Na John Gagarini, Kibaha
VIKUNDI vya Ujasiriamali wilyani Kibaha mkoani Pwani vinakabiliwa
na chanagamoto ya kutokuwa na akaunti jambo ambalo linasababisha fedha
wanazopewa na wafadhili kutotumika kwa malengo waliyoziombea.
Hayo yalibainika wakati wa ziara ya ofisi ya mbunge wa Jimbo
la Kibaha Mjini Silvestry Koka kukabidhi fedha na vifaa alivyoahidi kupitia
fedha za mfuko wa Jimbo na binafsi kwenye kata mbalimbali.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mara baada ya ziara
hizo msaidizi wa mbunge huyo Method Mselewa alisema kuwa vikundi vingi bado
havijaweza kufungua akaunti kwa ajili ya kutunza fedha zao hivyo fedha hizo
huishia kugawana.
“Jambo la kwanza kabla ya kuwapa fedha tunawashauri kufungua
akaunti ili fedha hizo zipitie huko kuliko kuwakabidhi fedha taslimu na endapo
tunawapa mkononi basi huwa tunawashirikisha wanachama wote pamoja na uongozi wa
serikali ya mtaa pamoja na chama ili kila mtu ashuhudie,” alisema Mselewa.
Alisema changamoto hii ni kubwa na endapo wanahitaji vifaa Fulani
hawawapi fedha bali wanawapatia vifaa ili kuepusha fedha kutumia vibaya ikiwa
ni pamoja na kugawana jambo ambalo liatawarudisha nyuma kimaendeleo.
“Lengo la kutoa fedha
na vifaa kwenye sekta mbalimbali ni kuchochea maendeleo ya wananchi kwa kuunga
mkono miradi ambayo wao wameiibua na ni changamoto kwao,” alisema Mselewa.
Alivitaka vikundi vya ujasiriamali kuhakikisha kuwa vinakuwa
na akaunti ili fedha zao ziweze kuwa salama kwa ustawi wa kiuchumi na maendeleo
ndani ya jamii.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata
ya Tumbi Charles Kapama alimshukuru mbunge huyo kwa kutekeleza ahadi zake kwa
lengo la kuhamasisha maendeleo kwa wakazi wa Jimbo hilo. Katika awamu ya pili
ya utekelezaji wa ahadi za mbunge jumla ya kiasi cha shilingi zaidi ya milioni
10 zimetumika.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WANAWAKE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Kibaha
wametakiwa kujitokeza kuwania nafasi za uongozi kwenye ngazi ya vitongoji,
vijiji na mitaa mwaka 2014 na si kusubiri viti vya kuteuliwa ili kufikia lengo
la 50 kwa 50.
Hayo yalisemwa na mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)
Kibaha Mjini Mwanaid Kiongoli alipokuwa
akiongea na wajumbe wa baraza la utekelezaji la kata ya Kibaha.
Kiongoli alisema kuwa endapo kuna wanawake wanauwezo ni vema
wakaungwa mkono na si kuwawekea ngumu ili waweze kuwania nafasi hizo za uongozi.
“Tusibweteke kwenye nafasi za kuteuliwa lazima nasi tujiamini
kwa kuingia kwenye kinyanganyiro kwa wale wenye uwezo wa kuongoza kwani
tumeshawezeshwa sasa na sisi tujitegemee kwa kuingia kwenye kinyanganyiro
kuanzia 2014 hadi 2015 kwenye uchaguzi mkuu,” alisema Kiongoli.
Aidha alisema kuwa wanawake wasiwakatishe tama wale wanaotaka
kuwania nafasi za uongozi kwa kuwaunga mkono na wawe na upende na mshikamano
kwani wao ndiyo wapiga kura wakubwa hivyo ni rahisi kuwachagua kuwa viongozi.
“Huku tukijiingiza
kwenye harakati za kuwnaia uongozi pia tukumbuke kuwa na miradi ya maendeleo
hasa ile ya ujasiriamali ili kuweza kuziinua familia zetu na kuacha kubweteka
na kutochangamkia fursa za kiuchumi,” alisema Kiongoli.
Aliwataka wanawake kuwa na umoja na kuacha kutengana na
manunguniko ambayo hayataweza kuwasaidia kujikwamua na hali ngumu ya kimaisha
kwani endapo watakuwa na miradi wataweza kuwasomesha watoto wao na kuwapunguzia
mzigo akinababa.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
CHIPUKIZI kupitia Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM)
wametakiwa kuchagua viongozi bora na si kuchagua mtoto wa mkubwa fulani.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mwenyekiti wa Chipukizi Taifa
Gabriel Amos Makala alipofanya ziara ya siku moja mkoani Pwani na kusema kuwa
endapo watachagua watoto wa wakubwa wale wazazi wao ambao ni watu wachini
hawataweza kupata fursa hiyo.
Makala alisema kuwa kwa kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi
wa chipukizi kila mtu bila ya kujali kuw ani mtoto wa nani ana haki ya kuwa
kiongozi.
“Chagueni kiongozi ambaye atafaa kuongoza na si kuangalia
huyu ni mtoto wa Fulani kuwa ndiye anafaa kuongoza hapan hiyo si sahihi kila
mtu ana mwenye sifa anauwezo wa kuongoza hata Yule wa mkulima anaweza kuja kuwa
kiongozi,” alisema Makala.
Alisema kuwa kinachohitajika ni mshikamano baina ya viongozi
na wanachama na kuachana na makundi ambayo si mazuri ndani ya chama kwani
yanakigawa chama na kusabnabisha wapinzani kupata nguvu hasa kipindi ch
auchaguzi.
Kwa upande wake Omary Moris ambaye ni katibu wa hamasa chipukizi
Tiafa na mjumbe wa kiamati kuu ya (CCM NEC) alisema kuwa kazi yake kubwa ni
kuifufua chuipukizi ambayo kwa kipindi Fulani iliyumba.
“Chipukizi wakithaminiwa watalisaidia Taifa na wasiwe
wanatumikia kipindi cha uchaguzi pekee kwani endapo wataandaliwa kwenye miradi
wanaweza kuwa tegemeo kubwa kwa chama na Taifa kwa ujumla,” alisema Moris.
Aliwataka vijana kuwa na mshikamano kwani wao ndiyo tegemeo
la nchi na waache kuwa na makundi ambayo hayatasaidia zaidi ya kuleta
mifarakano.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WATANZANIA wametakiwa kuacha kulalamika juu ya baadhi ya
mambo kutokwenda vizuri badala yake watoe ufumbuzi ya nini kifanyike kuhusiana
na masuala mbalimbali ya kimaendeleo.
Hayo yalisemwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa (CCM NEC) kutokea
Kibaha Mjini Rugemalila Rutatina, wakati wa hafla ya kuchangia ujenzi wa kituo
cha afya cha kanisa la Living Weter Centre kinachojengwa Kilimahewa kata ya
maili Moja wilayani Kibaha.
Rutatina alisema kuwa watu wamekuwa mahiri kulalamika kuwa
jambo Fulani haliendi vizuri lakini hawatoi njia ya kufanyika ili jambo husika
kwenda sawa.
“Tunalishukuru kanisa kwa kutoa jibu la changamoto ya huduma
ya afya haya ndiyo watu wanapaswa kutoa majibu ya nini kifanyike na si kulaumu
tu na hawa sasa baada ya kuona kuna tatizo la huduma hii wametoa suluhisho,”
alisema Rutatina.
Aidha alisema kuwa ni kweli serikali inakabiliwa na
chanagamoto nyingi lakini sekta binafsi nayo inatakiwa kushirikiana na wananchi
ili kutoa majibu ya kero mbalimbali.
“Tunalipongeza kanisa kwa kuona chanagamoto hiyo katika kata
ya Maili Moja ambayo haina kituo cha afya jambo ambalo linawafanya wananchi wa
kata hiyo kupata huduma mbali na maeneo yao na nitatoa kiasi cha shilingi
milioni 2 kuunga mkoni jitihada hizi,” alisema Rutatina.
Kwa upande wake mchungaji wa kanisa hilo Paschal Mnemwa
alisema kuwa alifikia uamuzi wa kujenga kituo cha afya baada ya kuona mama
mjamzito akitaabika kwa kubebwa kwenye pikipiki kupelkwa hospitali umbali wa
kilomita zaidi ya saba.
“Kitu kingine kilichonifanya nifikirie kujenga kituo cha afya
kwa kushirikiana na waumini na wadau wengine ni kifo cha mtoto ambaye alikuwa
akifika kanisani hapo kufariki baada ya kuzidiwa na homa na kabla ya kupata
matibabu kutokana na umbali alifariki dunia,” alisema Mch Mnemwa.
Mch. Mnemwa alisema kuwa wanahitaji kiasi cha shilingi
milioni 335 katika awamu ya kwanza ya ujenzi itakayochukua mwaka mmoja na hadi
kitakapokamilika kitatumia zaidi ya shilingi bilioni 1.5 hadi sasa wametumia
kisi cha shilingi milioni 40 ikiwa ni sadaka za waumini wa kanisa hilo.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka amelipongeza
kanisa la Living Water Centre wilayani Kibaha kwa kuanzisha ujenzi wa kituo cha
afya ili kukabiliana na chanagamoto ya ukosefu wa huduma za kiafya kwenye kata
ya Maili Moja.
Aliyasema hayo mjini Kibaha alipokuwa mgeni rasmi alipomwakilisha
Naibu Waziri wa Fedha Janeth Mbene wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa
kituo hicho utakaogharimu kiasi cha shilingi milioni 335.
Koka alisema kuwa ni watu wachache ambao wamekuwa na maono
kisha kuyafanyia kazi kwa lengo la kuisaidia jamii na kufikiri kuwa kila kitu
kitafanywa na serikali.
“Hii ndiyo kazi ya Mungu kuisaidia jamii na serikali kwani
kama tujuavyo mipango ya serikali ni mingi hivyo hata utekelezaji wake
unachukua muda mrefu hivyo hawa wameonyesha njia ya kuwajibika hivyo lazima
tuwaunge mkono kwa kazi nzuri,” alisema Koka.
Alisema kuwa kwa sasa kituo cha afya cha Mkoani kimeelemewa
na wagonjwa na hospitali ya Tumbi baada ya kufanywa kuwa ya Rufaa imekuwa
haichukui wagonjwa wa moja kwa moja hivyo ujenzi huu utasaidia kukabiliana na
changamoto ya matibabu kwa wananchi wa Maili Moja na wilaya ya Kibaha.
“Hili ni jambo letu sote kwani mara kitakapokamilika kitapunguza
msongamano kwani kwa sasa kituo cha Mkoani na Tumbi bado zinakabiliwa na changamoto
kwani maandalizi ya kuwa kama inavyotakiwa yalikuwa bado hivyo changamoto ni
nyingi,” alisema Koka.
Akielezea juu ya ujenzi huo Mchungaji wa kanisa hilo Paschal
Mnemwa alisema kuwa maono ya kujenga kituo hicho kwa ushirikiano na wamuni
yalikuja baada ya kuona wakazi wa kata ya maili Moja wakienda umbali mrefu
kupata huduma za afya.
Alisema kuwa tayari wameshapata eneo na ujenzi umeshaanza
ambapo tayari hadi sasa wameshatumia zaidi ya milioni 40 na wanahitaji kiasi
cha shilingi milioni 335 kwa ajili ya awamu ya kwanza na hadi kukamilika
zitatumika bilioni 1.5.
Koka aliahidi kuchangia kisi cha shilingi milioni 1.5,
Profesa samweli Wangwe aliahidi kuchangia kiasi cha shilingi milioni 2, mjumbe
wa halmashauri kuu ya CCM Nec Rugemalila Rutatina aliahidi kutoa kiasi cha
shilingi milioni 2 ambapo fedha taslimu ilikuwa milioni 70 na ahadi milioni 20.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MKAZI wa Mwendapole Charles Beatus 31 Maarufu Ngoye amehukumiwa
kwenda jela miaka 10 kwa kupatikana na hatia ya wizi wa Mtandaoni na kuaminiwa kiasi
cha Milioni 7,610,000 za Gwelimo Wlfred mkazi wa Kongowe wilayani Kibaha mkoani
Pwani.
Alihukumiwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha HeriethMwailolo,
baada ya mtuhumiwa kupatikana na makosa hayo mawili.
Kesi hiyo ambayo ilikuwa chini ya Wakili wa Serikali Salim
Msemo ilimkuta na hatia, ambpo kosa la kwanza mahakama ililezwa kuwa mnamo
3.5.2011 ni alihamisha fedha kiasi cha m 3,180,000 Kwenye akaunti ya
mlalamikaji Gwelino Wilfred mkazi wa Kongowe.
Ilielezwa kuwa mtuhumiwa alihamisha fedha hizo kutoka kwenye
akaunti namba 2121606490 ya NMB kwa njia ya mtandao wa simu ya mkononi
0767122144 (Nmb Mobile) kwenda kwenye Akaunti yake namba 2031614880.
Kosa la iili ni wizi wa kuaminiwa kiasi cha shilingi milioni
4,430,000 hivyo kukutwa na hatia na baada mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa
Mahakamani hapo mahakama iliamuru alipe kiasi hicho lakini alishindwa na kulipa
shilingi milioni 2,800,000 tu hivyo kushindwa kujinusuru na kuhukumiwa kwenda jela
miaka 10.
Mwisho.