Saturday, March 4, 2017

HABITAT FOR HUMANITY TANZANIA YAKARABATI VYOO KIBWEGERE

 Ofisa Elimu Vifaa na Takwimu Halmashauri ya Ubungo Hussein Masoud akiongea wakati wakukabidhi vyoo vya shule ya Msingi ya Kibwegere kata ya Kibamba wilaya ya Ubungo Jijini Dar es Salaam vilivyokarabatiwa na Shirika la Habitat For Humanity Tanzania, kushoto ni mkurugenzi wa shirika hilo Danny Mpogole na kulia ofisa elimu kata ya Ubungo.  

 Ofisa Elimu kata ya Ubungo Jijini Dar es Salaam katikati akiongea kushoto ni ofisa elimu vifaa na Takwimu Halmashauri ya Ubungo Hussein Masoud na kulia mwalimu mkuu shule ya Msingi Kibwegere kata ya Kibamba wilaya ya Ubungo  Maragareth Mkwekwe wakati wa kukabidhi vyoo vilivyokarabatiwa na shirika la Habitat for Humanity Tanzania.

 Mwenyekiti wa Mtaa wa Kibwegere Edson Nyingi akiongea wakati wa kukabidhi vyoo vilivyokarabatiwa na shirika la Habitat for Humanit Tanzania

 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kibwegere kata ya Kibamba Halmashauri ya Ubungo wakishangilia baada ya kufanyika zoezi la kukabidhi vyoo vilivyokarabatiwa na shirika la Habitat for Humanity Tanzania

 Mkurugenzi wa Shirika la Habitat for Humanity Tanzania Danny Mpogole akiongea wakati wa zoezi la kukabidhi vyoo vilivyokarabatiwa na shirika hilo kwa shule ya Msingi Kibwegere kulia ni mgeni rasmi Ofisa elimu Vifaa na Takwimu wa Halmashauri ya Ubungo Hussein Masoud

 Mwanafunzi wa darasa la nne shule ya Msingi KibwegereWitnes Hamaro akisoma risala ya shule wakati wa kukabidhiwa vyoo vilivyokarabatiwa na shirika la Habitat for Humanity Tanzania   

 Kushoto ni Ofisa elimu Vifaa na Takwimu Hussein Masoud akikata utepe kuashiria kukukabidhiwa vyoo hivyo vilivyojengwa na Habitat for Humanity Tanzania ambapo kulia ni mkurugenzi wa shirika hilo Danny Mpogole

 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Kibwegere
Na John Gagarini
JAMII imetakiwa kutoitumia vibaya dhana ya elimu bure na kuacha uchangiaji kwenye sekta ya elimu kwa kutotoa mchango wake kwa madai kuwa elimu inatolewa bure.
Hayo yalisemwa na ofisa Elimu Vifaa na Takwimu wa Manispaa ya Ubungo Hussein Masoud wakati wa kupokea msaada wa ukarabati wa choo uliofanywa na Shirika lisilo la Kiserikali la Habitat for Humanity Tanzania kwenye shule ya Msingi Kibwegere kata ya Kibamba wilaya ya Ubungo.
Masoud alisema kuwa katika kuwaondolea kero serikali iliondoa baadhi ya michango iliyokuwa ikichangwa na wazazi ikiwemo ada lakini haijakataza wadau kuchangia changamoto mbalimbali kwenye shule za msingi na sekonadri.
“Serikali haijafunga milango kwa jamii kuchangia shule zetu kwani haiwezi ikafanya kila kitu kutokana na uwezo wake bali inasaidiana na wadau wake kuchangia ili kuzikabili changamoto mbalimbali zilizopo kwenye shule,” alisema Masoud.
Alisema kuwa shule zina changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na upungufu wa madawati, upungufu wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo, vitabu na mambo mengine ya kitaaluma.
“Tunaomba wadau kama hawa waendelee kujitokeza na kuchangia pale wanapoona kuna hitaji msaada ili watoto wetu waweze kusoma kwenye mazingira mazuri yatakayowafanya wapate elimu bora,” alisema Masoud.
Naye mkurugenzi wa Habitat For Humanity Tanzania Danny Mpogole alisema kuwa baada ya kupokea changamoto hiyo wao kama wafanyakazi wa shirika hilo na wajumbe wa bodi walijichangisha na kufanikisha ujenzi wa matundu matatu na sehemu ya kunawia na kugharimu kiasi cha shilingi milioni 3.3.
Mpogole alisema kuwa kufanikiwa ukarabati huo kutasaidia mazingira ya wanafunzi kufanya vizuri na kuongeza ufaulu kwani itaongeza hamasa ya wanafunzi kusoma kwani mazingira yao yatakuwa mazuri.
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Margareth Lukwekwe alilishukuru shirika hilo na kusema kuwa limewapunguzia wanafunzi kero ya choo ambapo shule hiyo ina wanafunzi 1,268.
Mwisho.

   

No comments:

Post a Comment