Na Mwandishi Wetu, Bagamoyo
WABUNGE nchini wametakiwa kuwa wazi juu ya matumizi ya fedha
za maendeleo za mfuko wa Jimbo ili wananchi waweze kujua fedha hizo namna
zinavyotumika.
Hayo yalisemwa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani
Bagamoyo mkoani Pwani alipokuwa akizungumza kwenye halmashauri za Chama Cha
Mapinduzi (CCM) za kata za Kiwangwa na Fukayosi.
Bwanamdogo alisema kuwa baadhi ya wabunge wamekuwa
wakizitumia fedha hizo kwa manufaa binafsi kinyume na taratibu za fedha za
mfuko wa Jimbo.
“Baadhi ya wabunge wamekuwa wakizitumia fdedha hizo kwa siri
kwa manufaa yao badala ya kuzitumia kwa shughuli za maendeleo ya wananchi jambo
ambalo si zuri kwani ni kuwakatisha tama watu kuchangia shughuli za maendeleo,”
alisema Bwanamdogo.
Alifafanua kwa kusema kuwa fedha hizo lazima mbunge aonyeshe
namna zilivyotumika kwani fedha hizo hazina siri yoyote kwani ni za maendeleo.
“Ni vema wabunge wakaweka wazi mapato na matumizi ya fedha
hizo na kuwaeleza wananchi jinsi zilivyotumika kwani ni haki yao kujua lakini
wengine wanazipiga (wanazila) huku wengine wakielekeza wazabuni Fulani ndiyo
wapitishwe kufanya miradi mbalimbali,” alisema Bwanamdogo.
Aidha alisema kama yanavyosomwa mapato na matumizi ya sekta
zingine hata fedha za mfuko wa Jimbo lazima zisomwe kwa wananchi ili wajue
matumizi yalivyokwenda.
Katika kuweka sawa suala la uwazi wa mapato na matumizi ya fedha
za mfuko wa Jimbo mbunge huyo ameelezea mapato na matumizi ya fedha hizo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment