Friday, May 29, 2015

UMISSETA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha
WACHEZAJI wa michezo ya Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) mkoa wa Pwani wametakiwa kushindana na si kushiriki kwenye michuano hiyo ngazi ya Kanda ili mkoa utoe wachezaji wengi.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na ofisa elimu wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani Benjamini Majoya wakati wa ufungaji wa michezo hiyo ngazi ya mkoa kwenye viwanja vya Filbert Bayi na kusema kuwa ushindani ndiyo unaotakiwa na si ushiriki.
Majoya alisema kuwa mashindano ya Kanda ambayo yatafanyika mkoani Morogoro mwezi ujao ili kupata timu itakayounda kanda ya Mashariki inayoundwa na mikoa ya Pwani na Morogoro kwa ajili ya timu itakayokwenda mkoani Mwanza kwenye mashindano ya Taifa.
“Michezo ni sehemu ya kuendeleza taaluma hivyo lazima mcheze ip[asavyo na si muende kwa ajili ya kushiriki tu lazima mpambane na kuonyesha vipaji vyenu ili muwakilishe vyema mkoa na kutoa wachezaji wengi kuwakilisha kanda ya Mashariki,” alisema Majoya.
Aidha aliwataka wanamichezo hao kuonyesha nidhamu wakati wanacheza michezo kwani nidhamu ndiyo mafanikio ya michezo kwani bila ya kuwa na nidhamu itakuwa vigumu kufanikiwa.
Kwa upande wake ofisa michezo wa mkoa wa Pwani Grace Bureta alisema kuwa michezo hiyo ilihusisha wilaya sita za mkoa huo ambapo jumla ya wachezaji 136 wa michezo mbalimbali walichaguliwa kwa ajili ya kuunda timu ya mkoa.
Bureta alisema kuwa timu hiyo itaingia kambini kwa muda wa siku nne hadi Mei 31 ambapo Juni Mosi wataelekea mkoani Morogoro kwa ajili ya mashindano ya kanda ya Mashariki.
Alisema kuwa wachezaji waliochaguliwa ni wazuri na anategemea watafanya vizuri kwa kutoa wachezaji wengi kuunda timu ya Kanda na kufanikiwa kutetea ubingwa wa jumla wa mashindano hayo kitaifa mjini Mwanza.

Mwisho.Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani umechagua jumla ya wanamichezo 136 wa michezo mbalimbali kwa ajili ya kuunda timu ya mkoa ya Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) kwa ajili ya kushiriki michezo ya Kanda ya Mashariki.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa Michezo wa mkoa wa Pwani Grace Bureta wakati wa ufungaji wa michezo hiyo ngazi ya wilaya iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya Filbert Bayi.
Bureta alisema kuwa mashindano hayo ambayo yaliwahusisha wachezaji toka kwenye shule za sekondari za wilaya sita za mkoa huo ambazo ni Mafia, Rufiji, Kibaha Mjini na Vijijini, Kisarawe, Mkuranga na Bagamoyo walifanikiwa kupata wachezaji ambao walifanya vizuri.
“Mara baada ya michezo kukamilika na kuchaguliwa wachezaji hao timu itaingia kambini kwa muda wa siku nne hadi Mei 31 ambapo Juni Mosi wataelekea mkoani Morogoro kwa ajili ya mashindano ya kanda ya Mashariki,” alisema Bureta.
Alisema kuwa wachezaji waliochaguliwa ni wazuri na anategemea watafanya vizuri kwa kutoa wachezaji wengi kuunda timu ya Kanda na kufanikiwa kutetea ubingwa wa jumla wa mashindano hayo kitaifa mjini Mwanza.
Benjamini Majoya aliwataka wanamichezo wa mkoa huo kushindana na si kushiriki kwenye michuano hiyo ngazi ya Kanda ili mkoa utoe wachezaji wengi watakaounda kanada hiyo.
Majoya alisema kuwa mashindano ya Kanda ambayo yatafanyika mkoani Morogoro mwezi ujao ili kupata timu itakayounda kanda ya Mashariki inayoundwa na mikoa ya Pwani na Morogoro kwa ajili ya timu itakayokwenda mkoani Mwanza kwenye mashindano ya Taifa.
“Michezo ni sehemu ya kuendeleza taaluma hivyo lazima mcheze ip[asavyo na si muende kwa ajili ya kushiriki tu lazima mpambane na kuonyesha vipaji vyenu ili muwakilishe vyema mkoa na kutoa wachezaji wengi kuwakilisha kanda ya Mashariki,” alisema Majoya.
Aidha aliwataka wanamichezo hao kuonyesha nidhamu wakati wanacheza michezo kwani nidhamu ndiyo mafanikio ya michezo kwani bila ya kuwa na nidhamu itakuwa vigumu kufanikiwa, michezo iliyoshindaniwa ni pamoja na soka, pete, wavu, kikapu, riadha na bao.
Mwisho.

 Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani umechagua jumla ya wanamichezo 136 wa michezo mbalimbali kwa ajili ya kuunda timu ya mkoa ya Umoja wa Michezo na Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) kwa ajili ya kushiriki michezo ya Kanda ya Mashariki.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Ofisa Michezo wa mkoa wa Pwani Grace Bureta wakati wa ufungaji wa michezo hiyo ngazi ya wilaya iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya Filbert Bayi.
Bureta alisema kuwa mashindano hayo ambayo yaliwahusisha wachezaji toka kwenye shule za sekondari za wilaya sita za mkoa huo ambazo ni Mafia, Rufiji, Kibaha Mjini na Vijijini, Kisarawe, Mkuranga na Bagamoyo walifanikiwa kupata wachezaji ambao walifanya vizuri.
“Mara baada ya michezo kukamilika na kuchaguliwa wachezaji hao timu itaingia kambini kwa muda wa siku nne hadi Mei 31 ambapo Juni Mosi wataelekea mkoani Morogoro kwa ajili ya mashindano ya kanda ya Mashariki,” alisema Bureta.
Alisema kuwa wachezaji waliochaguliwa ni wazuri na anategemea watafanya vizuri kwa kutoa wachezaji wengi kuunda timu ya Kanda na kufanikiwa kutetea ubingwa wa jumla wa mashindano hayo kitaifa mjini Mwanza.
Benjamini Majoya aliwataka wanamichezo wa mkoa huo kushindana na si kushiriki kwenye michuano hiyo ngazi ya Kanda ili mkoa utoe wachezaji wengi watakaounda kanada hiyo.
Majoya alisema kuwa mashindano ya Kanda ambayo yatafanyika mkoani Morogoro mwezi ujao ili kupata timu itakayounda kanda ya Mashariki inayoundwa na mikoa ya Pwani na Morogoro kwa ajili ya timu itakayokwenda mkoani Mwanza kwenye mashindano ya Taifa.
“Michezo ni sehemu ya kuendeleza taaluma hivyo lazima mcheze ip[asavyo na si muende kwa ajili ya kushiriki tu lazima mpambane na kuonyesha vipaji vyenu ili muwakilishe vyema mkoa na kutoa wachezaji wengi kuwakilisha kanda ya Mashariki,” alisema Majoya.
Aidha aliwataka wanamichezo hao kuonyesha nidhamu wakati wanacheza michezo kwani nidhamu ndiyo mafanikio ya michezo kwani bila ya kuwa na nidhamu itakuwa vigumu kufanikiwa, michezo iliyoshindaniwa ni pamoja na soka, pete, wavu, kikapu, riadha na bao.
Mwisho.














No comments:

Post a Comment