Tuesday, July 23, 2024

MKUU WA MKOA PWANI AKABIDHI WAKUU WA WILAYA MAGARI




MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amekabidhi magari mawili kwa wakuu wa Wilaya za Kisarawe na Bagamoyo kwa ajili ya urahisishaji utekelezaji wa majukumu yao ya kazi.

Wakuu waliokabidhiwa magari hayo aina ya Toyota yaliyotolewa na Serikali ni Petro Magoti wa Wilaya ya Kisarawe na Halima Okashi wa Wilaya ya Bagamoyo.

Kunenge alikabidhi magari hayo Mjini Kibaha mbele ya wakuu wengine wa Wilaya za Mkoa huo alisema yatawasaidia kufanya kazi zao kwa uharaka katika kuwatumikia wananchi.

Alisema kuwa mkoa una wilaya saba ambapo gari moja litakuja na manne yatakuja kwa bajeti ya mwaka huu ambapo hata wao wamepata magari kuhudumia wananchi.

"Kupata magari haya yatasaidia kuwafikia wananchi kwa urahisi kwani upatikanaji wa magari hayo ni sehemu ya kurahisisha njia ya kuwafikia wananchi,"alisema Kunenge.

Aidha alisema kuwa wanampongeza Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa magari hayo ili kuwarahisishia usafiri kwenda kuwatumikia wananchi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Okashi alisema kuwa magari hayo yatawasaidia kuketa ufanisi watayatunza ili waweze kuwafikia wananchi kwa urahisi na kwa wakati ili watatue changamoto zinazo wakabili.

Alisema kuwa magari hayo watayatunza kwani ni kwa ajili ya kuhudumia wananchi na wanaipongeza serikali kwa kuwapatia magari hayo.

Kwa upande wake Magoti alisema kuwa usafiri huo utawasaidia kuwafikia wananchi waliomoko hata maeoneo yaliyoko mbali watayafikia kwa urahisi na kutoa huduma bora. 

Magoti alisema kuwa sasa hatarudi nyumbani kwani atahakikisha anawafikia wananchi na kuwasikiliza wananchi maeneo mbalimbali.

Monday, July 22, 2024

UNDERSTANDING THE REASONS BEHIND THE VOLUNTARY RESETTLEMENT OF NGORONGORO RESIDENTS WITHIN THE RESERVE.








By Our Correspondent, Ngorongoro.

For nearly two years, the initiative to resettle residents living within the Ngorongoro Conservation Area (NCA) has been underway, with residents voluntarily choosing to move to Msomera village in Handeni district, Tanga region, or other selected locations.

This process is spearheaded by the Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA), which begins by educating the public about the resettlement exercise and its benefits.

Once a resident comprehends and agrees to the voluntary resettlement, they are registered before being moved.

According to Flora Assey, the project manager of this initiative, public education involves all residents of the Ngorongoro division through various methods, including public meetings, door-to-door campaigns, and local and national media.

Recent implementation reports by Ms. Assey indicate that the number of residents registering for voluntary resettlement has increased, driven by the awareness raised through public education.

Since the initiative began in June 2022, up to June 2024, a total of 1,519 households comprising 9,251 people and 38,784 livestock have moved from the Ngorongoro Conservation Area to Msomera village and other locations.

“Contrary to what some may suggest, we do not use force in this exercise; our approach is to educate residents so they can voluntarily choose to resettle, which explains the fluctuating pace of the resettlement as it depends on individual decisions, and our goal is not to hastily resettle people but to ensure they move with clear understanding and willingness,” said Ms. Assey.

Ms. Assey further explained that if the government were using force, the resettlement would have been completed by now. 

However, because it is a voluntary exercise requiring a high level of precision, they spend considerable time educating residents to ensure those who decide to resettle do so happily.

“We only proceed with the resettlement after the resident fully understands the benefits, often observed through peers who have already resettled to Msomera or other chosen areas. This engagement makes us part of the community, as we are involved in educating the Ngorongoro division residents,” Ms. Assey added.

According to various documents from the Ngorongoro Conservation Area, the reserve was established in 1959, covering 8,292 square kilometers with approximately 8,000 residents and fewer than 260,000 livestock.

Currently, the area’s population is estimated to exceed 110,000, with over 800,000 livestock, a significant number of wildlife, and ongoing human activities, while the area size remains unchanged.

This situation affects the residents' livelihoods and increases human-wildlife conflicts, resulting in injuries and deaths caused by wild animals such as lions, elephants, buffaloes, hyenas, and hippos.

The imbalance in the NCAA's three core mandates—conservation, tourism, and community development—has been evident, as the government's efforts to enhance community development often negatively impact conservation activities.

As the government strengthens conservation efforts, residents' development is adversely affected due to the growing population and their increasing economic, social services, and other needs.

This imbalance has heightened conflicts, resulting in residents being injured by wild animals, livestock being preyed upon, and diseases like malignant catarrhal fever, rabies, and East Coast fever transmitted from wildlife to domestic animals like cattle, goats, sheep, and donkeys.

Speaking on the high motivation among residents to resettle to Msomera village in Handeni, Tanga, Ms. Assey said this is driven by government initiatives in the village and compensation offered to households willing to move voluntarily.

Among the incentives motivating residents to voluntarily resettle are compensation for developed properties within the reserve, a resettlement bonus of TZS 10 million for those moving to Msomera and TZS 15 million for those resettling elsewhere, and a three-bedroom house with a living room on a 2.5-acre plot.

“Other incentives include a five-acre titled farm for agricultural activities, free transportation of furniture and livestock to the resettlement site and ample grazing land in Msomera,” Ms. Assey noted.

According to Ms. Assey, the government has ensured that the resettled residents, mostly pastoralists, receive essential livestock services such as dipping tanks, water for domestic and livestock use, and other necessary services in line with its sustainable development goals to provide every Tanzanian with basic social services.

“Infrastructure for social services like health centers, schools, water, electricity, roads, communication networks, postal services, and livestock watering ponds are all available in Msomera village,” the coordinator stated.

To ensure that residents resettling to Msomera village enjoy freedom compared to life within the Ngorongoro reserve, the Handeni district council has been at the forefront of safeguarding their freedom to engage in economic activities like farming, business, building quality homes, and ensuring their security.

Handeni district commissioner Albert Msando, who chairs the district security committee, stated that students have greater freedom to travel to and from school than the reserve, as the area is free from dangerous wildlife.

“We receive residents from Ngorongoro almost every month, our main role as the government is to ensure their safety, so we have established a police station within Msomera village, allowing residents to conduct their economic activities 24/7,” said Mr. Msando.

He added that residents in Msomera enjoy greater freedom than life within the reserve, where laws and regulations prohibited farming, building permanent homes, operating motorcycles, and owning land.

The government, through the NCAA, continues to resettle voluntarily registered residents to improve their lives outside the reserve, away from the challenges of living alongside wildlife, thus avoiding attacks and fatalities from wild animals.
End.

*MABULA: NCAA ENDELEENI KUBUNI MAZAO MAPYA YA UTALII NA KUYATANGAZA.*





Na Kassim Nyaki, Ngorongoro.

Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na utalii anayeshughulikia utalii -Nkoba Mabula ameielekeza Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) kuendelea kubuni mazao mapya ya utalii ili kuwavutia watalii wengi zaidi wanaotembeela nchi yetu.

Mabula ametoa maelekezo hayo baada ya kupokea wasilisho kuhusu hali ya utalii katika hifadhi ya Ngorongoro, uboreshaji wa huduma za utalii, utangazaji wa vivutio vya utalii, mipango ya kubuni na kuendeleza mazao mapya ya utalii pamoja na  kuyatangaza kwenye mataifa mbalimbali.

Akiwa katika kikao na menejimenti ya NCAA Mabula amepokea wasilisho la hali ya Utalii katika eneo hilo na  mazao mapya ya utalii ambayo yapo kwenye utaratibu wa kutangazwa hivi karibuni ambayo ni Utalii wa baiskeli katika eneo la Olduvai, Utalii wa boti (canoeing) katika kreta ya Empakaai, utalii wa usiku (Night game drive) na utalii wa kuruka Kamba (Zipline tourism).

“Nimeona mikakati ya kuzindua mazao mapya ya Utalii kama utalii wa baiskeli, Zipline, utalii wa boti, endeleeni kuyafanyia utafiti wa kina na muongeze mazao mapya zaidi na yatangazwe katika fursa zenye majukwaa ya kimataifa ili kuendelea kuvutia wageni wengi wanaotembelea nchi yetu” amesisitiza Mabula.

Katika ziara hiyo mabula amekagua pia uboreshaji wa miundomnibu katika barabara kuu ya kutoka lango la Loduare hadi geti la Nabi, barabara ya kushuka bonde la Kreta, vyoo katika bonde la Ngorongoro, mifumo ya Tehama inayotumika katika malipo na kambi maalum za kulala wageni (Campsite).

Ameongeza kuwa “Tuendelee kuboresha miundombinu ya vivutio vingine ambavyo havijafikika ili kuongeza uzoefu wa maeneo mengine kwa wageni wetu tofauti na Wanyama ambao wameshazoeleka. Tayari Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameonyesha njia kwa Filamu ya Tanzanzia the Royal tour na idadi ya wageni imeanza kuongezeka, tuendeleze zaidi ili kufikia idadi ya watalii milioni 5 kama ilani ya chama tawala inavyotuelekeza”  ameongeza Mabula

Naibu Kamishna wa Uhifadhi NCAA (Uhifadhi, utalii na Maendeleo ya Jamii) Vicktoria Shayo ameeleza kuwa NCAA inaendelea kuboresha huduma utalii na kujitangaza katika majukwaa mbalimbali ndani na nje ya nchi kwa kushirikiana na wadau wa Utalii hali iliyowezesha eneo la hifadhi ya Ngorongoro pekee katika mwaka wa fedha 2023/2024 lilipokea wageni Watalii ni 908,627 ambapo Watalii wa ndani walikuwa 354,752 na watalii wa nje 553,875.

Kwa upande wake Kamishna Msaidizi Mwandamizi huduma za Utalii NCAA Mariam Kobelo amesema ili kuboresha huduma kwa wateja mamlaka hiyo inaendelea kuboresha miundombinu ya Tehama, mafunzo ya huduma kwa wateja na ukaribu kwa wageni na kuweka miundombinu rafiki katika mageti yanayoingiza wageni hifadhini ili wakifika maeneo hayo waatumie muda mfupi wa kupata huduma kwa ajili ya kuendelea na shughuli za utalii kwa wageni.

KAMPENI KUPINGA UKATILI DHIDI YA WATOTO NA WATU WENYE UALBINO




(ATFT) KWA KUSHIRIKIANA NA  HALMASHAURI YA KIBAHA MJI Yaendeleza kampeni yake ya  kupinga ukatili dhidi ya watoto na watu wenye mahitaji maalum, kwakutumia michezo na sanaa, kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka (18) na kuendelea, kama njia moja wapo ya kutoa elimu kwa jamii mbalimbali, ATIFITI CUP) Itakayo zinduliwa trh 23/08/2024 ikidhaminiwa vinywaji na kampuni U-FRESH, tarehe 20/07/2024, USHIRIKI WAKO NI MUHIMU  KUENEZA ELIMU TAJWA HAPO JUU.

AWESO AAHIDI KUONDOA CHANGAMOTO UKOSEFU MAJI KILUVYA




WAZIRI wa Maji Juma Aweso ameahidi kupeleka wataalamu Kata ya Kiluvya Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani ili kufanya tathmini ya maeneo yenye changamoto ya maji.

Aweso alitoa ahadi hiyo kwa njia ya simu kwenye mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti uliofanyika eneo la Kiluvya Madukani kutatua changamoto za wananchi.

Alisema atatuma timu yake leo Jumatatu ili wafanye kazi hiyo lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi hao wanapata maji na kuondokana na changamoto za ukosefu wa maji.

"Ombi lenu nimelisikia Jumatatu natuma timu itakuja kufanya tathmini kwa yale maeneo ambayo yana changamoto hivyo msiwe na wasiwasi tutatatua shida hiyo,"alisema Aweso.

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti alipiga simu ili kuwapatia majibu wananchi waliokuwa wakilalamika kukosa maji kwenye baadhi ya maeneo.

Magoti alisema kuwa wananchi wawe na uvumilivu kidogo kwani serikali inawasikiza na wanafanya kazi kwa kushirikiana na ndiyo sababu amempigia Waziri wa Maji.

Alisema kuwa suala la maji ni jambo muhimu sana hivyo lazima lishughulikiwe kwa uharaka ili kuondoa changamoto ambapo Rais Dk Samia Suluhu Hassan amedhamiria kumtua mama ndoo kichwani.

Kwa upande wake meneja wa DAWASA Emanuel Mbwambo alisema kuwa mpango uliokuwa ni mwezi wa Agosti kuhakikisha baadhi ya maeneo yenye changamoto yanafikiwa na huduma hiyo.

Mbwambo alisema kuwa baadhi ya maeneo ambayo yana changamoto ya ukosefu wa maji kwenye Kata hiyo.

Moja ya wananchi aliyejitambulisha kwa jina la Meri Charles mkazi wa eneo la Makurunge Majumba 6 alisema kuwa maji kwao hawana maji kabisa.

Charles alisema kuwa wao wanakunywa maji ya bwawani huku wanafunzi wakitakiwa kubeba maji lita tano kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya shuleni.


Sunday, July 21, 2024

JISAJILI KWENYE KANZI DATA KWA USALAMA WAKO.





Jeshi la Polisi Mkoani Pwani kwa kushirikiana  na Maafisa usafirishaji Wilaya ya Kibaha (bodaboda) limezindua zoezi la uvaaji viakisi mwanga katika Wilaya hiyo ili kuwezesha  kuwa rasmi na kuepuka kukumbwa na majanga mbalimbali ikiwemo kuporwa vyombo vyao vya moto.

Akizungumza katika uzinduzi huo,  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Pius Lutumo amewataka maafisa hao kuhakikisha wanajisajili katika kanzi data ili kutambulika wao na vijiwe wanavyofanyia kazi.

Amesema endapo wadau hao watajisajili kati kanzi data na kutii sheria za usalama barabarani ajali zitapungua kwa kiasi kikubwa, matukio ya wizi kwa kutumia Bodaboda yatakwisha na wahalifu wanaojificha kwa mgongo wa  bodaboda watadhibitiwa.

Lutumo amewakumbusha madereva waliosajiliwa kwenye kanzi data kutowaazima viakisi mwanga vilivyo na namba za utambulisho kwa wenzao ambao hawajajisajili kwani wanaweza kufanya matukio ya kihalifu na viakisi mwanga vikatumika kama utambulisho wa watuhumiwa hao kisha kuchukuliwa hatua za kisheria.

Kwa upande wake Katibu wa  Chama cha Maafisa Usafirishaji Wilaya ya Kibaha Mwinyichande Mungi amesema watatekeleza zoezi hilo kwa weledi na kuhakikisha kila anayetaka kufanya kazi hiyo anafuata taratibu ikiwa ni pamoja na kujisajili na kupata namba ya utambulisho.

Aidha mwenyekiti wa CCM Kata ya Kongowe Saimon Mbelwa amewataka madereva hao kutambua kazi yao ina mchango mkubwa kwa jamii hivyo wale wenye kuingia kwenye kazi hiyo kwa lengo la kufanya vitendo vya Uhalifu wanapaswa kupigwa vita na kufichuliwa.

MADEREVA WA SERIKALI PWANI WAKUMBUSHANA UWAJIBIKAJI




Na Mwandishi wetu, KIBAHA 

CHAMA cha Madereva wa Serikali Mkoa wa Pwani kimewakumbusha madereva kuwajibika katika majukumu yao Ili waweze kupata haki zao wanazostahili.

Mwenyekiti wa Chama hicho Michael Mbilinyi aliyasema hayo Julai 21 katika mkutano uliofanyika mjini Kibaha ambao ulihudhuriwa na viongozi wa chama hicho kutoka Halmashauri za mkoa wa Pwani .

Katika mkutano huo ambao ulilenga kujadili mambo mbalimbali ya chama uliambatana na semina elekezi ilivyokuwa ikielezea wajibu wa madereva wawapo kazini na mambo ya kufuata kabla hawajadai haki zao za msingi.

"Tutekeleze wajibu wetu halafu tutadai haki zetu za msingi, tuzingatie kufuata muda wa kazi na lugha sahihi pindi tunapokuwa na viongozi wetu utii na uwajibikaji utaondoa ukakasi wakati wa kudai haki," amesema Mbilinyi.

Mwenyekiti huyo amesema chama hicho ambacho uongozi wake ni kuanzia ngazi ya Taifa pamoja na mambo mengine kinatetea haki za madereva kwa mwajiri pindi anapoenda tofauti lakini pia dereva akienda kinyume wanamrudisha kwenye maadili.

Katibu wa chama hicho Isack Chambo aliwasisitiza wanachama kuzingatia michango waliyoiweka Ili kuendelea kuwa hai lakini pia kufanya mambo ambayo yapo ndani ya chama hicho kwa mujibu wa katiba yao.

Naye mmoja wa Wajumbe wa mkutano huo kutoka Halmashauri ya Chalinze Mkombozi Maskuzi ameomba viongozi wao kuwaandalia semina elekezi za mara kwa mara lakini pia waweatembelee kwenye maeneo yao huku wakizingatia kutoa taarifa sehemu zao za kazi Ili kuonyesha umuhimu wa nafasi zao.

Mjumbe mwingine aliyeshiriki mkutano huo Briton Kidinzi amewataka madereva kuwa mfano kwenye utendaji kazi wao mahala pa kazi kwa kufuata Sheria na maadili.


Mwisho