Saturday, March 4, 2017

MAPAMBANO DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA WATANZANIA WATAKIWA KUUNGA MKONO MAPMBANO



Na John Gagarini
WATANZANIA wametkiwa kuunga na serikali ya awamu ya tano katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya na matumizi ya pombe za viroba kwa kutowajengea chuki wale wanaokabili suala hilo.
Hayo yalisemwa na Kuhani mkuu wa Kituo cha Maombi na Maombezi cha Gombo Gambusi Alista Albano kilichopo Kibamba Jijini Dar es Salaam na kusema kuwa vita hiyo ni ya wananchi wote ili kuwanusuru Watanzania.
Albano alisema kuwa dawa hizo na pombe hiyo imewafanya watumiaji kudhurika na kushindwa kufanya kazi zao kikamilifu ambapo baadhi wamejikuta wakiwa wagonjwa na wengine kufikia hatua ya kupoteza maisha.
“Tumuunge mkono Rais wetu Dk John Magufuli katika vita hii ambayo imepewa nguvu na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda lakini kuna abaadhi ya watu wameonekana kupingana na mapambano hayo jambo ambalo linashangaza,” alisema Albano.
Alisema kuwa athari ya matumizi ya dawa na pombe hizo ni makubwa tofauti na watu wanavyofikiria ambapo nguvu kazi kubwa imeathirika na kushindwa kuzalisha kutokana na matumizi hayo.
“Sisi kama kaanisa tunapaswa kuliombea Taifa ikiwa ni pamoja na viongozi wetu ambao wanajaribu kuhakikisha wanatuletea maendeleo lakini kwanza wanaondoa vikwazo vilivyokuwa vinazuia nchi ishindwe kupiga hatua ikiwemo dawa na pombe hizo,” alisema Albano.
Aidha alisema Magufuli ni moja ya viongozi ambao ni bora na wataleta mabadiliko makubwa ya nchi na kuifanya Tanzania kuwa nchi ambayo itazalisha na kutoa misaada tofauti na ilivyo sasa imekuwa nchi ya kuomba wahisani.
“Hamasa yake ya kuifanya Tanzinia kuwa nchi ya viwanda itafanya nchi kuwa na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali hivyo itasababisha uchumi kukua na kuwa moja ya nchi zitakazokuwa zinatoa misaada kwa nchi nyingine,” alisema Albano.
Alibainisha kuwa nchi kwa sasa inapita kwenye kipindi cha mpito lakini baadaye kila mwananchi atafurahia maisha kwani anarejesha vile ambavyo viliporwa na watu wachache ili viweze kutumiwa na watu wengi.
“Ninachowaomb Watanzania wenzangu tuache kulalamika kwani tumebakia kulalamika badala ya kufanya kazi kwani malamiko hayataweza kutusaidia badala yake yatatufanya tusiwajibike,” alisema Albano.
Alisisitiza kuwa Rais Magufuli ni mkombozi wa Taifa hili hivyo watu wamwombee katika kuirekebisha nchi na kuiweka katika mazingira mazuri ya kutoa huduma nzuri kwa wananchi wake.
Mwisho.

   

No comments:

Post a Comment