HALMASHAURI ya Mji Kibaha imeitaka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) Kibaha kufanya utaratibu wa kupeleka maji kwenye Hospitali ya Wilaya ya Lulanzi ambapo ni miezi mitatu imepita tangu kutolewa hela kiasi cha milioni 60.
Wednesday, January 31, 2024
DAWASA YATAKIWA KUPELEKA MAJI HOSP YA WILAYA LULANZI
Wednesday, January 17, 2024
WATUHUMIWA KUKUTWA NA NOTI BANDIA NA MASHINE YA KUZITENGENEZEA
WATU wanne wakazi wa Jijini Dar es Salaam wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Pwani kwa tuhuma za kukutwa na noti bandia zenye thamani ya shilingi milioni 1.5.
Saturday, January 13, 2024
KATA YA MISUGUSUGU YAOMBA WADAU UKAMILISHWAJI JENGO LA WAZAZI
KATA ya Misugusugu Wilayani Kibaha Mkoani Pwani imeomba wadau mbalimbali kuwachangia kiasi cha shilingi milioni 39 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa jengo la mama na mtoto ili kuwaepusha wajawazito kujifungulia majumbani.
BUNGE SC KUCHUANA NA BUNGE LA WAWAKILISHI SC
Kombaini ya Wachezaji wa Bunge SC na BLW SC Katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Maspika wa Bunge Mhe. Dkt Tulia Ackson na Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe Zubeir Ally Maulid Kabla ya mchezo wa Kombaini Hiyo na NMB. NMB waliibuka washindi kwa magoli 7-2. Leo Jumamosi tarehe 13.01.2024 Bunge SC itavaana na BLW Katika mchezo wa utangulizi kabla ya fainali ya Mapinduzi Cup
Friday, January 12, 2024
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE MKOA WA PWANI YATOA MISAADA KWA WAFUNGWA
KATIBU wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani Ndugu Omary Punzi ametuma salamu za Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Taifa Mhe.Paul Petro Kimiti na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Taasisi Mhe.Mizengo Peter Pinda (Waziri Mkuu Mstaafu) kwa kutoa misaada mbalimbali kwa wafungwa.
KATA PICHA YA NDEGE YAISHUKURU SERIKALI KUWAPATIA MILIONI 340 UJENZI MADARASA PICHA YA NDEGE SEKONDARI
KATA ya Picha ya Ndege imefanikiwa kuongeza madarasa 17 kwenye Shule ya Sekondari Picha ya Ndege ambayo awali ilikuwa na madarasa sita lakini kwa sasa ni madarasa 23 ambapo zimetumika kiasi cha shilingi milioni 340 kwa madarasa hayo yaliyoongezeka.
Thursday, January 11, 2024
WATANZANIA WATAKIWA WAPANDE MITI KULINGANA NA UMRI WAO
WATANZANIA wametakiwa kuadhimisha siku za kumbukumbu zao za kuzaliwa kwa kupanda miti kutokana na umri wao ili kukabili mabadiliko ya tabianchi.
Monday, January 8, 2024
HALMASHAURI YAWATAKA WAVAMIZI SHAMBA LA MITAMBA KUONDOKA.
HALMASHAURI ya Mji Kibaha imewataka wavamizi waliovamia Shamba la Mitamba namba 34 kuondoa maendelezo waliyoyafanya kabla ya zoezi la kuwaondoa kufanyika ili wasipate hasara.
Saturday, January 6, 2024
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE MKOA WA PWANI INATARAJIA KUJENGA KITUO WATOTO WANAOISHI KWENYE MAZINGIRA MAGUMU
Monday, January 1, 2024
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE PWANI YATOA VYETI VYA PONGEZI KWA WADAU
TAASISI ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mkoa wa Pwani imetoa vyeti vya shukrani kwa vyombo vya habari na wadau mbalimbali ambao ilishirikiana nao katika shughuli zake za maendeleo.
Akikabidhi vyeti hivyo hakimu mkazi mstaafu mkoa wa Pwani Stephen Mbungu amewataka waandishi wa habari na wadau kudumisha amani kwa kuzingatia maadili ya nchi.
Naye naibu katibu mkuu wa taasisi hiyo Neema Mkwachu alisema kuwa moja ya kazi zao ni kufundisha maadili kwa Watanzania ili nchi iendelee kuwa na amani.
Naye Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dk Abdulsalaam Omar alisema kuwa wanashirikiana na taasisi na mashirika katika utoaji huduma ikiwa ni sehemu ya kuleta maendeleo.
Mwakilishi wa kamishna wa uhifadhi wa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) Mathew Ntilicha aliwataka wananchi kulinda mazingira kwa kupanda miti na ufugaji wa nyuki.
Meneja wa Shirika la Ugavi la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Pwani Mhandisi Mahawa Mkaka alisema kuwa wataendelea kushirikiana na taasisi hiyo ili iendelee kuihudumia jamii.
Mwenyekiti wa (CCM) Mkoa wa Pwani Mwinshehe Mlao alisema kuwa elimu inapaswa kutolewa kwa viongozi wakiwemo madiwani na viongozi wa umma kwani baadhi hawana maadili mazuri.
Mhamasishaji wa taasisi hiyo kitaifa Jirabi alisema kuwa lengo kuu ni kuwaunganisha Watanzania ili kujua falsafa za Nyerere ambaye alikuwa akipambana na adui watatu wa Taifa ambao ni Ujinga, Maradhi na Umaskini.
Kwa upande wake katibu wa taasisi hiyo Mkoani Pwani Omary Punzi alisema kuwa wamefanya hafla hiyo ikiwa ni sehemu ya kutoa shukrani kwa wadau mbalimbali ambao imeshirikiana nayo katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.