WANAFUNZI WATORO JIJINI DODOMA KUTAFUTWA WARUDI MASHULENI.
Na Wellu Mtaki, Dodoma
MKUU wa mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule amewataka viongozi wa kata, walimu, wazazi na walezi kushirikiana kuwatafuta wanafunzi ambao hawataripoti shuleni baada ya siku 90 mara shule za sekondari zitakapofunguliwa watatafutwa na kurudishwa shuleni.
Ameyasema leo katika kikao kazi kilichojumuisha maofisa elimu wa Wilaya za wa Mkoa pamoja na walimu wa wilaya zote Jijini Dodoma.
Sinyamule amesema kuwa zipo changamoto nyingi ambazo zinapelekea watoto kutokufika shuleni kama watoto kupelekwa kwenda kufanya kazi za ndani pamoja na changamoto za kimaisha zilizopelekea mtoto kutokufika shule.
Amesema kuwa mpaka Sasa wanafunzi 4,000 tayari wamepatikana na hivyo wataaza masomo yao muhulah uu wa mwaka 2023 huku akisisitiza kuwa Halmashauri zote Dodoma kuhakikisha wanafunzi wanasajiliwa kwa asilimia 100.
Amewataka walimu kuwapokea wanafunzi hata wale ambao hawana sare za shule ila watoe taarifa kwa watendaji wa kata au Kijiji kwa lengo la kuwahimiza wazazi au walezi kutimiza majukumu yao huku watoto wakiendelea na masomo.
Kwa upande wake Mkurugezi wa elimu ofisi ya Rais (TAMISEMI) amesema kuwa watahakikisha kupitia mkutano huo wa kupeana maelekezo na utekelezaji wataenda kuimarika katika nafasi zao pamoja na kuhakikisha wanafanya vizuri katika sekta ya Elimu.
No comments:
Post a Comment