Wednesday, May 15, 2013

WAMWAGIWA VIFAA VYA MICHEZO


Na John Gagarini, Kibaha
MJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Pwani David Mramba ametoa mipira sita kwa timu za mpira wa pete za kata ya Kibaha.
Mramba alikabidhi mipira hiyo kwa manahodha wa timu za Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa matawi ya kata hiyo kwa lengo la kucheza ligi ili kupta timu ya kata.
Alisema kuwa  aliona changamoto kubwa ya ukosefu wa vifaa vya michezo ikiwemo mipira ndiyo sababu ya yeye kutoa mipira hiyo ili iweze kusaidia kukabiliana na changamoto hiyo.
“Mipira hii iwe changamoto kwenu katika kukabiliana na ukosefu wa vifaa kwani kwa sasa michezo mbali ya kuimarisha afya zenu pia ni ajira hasa kwa vijana ambao wengi hawana ajira,” alisema Mramba.
Aidha alisema kuwa mipira hiyo itasaidia kufanikisha kufanya mashindano ya ngazi ya matawi ambayo inatarajiwa kuanza kufanyika mwezi wa Julai.
“Mashindano hayo yataleta mahusiano mazuri baina ya wanachama wa CCCM na hata jamii kwa ujumla hivyo mipira hiyo itumike na si kuiweka ndani kama mapambambo,” alisema Mramba.
Naye Diwani wa Viti Maalumu Selina Wilson alizitaka timu hizo kuanza maandalizi mapema kwani tayari wameshapata mipira ambayo ilikuwa ikiwafanya washindwe kufanya mazoezi na kukutana kwenya mashindano tu.
Akishukuru kukabidhiwa mipira hiyo katibu wa UWT kata ya Kibaha Sada Duda alisema kuwa kwao hiyo ni changamoto ambayo itawafanya wahamasike na kushiriki michezo ipasavyo. Matawi yaliyopewa mipira hiyo kila tawi likipata mpira mmoja ni Mwendapole A, Kwa Mfipa, Changombe, Kitende, Simbani na Mwendapole B.
Mwisho.   







No comments:

Post a Comment