Tuesday, January 3, 2023

DODOMA WAASWA UPANDAJI MITI



Na Wellu Mtaki, Dodoma

MKUU wa mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule amewataka wazazi na walezi wahakikishe wanawapeleka watoto wao shuleni mara baada ya shule kufunguliwa.

Sinyamule ameyasema leo katika ziara ya Kampeni ya upandaji wa miti iliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Chemba Jijini Dodoma.

Amesema kuwa zipo Sheria ambazo italazimika kuzifuata kuhakikisha kuwa mtoto anapata haki yake ya kwenda shule hivyo inapaswa wazazi na walezi watambue lengo na makusudi ya serikali ya awamu ya sita kwa watoto wa kidato cha kwanza.

Aidha amesema huku kuna umuhimu wa upandaji wa miti ili kurudisha uoto wa asili na kupambana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo kuna maelekezo ambayo yametolewa na serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha tunatunza mazingira.

Amebainisha kuwa hilo ni jukumu la kila mwanafunzi kuwa na mti wake shuleni ambao atautuza kwa kipindi chote awapo shuleni na wazazi watambue kama elimu ya vitendo.

Amezitaka shule kuanzisha miradi ambayo itawezesha shule kujikimu na chakula kwani imeonyesha moja ya njia ambazo zitapunguza utoro mashuleni ni pamoja na watoto kupata chakula.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment