HALMASHAURI ya wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani imewapatia Pikipiki watendaji wa Kata tano ili kuondoa changamoto ya kushindwa kuyafikia maeneo ambayo hayafikiki kirahisi.
Wednesday, March 1, 2023
WATENDAJI KATA WAKABIDHIWA PIKIPIKI
WALIMU KUZAWADIWA VIWANJA
KATIKA kuhakikisha wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne hawapati sifuri Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amesema itatoa viwanja kwa walimu shule zao zitakazofanya vizuri.
Tuesday, February 28, 2023
IRUWASA YAONGOZA KUFUNGA MITA ZA MAJI KABLA YA MALIPO
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MAMLAKA ya Maji na Usafi wa Mazingira Iringa (IRUWASA) imevunja rekodi kwa kuongoza nchini kwa kufunga mita 6,752 za malipo ya Maji Kabla ambazo zimekuwa suluhisho na kupunguza idadi ya wadaiwa sugu wa ankra za maji.
Akizungumza Jijini Dodoma Mkurugenzi Mtendaji wa IRUWASA, David Pallangyo amesema, Mamlaka hiyo iliyoanza daraja C hadi sasa ipo daraja A na inajitegemea gharama za matengenezo na uendeshaji na sehemu ya uwekezaji, imefanikiwa katika eneo la TEHAMA kwa kufunga mita za malipo kabla kwa wateja hao.
Pallangyo amesema kuwa kutokana na kufunga mita za malipo kabla kwa viongozi wa serikali na taasisi mbalimbali, kumepunguza ongezeko la madeni ya watumiaji maji bila kulipa na kubaki deni la shilingi bilioni mbili ambalo wadaiwa wengi ni watu wa kawaida.
Amesema kuwa mamlaka hiyo pia imevuka lengo la Sera ya Maji ya 2002 na Ilani ya CCM ya kutoa huduma ya usambazaji maji kwa mji wa Iringa na maeneo ya pembezoni kwa kuunganisha wateja 40,459 sawa na asiimia 97 ya wakazi ambazo ni zaidi ya asilimia 95 zinazoelekezwa kwenye sera na Ilani.
Aidha amesema kuwa katika mpango wa muda mrefu, Serikali kupitia IRUWASA inakusudia kutekeleza mradi mkubwa wa uboreshaji huduma ya majisafi na majitaka katika manispaa ya Iringa, miji ya Kilolo pamoja na baadhi ya vijiji kando ya bomba la maji litakapopita.
"Mradi huu unalenga kuanzisha chanzo kipya katika mto Mtitu uliopo Wilaya ya Kilolo utaongeza upatianaji wa maji ya kutosha kwa miaka 20 ijayo na utaongeza utoaji wa majitaka zaidi ya asilimia 30 ya wakazi wa Iringa kutoka asilimia 6.8 za sasa,"amesema Pallangyo.
Ameongeza kuwa mradi huo utekelezwa kwa ushirikiano wa serikali kupitia mkopo wenye masharti nafuu kutoka serikali ya Korea wa dola za Kimarekani milioni 88.4 utaanza kutekelezwa Mei 2023 na ujenzi utaanza Aprili 2024 na utakamilika 2027.
Amesisitiza kuwa mradi utakapokamilika huduma za maji safi na salama kwa miji ya Iringa, Kilolo na Ilula zitafikia asiimia 100 kwa saa 24 kwa siku saba.
Jumla ya wananchi 456,010 watanufaika na huduma ya majisafi hadi mwaka 2045, huku wananchi 141,543 watanufaika na huduma ya uondoaji majitaka na Watanzania 6,455 watanufaika na kazi za mikataba na utachangia uchumi na ustawi wa jamii.
Thursday, February 23, 2023
MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO KUONGEZA UWEZO WA MAWASILIANO
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MAMLAKA ya serikali Mtandao (eGA) imepanga kupanua uwezo wa Mtandao wa mawasiliano serikalini ( Government Network) na kuufikisha wilaya zote nchini Ili kurahisisha utekelezaji wa jitihada za serikali Mtandao na kuwafikishia huduma wananchi wote popote walipo.Hayo yamesemwa na Mkurugezi mkuu wa mamlaka ya serikali mtandao Mhandisi Benedict Ndomba wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa mamlaka hiyo.
Ndomba amesema kuwa mfumo wa ubadilishaji taarifa serikalini imewezesha zaidi ya taasisi 50 kubadilishana taarifa kupitia mfumo huo na amezitaka taasisi za umma ambazo hazijaunganishwa katika mfumo huo ziunganishwe Ili ziweze kubadilishana taarifa na taasisi nyingine pale inapohitajika.
"Jumla ya taasisi 200 zinatumia mfumo wa ofisi Mtandao kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi katika taasisi za umma pia umesaidia kupunguza matumizi ya karatasi kutunza mazingira na kuokoa fedha za serikali,"alisema Ndomba.
Serikali mtandao ni matumizi ya Teknolojia ya habari na mawasiliano ( TEHAMA) Katika utendaji kazi wa taasisi za umma na utoaji wa huduma kwa wananchi wenye lengo la kuongeza ufanisi wa utendaji kazi Katika taasisi ya umma pamoja na kuboresha utoaji huduma kwa umma Ili huduma hizo zipatikane kwa urahisi haraka na gharama nafuu.
WASIOENDELEZA ARDHI KUNYANGANYWA
NAIBU Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete amezitaka Serikali za Vijiji kuorodhesha majina ya wawekezaji ambao wamehodhi ardhi bila kuiendeleza ili irudishwe kwa ajili ya matumizi mengine.
TANESCO KUONGEZA UZALISHAJI UMEME
Na Mwandishi Wetu Dodoma
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) linatarajia kuzalisha megawati 5,000 kupitia miradi mbalimbali ifikapo kwa mwaka 2025 hivyo kuongeza uzalishaji umeme kupitia gridi ya Taifa.
Hayo yamesemwa na kaimu Mkurugezi wa huduma kwa wateja wa shirika la umeme Tanzania ( TANESCO) Martin Mwambene wakati akielezea utekelezaji wa shughuli mbalimbali ya shirika hilo na uelekeo wake kwa mwaka wa 2023 .
Mwambene amesema kuwa kwa sasa shirika hilo lina uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 1,820 wakati mitambo iliyopo ina uwezo wa kuzalisha megawati 1,300 pekee.
Amesema kuwa TANESCO kwa kutambua matatizo ya umeme yaliyopo nchini imekuja na mradi wa Gridi Imara ambapo katika bajeti ya mwaka huu imetengewa shilingi bilioni 500 kwa ajili ya kuanza utekelezaji wake.
"Katika mradi wa Grid Imara utajumuisha ununuzi wa mashine umba 6000, mita 700,000 za umeme, nguzo 380,000 ununuzi na ufungaji wa nyaya zenye urefu wa km 40,000, ujenzi wa njia za kusafirisha umeme mkubwa takribani kilomita 948 na ujenzi wa vituo 14 vya kupooza umeme,"amesema Mwambene.
Aidha amezungumzia pia maendeleo ya ujenzi katika Bwawa la Mwalimu NYerere kuwa upo katika asilimia 88 na zoezi la uwekaji maji limefikia mita za ujazo 133 kutoka usawa wa bahari