Tuesday, March 14, 2017

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI WAANDISHI WACHAGIZA


 Mratibu wa Chama Cha Waandishi wa Habari Tanzania TAMWA akizungumza wakati wa sherehe za siku ya mwanamke duniani zilizofanyika Maili Moja Kibaha mkoani Pwani zilizoandaliwa na Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Mkoa wa Pwani PWMO.


Mwakilishi wa Mahakama ya Mkoa wa Pwani Herieth Mwailolo akizungumza wakati wa sherehe za siku ya mwanamke zilizofanyika Maili Moja wilayani Kibaha.
Mwenyekiti wa Kituo cha Msaada wilaya ya Kibaha KPC Catherine Mlenga akizungumza wakati wa maadhimisho hayo



Mwanasheria wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Isihaka Ibrahimu akizungumza.
  

Gladys Munuo katikati ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe hizo akizungumza kushoto ni mwenyekiti wa chama cha waandishi wa Habari wanawake mkoa wa Pwani PWMO Mwamvua Mwinyi


Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari wanawake mkoa wa Pwani PWMO Mwamvua Mwinyi akizungumza wakati wa sherehe za siku ya mwanamke duniani iliyofanyika Maili Moja wilayani Kibaha kushoto ni Herieth Mwailolo mwakilishi wa Mahakam ya mkoa wa Pwani na kulia ni Gladys Munuo mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA.


Mratibu wa Chama cha waanidhi wa habari mkoa wa Pwani PWMO Selina Wilson akisoma risala ya chama hicho wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani iliyofanyika Maili Moja wilayani Kibaha.   

Na John Gagarini, Kibaha

CHAMA cha waandishi wa Habari wanawake mkoani Pwani (PWMO) kimeviomba vyombo vya sheria ikiwa ni pamoja na Mahakama polisi na mawakili kufanya kazi wa kuzingatia haki na kumaliza kesi zinazohusisha wabakaji na wanaofanya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Chama hicho Mwamvua Mwinyi wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyoandaliwa na (PWMO) na kusema kuwa watoto na wanawake wengi wamekuwa wakinyimwa haki zao baada ya kufanyiwa vitendo hivyo.

Mwinyi alisema kuwa kuna haja ya vyombo vinavyohusika na utoaji haki kuwajibika bila ya upendeleo au rushwa ili kusababisha haki za wahanga kupotea kutokana na sherian kupindishwa.

“Endapo vyombo hivyo vya kutoa haki vingezingatia haki hakika walengwa wanaohusika na matukio hayo wangepewa adhabu kubwa ambazo zingewafanya wasiendeleze vitendo hivyo,” alisema Mwinyi.

Alisema kuwa haki za wahanga zinapotea kutokana na mashauri hayo kuchukua muda mrefu na hatimaye haki kupotea kabisa kwani ucheleweshaji wa makausudi mashauri hayo hupoteza haki.

“Wanaume wanaofanya unyanyasaji wa kijinsia,kubaka na kulawiti tatizo kubwa ni tamaa pamoja na kujihusisha na vitendo vya kishirikina vinavyo sababisha matukio hayo inayosababisha kukua kwa vitendo hivyo naomba kila mmoja awe mlinzi wa mwenzake na jamii irudishe majukumu yake kwa kulinda watoto kwenye maadili mema,” alisema Mwinyi.

Akizungumzia kauli mbiu ya siku ya wanawake mwaka huu,Tanzania ya viwanda wanawake ni msingi wa mabadiliko ya kiuchumi,alieleza,mkoa wa Pwani umedhamiria kuwa ukanda wa viwanda na uwekezaji.

“Kutokana na hilo utakuwa mkoa wa ajabu kuwa na ufahari wa kuwa na viwanda vingi huku ukiacha kutoa ajira kwa wazawa, akinamama ,wasichana na wengine huku vijana wetu wakiwa wanaongoza kukaa vijiweni kwa kukosa ajira,”alisisitiza Mwinyi.

Naye Mwenykiti Kituo cha Msaada wa Kisheria cha Kibaha (KPC) Catherine Mlenga alisema kuwa wananchi wa Wilaya hiyo wanapaswa kutembelea kito hicho ili waweze kusaidiwa masuala mbalimbali ya kisheria kabla ya kwenda mahakamani.

Mlenga alisema kuwa wao kama watoa msaada wa kisheria wamapewa mafunzo na wanauwezo wa kutatua masuala hivyo kupunguza mzigo kwa mahakama kwa kuyamaliza mashauri kituoni kwao.  

Chama cha wanahabari wanawake Pwani kilianzishwa mwaka 2013 kikiwa na wanachama 15 huku kikikabiliwa na ubaha wa fedha kufika maeneo ya vijijini kuibua vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na changamoto nyingine za kijamii.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment