Friday, May 17, 2013

AJIFANYA USALAMA ADAKWA


Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani linamshikilia John Semindu mkazi wa Kibamba CCM kwa tuhuma za kujifanya kuwa ni mtumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha usalama na kujipatia fedha kwa watu mbalimbali kwa ahadi ya kuwatafutia kazi serikalini.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoani humo Ulrich Matei alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia kitambulisho cha usalama wa Taifa kujipatia fedha kwa njia hiyo ya udanganyifu.
Matei alisema kuwa katika upekuzi mtuhumiwa alikutwa na vyeti vya watu mbalimbali vya kitaaluma kwa madai ya kuwatafutia nafasi za kazi serikalini.
“Mtuhumiwa tunamshikilia na uchunguzi bado unaendelea ambapo alikuwa akitumia gari aina ya Suzuki Escudo rangi ya bluu yenye namba za usajili T 383 ARA,” alisema Matei.
Kamanda Matei aliongeza kuwa mtuhumiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani siku ya Jumatatu ijayo kujibu tuhuma hizo zinazomkabili.
Mwisho.


  

No comments:

Post a Comment