Tuesday, January 31, 2023

HESHIMUNI VIAPO VYENU

VIONGOZI WATAKIWA KUHESHIMU VIAPO VYAO.



Na Elizabeth Paulo,Dodoma

WAKUU wa wilaya wapya walioteuliwa wametakiwa kuheshimu na kuviishi viapo vyao walivyoviapa kwa uadilifu na uaminifu mkubwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. 

Katibu  Msaidizi  wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kanda ya kati Dodoma Bibi Jasmini Awadhi alitoa kauli hiyo alipokuwa akimwapisha Mkuu wa wilaya ya Chemba Gelard Mongela  katika hafla fupi iliyofanyika  katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Dodoma.

Awadhi aliisema kuwa wakuu hao wa Wilaya wahakikishe wanajitoa kutumikia viapo walivyoapa mbele na kuviweka katika kumbukumbu zao za kila siku ili viwasidie kuyakumbuka yale yote yaliyoelezwa katika viapo hivyo wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku.

Katika hatua nyingine  alimpongeza Mkuu wa wilaya ya Chemba  kwa kuteuliwa kwake na kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amempatia heshima kubwa ya kuiongoza wilaya ya Chemba.

Adha aliwapongeza wakuu wengine wapya wa wilaya za Bahi Godwini Gondwe na Mpwapwa Sophia Kizigo waliohamishiwa mkoani Dodoma katika mabadiliko ya vituo vya wakuu wa wilaya yaliyofanyika hivi karibuni.

Hafla ya kumuapisha Mkuu wa wilaya ya Chemba na kuwakaribisha wakuu wa wilaya wapya ilifunguliwa na mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyemule ambayo pia ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Dodoma, Viongozi  wa dini, Viongozi wa vyama vya siasa, kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa pamoja na Menejimenti ya Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Dodoma.

Sunday, January 29, 2023

SHULE BORA KUINUA KIWANGO CHA UBORA WA ELIMU AWALI NA MSINGI

 


Na Wellu Mtaki, Dodoma

SERIKALI kupitia mradi wa Shule Bora wenye lengo la kuinua ubora wa Elimu ya awali na Msingi  utahakikisha unaongeza ufaulu wa masomo kwa wanafunzi kwa kuboresha ujifunzaji, Ufundishaji, kuimalisha Ujumuishi.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Dk.Fatuma Mganga wakati akifungua mafunzo ya mpango wa Serikali wa SHULE BORA kwa waandishi wa habari Jijini Dodoma.

Dk Mganga amesema kuwa moja ya malengo yaliyopo kwa sasa mkoani humo kwa mwaka 2023 ni kuongeza ufaulu kwa asili 95 ya matokeo ya mtihani wa darasa la saba na asilimia 75 ya wanafunzi wanaohitimu kidato cha nne wawe na ufaulu wa daraja la kwanza hadi la tatu.

"Suala la Elimu katika Mkoa wa Dodoma bado halijatangazwa vizuri na kuwataka waandishi wa habari wakatumie kalamu zao wakawe chachu katika kuielimisha jamii kuwa wanajukumu la kushiriki kikamilifu katika kuboresha elimu,"alisema Dk Mganga.

Amesema kuwa Mwaka huu peke yake zaidi ya wanafunzi 90,000 wanatarajiwa kuanza masomo ambapo hadi kufikia Januari 26  asilimia 89.7 ya wanafunzi wa darasa la awali wameripoti shule huku asilimia 94.2 kwa darasa la kwanza na asilimia 66.95 kidato cha kwanza wakiwa wameripoti shuleni.

Naye Mratibu wa mpango wa SHULE BORA Mkoa wa Dodoma Mtemi Zombwe amesema kuwa ili kufanikisha mchakato wa kuinua na kuboresha elimu ni vyema kila mmoja akatambua kuwa anajukumu la kushiriki katika mchakato huo.

Zombwe amesema kuwa katika ngazi ya kitaifa SHULE BORA itatoa pia msaada wa kiufundi kwa serikali ya Tanzania, pamoja na utekelezaji wa mradi wa pili wa LIPWA KWA MATOKEO yaani Education Program for Results Two.

Mradi wa Shule Bora ni Mpango wa Serikali ya  Tanzania, ikifadhiliwa na Serikali ya Uingereza kwa lengo la kuinua ubora wa elimu ya Awali na Msingi katika mikoa tisa hapa nchini kwa ushauri elekezi kutoka Cambridge Education ikishirikiana na mashirika ya ADD International, International Rescue Committee na Plan International.

WANAOFANYA VITENDO VYA UKATILI WATAKIWA KUACHA MARA MOJA



Na Elizaberth Paulo,Dodoma

MKUU wa mkoa wa Dodoma Mheshimiwa Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wanaume pamoja na wale wote wanaotenda vitendo vya kikatili kuacha mara moja kwani kundi kubwa linaloathirika na vitendo hivyo ni watoto na wanawake.

Aidha amesema mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa mikoa ambayo kuna vitendo vya ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto.

Senyamule ametoa wito huo katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma (General Hospital) alipokua akizindua kituo jumuishi cha utoaji wa huduma kwa manusura wa vitendo vya Ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto.

"Mradi huu wa USAID AFYA YANGU umekuja wakati muafaka hapa Jijini na tunashukuru kwa sababu mkoa huu pia una changamoto ya vitendo vya kikatili,"amesema Senyamule.

Amesema kuwa manusura wa vitendo vya kikatili wamekuwa wakipata changamoto katika kupata huduma kwa haraka na kwa taratibu kutokana na mtawanyiko wa maeneo ya huduma muhimu wanayohitaji ikiwemo huduma za afya, ustawi wa jamii na huduma za kisheria.

"Jengo hili la kutoa huduma jumuishi kwa manusura wa vitendo vya ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto ni moja ya malengo ya mpango jumuishi wa utoaji huduma kwa walengwa iliyozinduliwa mwaka 2013 kwa lengo la kuhakikisha huduma inatolewa kwa manusura wa ukatili kwa haraka, uratibu mzuri, na kurahisisha mfumo wa rufaa kwa manusura kwa kupata huduma maalum kama msaada wa Kisheria,"amesema Senyamule.

Ameongeza kuwa hali hiyo imesababisha baadhi ya manusura kukosa huduma kwa wakati na kupata madhara yakiwemo maambukizi ya virusi vya Ukimwi, Ulemavu wa kudumu, mimba zisizotarajiwa na mimba za utotoni kutokana na vitendo vya ukatili alivyofanyiwa.

"Baadhi ya manusura kurubuniwa na kupoteza ushahidi ambao ungesaidia manusura kupata haki yake pindi shauri linapofikishwa katika vyombo vya Sheria, kutumia gharama kubwa katika kufikia maeneo ya kupatia huduma hivyo kusababisha matukio mengi ya ukatili kutokutolewa taarifa katika vyombo vya Sheria hali Iliyosababisha manusura kukosa huduma mbalimbali pamoja na haki za kisheria,"amesema Senyamule

Ameagiza wahudumu wa jengo ambalo wanatoa huduma kwa manusura kufanya kazi saa 24 kwani vitendo vya kikatili vinatokea muda wowote hivyo kuanzisha utaratibu wa kuwa katika hospitali hiyo muda wote na kuwaasa kutumia vifaa kwa umakini mkubwa na kwa weledi kwa manufaa ya kuchakata takwimu za manusura wanaopatiwa huduma katika jengo hilo lililozinduliwa ndani ya hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma.

Kwa upande wake Chip Lyons Rais wa shirika la EGPAF ambao ni wadau waliofadhili ukarabati wa jengo hilo la utoaji wa huduma kwa manusura wa vitendo vya ukatili amesema mradi huo unatakribani miaka 13 tangu kuanzishwa kwake kutokana na ushirikiano mzuri na Viongozi wa Tanzania hata uongozi wa mkoa wa Dodoma.

Naye Anna Hoffman Naibu Mkurugenzi wa Shirika la afya la USAID amesema mradi huo Unatekelezwa katika mikoa Sita nchini ikiwemo mkoa wa Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tabora na Dodoma huku Ukilenga kufikia maeneo mengi hapa Tanzania.


Thursday, January 26, 2023

MNEC WAZAZI TAIFA ATAKA CCM WATANGAZE MAFANIKIO YA RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN

MJUMBE wa Halmashauri Kuu Chama Cha Mapinduzi Taifa (MNEC) Wazazi Hamoud Jumaa amewataka viongozi wa CCM kutumia mikutano ya hadhara iliyoruhusiwa na Rais Dk Samia Suluhu Hassan kueleza miradi ya maendeleo inayofanywa na kutekelezwa na Serikali ya awamu ya sita.

Akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Kibaha Vijijini pamoja na baadhi ya viongozi na wanaCCM kusiwe na kigugumizi kukisemea Chama na kusimamia miradi mbalimbali inayotekelezwa.

Jumaa alisema kuwa Rais ametoa fursa nzuri kuruhusu mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa hivyo ni wakati sasa kwa viongozi na wanaccm kuelezea yale yaliyofanywa katika kuleta maendeleo ya wananchi.

"Viongozi wenzangu, madiwani,wabunge na wanaCCM tutoke kusemea Chama na kupanda majukwaani kuitendea haki ilani ambayo utekelezaji wake unafanya vizuri,"alisema Jumaa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kibaha Vijijini Mkali Kanusu alisema kuwa watahakikisha wanasimamia utekelezaji wa miradi na watashirikiana na watendaji wa serikali ili kufanikisha miradi ya maendeleo kwa wananchi.

Naye Katibu wa CCM Safina Nchimbi alisema kuwa anamshukuru MNEC Taifa kuahidi kujenga ofisi ili ziendane na umri wa Chama na kinaendelea na mipango yake mbalimbali ya kimaendeleo na kuhakikisha chama kinakubalika kwa wananchi.


Tuesday, January 17, 2023

UJENZI TAASISI ZA SERIKALI UZINGATIE BAJETI

Na Wellu Mtaki Dodoma

SERIKALI kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) imetoka wito kwa taasisi zote zinazoendelea na ujenzi Dodoma zihakikishe ujenzi huo unakamilika kwa kizingatia taratibu zote za ujenzi ikiwemo ubora, muda , bajeti iliyotengwa na thamani ya fedha Ili kuleta tija.

Wito huo umetolewa Jijini Dodoma na Mhe. George Simbachawene Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera , Bunge na Uratibu wakati wa hafla ya kukabidhi vibali vya ujenzi wa ofisi za taasisi Dodoma huku akiagiza taasisi nyingine ambazo bado hazijaaza maandalizi ya ujenzi Dodoma ziwasilishwe Ofisi ya Waziri Mkuu mahitaji ya viwanja vya ujenzi wa ofisi za taasisi Dodoma kwa ajili ya uratibu wa pamoja.

Simbachawene amesema kuwa serikali ya awamu ya sita imeendelea kutekeleza kikamilifu Mpango wa kuhamia Dodoma ambapo wananchi wanapata huduma zote katika makao makuu ya nchi na kwamba watumishi wote wa serikali ikiwemo wizara zote, vyombo vya ulizi na usalama, muhimili wa bunge na baadhi ya taasisi zimeamia Dodoma na wanaendelea kutekeleza majukumu yao.

Aidha amesema kuwa ifikapo march 2023 muhimili wa mahakama unatarajiwa kuhamia Jijini Dodoma kwani ujenzi wa jengo hilo umefika zaidi ya asilimia 90.

Pia ametoa rai kwa viongozi wa mkoa wa Dodoma, Wizara, Halmashauri, taasisi za serikali, sekta binafsi, wananchi na wadau wengine kuendelea kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa Mpango wa serikali wa kuahamia Dodoma pamoja na ujenzi wa makao makuu Ili kufikia malengo ya kuwa na Jiji Bora la kuvutia litakalokidhi mahitaji ya kijamii na kiuchumi kwa miaka mingi ijayo.

Lengo la hafla hiyo ni kukabidhi vibali vya ujenzi kwa taasisi zilizopewa idhini ya ujenzi wa ofisi Jijini Dodoma kama sehemu ya kutambua mchango wa taasisi hizo katika kuunga mkono utekelezaji wa Mpango wa serikali kuhamisha shughuli zake Jijini Dodoma.

CHONGOLO ATAKA VIJANA KUSHIRIKI KUJIKWAMUA KIUCHUMI

 

CHONGOLO ATAKA VIJANA WAJENGEWE FIKRA ZA KIUCHUMI

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo amewataka viongozi wa vyama vya Ukombozi Kusini mwa Afrika kuleta msukumo wa kuwajengea uwezo vijana kifikra na kiuchumi.

Chongolo meyasema hayo kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopo Kibaha Mkoani Pwani wakati akifungua kikao kazi cha makatibu wakuu wa vyama rafiki wanaounda kamati ya usimamizi wa shule hiyo. 

Chongolo amesema kuwa Ukombozi wa nyuma ulikuwa ni wa kujikomboa kutoka kwa wakoloni lakini kujikomboa kwa sasa ni kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kifikra.

"Makatibu Wakuu  kutoka nchi sita marafiki  wanapaswa kudumisha uzalendo ulioasisiwa na viongozi waliotangulia ambao waliweka misingi ya ushirikiano,"alisema Chongolo. 

Aidha amesema kuwa Rais Dk Samia Suluhu Hassan anawakaribisha nchini huku akiwawakikishia usalama wao kwa muda wote watakaokuwa hapa nchini hadi watakaporudi makwao.

"Mwaka jana tulipokutana tulijadili mambo mengi kwa kikao kilichofanyika kwa njia ya mtandao sasa leo tumekutana ili tuweze kuchakata  kwa kina yale yote tuliyojadili,"amesema Chongolo.  

Naye Katibu Itikadi na Uenezi CCM Sophia Mjema amesema kuwa kila kitakachokifanyiwa maamuzi  kitajengwa katika sura ya umoja kama ulivyojengwa  katika  historia ya nchi hizo rafiki.

Vyama hivyo vilivyoshiriki ni CCM Tanzania, ZANU PF Zimbabwe, FRELIMO Msumbiji, MPLA Angola, SWAPO Namibia na ANC Afrika Kusini.


Sunday, January 8, 2023

WATANO WAFA AJALINI



WATANO WAFA 10 WAJERUHIWA AJALINI

WATU watano wamefariki dunia na wengine 10 kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria aina ya Toyota Coaster na gari la mizigo aina ya Mitsubishi Canter.

Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani ACP Pius Lutumo alisema kuwa majeruhi wako hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo kwa matibabu zaidi.

Lutumo alisema kuwa ajali hiyo ilitokea Januari 8 mwaka huu majira ya saa 1:40 asubuhi eneo la Mwavi kata ya Kiwangwa Wilayani Bagamoyo ambapo watu watano wamefariki eneo la ajali huku 10 wakijeruhiwa.

Alisema kuwa basi hilo dogo lenye namba za usajili T 972 DCY lililokuwa likitoka Bagamoyo kwenda Morogoro liligongana na lori dogo lenye namba za usajili T 168 CAZ.

"Katika ajali hiyo waliofariki wanawake wawili na wanaume watatu ambapo majina yao bado hayajafahamika ambapo maiti na majeruhi wako hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo,"alisema Lutumo.

Chanzo cha ajali Coaster lilikuwa linapita gari lingine bila tahadhari na kugongana na gari lingine kusababisha ajali hiyo.

"Madereva wanapaswa kuchukua tahadhari ili kuepuka ajali zisizo za lazima kwa kufuata sheria bila shuruti kwa kuzingatia usalama wao na wengine,"alisema Lutumo.

Mwisho.

Thursday, January 5, 2023

WANAFUNZI WASIYO RIPOTI SHULENI KUTAFUTWA


WANAFUNZI WATORO JIJINI DODOMA KUTAFUTWA WARUDI MASHULENI.

Na Wellu Mtaki, Dodoma

MKUU wa mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule amewataka viongozi wa kata, walimu, wazazi na walezi kushirikiana kuwatafuta wanafunzi ambao hawataripoti shuleni baada ya siku 90 mara shule za sekondari zitakapofunguliwa watatafutwa na kurudishwa shuleni.

Ameyasema leo katika kikao kazi kilichojumuisha maofisa elimu wa Wilaya za wa Mkoa pamoja na walimu wa wilaya zote Jijini Dodoma.

Sinyamule amesema kuwa zipo changamoto nyingi ambazo zinapelekea watoto kutokufika shuleni kama watoto kupelekwa kwenda kufanya kazi za ndani pamoja na changamoto za kimaisha zilizopelekea mtoto kutokufika shule.

Amesema kuwa mpaka Sasa wanafunzi 4,000 tayari wamepatikana na hivyo wataaza masomo yao muhulah uu wa mwaka 2023 huku akisisitiza kuwa Halmashauri zote Dodoma kuhakikisha wanafunzi wanasajiliwa kwa asilimia 100.

Amewataka walimu kuwapokea wanafunzi hata wale ambao hawana sare za shule ila watoe taarifa kwa watendaji wa kata au Kijiji kwa lengo la kuwahimiza wazazi au walezi kutimiza majukumu yao huku watoto wakiendelea na masomo.

Kwa upande wake Mkurugezi wa elimu ofisi ya Rais (TAMISEMI) amesema kuwa watahakikisha kupitia mkutano huo wa kupeana maelekezo na utekelezaji wataenda kuimarika katika nafasi zao pamoja na kuhakikisha wanafanya vizuri katika sekta ya Elimu.

DKT BITEKO ASISITIZA UONGEZAJI THAMANI MADINI

Dkt. Biteko asisitiza wadau kuwekeza uongezaji thamani madini

WAZIRI wa Madini, Dkt. Doto Biteko amesema kuwa, Serikali iko mbioni kuanzisha upya Minada ya Madini ya Vito ili kuleta wanunuzi wakubwa, wafanyabiashara na wachimbaji wa madini hapa nchini.

Hayo yamebainishwa Januari 5, 2023 wakati akizindua duka la utalii wa madini la kampuni ya Tanzanite Experience katika eneo la Manyara Kibaoni wilaya ya Karatu Mkoani Arusha 

Amesema kupitia mnada huo kampuni ya Tanzanite Experience kupitia duka la utalii wa madini itapata madini mengi kwa ajili ya kuendeleza kituo hicho na maeneo mengine anayoyafanyia kazi.

Dkt. Biteko amesema kuwa, kupitia kituo hicho kilichopo katika ukanda wenye maeneo ya hifadhi imekuwa ni sehemu kubwa ya kivutio cha utalii kwa wageni kutoka ndani na nje ya nchi. 

"Madini ya Tanzanite yamekuwa yakinunuliwa hapa nchini kwa kiasi kikubwa na watalii wanaokuja kutembelea hifadhi zetu na kupitia wao madini haya yanaendelea kutangazwa duniani," amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza kuwa, Wizara ya Madini inapongeza uwekezaji huo ambao umefanywa kwa asilimia 100 na watanzania wakiunga juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan wakati akitangaza vivutio mbalimbali vilivyopo hapa nchini kupitia filamu ya "The Royal Tour" ambapo utalii na madini ya Tanzanite ilikuwa miongoni wa vivutio hivyo.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesema wizara inahamasisha uwekezaji wa namna hiyo ambao unaunga mkono moja kwa moja jitihada zinazofanywa na Serikali za kutangaza madini ya Tanzanite duniani hususan katika eneo la shughuli za uongezaji thamani.

"Duka hili linatarajia kuuza bidhaa mbalimbali za madini ya Tanzanite na Tsavourite ambazo kwa miaka mingi zimekuwa zikitengenezwa na kuuzwa nje ya nchi. Hii ni hatua kubwa ambayo nchi yetu inaendelea kuchukua katika kuhakikisha madini haya yanazalishwa hapa nchini," ameongeza Dkt. Biteko.

Dkt. Biteko ametoa wito kwa watu wote ambao wana nia ya kuwekeza kwenye uchongaji, ukataji wa madini kuwekeza kwenye uongezaji thamani wa madini ili madini hayo yaweze kutupatia ajira na kodi kubwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanzanite Experience Hassinne Sajani amesema kuwa, duka hilo limekuwa kivutio kikubwa kwa watanzania na watalii kutoka nje ya nchi ambao wananunua bidhaa za madini zilizopo. Aidha ameongeza kuwa, kampuni imeajiri wafanyakazi 80 na zaidi ya asilimia 80 ni wakazi wa maeneo ya Manyara Kibaoni.

Ameahidi kuongeza juhudi kuendelea kutangaza madini ya Tanzania ambayo ni zawadi kwa Watanzania ili madini hayo yaweze kupanda thamani duniani.

Kwa upande wake, Meneja wa Tanzanite Experience, Junaid Khan amesema kuwa, zaidi ya wageni 6000 wamefika kutembelea Kampuni ya Tanzanite Experience  

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Karatu Dadi Kolimba amesema biashara ya madini imefunguka katika wilaya ya Karatu na kuongeza mapato na kueleza kuwa ameipongeza kampuni hiyo kwa kutoa ajira zaidi ya 80 kwa watanzania katika nafasi mbalimbali.

Tuesday, January 3, 2023

DODOMA WAASWA UPANDAJI MITI



Na Wellu Mtaki, Dodoma

MKUU wa mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule amewataka wazazi na walezi wahakikishe wanawapeleka watoto wao shuleni mara baada ya shule kufunguliwa.

Sinyamule ameyasema leo katika ziara ya Kampeni ya upandaji wa miti iliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Chemba Jijini Dodoma.

Amesema kuwa zipo Sheria ambazo italazimika kuzifuata kuhakikisha kuwa mtoto anapata haki yake ya kwenda shule hivyo inapaswa wazazi na walezi watambue lengo na makusudi ya serikali ya awamu ya sita kwa watoto wa kidato cha kwanza.

Aidha amesema huku kuna umuhimu wa upandaji wa miti ili kurudisha uoto wa asili na kupambana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo kuna maelekezo ambayo yametolewa na serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha tunatunza mazingira.

Amebainisha kuwa hilo ni jukumu la kila mwanafunzi kuwa na mti wake shuleni ambao atautuza kwa kipindi chote awapo shuleni na wazazi watambue kama elimu ya vitendo.

Amezitaka shule kuanzisha miradi ambayo itawezesha shule kujikimu na chakula kwani imeonyesha moja ya njia ambazo zitapunguza utoro mashuleni ni pamoja na watoto kupata chakula.

Mwisho.