Monday, May 20, 2013

VIONGOZI WAASWA


Na John Gagarini, Kibaha
VIONGOZI Umma nchini wametakiwa kuzingatia weledi wakati wa kutimiza wajibu wao kwa watumishi na wananchi ili waweze kuleta ufanisi kwenye utendaji kazi.
Hayo yamesemwa mjini Kibaha na Kamishna ofisi ya Rais - Tume ya Utumishi wa Umma, Cecilia Shirima alipoongea na sekretarieti na watumishi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Pwani.
 Shirima amesema kuwa ili kufanikisha utendaji kazi kwa viongozi ni vema wakatumia sharia kanuni na taratibu za utumishi wa umma katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
“Amesema viongozi wanapaswa kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani bila ya kuzingatia utartibu wa utumishi wa umma kutasababisha ufanisi wa kazi kuwa chini na kutokuwa na tija,” alisema Shirima.
Kwa upande wake katibu wa tume hiyo Claudia Mpangala amesema kuwa lengo la kuja hapo ni kupeleka ujumbe kwa wadau wa tume hiyo kwenye mikoa kote nchini juu ya kuzingatia weledi wakati wa kufanya kazi zao.
Mpangala amesema kuwa kiongozi bora ni Yule anayefanya kazi kwa kutumia taratibu zilizopangwa juu ya utumishi uliotukuka na kuacha kufanya kazi kwa matakwa yao.
Ameongeza kuwa ili nchi iweze kufanikiwa viongozi na watumishi wanapaswa kuzingatia taratibu za utumishi wa Umma kama zinavyoelekeza.
Amebainisha kuwa tume hiyo tayari imeshatembelea mikoa 21 na sasa inatarajia kutembelea wakala wa serikali na ilianza kutekeleza majukumu yake mwaka 2004, ikiwa na kazi kubw aya kufuatilia na kusimamia utumishi wa umma ili kuhakikisha unaendeshwa kwa mujibu wa sharia, kanunia na taratibu.
Mwisho.   

Kamishna ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Umma Cecilia Shirima katikati akizungumza na sekretarieti ya mkoa na watumishi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Pwani, kushoto ni katibu Tawala mkoa huo Beartha Swai na kulia ni katibu wa tume ya utumishi wa umma Claudia Mpangala.

No comments:

Post a Comment