Na John Gagarini, Kibaha
MKOA wa Pwani umepitisha mapendekezo ya kugawanywa kwa Wilaya ya
Rufiji kuwa wilaya mbili za Rufiji na Kibiti na kuligawa Jimbo la Chalinze kuwa
majimbo mawili ya Chalinze na Saadani.
Mbali ya kupitisha wilaya mpya ya Kibiti na Jimbo la Saadani umepitisha
mapendekezo yaliyowasilishwa na Halmashauri ya Kibaha Mji ya kugawa Tarafa ya Kibaha
na kuwa na Tarafa mpya ya Kongowe.
Maamuzi hayo yalifanywa
mjini Kibaha kwenye Kiko cha Usahauri cha Mkoa (RCC) kilichokaa mwishoni mwa
wiki chini ya kaimu mkuu wa mkoa wa Pwani ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya
Kibaha Halima Kihemba
Kihemba alisema kuwa mapendekezo
hayo yamefuata sheria na taratibu zinazostahili kwa upande wa wilaya na Jimbo
ni pamoja na Jimbo kuwa ndani ya wilaya moja ama Halmashauri moja, idadi kubwa
ya watu ,upatikanaji wa mawasiliano ikiwemo mitandao ya simu, barabara, huduma
za kiuchumi na jiografia ya eneo husika.
Naye Mkuu wa wilaya ya
Rufiji Nurdin Babu alisema kuwa anpongeza kikao hicho kuweza kupitisha
uanzishwaji wa wilaya mpya ya Kibiti kwani itawasogezea huduma mbalimbali za
kijamii karibu.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga alisema
kugawanywa kwa Jimbo la Chalinze ni mchakato wa wilaya ya Bagamoyo kugawanywa
katika wilaya mbili
Mwanga alisema kuwa endapo utaratibu huo utakuwa umekamilika
wilaya hiyo itakuwa na majimbo matatu ya uchaguzi ambayo ni Bagamoyo,Saadani na
Chalinze kutokana na ukubwa wa wilaya hiyo.
Jimbo la Bagamoyo litakuwa na kata za Dunda,Magomeni,Nia Njema
,Kisutu, Makurunge, Kiromo,Zinga ,Kerege, Mapinga, Yombo na Fukayosi ambayo
itatolewa kutoka jimbo la Chalinze.
Huku Jimbo la Chalinze likiwa na kata za Vigwaza ambayo
imeondolewa katika Jimbo la Bagamoyo, Kiwangwa, Msata, Lugoba,Talawanda, Ubena,
Pera, Bwiringu na Msoga na Jimbo jipya la Saadani makao
makuu yatakuwa Miono na Jimbo hilo likiwa na kata za Kibindu, Mbwewe, Kimange, Mandela,
Miono na Mkange.
Mwisho
No comments:
Post a Comment