Tuesday, April 16, 2024
WANAOTUKANA VIONGOZI KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA
Sunday, April 14, 2024
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA PWANI YATOA SHUKRANI KWA CHUO CHA VETA MKOA WA PWANI KUWAPATIA USAFIRI KUSHIRIKI MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA 102 KUZALIWA KWA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA DODOMA
Katibu wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ndugu Omary Abdul Punzi kwa niaba ya uongozi ameshukuru chuo cha Veta Pwani kupitia Mkuu wa chuo hicho Madam Crala Kibodya kuwezesha safari hiyo kwa kutoa usafiri wa Coaster.
Ndugu Omary Punzi amesema huo ni uzalendo mkubwa kawa wadau nchini wasisite kusaidia katika shughuli nyingine.
Maadhimisho hayo yaliyofana yaliyohudhiliwa na Wananchi wengi wanafunzi na makundi mengine Mgeni Rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt Philip Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MWAKILISHI WA BALOZI WA UGANDA YAPONGEZA UBUNIFU WA TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA PWANI
Akipokeaa Tshirt hizo yeye na mke wake katika maadhimisho hayo ya miaka 102 ya kuzaliwa kwa Mwl Julius Kambarage Nyerere lililofanyika katika Ukumbi wa Mji wa Mtumba Mkoani Dodoma tarehe 13.4.2024
MEJA JENERALI BALOZI ANSELM BAHATI SHIGONGO ATUMA SALAMU ZA MKOA WA PWANI KONGAMANO LA MIAKA 102 YA KUZALIWA KWA MWALIMU NYERERE DODOMA

Mh Meja Jenerali Balozi Bahati ameyasema hayo katika maadhimisho ya kitaifa ya miaka 102 ya kuzaliwa kwa Mwl Julius Kambarage Nyerere yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mtumba Mjini Dodoma tarehe 13.4.2024 maadhimisho hayo yalihudhuliwa na Mh Daktari Philip Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Amewaomba wadau wa maendeleo nchini waende Mkoani Pwani kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda na shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
KIMITI AIPONGEZA SERIKALI YA AWAMU YA SITA YA MH DKT SAMIA SULUHU HASSAN RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Kimiti ameyasema hayo katika Maadhimisho ya kitaifa ya kumbukumbu ya miaka 102 ya kuzaliwa kwa Mwl Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika Ukumbi wa Mtumba tarehe 13.4.2024 mkoani Dodoma ambapo mgeni rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt Philip Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wananchi wengi waliojitokeza kushuhudia Maadhimisho ya kumbukumbu hiyo.
Kimiti amesema kuwa jambo hilo litasaidia kutunza Kumbukumbu za Mwasisi huyo wa Taifa kwa kufanya vijana na makundi mengine kwenda kujifunza pia itaongeza pato la Taifa akiamini watu wa mataifa mengi watakuja kujifunza mambo mbalimbali yaliyofanywa na Nyerere.
Saturday, April 13, 2024
JAMII YAASWA ISILE MALI ZA YATIMA
Thursday, April 11, 2024
SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MFUMO MPYA WA KIELETRONIKI WA UNUNUZI WA UMMA NeST
Na Wellu Mtaki, Dodoma
Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika ujenzi wa Mfumo mpya wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma unaojulikana kama National e-Procurement System of Tanzania (NeST) kabla ya uwekezaji huu.
Ununuzi wa umma ulikuwa ukifanyika kwa kutumia mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma uliojulikana kama Tanzania National e-Procurement System (TANePS) ambao ulijengwa na kampuni ya kigeni kutoka Ugiriki lakini Serikali ilibaini changamoto nyingi kwenye ununuzi uliokuwa ukifanyika kupitia mfumo wa TANePS ikiwemo taarifa zote za Ununuzi wa umma kuwa chini ya usimamizi wa kampuni ya kigeni nje ya nchi.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa kujenga uwezo wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA), Amin Mcharo wakati akizungumza na vyombo vya habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Jijini Dodoma, kuhusu mafanikio makubwa waliyopata katika miaka mitatu ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Amesema kuwa changamoto hii na nyinginezo zilipelekea uamuzi wa kuanzisha mfumo mbadala ambao utakuwa bora zaidi, wenye kuleta tija, unaojengwa na wataalam wa ndani na kusimamiwa na Serikali.
Aidha amewaasa wananchi kujisajili katika mfumoNeST na kuomba zabuni mbalimbali zinazotangazwa na Serikali ili kuweza kujipatia kazi na kuhakikisha anayeomba amekidhi vigezo vinavyotakiwa katika kuomba zabuni husika na pindi wanapopata zabuni wazifanye kwa uadilifu na ufanisi ili waendelee kuaminiwa katika miradi mingine kutokana zaidi ya asilimia 70 ya bajeti ya Serikali inatumika kwenye ununuzi wa umma.
Ikumbukwe kuwa PPRA imekuwa ikitekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa kuwahudumia wananchi ili kutimiza lengo la Serikali iliyopo madarakani ya kupeleka huduma kwa wananchi na kuchochea matumizi ya utafiti, sayansi na teknolojia na ubunifu kama nyenzo ya maendeleo, kama inavyoonyesha katika Sura ya kwanza,Kipengele cha 8(e) ya Ilani hiyo wakati sura hiyohiyo kipengele cha 8 (f) ikielezea kujikita katika kutengeneza ajira zisizopungua milioni 8 katika sekta rasmi na zisizo rasmi kwa ajili ya vijana.