MTAA wa Miembe Saba B Wilayani Kibaha Mkoani Pwani umezanza zoezi la kuweka vifusi kwenye barabara ya Mtaa ili kuwaondolea kero wananchi wa Mtaa huo.
Monday, January 6, 2025
MTAA WA MIEMBE SABA WAWEKA VIFUSI KUBORESHA BARABARA YA MTAA
Sunday, January 5, 2025
WAHUKUMIWA MAISHA NA MIAKA 20 KWA UKATILI WA KIJINSIA
WATUHUMIWA wawili Mkoani Pwani waliokuwa wanakabiliwa kwa kesi za ukatili wa kijinsia wamehukimiwa vifungo tofauti ambapo mmoja amefungwa kifungo cha maisha jela na mwingine amefungwa kifungo cha miaka 20 jela.
Aidha jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani lilipeleka Mahakamani kesi 125 za makosa mbalimbali ambapo kati ya kesi hizo 47 zimepata mafanikio kwa watuhumiwa kuhukumiwa vifungo mbalimbali.
Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani ACP Salim Morcase alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio ya jeshi hilo kwa kipindi cha mwezi Disemba 2024.
Morcase amesema kuwa jumla ya kesi za ukatili wa kijinsia kulikuwa na kesi tano za makosa ya kubaka na kulawiti.
"Watuhumiwa hao wawili walipata adhabu hizo ambapo wa kwanza alipatikana na hatia ya kubaka na kulawiti na wa pili alikutwa na hatia ya unyanyasaji wa kingono,"amesema Morcase.
Amesema kuwa watuhumiwa 52 wamehukumiwa vifungo tofauti tofauti kutokana na aina ya makosa yaliyokuwa yakiwakabili.
MADEREVA 11 MKOANI PWANIWAFUNGIWA LESENI
COREFA KUJENGA OFISI UWANJA WAKE
COREFA KUANDAA VIJANA KWENYE VITUO KILA WILAYA
CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.
COREFA KUANDAA VIJANA KUPITIA VITUO KILA WILAYA
CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.
VIONGOZI WA DINI NCHINI JAMHURI YA AFRIKA YA KATI WAISHUKURU JWTZ

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya kutembelewa na Kamanda wa Kikosi cha Nane cha Ulinzi wa Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati Luteni Kanali Theofili Nguruwe wamesema uwepo wa JWTZ umekuwa na tija sana nchini humo kwani wamekuwa wakifanya kazi zao kwa weledi wa hali ya juu.
Akizungumza kwa niaba ya Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Berberati Mhashamu Koffi Denis, Karibu Mkuu wa Jimbo hilo Padre Jean Ancelimo amesema mbali na Ulinzi wa Amani pia limekuwa likitoa misaada mbalimbali ya hali na mali huku akitolea mfano wa ujenzi wa shule ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ambayo imepewa jina la Serengeti.
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Evenjeliko (AEC) Mhashamu Lucian Nday amesema uwepo wa JWTZ nchini hapo umewafanya waishi kwa amani na zaidi ya yote limewezesha ukuaji wa lugha adhimu ya kiswahili.
Sheikh Rashid Mohamoud Arouna ni Imam wa Masjid Nuur amesema JWTZ limekuwa mstari wa mbele kwenye kila jambo ambalo wanaombwa kutoa msaada kwa ajili ya kuhakikisha nchi yao inakuwa na amani.
Kwa upande wa Kamanda wa Kikosi cha Nane cha Ulinzi wa Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati Luteni Kanali Theofili Nguruwe amewashukuru viongozi hao na kuahidi kutekeleza majukumu yake kwa weledi wa hali ya juu.