Sunday, August 20, 2023

TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE YATOA SHUKRANI KWA WADAU MAANDALIZI NYERERE SUPER CUP

Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani inatoa shukrani Kwa Viongozi wote mliofanikisha safari yetu ya maandalizi ya NYERERE SUPER CUP Taasisi inashukuru 1.Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani 2.ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kibiti na Rufiji 3.Ofisi ya Mbunge Kibiti na Rufiji 4.Chama Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani COREFA 5.Chama cha Mpira wilaya Kibiti na Rufiji 6.Mdhamini Nssf na St David college Chuo Cha Afya kimara temboni,Madiwani wa Kibiti na Rufiji kuruhusu Viongozi wao kuhudhuria kikao na washiriki waliohudhuria UZALENDO NI KULIPENDA TAIFA LAKO MITANO TENA

*LYIDENGE ATAKA WAFANYAKAZI WA MIRADI KUWA NA NIDHAMU*

MKUU wa Polisi Wilaya ya Chalinze, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Sophia Lyidenge amewataka wafanyakazi wa mradi wa umeme wa serikali kuwa na nidhamu na kutokujihusisha na vitendo vya kihalifu.

Amebainisha hayo leo Agosti  20 alipotembela mradi huo wakati  akizungumza na wafanyakazi hao kuona kama wana changamoto zozote za kiusalama.

SSP Lyidenge aliwaeleza wafanyakazi hao kuwa wameaminiwa na serikali kufanya kazi hivyo wanatakiwa kuwa waadilifu na wasijihusishe na vitendo vya kihalifu ikiwemo wizi wa vitendea kazi na kuwataka wawe walinzi wa kwanza wa vifaa hivyo.

Sambamba na hayo SSP Lyidenge aliwasihi viongozi wa mradi huo kuwa na mahusiano mazuri na wafanyakazi ikiwemo lugha nzuri yenye staha ili kuongeza hamasa ya utendaji na kufikia malengo ya mradi kwa wakati uliokusudiwa.

"Niwaombe viongozi kuwatia moyo na kuwa na lugha shawishi kwa mnao wasimamia ili mradi huu uweze kukamilika kwa wakati, lugha zisizo na staha huwavunja moyo watendaji na kujikuta ikiwapunguzia morali ya kujituma". 

Sote tunatambua umuhimu wa mradi huu utakavyochochea maendeleo ya kiuchumi kwa kwa wakazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani na taifa kwa ujumla” alisema Lyidenge

CCM WAASWA KUFUATA UTARATIBU

 

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani wanaotoa misaada na kufanya shughuli za maendeleo wametakiwa kufuata utaratibu ili kuepusha mkanganyiko na viongozi waliochaguliwa na wananchi.

Hayo yalisemwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa Hamoud Jumaa wakati wa mkutano wa tathmini baada ya ziara ya CCM Kibaha Mjini.

Jumaa alisema kuwa kukisaidia chama siyo tatizo lakini kinachotakiwa ni utaratibu kufuatwa ili kusitokee tofauti baina ya wale wanaosaidia na wale waliochaguliwa.

"Tunajua kwa sasa ni kipindi cha kuelekea uchaguzi mwakani ni wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa na 2025 ni uchaguzi mkuu hivyo wanaotoa misaada ndani ya chama wafuate taratibu lakini siyo kosa kukisaidia chama,"alisema Jumaa.

Alisema chama kinasaidiwa na wanachama na wadau mbalimbali wana haki ya kufanya hivyo ili mradi wazingatie utaratibu uliowekwa na chama wa namna ya kuchangia.

"Chama kinajengwa na wanachama na wanaokichangia siyo tatizo hata mimi kwenye eneo langu nachangia lakini kwa kufuata utaratibu hivyo na wengine wafuate utaratibu wa chama,"alisema Jumaa.

Kwa upande wake mwentekiti wa CCM Kibaha Mjini Mwajuma Nyamka alisema kuwa utekelezaji wa ilani umefanyika kwa asilimia zaidi ya asilimia 90 ndani ya kipindi cha miaka miwili tu.

Nyamka alisema kuwa wanamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Kibaha fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo ambapo miradi mingi inaendelea na mingine imekamilika.

Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa kwa kushirikiana na serikali na wananchi wameendelea kukabili changamoto kwenye jimbo hilo.

Koka alisema utekelezaji wa ilani unaendelea vizuri na hakuna kilichokwama kila kitu kinakwenda vizuri lengo likiwa ni kuwaondolea changamoto wananchi na kutimiza malengo ya Rais.

Naye mwenekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Focus Bundala alisema kuwa wanaishukuru serikali kutoa kwa kuipatia Halmashauri kiasi cha shilingi bilioni 8.

Bundala alisema kuwa baadhi ya fedha zimetumika kwenye ujenzi wa shule sita za sekondari na shule tisa za msingi na miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na barabara, maji na afya.

COREFA YAZINDUA KITUO CHA SOKA KWA VIJANA KIBAHA


CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimezindua kituo cha michezo kwa vijana chini ya miaka 17 kikiwa na lengo la kuibua na kukuza vipaji vya vijana ndani ya mkoa huo.

Akizindua kituo hicho kwa Kanda ya Kaskazini kaimu mkuu wa wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema kuwa uwekezaji kwa vijana kutasaidia kuwa na timu bora za baadaye.

Magogwa ambaye ni katibu tawala wa wilaya (DAS) na mwenyekiti wa kamati ya michezo wa wilaya alisema kuwa serikali inaunga mkono suala la michezo kwani ni sehemu ya kutoa ajira kwa vijana.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Pwani Robert Munisi alisema kuwa malengo ya kuanzisha kituo hicho na vingine kwenye kila wilaya itakuwa na vituo vitatu ambapo kutakuwa na vituo 21 kwa mkoa mzima ni kuibua vipaji na kuviendeleza.

Naye mratibu wa kituo hicho Abdulakarimu Alawi alisema kuwa jumla ya vijana 500 wa shule za msingi na sekondari ambapo vijana wanacheza kutegemeana na umri wao.

JAMII IMETAKIWA KUPANDA MITI KWENYE MIRADI ILI KUHIFADHI MAZINGIRA

 

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Switbert Mkama ameitaka jamii kupanda miti kuzunguka maeneo yenye miradi ili kuhifadhi mazingira na kuifanya kuwa endelevu.

Amesema hayo alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa Mradi ya Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa Kutumia Mfumo Mfumo Ikolojia Vijijini (EBARR) katika Wilaya ya Kaskazini ‘A‘ Mkoa wa Kaskazini, Unguja - Zanzibar.

Akikagua visima, ujenzi wa majengo ya vituo vya wajasiriamali wa ufugaji, ushonaji, utengenezaji wa sabuni pamoja na vitalu nyumba katika Shehia za Jugakuu, Mbuyutende na Kijini, Dkt. Mkama amesema ameridhishwa hatua iliyofikiwa.

Aidha, aliwahimiza viongozi wakiwemo masheha wa shehia hizo ambazo zimefaidika na miradi ya visima kuwasimamia wananchi kupanda miti na kuimwagilia.

“Binafsi nimeridhishwa na namna mnavyosimamia miradi hii na nawapongeza masheha kwa kuisimamia na wananchi kwa kuipokea na kushiriki kikamilkfu katika kuitekeleza, niwaombe mhakikishe inaendelea kuwa na ubora ule ule,“ amesisitiza.

Kwa vile ujenzi wa majengo ya wajasiriamali wa ushonaji na uzalishaji wa sabuni utahusisha mashine na vifaa, Dkt. Mkama alisema ni muhimu kuwepo na mpango mkakati ili mradi uwe endelevu hata pale utakapokwisha muda wake.

Alisema vyerehani vitakavyotolewa pamoja na vifaa vingine vikiwemo taa na mabomba ya maji vitahitaji matengenezo madogo madogo na kulipiwa umeme hivyo wanajamii waangalie namna ya kuuhudumia bila kusubiri serikali.

Saturday, August 19, 2023

NYERERE SUPER CUP KUFANYIKA KIBITI NA RUFIJI KUANZA SEPT 23 MWAKA HUU

Katika kuelekea kumbukizi ya Miaka 23 ya kifo Cha Mwalimu Julius kambarage Nyerere na kuenzi FIKRA zake kwa vitendo Taasisi ya kumbukumbu ya mwalimu Julius Kambarage Nyerere Tarehe 19.8.2023 imefanya kikao cha maandalizi ya NYERERE SUPER CUP.

Wilaya ya Kibiti itashirikisha timu 6 Bungu Jaribu, Mtawanya, Kibiti, Mchukwi, na Dimani na Wilaya ya Rufiji timu 6 Ngorongo, Utete, Mgomba, Muhoro, Umwe na Mkongo.

Mashindano hayo yanatarajiwa kunaza Tarehe 23.9.2023 na kwisha 12.10.2023 tunashukuru 1.Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani 2.Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kibiti 3.Ofisi ya Mkuu wa Mkuu wa wilaya ya Rufiji 4.Ofisi ya Mbunge wa Kibiti na Rufiji 6.Madiwani wa Rufiji na Kibiti 7.Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani COREFA 8.Chama Cha Mpira wa Miguu Kibiti na Rufiji 9.Chuo Cha Afya St David college kimara 10. Mfuko wa NSSF Temboni na wadau wote kufanikisha Safari hii UZALENDO NI KULIPENDA TAIFA LAKO MITANO TENA

MNEC HAMOUD JUMAA ATAKA SUALA LA BANDARI RAIS ASISEMWE VIBAYA





MJUMBE wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) Hamoud Jumaa amevitaka baadhi ya vyama vya upinzani nchi kuacha kumsema vibaya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuhusu suala la mkataba wa Bandari badala yake watoe ushauri.

Jumaa aliyasema hayo Kata ya Mtambani Mlandizi Kibaha alipokuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa operesheni ya kuanza maandalizi ya uchaguzi ngazi ya serikali za vijini yenye kauli mbiu ya Simika Bendera.

Alisema kuwa anawashangaa wapinzani kutoa maneno mabaya kwa Rais kuhusu mkataba wa Bandari ambapo walipaswa kutoa ushauri na si kumsema vibaya.

"Suala la mkataba wa bandari ni jambo la msingi na Rais yuko makini na mkataba huo ili kuongeza mapato ya nchi na kama wao wanaona kuna jambo basi washauri na siyo kutoa maneno yasiyofaa,"alisema Jumaa.

Aidha alisema kuwa wanamshukuru Rais kwani ameonyesha uvumilivu mkubwa licha ya kusakamwa kuhusu suala la bandari ambalo mchakato wake bado unaendelea.

"Tumechoka kusikia Rais anasemwa vibaya yule ni kiongozi hivyo lazima aheshimiwe ila tunampongeza kwa ustaamilivu anaouonyesha kwani hawajibu licha ya kusemwa vibaya,"alisema Jumaa.

Aliwataka viongozi kuwajali viongozi wa ngazi za chini hususani mabalozi na viongozi wa mashina kwani wao ndiyo wako karibu na wanachama kwani ili kushinda uchaguzi kwani ndiyo malengo ya chama chochote.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Said Kanusu alisema kuwa anashangazwa na watu kutoa maneno kuwa eti bandari imeuzwa wapinzani wameishiwa hoja.

Kanusu alisema kuwa wananchi wawe na imani na wasikatishwe tamaa na wanaoleta hoja zisizo na msingi ajenda ya nchi ni kuleta maendeleo na miradi.

Naye Diwani wa Kata ya Mtambani Godfrey Mwafulilwa alisema kuwa kauli mbiu hiyo ni kuimarisha ngazi ya chini ya mabalozi kuwapa nguvu kwani wanakazi kubwa kukiimairisha chama.

Mwafulilwa alisema kuwa ngazi ya msingi sana ni balozi ambapo chama kinarudi chini ambako huko ndiko kwenye wanachama na hoja za wanachama na wananchi.

Alisema kuwa Rais ni mvumilivu na hawavutiwi na tabia inayofanywa na watu wanamchafua wao wanapaswa kuja na hoja na ushauri ila siyo kumchafua.