Sunday, May 26, 2013

DKT AISHI CHUMBA CHA KUZALISHIA



Na John Gagarini, Bagamoyo
 WANANCHI wa Kijiji cha Msinune kata ya Kiwangwa wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wameiomba serikali kuwasaidia kujenga nyumba ya mganga ambaye anaishi kwenye chumba cha kuzalishia kwenye zahanati ya kijiji hicho.
Akizungumza mbele ya mbunge wa Jimbo la Chalinze Said Bwanamdogo wakati wa kikao cha Halamshauri ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Kiwangwa, mwenyekiti wa Kijiji hicho Kesi Hassan alisema mganga huyo inabidi afanye hivyo kutokana na kukosa nyumba.
Hassan alisema kuwa mganga pamoja na muuguzi wanatumia wanaishi humo kutokana na uhaba wa nyumba za watumishi katika kijiji hicho.
“Tunaiomba serikali na kwa kupitia kwako kutusaidia ujenzi wa nyumba za watumishi kwani kutumia chumba kinyume na matumizi si sawa na haipendezi mazingira ni magumu,” alisema Hassan.
Aidha alisema kuwa watumishi wengi hawana nyumba za kuishi hivyo kuwapa wakati mgumu katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku ya kuwahudumia wananchi.
“Suala la nyumba za watumishi ni changamoto ambayo inatukabili hivyo ni vema kukawa na nguvu ya ziada kutoka juu ili kutusaidia watumishi wetu waweze kukaa kwenye mazingira mazuri.
Kwa upande wake Bwanamdogo alisema kuwa suala hilo amelipata na ataangalia jinsi gani ya kuweza kulifanyia kazi ili mganga huyo na watumishi wengine waweze kuweza kuwa na nyumba.
Bwanamdogo aliwataka viongozi na wananchi kwenye vijiji vya Jimbo hilo kujitolea kwa kutumia nguvu zao ili kuanzisha ujenzi wa nyumba za watumishi na ofisi yake itachangia.
Mwisho.

DKT AISHI CHUMBA CHA KUZALISHIA



Na John Gagarini, Bagamoyo
 WANANCHI wa Kijiji cha Msinune kata ya Kiwangwa wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wameiomba serikali kuwasaidia kujenga nyumba ya mganga ambaye anaishi kwenye chumba cha kuzalishia kwenye zahanati ya kijiji hicho.
Akizungumza mbele ya mbunge wa Jimbo la Chalinze Said Bwanamdogo wakati wa kikao cha Halamshauri ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Kiwangwa, mwenyekiti wa Kijiji hicho Kesi Hassan alisema mganga huyo inabidi afanye hivyo kutokana na kukosa nyumba.
Hassan alisema kuwa mganga pamoja na muuguzi wanatumia wanaishi humo kutokana na uhaba wa nyumba za watumishi katika kijiji hicho.
“Tunaiomba serikali na kwa kupitia kwako kutusaidia ujenzi wa nyumba za watumishi kwani kutumia chumba kinyume na matumizi si sawa na haipendezi mazingira ni magumu,” alisema Hassan.
Aidha alisema kuwa watumishi wengi hawana nyumba za kuishi hivyo kuwapa wakati mgumu katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku ya kuwahudumia wananchi.
“Suala la nyumba za watumishi ni changamoto ambayo inatukabili hivyo ni vema kukawa na nguvu ya ziada kutoka juu ili kutusaidia watumishi wetu waweze kukaa kwenye mazingira mazuri.
Kwa upande wake Bwanamdogo alisema kuwa suala hilo amelipata na ataangalia jinsi gani ya kuweza kulifanyia kazi ili mganga huyo na watumishi wengine waweze kuweza kuwa na nyumba.
Bwanamdogo aliwataka viongozi na wananchi kwenye vijiji vya Jimbo hilo kujitolea kwa kutumia nguvu zao ili kuanzisha ujenzi wa nyumba za watumishi na ofisi yake itachangia.
Mwisho.

WEKENI WAZI MATUMIZI FEDHA MFUKO WA JIMBO



Na Mwandishi Wetu, Bagamoyo
WABUNGE nchini wametakiwa kuwa wazi juu ya matumizi ya fedha za maendeleo za mfuko wa Jimbo ili wananchi waweze kujua fedha hizo namna zinavyotumika.
Hayo yalisemwa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani alipokuwa akizungumza kwenye halmashauri za Chama Cha Mapinduzi (CCM) za kata za Kiwangwa na Fukayosi.
Bwanamdogo alisema kuwa baadhi ya wabunge wamekuwa wakizitumia fedha hizo kwa manufaa binafsi kinyume na taratibu za fedha za mfuko wa Jimbo.
“Baadhi ya wabunge wamekuwa wakizitumia fdedha hizo kwa siri kwa manufaa yao badala ya kuzitumia kwa shughuli za maendeleo ya wananchi jambo ambalo si zuri kwani ni kuwakatisha tama watu kuchangia shughuli za maendeleo,” alisema Bwanamdogo.
Alifafanua kwa kusema kuwa fedha hizo lazima mbunge aonyeshe namna zilivyotumika kwani fedha hizo hazina siri yoyote kwani ni za maendeleo.
“Ni vema wabunge wakaweka wazi mapato na matumizi ya fedha hizo na kuwaeleza wananchi jinsi zilivyotumika kwani ni haki yao kujua lakini wengine wanazipiga (wanazila) huku wengine wakielekeza wazabuni Fulani ndiyo wapitishwe kufanya miradi mbalimbali,” alisema Bwanamdogo.
Aidha alisema kama yanavyosomwa mapato na matumizi ya sekta zingine hata fedha za mfuko wa Jimbo lazima zisomwe kwa wananchi ili wajue matumizi yalivyokwenda.
Katika kuweka sawa suala la uwazi wa mapato na matumizi ya fedha za mfuko wa Jimbo mbunge huyo ameelezea mapato na matumizi ya fedha hizo.
Mwisho.

SHULE KUWEKEWA FIRST AID KIT

Na John Gagarini, Bagamoyo
MBUNGE wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Said Bwanamdogo anatarajia kuzindua mpango wa kuweka kuweka vifaa vya huduma ya kwanza kwenye shule ambazo ziko mbali na huduma za afya katika jimbo hilo Julai mwaka huu.
Akizungumza na vikundi vya wajasiriamali vya Upendo Saccos na Uamke Saccos kwenye kata za Miono na Mkange wilayani humo,alisema kuwa uzinduzi huo anatarajia kuufanya Julai mwaka huu.
Bwanamdogo alisema kuwa gharama za kutekeleza mpango huo ni kiasi cha shilingi milioni 31 ambapo tayari ameshapata kiasi cha shilingi milioni 12 kwa ajili ya mpango huo.
“Baadhi ya shule ziko mbali na huduma za afya sasa haiwezekani mwanafunzi anaumwa ugonjwa mdogo anashindwa hata kupata panado ni jambo ambalo halipendezi ndiyo sababu ya mimi kubuni mpango huo kwa shule zote ambazo ziko mbali na huduma hizo,” alisema Bwanamdogo.
Katika hatua nyingine amewataka viongozi wakuchaguliwa katika jimbo la chalinze wilaya ya Baagamoyo Mkoani Pwani kutekeleza  ahadi mbalimbali walizozitoa kwa wananchi ili  kujenga imani na ili kuleta maendeleo ya eneo husika.
Aidha alisema wakati alipokuwa akigombea ubunge aliahidi kuwezesha wanawake,vijana,sekta ya afya,elimu na miradi suala ambalo amelivalia njuga na tayari ameshawezesha kiasi cha sh m 170 katika vijiji 66 kati ya 75 jimboni humo.
“Ni vijiji tisa vilivyobaki natarajia kukamilisha maombi yao mapema kabla ya mwaka huu kwisha na kuendelea na mipango mingine aliyojiwekea kwa kipindi cha miaka miwili na nusu iliyobaki.
Katika kata ya Miono ameweza kutoa sh M 32 na alikabidhi kiasi cha sh Milioni moja kwa kwa Saccos ya akinamama Upendo na UWAMKE milioni moja.
Mwisho 

Thursday, May 23, 2013

MBUNGE KUSAIDIA VIKUNDI VYA SANAA NA MICHEZO


Na John Gagarini, Bagamoyo
MBUNGE wa Chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani Said Bwanamdogo amevitaka vikundi vya sanaa na michezo kwenye kata ya Miono kumpelekea mahitaji yao ili aweze kuwasaidia.
Alitoa ahadi hiyo wakati akikabidhi fedha kwa kikundi cha akinamama cha upendo cha Upendo Saccos cha Miono na kusema kuwa vikundi hivyo vinahitaji misaada ili viweze kukua.
Bwanamdogo alisema kuwa vipaji vingi vijijini huwa vinapotea kutokana na kushindwa kuendelezwa kutokana na kukosa vifaa na mahitaji mbalimbali.
“Lengo ni kutaka kusaidia vikundi mbalimbali ili viweze kujiendeleza hasa tukizingatia kuwa sanaa na michezo ni sehemu ya ajira na si kujairiwa maofisini pekee,” alisema Bwanamdogo.
Aidha alisema kuwa vikundi vya sanaa na michezo viko vingi lakini havina sehemu ya kusaidiwa ili viweze kuwa na ustawi kama vilivyokuwa vya mijini.
“Nimeona vikundi vingi vya sanaa na michezo vinauwezo mkubwa lakini havijaendelezwa hivyo nitahkikisha kuwa navisaidia ili viweze kusonga mbele,” alisema Bwanamdogo.
Aliongeza kuwa kwa sasa anajipanga vema ili aweze kuandaa mashindano mbalimbali ya michezo kwa vijana waweze kuonyesha vipaji vyao.
Mwisho. 

SHULE KUPATIWA VIFAA VYA HUDUMA YA KWANZA


Na John Gagarini, Bagamoyo
MBUNGE wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Said Bwanamdogo anatarajia kuzindua mpango wa kuweka kuweka vifaa vya huduma ya kwanza kwenye shule ambazo ziko mbali na huduma za afya katika jimbo hilo Julai mwaka huu.
Akizungumza na vikundi vya wajasiriamali vya Upendo Saccos na Uamke Saccos kwenye kata za Miono na Mkange wilayani humo,alisema kuwa uzinduzi huo anatarajia kuufanya Julai mwaka huu.
Bwanamdogo alisema kuwa gharama za kutekeleza mpango huo ni kiasi cha shilingi milioni 31 ambapo tayari ameshapata kiasi cha shilingi milioni 12 kwa ajili ya mpango huo.
“Baadhi ya shule ziko mbali na huduma za afya sasa haiwezekani mwanafunzi anaumwa ugonjwa mdogo anashindwa hata kupata panado ni jambo ambalo halipendezi ndiyo sababu ya mimi kubuni mpango huo kwa shule zote ambazo ziko mbali na huduma hizo,” alisema Bwanamdogo.
Katika hatua nyingine amewataka viongozi wakuchaguliwa katika jimbo la chalinze wilaya ya Baagamoyo Mkoani Pwani kutekeleza  ahadi mbalimbali walizozitoa kwa wananchi ili  kujenga imani na ili kuleta maendeleo ya eneo husika.
Aidha alisema wakati alipokuwa akigombea ubunge aliahidi kuwezesha wanawake,vijana,sekta ya afya,elimu na miradi suala ambalo amelivalia njuga na tayari ameshawezesha kiasi cha sh m 170 katika vijiji 66 kati ya 75 jimboni humo.
“Ni vijiji tisa vilivyobaki natarajia kukamilisha maombi yao mapema kabla ya mwaka huu kwisha na kuendelea na mipango mingine aliyojiwekea kwa kipindi cha miaka miwili na nusu iliyobaki.
Katika kata ya Miono ameweza kutoa sh M 32 na alikabidhi kiasi cha sh Milioni moja kwa kwa Saccos ya akinamama Upendo na UWAMKE milioni moja.
Mwisho 

Monday, May 20, 2013

WAKAZI WAHITAJI DARAJA LA KUDUMU


Na John Gagarini, Kibaha
MTAA wa Lumumba wilayani Kibaha unahitaji zaidi ya shilingi milioni tisa kwa ajili ya kuweka nguzo tatu za daraja la mbao kwenye kivuko cha mto Mpiji mpakani mwa wilaya ya Kibaha na Kinondoni.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwenyekiti wa mtaa huo Gidion Tarimo alisema kuwa daraja hilo ni muhimu kwao kwa ajili ya kupata mahitaji yao ya kila siku ambayo huyapata mtaa wa Kibwegere wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Tarimo alisema kuwa wilaya ya Kinondoni kwao ni karibu ukilinganisha na Kibaha Maili Moja hivyo daraja hilo linahitaji kufanyiwa matengenezo ili liweze kupitika kwa urahisi hasa kupitisha magari mbapo kwa sasa hayapiti.
“Tumeazimia kujenga daraja hilo hadi magari yaweze kupita ambapo kwa sasa magari hayapiti hata hivyo tumepiga hatua kwani zamani watu walikuwa wakipita mtoni moja kwa moja lakini kwa sasa hawagusi maji na maji yalipokuwa yakijaa watu walikuwa hawawezi kuvuka kwenda ngambo ya pili,” alisema Tarimo.
Alisema kuwa hadi kufikia hatua hiyo wametumia kiasi cha shilingi milioni nane ambapo wananchi wamejitolea huku fedha za mfuko wa Jimbo ni kiasi cha shilingi milioni mbili.
“Changamoto za matumizi ya daraja hili ni kubwa kwani ili mtu upate huduma mbalimbali za kijamii lazima uvuke na kama kuna mamamjamzito lazima ashushwe kwenye pikipiki ambazo hutumika hali ambayo si salama kwa wagonjwa wa namna hiyo,” alisema Tarimo.
Aidha alisema kuwa tayari wameshapeleka barua kwa mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha kwa ajili ya kusaidiwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo.
Aliwaomba watu na mashirika mbalimbali kuwasaidia ili kufanikisha ujenzi huo ambao unatarajiwa kukamilika ifikapo mwaka 2015 ili kurahisisha mawasiliano na sehemu za huduma.
Mwisho.
    
   
 Mwenyekiti wa mtaa wa Lumumba Gidioni Tarimo akipita juu ya daraja la mbao la Mto Mpiji ambapo wanahitaji kiasi cha shilingi milioni tisa kwa ajili ya kuweka nguzo kwa lengo la kuliimarisha ili liweze kupitika ambapo kwa sasa magari hayawwezi kupita, wakazi wa mtaa huo hupata huduma za Kijamii mtaa wa Kibwegere wilaya ya Kinondoni

VIONGOZI WAASWA


Na John Gagarini, Kibaha
VIONGOZI Umma nchini wametakiwa kuzingatia weledi wakati wa kutimiza wajibu wao kwa watumishi na wananchi ili waweze kuleta ufanisi kwenye utendaji kazi.
Hayo yamesemwa mjini Kibaha na Kamishna ofisi ya Rais - Tume ya Utumishi wa Umma, Cecilia Shirima alipoongea na sekretarieti na watumishi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Pwani.
 Shirima amesema kuwa ili kufanikisha utendaji kazi kwa viongozi ni vema wakatumia sharia kanuni na taratibu za utumishi wa umma katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
“Amesema viongozi wanapaswa kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani bila ya kuzingatia utartibu wa utumishi wa umma kutasababisha ufanisi wa kazi kuwa chini na kutokuwa na tija,” alisema Shirima.
Kwa upande wake katibu wa tume hiyo Claudia Mpangala amesema kuwa lengo la kuja hapo ni kupeleka ujumbe kwa wadau wa tume hiyo kwenye mikoa kote nchini juu ya kuzingatia weledi wakati wa kufanya kazi zao.
Mpangala amesema kuwa kiongozi bora ni Yule anayefanya kazi kwa kutumia taratibu zilizopangwa juu ya utumishi uliotukuka na kuacha kufanya kazi kwa matakwa yao.
Ameongeza kuwa ili nchi iweze kufanikiwa viongozi na watumishi wanapaswa kuzingatia taratibu za utumishi wa Umma kama zinavyoelekeza.
Amebainisha kuwa tume hiyo tayari imeshatembelea mikoa 21 na sasa inatarajia kutembelea wakala wa serikali na ilianza kutekeleza majukumu yake mwaka 2004, ikiwa na kazi kubw aya kufuatilia na kusimamia utumishi wa umma ili kuhakikisha unaendeshwa kwa mujibu wa sharia, kanunia na taratibu.
Mwisho.   

Kamishna ofisi ya Rais Tume ya Utumishi wa Umma Cecilia Shirima katikati akizungumza na sekretarieti ya mkoa na watumishi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Pwani, kushoto ni katibu Tawala mkoa huo Beartha Swai na kulia ni katibu wa tume ya utumishi wa umma Claudia Mpangala.

Friday, May 17, 2013

AJIFANYA USALAMA ADAKWA


Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani linamshikilia John Semindu mkazi wa Kibamba CCM kwa tuhuma za kujifanya kuwa ni mtumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha usalama na kujipatia fedha kwa watu mbalimbali kwa ahadi ya kuwatafutia kazi serikalini.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoani humo Ulrich Matei alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia kitambulisho cha usalama wa Taifa kujipatia fedha kwa njia hiyo ya udanganyifu.
Matei alisema kuwa katika upekuzi mtuhumiwa alikutwa na vyeti vya watu mbalimbali vya kitaaluma kwa madai ya kuwatafutia nafasi za kazi serikalini.
“Mtuhumiwa tunamshikilia na uchunguzi bado unaendelea ambapo alikuwa akitumia gari aina ya Suzuki Escudo rangi ya bluu yenye namba za usajili T 383 ARA,” alisema Matei.
Kamanda Matei aliongeza kuwa mtuhumiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani siku ya Jumatatu ijayo kujibu tuhuma hizo zinazomkabili.
Mwisho.


  

Wednesday, May 15, 2013

WAMWAGIWA VIFAA VYA MICHEZO


Na John Gagarini, Kibaha
MJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Pwani David Mramba ametoa mipira sita kwa timu za mpira wa pete za kata ya Kibaha.
Mramba alikabidhi mipira hiyo kwa manahodha wa timu za Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kwa matawi ya kata hiyo kwa lengo la kucheza ligi ili kupta timu ya kata.
Alisema kuwa  aliona changamoto kubwa ya ukosefu wa vifaa vya michezo ikiwemo mipira ndiyo sababu ya yeye kutoa mipira hiyo ili iweze kusaidia kukabiliana na changamoto hiyo.
“Mipira hii iwe changamoto kwenu katika kukabiliana na ukosefu wa vifaa kwani kwa sasa michezo mbali ya kuimarisha afya zenu pia ni ajira hasa kwa vijana ambao wengi hawana ajira,” alisema Mramba.
Aidha alisema kuwa mipira hiyo itasaidia kufanikisha kufanya mashindano ya ngazi ya matawi ambayo inatarajiwa kuanza kufanyika mwezi wa Julai.
“Mashindano hayo yataleta mahusiano mazuri baina ya wanachama wa CCCM na hata jamii kwa ujumla hivyo mipira hiyo itumike na si kuiweka ndani kama mapambambo,” alisema Mramba.
Naye Diwani wa Viti Maalumu Selina Wilson alizitaka timu hizo kuanza maandalizi mapema kwani tayari wameshapata mipira ambayo ilikuwa ikiwafanya washindwe kufanya mazoezi na kukutana kwenya mashindano tu.
Akishukuru kukabidhiwa mipira hiyo katibu wa UWT kata ya Kibaha Sada Duda alisema kuwa kwao hiyo ni changamoto ambayo itawafanya wahamasike na kushiriki michezo ipasavyo. Matawi yaliyopewa mipira hiyo kila tawi likipata mpira mmoja ni Mwendapole A, Kwa Mfipa, Changombe, Kitende, Simbani na Mwendapole B.
Mwisho.   







MATAWI YA CCM YATAKIWA KUANZISHA VITEGA UCHUMI


Na John Gagarini, Kibaha
MATAWI ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchini yametakiwa kuanzisha vitega uchumi ili kujiongezea kipato badala ya kuyafanya matawi hayo vijiwe vya kukaa bila ya tija.
Hayo yalisemwa na mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) kutoka wilaya ya Kibaha mkoani Pwani Rugemalira Rutatina, wakati akizindua tawi la Mtazamo lililopo kata ya Tumbi wilayani humo.
Rutatina alisema kuwa matawi hayo ndiyo msingi wa chama hivyo lazima matawi hayo yajianzishie vyanzo vya kupata mapato badala ya kukaa tu na kubweteka.
“Hili ni kati ya matawi ambayo yameonyesha mwanga kwani kuwa na fedha kwa ajili ya kufanya shughuli za maendeleo ni kitu muhimu na si vema tawi kuwa sehemu ya kukaa tu bila ya kubuni vyanzo vya mapato na si kusubiri kusaidiw akwa kila kitu,” alisema Rugemalila.
Alisema kuwa kwa kuwa matawi ndipo sehemu ya kukiimarisha chama lazima matawi hayo yawe na nguvu za kiuchumi ili waweze kukiimarisha chama.
“Mkiwa na uchumi imara mnaweza kuisaidia jamii mfano kutoa vitanda kwa wagonjwa kwenye hospitali au kuihudumia kwa njia yoyote ile ili iwe mfano mzuri,” alisema Rutatina.
Aidha alisema kuwa wanachama wa CCM wanatakiwa kuwaeleza viongozi changamoto zilizopo na si kuanzisha makundi ambayo hayana manufaa.
Aliwataka Watanzania kuwa na imani na chama na kukataa propaganda za wapinzani kuwa hakuna kilichofanyika tangu nchi kupata uhuru jambo ambalo ni upotoshaji.
Mwisho.