BENKI ya inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya kuchangia shughuli za maendeleo kwa mwaka wa 2025.
Monday, March 31, 2025
NMB KUTUMIA ZAIDI YA BILIONI 6 MIRADI YA MAENDELEO
Sunday, March 30, 2025
WAZIRI MKUU MAJALIWA AUPIGIA DEBE UWANJA WA SHIRIKA LA ELIMU KIBAHA KUTUMIWA NA TIMU ZA CHAN NA AFCON
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameupigia debe uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha kutumiwa na Timu za Taifa zitakazokuwa zinajiaandaa na michuano ya CHAN na AFCON kwa ajili ya mazoezi.
WAZIRI MKUU MAJALIWA ARIDHISHWA MAANDALIZI UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU PWANI 2025
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea kuangalia maandalizi ya uwanja utakaotumika kuzindua mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2025 mkoani Pwani.
Majaliwa alitembelea uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha kuangalia maandalizi ya uzinduzi huo na kuridhishwa na maandalizi hayo na kutaka wakamilishe sehemu ambazo bado hazijakamilika.
Alisema kuwa ameridhishwa na maandalizi hayo ambapo pia alitumia muda huo kutembelea watoto wa halaiki na kusema amefurahishwa na jinsi walivyokuwa na hamasa ya uzinduzi huo.
"Nawapongeza kwa maandalizi mnayoendelea nayo nimeridhishwa kamilisheni sehemu zilizosalia ili kukamilisha mapema,"alisema Majaliwa.
Alisema kuwa amefurahishwa kuona viongozi wakiwemo mawaziri na makatibu wakuu wakiwa mstari wa mbele kuhakikisha maandalizi yanakuwa mazuri.
"Alikeni hata mikoa ya jirani Dar es Salaam, Morogoro na Tanga na watu mbalimbali kwani hili ni jambo la kitaifa shirikisheni wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ili hamasa iwe kubwa,"alisema Majaliwa
Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Watu Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete maandalizi yako vizuri ila baadhi ya maeneo ikiwemo katikati ya uwanja ndiyo kunahitaji marekebisho kidogo.
Kikwete alisema kuwa mialiko kwa wageni mbalimbali imetolewa ikiwa ni pamoja na wakuu wa mikoa, wakurugenzi na watu wengine ili kushiriki uzinduzi huo.
Friday, March 28, 2025
VIJANA WAFUNDISHWE UMUHIMU WA MBIO ZA MWENGE

Wednesday, March 26, 2025
MAKAMU WA RAIS DK MPANGO KUZINDUA MBIO ZA MWENGE KITAIFA PWANI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya juu ya uzinduzi huo amesema kuwa maandalizi ya uzinduzi yanaenda vizuri.
Kikwete amesema kuwa tayari Makamu wa Rais ameshathibitisha kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo wa mbio za Mwenge kwa mwaka 2025.
"Kwa vitu vilivyobakia niwaombe mhakikishe vinafika kwa wakati ili kila kitu kiwe kwenye sehemu yake na bado tutaendelea kuangalia maandalizi ili siku hiyo mambo yawe mazuri,"amesema Kikwete.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maandalizi yako vizuri ambapo hadi Machi 29 mambo mengi yatakuwa yamekamilika.
Kunenge amesema kuwa huduma zote zitapatikana kuanzia suala la afya, vyoo, maji, taa kubwa, umeme ambapo kutakuwa na jenereta endapo umeme utakatika.
Amewataka wananchi wa Mkoa huo na mikoa jirani na Watanzania kwa ujumla kujitokeza siku hiyo ili kuweka historia ya Pwani kuzindua mbio za Mwenge Kitaifa.
Tuesday, March 25, 2025
JK AWASILISHA UJUMBE MAALUMU KWA RAIS WA SENEGAL KUTOKA KWA RAIS SAMIA
Mhe. Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewasilisha ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Senegal, Mhe. Bassirou Diomaye Faye jijini Dakar.
Katika mazungumzo yao ya kirafiki, Rais Mstaafu alieleza dhamira ya dhati ya Rais Samia na Serikali anayoiongoza ya kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia, kiuchumi na kijamii kati ya Tanzania na Senegal.
Pamoja na masuala ya ushirikiano wa kiserikali, Rais Mstaafu pia alisisitiza umuhimu wa kukuza uhusiano baina ya wananchi wa mataifa haya mawili kupitia sekta za elimu, biashara, utalii, na maendeleo ya vijana na wanawake.
Ziara hii ni sehemu ya juhudi endelevu za Tanzania kuimarisha uhusiano wa kimataifa na mataifa ya Afrika Magharibi, huku ikiweka msisitizo kwa diplomasia ya uchumi na ushirikiano wa watu kwa watu.
MAANDALIZI UWASHWAJI MWENGE WA UHURU KITAIFA PWANI MBIONI KUKAMILIKA
Thursday, March 20, 2025
TANROADS YATOA UFAFANUZI LORI LILILOZIDISHA UZITO MIZANI YA VIGWAZA.
WAKALA wa Barabara Tanzania (TANROADS) imetoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ya lori la mizigo lililokamatwa kwenye mizani ya Vigwaza kuwa taratibu za kulikamata lori hilo ulifuatwa.
TCRA KUSHIRIKIANA NA TBN KUSADIA KUZALISHA MAUDHUI YENYE TIJA
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeahidi kufanyakazi na Mtandao wa Wana Blogu Tanzania (TBN) pamoja na vyama vingine vya waandishi wa habari ambavyo vinawakilisha mahitaji na matakwa ya wanachama wao.
Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 19 Machi 2025 Jijini Dar es Salaam na Meneja wa Huduma za Utangazaji wa TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka, alipokutana na ujumbe wa TBN ofisini kwake, katika kikao cha kujadiliana changamoto mbalimbali zinazowakabili Bloga nchini.
“Sisi huwa tunapenda kufanya kazi na vyama ambavyo vinawakilisha mahitaji na matakwa ya wanachama wao, badala ya kufanyakazi na mwaandishi mmoja mmoja…tunafurahi sana kufanyakazi na waandishi kupitia vyama vyao,” amesema Mhandisi Kisaka.
Mhandisi Kisaka amesema kuwa TCRA imefurahi kukutana na TBN kwa kuwa wanafahamu kuwa Bloga wanasehemu kubwa sana kwenye maudhui ya ndani, na hata kwenye usajili wa TCRA Bloga wanachukua nafasi kubwa sana katika maudhui ya mtandaoni.
“Kwa hiyo TBN mtakuwa silaha moja wapo nzuri sana yakutuwezesha sisi kama Mamlaka ya Mawasiliano nchini, tunao simamia utangazaji pamoja na maudhui ya mtandaoni kuwa karibu na nyinyi na kuhakikisha maudhui ya mtandaoni yanaleta tija na maendeleo kwa wananchi,” amesema Mhandisi Kisaka.
Friday, March 14, 2025
RAIS MSTAAFU DK KIKWETE AFANYA ZIARA NCHINI JAPAN KUIMARISHA USHIRIKIANO KATI YA BODI YA SHIRIKA LA ELIMU LA KIMATAIFA (GPE) NA JAPAN
Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Elimu la Kimataifa (GPE), yupo Tokyo nchini Japan kwa ziara maalum yenye lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya GPE na serikali ya Japan katika kutatua changamoto za elimu ya msingi katika nchi zinazoendelea.
Katika siku yake ya kwanza Tokyo, Dkt. Kikwete amefanya mazungumzo na Waziri wa Fedha wa Japan, Mhe. Shin-ichi Yokohama, pamoja na Naibu wake, Mhe. Atsushi Mimura.
Mazungumzo hayo yalijikita katika ushirikiano wa kifedha ili kusaidia miradi ya elimu inayosimamiwa na GPE, ikiwemo upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wa nchi zinazoendelea.
Baada ya mazungumzo hayo, Rais Mstaafu Kikwete alikutana na Bw. Akihiko Tanaka, Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA).
Shirika hili limekuwa na mchango mkubwa katika miradi ya maendeleo barani Afrika, na mazungumzo yalihusu namna JICA inaweza kusaidia jitihada za GPE katika kukuza elimu bora.
Dkt. Kikwete pia alikutana na Bw. Yohei Sasakawa, Mwenyekiti wa Taasisi ya Nippon. Bw. Sasakawa, mwenye umri wa miaka 86, ni mtu mashuhuri wa kusaidia miradi ya kijamii duniani.
Katika mazungumzo yao, waligusia nafasi ya sekta binafsi katika kusaidia elimu, hasa kupitia taasisi zisizo za kiserikali. Vilevile, Bw. Sasakawa alishangaza dunia baada ya kufanikisha kupanda Mlima Kilimanjaro tarehe 12 Februari 2024, kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 85 ya kuzaliwa kwake – hatua inayothibitisha kuwa umri si kikwazo kwa ndoto kubwa.
Katika siku zinazofuata, Rais Mstaafu Kikwete anatarajiwa kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. T. Miyaji, pamoja na wabunge wa Bunge la Japan, ambapo ajenda kuu itakuwa nafasi ya elimu na teknolojia katika maendeleo ya jamii.
Pia, atashiriki mijadala maalum kuhusu elimu na teknolojia, kufanya mahojiano na vyombo vya habari, pamoja na kukutana na Mhe. Tetsuro Yano, Rais wa Taasisi ya AFRECO, ambayo inahusika na kukuza ushirikiano kati ya Japan na Afrika.
Ziara hii ni sehemu ya juhudi endelevu za Dkt. Kikwete katika kuboresha mifumo ya elimu duniani, hasa katika nchi zinazoendelea.
Japan ni mshirika muhimu wa maendeleo ya elimu barani Afrika, na ushirikiano huu unaweza kuwa na mchango mkubwa katika kuhakikisha watoto wengi zaidi wanapata fursa ya elimu bora.
Thursday, March 13, 2025
KIWANDA CHA KEDS CHATOA MSAADA KWA WANAWAKE
KIWANDA cha kuzalisha sabuni cha Keds Tanzania Company Ltd cha Kibaha Mkoani Pwani kimetoa misaada ya sabuni kwa wanawake wa Mtaa wa Lulanzi ambao uko jirani na kiwanda hicho ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe ya siku ya wanawake Duniani.
KEDS KUENDELEA KUZALISHA BIDHAA BORA
KIWANDA cha Keds Tanzania Company Ltd kimesema kitaendelea kuzalisha bidhaa zenye ubora na bei nafuu kulingana na hali ya soko.
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA (THBUB) YATEMBELEA VIWANDA PWANI
Wednesday, March 12, 2025
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA (THBUB) INAFANYA ZIARA KWENYE VIWANDA MKOANI PWANI KUANGALIA UZINGATIWAJI WA HAKI ZA BINADAMU
Wednesday, March 5, 2025
DOWEICARE YATOA YATOA MSAADA WA FEDHA UJENZI WA DARAJA LULANZI
WATAALAMU UDSM WAKUTANA NA VIONGOZI TBN

Hatua hiyo ya kukusanya maoni imekuja kufuatia wataalamu hao kuagizwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambayo ipo katika utafiti maalum kwa nia ya dhati kuboresha Sera na kanuni zake mbalimbali katika eneo hilo la majukwaa ya mtandaoni.
Kikao hicho kimefanyika kwa mafanikio katika ofisi za TBN zilizopo kwa Aziz Ali, Temeke, watafiti hao wamechukua maoni ya TBN Makao Makuu, wakisema pia watafika katika Ofisi za Kanda za TBN.
Akizungumza Katibu Mkuu wa TBN Khadija Kalili amesema TCRA imefanya uamuzi sahihi kukutana na wadau wake kwa kupitia wataalamu hao kwani maoni yao yatawapa picha halisi juu ya tasnia ya habari na blogging kwa ujumla wake.
Amesema kilio kikubwa cha wana TBN ni gharama za usajili na tozo ya leseni kiasi ni kikubwa ambacho kwa uhalisia wengi bado hawamudu kulipia.
Amesema hali hiyo imefanya idadi kubwa ya wana TBN kushindwa kumudu kuendesha mitandao yao kutoka 300+ waliokuwapo kwanza hadi kufikia 100+ tu wanaoweza kulipia na kwa kusuasua.
Ameshauri pia TCRA kuendeleza utamaduni wa kukutana na wadau wake ikiwamo kwa mafunzo ya kuwaimarisha uwezo wao pamoja na kuangazia athari za gharama za bando za mtandao na vifaa.
Amesema ikiwa sekta ya blogging ndani ya tasnia ya habari ikisimamiwa vizuri kwa ushirikiano wa karibu na TCRA ni wazi kwamba Tanzania itanufaika na maudhui bora na yenye viwango ambayo yatasaidia kulinda maadili ya jamii yetu.
TBN yenye wanachama 300 waliopo wanaendesha mitandao kwa kusuasua kutokana na ada na tozo.
Watalaam hao walionesha kushangazwa na kuwapo kwa Chama Cha Bloggers chenye usajili kamili na wanachama zaidi ya 300, na pia wakaelewa bloggers ni tofauti na jumuiya zingine za waandishi wa mitandao ambao hawana blogs.
Wataalamu hao ni pamoja na Prof. Siasa Mzenzi, Dkt. Patrokil Kanje , Dkt. Said Suluo.
Wengine ni Mjata Daffa , Ally Mshana na Viongozi na wajumbe wa TBN, wakiongozwa na Katibu Mtendaji Khadija Kalili , Beda Msimbe na Rahel Pallangyo.
Mwisho
DOWEI CARE YATOA MSAADA WA FEDHA UJENZI WA DARAJA LULANZI
Monday, March 3, 2025
VYAMA SITA RAFIKI KUSINI MWA AFRIKA VISIYUMBISHWE VISIMAMIE SHABAHA YA KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO

Hayo yalisemwa jana kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Mjini Kibaha na Makamu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Steven Wassira wakati akifungua mafunzo kwa viongozi wa vyama hivyo.
Wassira alisema kuwa baadhi ya nchi duniani havipendi kuona vyama hivyo vinaongoza wao wanaona demokrasia ni kuviondoa vyama hivyo madarakani.
"Mabadikiko ni mengi duniani lakini yasivitoe vyama vyetu kwenye shabaha yake ya msingi ambayo ni maisha bora na mazuri kwa wananchi huu ndiyo msingi wa vyama hivi,"alisema Wassira.
Alisema kuwa hiyo ndiyo misingi iliyowekwa na waasisi wa mataifa hayo ambayo yalipigania Uhuru wa nchi zao na kuacha misingi imara ambayo inapaswa kufuatwa.
Kwa upande wake Katibu wa masuala ya siasa uhusiano wa kimataifa na Halmashauri Kuu ya CCM NEC Rabia Hamidu alisema kuwa nchi hizo zinapaswa kuonyesha umoja wao ili kuzisaidia nchi za Afrika.
Naye Naibu Mkurugenzi wa idara ya masuala ya Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na idara ya kimataifa ya kamati kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na mkuu wa ujumbe wa IDPC Zhang Yanhong alisema kuwa ni jambo zuri kwa ushirikiano wa vyama hivyo sita na CPC.
Naye Mkuu wa Shule ya Mwalimu Julius Nyerere Profesa Marcelina Chijoriga alisema wanatoa mafunzo kwa viongozi wa vyama vya siasa, taasisi za umma na serikali pamoja na taasisi za watu binafsi.
SERA YA TAIFA YA MAENDELEO YA VIJANA 2007 YAENDELEA KUNADIWA
Kwa ajili ya Kuinadi na kuineza Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana
Amemtembelea Mheshiwimiwa Godfrey Eliakimu Mzanva Mkuu wa Wilaya ya Moshi kwa ajili ya kumpongeza kwa Kuaminiwa na Mheshiwimiwa Dk Samia Suluhu Hasani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya.
Unakumbuka kuwa Mheshiwimiwa Godfrey Eliakimu Mzanva ni miongoni mwa wakimbiza mwenge mwaka 2024 waliofanya vizuri katika kuendesha Makongamano ya vijana.
Aidha mazungumzo hayo yalitoa mwafaka wa Kuandaa Kongamano la Vijana Kuhusu Umuhimu wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Ambalo litajikita zaidi kuelezea historia ya Tanzania, Itifaki, Maadili na Uzalendo kwa Vijana,Madhara ya matumizi ya madawa ya kulevya, utunzaji wa Mazingira na Fursa zinatopatikana Wilaya ya Moshi Mkoa wa Kilimanjaro