Na John Gagarini, Kibaha
MADEREVA saba wamejeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili kisha kuwapora
fedha kiasi cha shilingi 920,000 baada ya watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi
kufunga barabara ya Kilwa kwa kutumia magogo.
Aidha watu hao licha ya kuwajeruhi na kuwapora fedha pia waliwaibia
madereva hao simu saba na kutoweka kusikojulikana.
Kwa Mujibu wa taarifa zilizotolewa mjini Kibaha na kamanda wa Polisi mkoani Pwani
Onesmo Lyanga amesema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 22 majira ya saa saba
usiku katika kijiji cha Kitembo kata ya Mchukwi wilaya ya Kibiti.
Kamanda Lyanga amesema kuwa watu hao sita wanaotuhumiwa kuwa ni
majambazi walikuwa na silaha za jadi ikiwa ni pamoja na mapanga na marungu na
walizitumia kuwajeruhi madereva hao.
Amesema kuwa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusina na tukio hilo na
wanaendelea na msako kuhakikisha watu hao wanakamatwa na kufikishwa kwenye
vyombo vya sheria waweze kujibu tuhuma hizo.
Aidha amewataja madereva waliojeruhiwa kwa mapanga kuwa ni Issa Juma (26)
mkazi wa Jijini Dar es Salaam aliyejeruhiwa shavu la kulia, Badru Uwesu (31) mkazi
wa Kisemvule Mkuranga aliyejeruhiwa shavu la kulia na mgongoni, Edward Safari (37)
mkazi wa Morogoro.
Amewataja wengine kuwa ni Ramadhan Ally (34), Nasoro Mohamed (26),
Kassimu Omary (36), Khalifa Mohamed wote wakazi wa Mbagala Jijini Dar es Salaam
ambapo majeruhi wote walitibiwa kwenye Hospitali ya Misheni ya Mchukwi na
kuruhusiwa kuondoka.
Katika tukio lingine ngombe 102 wamekufa baada ya kunywa maji ambayo
yanasadikiwa kuwa hayafai kutumika kwa matumizi yoyote kwenye machimbo ya
kokoto.
Kamanda Lyanga amesema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 22 mwaka huu
majira ya saa 9 alasiri kwenye Kijiji cha Pongwe Msungura Chalinze wilayani
Bagamoyo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment