa vitendo vya Ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto.
"Mradi huu wa USAID AFYA YANGU umekuja wakati muafaka hapa Jijini na tunashukuru kwa sababu mkoa huu pia una changamoto ya vitendo vya kikatili,"amesema Senyamule.
Amesema kuwa manusura wa vitendo vya kikatili wamekuwa wakipata changamoto katika kupata huduma kwa haraka na kwa taratibu kutokana na mtawanyiko wa maeneo ya huduma muhimu wanayohitaji ikiwemo huduma za afya, ustawi wa jamii na huduma za kisheria.
"Jengo hili la kutoa huduma jumuishi kwa manusura wa vitendo vya ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto ni moja ya malengo ya mpango jumuishi wa utoaji huduma kwa walengwa iliyozinduliwa mwaka 2013 kwa lengo la kuhakikisha huduma inatolewa kwa manusura wa ukatili kwa haraka, uratibu mzuri, na kurahisisha mfumo wa rufaa kwa manusura kwa kupata huduma maalum kama msaada wa Kisheria,"amesema Senyamule.
Ameongeza kuwa hali hiyo imesababisha baadhi ya manusura kukosa huduma kwa wakati na kupata madhara yakiwemo maambukizi ya virusi vya Ukimwi, Ulemavu wa kudumu, mimba zisizotarajiwa na mimba za utotoni kutokana na vitendo vya ukatili alivyofanyiwa.
"Baadhi ya manusura kurubuniwa na kupoteza ushahidi ambao ungesaidia manusura kupata haki yake pindi shauri linapofikishwa katika vyombo vya Sheria, kutumia gharama kubwa katika kufikia maeneo ya kupatia huduma hivyo kusababisha matukio mengi ya ukatili kutokutolewa taarifa katika vyombo vya Sheria hali Iliyosababisha manusura kukosa huduma mbalimbali pamoja na haki za kisheria,"amesema Senyamule
Ameagiza wahudumu wa jengo ambalo wanatoa huduma kwa manusura kufanya kazi saa 24 kwani vitendo vya kikatili vinatokea muda wowote hivyo kuanzisha utaratibu wa kuwa katika hospitali hiyo muda wote na kuwaasa kutumia vifaa kwa umakini mkubwa na kwa weledi kwa manufaa ya kuchakata takwimu za manusura wanaopatiwa huduma katika jengo hilo lililozinduliwa ndani ya hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma.
Kwa upande wake Chip Lyons Rais wa shirika la EGPAF ambao ni wadau waliofadhili ukarabati wa jengo hilo la utoaji wa huduma kwa manusura wa vitendo vya ukatili amesema mradi huo unatakribani miaka 13 tangu kuanzishwa kwake kutokana na ushirikiano mzuri na Viongozi wa Tanzania hata uongozi wa mkoa wa Dodoma.
Naye Anna Hoffman Naibu Mkurugenzi wa Shirika la afya la USAID amesema mradi huo Unatekelezwa katika mikoa Sita nchini ikiwemo mkoa wa Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tabora na Dodoma huku Ukilenga kufikia maeneo mengi hapa Tanzania.
Thursday, January 26, 2023
MNEC WAZAZI TAIFA ATAKA CCM WATANGAZE MAFANIKIO YA RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN
MJUMBE wa Halmashauri Kuu Chama Cha Mapinduzi Taifa (MNEC) Wazazi Hamoud Jumaa amewataka viongozi wa CCM kutumia mikutano ya hadhara iliyoruhusiwa na Rais Dk Samia Suluhu Hassan kueleza miradi ya maendeleo inayofanywa na kutekelezwa na Serikali ya awamu ya sita.
Akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Kibaha Vijijini pamoja na baadhi ya viongozi na wanaCCM kusiwe na kigugumizi kukisemea Chama na kusimamia miradi mbalimbali inayotekelezwa.
Jumaa alisema kuwa Rais ametoa fursa nzuri kuruhusu mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa hivyo ni wakati sasa kwa viongozi na wanaccm kuelezea yale yaliyofanywa katika kuleta maendeleo ya wananchi.
"Viongozi wenzangu, madiwani,wabunge na wanaCCM tutoke kusemea Chama na kupanda majukwaani kuitendea haki ilani ambayo utekelezaji wake unafanya vizuri,"alisema Jumaa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kibaha Vijijini Mkali Kanusu alisema kuwa watahakikisha wanasimamia utekelezaji wa miradi na watashirikiana na watendaji wa serikali ili kufanikisha miradi ya maendeleo kwa wananchi.
Naye Katibu wa CCM Safina Nchimbi alisema kuwa anamshukuru MNEC Taifa kuahidi kujenga ofisi ili ziendane na umri wa Chama na kinaendelea na mipango yake mbalimbali ya kimaendeleo na kuhakikisha chama kinakubalika kwa wananchi.
Tuesday, January 17, 2023
UJENZI TAASISI ZA SERIKALI UZINGATIE BAJETI
Na Wellu Mtaki Dodoma
SERIKALI kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) imetoka wito kwa taasisi zote zinazoendelea na ujenzi Dodoma zihakikishe ujenzi huo unakamilika kwa kizingatia taratibu zote za ujenzi ikiwemo ubora, muda , bajeti iliyotengwa na thamani ya fedha Ili kuleta tija.
Wito huo umetolewa Jijini Dodoma na Mhe. George Simbachawene Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera , Bunge na Uratibu wakati wa hafla ya kukabidhi vibali vya ujenzi wa ofisi za taasisi Dodoma huku akiagiza taasisi nyingine ambazo bado hazijaaza maandalizi ya ujenzi Dodoma ziwasilishwe Ofisi ya Waziri Mkuu mahitaji ya viwanja vya ujenzi wa ofisi za taasisi Dodoma kwa ajili ya uratibu wa pamoja.
Simbachawene amesema kuwa serikali ya awamu ya sita imeendelea kutekeleza kikamilifu Mpango wa kuhamia Dodoma ambapo wananchi wanapata huduma zote katika makao makuu ya nchi na kwamba watumishi wote wa serikali ikiwemo wizara zote, vyombo vya ulizi na usalama, muhimili wa bunge na baadhi ya taasisi zimeamia Dodoma na wanaendelea kutekeleza majukumu yao.
Aidha amesema kuwa ifikapo march 2023 muhimili wa mahakama unatarajiwa kuhamia Jijini Dodoma kwani ujenzi wa jengo hilo umefika zaidi ya asilimia 90.
Pia ametoa rai kwa viongozi wa mkoa wa Dodoma, Wizara, Halmashauri, taasisi za serikali, sekta binafsi, wananchi na wadau wengine kuendelea kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa Mpango wa serikali wa kuahamia Dodoma pamoja na ujenzi wa makao makuu Ili kufikia malengo ya kuwa na Jiji Bora la kuvutia litakalokidhi mahitaji ya kijamii na kiuchumi kwa miaka mingi ijayo.
Lengo la hafla hiyo ni kukabidhi vibali vya ujenzi kwa taasisi zilizopewa idhini ya ujenzi wa ofisi Jijini Dodoma kama sehemu ya kutambua mchango wa taasisi hizo katika kuunga mkono utekelezaji wa Mpango wa serikali kuhamisha shughuli zake Jijini Dodoma.
CHONGOLO ATAKA VIJANA KUSHIRIKI KUJIKWAMUA KIUCHUMI
CHONGOLO ATAKA VIJANA WAJENGEWE FIKRA ZA KIUCHUMI
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo amewataka viongozi wa vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika kuleta msukumo wa kuwajengea uwezo vijana kifikra na kiuchumi.
Chongolo meyasema hayo kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopo Kibaha Mkoani Pwani wakati akifungua kikao kazi cha makatibu wakuu wa vyama rafiki wanaounda kamati ya usimamizi wa shule hiyo.
Chongolo amesema kuwa Ukombozi wa nyuma ulikuwa ni wa kujikomboa kutoka kwa wakoloni lakini kujikomboa kwa sasa ni kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kifikra.
"Makatibu Wakuu kutoka nchi sita marafiki wanapaswa kudumisha uzalendo ulioasisiwa na viongozi waliotangulia ambao waliweka misingi ya ushirikiano,"alisema Chongolo.
Aidha amesema kuwa Rais Dk Samia Suluhu Hassan anawakaribisha nchini huku akiwawakikishia usalama wao kwa muda wote watakaokuwa hapa nchini hadi watakaporudi makwao.
"Mwaka jana tulipokutana tulijadili mambo mengi kwa kikao kilichofanyika kwa njia ya mtandao sasa leo tumekutana ili tuweze kuchakata kwa kina yale yote tuliyojadili,"amesema Chongolo.
Naye Katibu Itikadi na Uenezi CCM Sophia Mjema amesema kuwa kila kitakachokifanyiwa maamuzi kitajengwa katika sura ya umoja kama ulivyojengwa katika historia ya nchi hizo rafiki.
Vyama hivyo vilivyoshiriki ni CCM Tanzania, ZANU PF Zimbabwe, FRELIMO Msumbiji, MPLA Angola, SWAPO Namibia na ANC Afrika Kusini.
Sunday, January 8, 2023
WATANO WAFA AJALINI
WATANO WAFA 10 WAJERUHIWA AJALINI
Thursday, January 5, 2023
WANAFUNZI WASIYO RIPOTI SHULENI KUTAFUTWA
WANAFUNZI WATORO JIJINI DODOMA KUTAFUTWA WARUDI MASHULENI.
Na Wellu Mtaki, Dodoma
MKUU wa mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule amewataka viongozi wa kata, walimu, wazazi na walezi kushirikiana kuwatafuta wanafunzi ambao hawataripoti shuleni baada ya siku 90 mara shule za sekondari zitakapofunguliwa watatafutwa na kurudishwa shuleni.
Ameyasema leo katika kikao kazi kilichojumuisha maofisa elimu wa Wilaya za wa Mkoa pamoja na walimu wa wilaya zote Jijini Dodoma.
Sinyamule amesema kuwa zipo changamoto nyingi ambazo zinapelekea watoto kutokufika shuleni kama watoto kupelekwa kwenda kufanya kazi za ndani pamoja na changamoto za kimaisha zilizopelekea mtoto kutokufika shule.
Amesema kuwa mpaka Sasa wanafunzi 4,000 tayari wamepatikana na hivyo wataaza masomo yao muhulah uu wa mwaka 2023 huku akisisitiza kuwa Halmashauri zote Dodoma kuhakikisha wanafunzi wanasajiliwa kwa asilimia 100.
Amewataka walimu kuwapokea wanafunzi hata wale ambao hawana sare za shule ila watoe taarifa kwa watendaji wa kata au Kijiji kwa lengo la kuwahimiza wazazi au walezi kutimiza majukumu yao huku watoto wakiendelea na masomo.
Kwa upande wake Mkurugezi wa elimu ofisi ya Rais (TAMISEMI) amesema kuwa watahakikisha kupitia mkutano huo wa kupeana maelekezo na utekelezaji wataenda kuimarika katika nafasi zao pamoja na kuhakikisha wanafanya vizuri katika sekta ya Elimu.
DKT BITEKO ASISITIZA UONGEZAJI THAMANI MADINI
Dkt. Biteko asisitiza wadau kuwekeza uongezaji thamani madini
WAZIRI wa Madini, Dkt. Doto Biteko amesema kuwa, Serikali iko mbioni kuanzisha upya Minada ya Madini ya Vito ili kuleta wanunuzi wakubwa, wafanyabiashara na wachimbaji wa madini hapa nchini.
Hayo yamebainishwa Januari 5, 2023 wakati akizindua duka la utalii wa madini la kampuni ya Tanzanite Experience katika eneo la Manyara Kibaoni wilaya ya Karatu Mkoani Arusha
Amesema kupitia mnada huo kampuni ya Tanzanite Experience kupitia duka la utalii wa madini itapata madini mengi kwa ajili ya kuendeleza kituo hicho na maeneo mengine anayoyafanyia kazi.
Dkt. Biteko amesema kuwa, kupitia kituo hicho kilichopo katika ukanda wenye maeneo ya hifadhi imekuwa ni sehemu kubwa ya kivutio cha utalii kwa wageni kutoka ndani na nje ya nchi.
"Madini ya Tanzanite yamekuwa yakinunuliwa hapa nchini kwa kiasi kikubwa na watalii wanaokuja kutembelea hifadhi zetu na kupitia wao madini haya yanaendelea kutangazwa duniani," amesema Dkt. Biteko.
Ameongeza kuwa, Wizara ya Madini inapongeza uwekezaji huo ambao umefanywa kwa asilimia 100 na watanzania wakiunga juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan wakati akitangaza vivutio mbalimbali vilivyopo hapa nchini kupitia filamu ya "The Royal Tour" ambapo utalii na madini ya Tanzanite ilikuwa miongoni wa vivutio hivyo.
Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesema wizara inahamasisha uwekezaji wa namna hiyo ambao unaunga mkono moja kwa moja jitihada zinazofanywa na Serikali za kutangaza madini ya Tanzanite duniani hususan katika eneo la shughuli za uongezaji thamani.
"Duka hili linatarajia kuuza bidhaa mbalimbali za madini ya Tanzanite na Tsavourite ambazo kwa miaka mingi zimekuwa zikitengenezwa na kuuzwa nje ya nchi. Hii ni hatua kubwa ambayo nchi yetu inaendelea kuchukua katika kuhakikisha madini haya yanazalishwa hapa nchini," ameongeza Dkt. Biteko.
Dkt. Biteko ametoa wito kwa watu wote ambao wana nia ya kuwekeza kwenye uchongaji, ukataji wa madini kuwekeza kwenye uongezaji thamani wa madini ili madini hayo yaweze kutupatia ajira na kodi kubwa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanzanite Experience Hassinne Sajani amesema kuwa, duka hilo limekuwa kivutio kikubwa kwa watanzania na watalii kutoka nje ya nchi ambao wananunua bidhaa za madini zilizopo. Aidha ameongeza kuwa, kampuni imeajiri wafanyakazi 80 na zaidi ya asilimia 80 ni wakazi wa maeneo ya Manyara Kibaoni.
Ameahidi kuongeza juhudi kuendelea kutangaza madini ya Tanzania ambayo ni zawadi kwa Watanzania ili madini hayo yaweze kupanda thamani duniani.
Kwa upande wake, Meneja wa Tanzanite Experience, Junaid Khan amesema kuwa, zaidi ya wageni 6000 wamefika kutembelea Kampuni ya Tanzanite Experience
Naye, Mkuu wa Wilaya ya Karatu Dadi Kolimba amesema biashara ya madini imefunguka katika wilaya ya Karatu na kuongeza mapato na kueleza kuwa ameipongeza kampuni hiyo kwa kutoa ajira zaidi ya 80 kwa watanzania katika nafasi mbalimbali.
Tuesday, January 3, 2023
DODOMA WAASWA UPANDAJI MITI
Na Wellu Mtaki, Dodoma
MKUU wa mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule amewataka wazazi na walezi wahakikishe wanawapeleka watoto wao shuleni mara baada ya shule kufunguliwa.
Sinyamule ameyasema leo katika ziara ya Kampeni ya upandaji wa miti iliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Chemba Jijini Dodoma.
Amesema kuwa zipo Sheria ambazo italazimika kuzifuata kuhakikisha kuwa mtoto anapata haki yake ya kwenda shule hivyo inapaswa wazazi na walezi watambue lengo na makusudi ya serikali ya awamu ya sita kwa watoto wa kidato cha kwanza.
Aidha amesema huku kuna umuhimu wa upandaji wa miti ili kurudisha uoto wa asili na kupambana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo kuna maelekezo ambayo yametolewa na serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha tunatunza mazingira.
Amebainisha kuwa hilo ni jukumu la kila mwanafunzi kuwa na mti wake shuleni ambao atautuza kwa kipindi chote awapo shuleni na wazazi watambue kama elimu ya vitendo.
Amezitaka shule kuanzisha miradi ambayo itawezesha shule kujikimu na chakula kwani imeonyesha moja ya njia ambazo zitapunguza utoro mashuleni ni pamoja na watoto kupata chakula.
Mwisho.