Tuesday, September 12, 2023

*ASKARI WA TAWA WAMUOKOA MTOTO WA TEMBO ALIYETUMBUKIA SHIMONI*

 

Na Beatus Maganja, TAWA

Askari wahifadhi kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) septemba 11, 2023 walifanikiwa kumuokoa mtoto wa tembo anayekadiriwa kuwa na umri wa wiki nne (4) aliyezama katika shimo lenye matope katika Kijiji cha Kwamsanja kilichopo kata ya kibindu  halmashauri ya Chalinze jirani na Pori la Akiba Wamimbiki.

Taarifa za Mtoto huyo wa tembo aliyetelekezwa na kundi lake kutumbukia shimoni zilitolewa na raia mwema aitwaye Manase Thomas Baha mkazi wa Kijiji cha Kwamsanja na kumlazimu Kamanda wa Pori la Akiba Wamimbiki Emmanuel Lalashe kutuma timu ya askari wanne (4) walioshirikiana na askari wa Jeshi la Akiba (migambo) sita (6) kwa ajili ya zoezi zima la kumuokoa mtoto huyo wa tembo.

Akizungumza baada ya zoezi la uokoaji, Kamanda Emmanuel Lalashe aliwashukuru wananchi wanaoishi pembezoni mwa hifadhi ya Wamimbiki kwa ushirikiano wanaoutoa katika kulinda rasilimali za Nchi yetu zilizopo katika hifadhi hiyo hususan rasilimali Wanyamapori ambazo ni chachu ya shughuli za Utalii na Pato la Nchi.

Mahusiano mazuri yaliyojengwa kati ya wahifadhi wa hifadhi ya Wamimbiki na wananchi wanaoishi vijiji Jirani na hifadhi hiyo umekuwa na manufaa makubwa siku za hivi karibuni kwani wananchi wamekuwa wakitoa ushirikiano mkubwa katika shughuli za uhifadhi.

*DKT JAFO AFUNGUA MRADI WA MAJI KITUO CHA AFYA MZENGA*

Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi ofisi ya makamu wa RAIS Muungano na Mazingira Mhe Dkt Selemani Saidi Jafo amefungua Mradi wa Maji katika Kituo Cha Afya Mzenga na kuwataka wananchi kuutunza Mradi huo 12.09.2023.

Akiziungumza wakati wa kufungua Mradi huo wa Maji alisema ni wajibu wa wananchi Hao wa Mzenga kuitunza miundombinu ya Mradi ili uweze kudumu kwa Muda mrefu huku ukiwahudimia wananchi mbalimbali na wale wanaofika Katika kituo cha Afya Mzenga,

*"Ndugu wananchi nimehangaika sehemu mbalimbali kutafuta wafadhili na kuwapata Hawa ndugu zetu Afrika Relief ambao wameweza kutusaidia kutatua hii kero ya maji hapa Mzenga niwashukuru sana Hawa afrika  Relief kukubali kutujengea Mradi Huu mkubwa alisisitiza Mhe Dkt Jafo*"

Nae Meneja wa Taasisi ya Afrika Relief Kanda ya Tanzania Mohamed Gewily alishukuru kisarawe kwa kupokea msaada wa Mradi huo wa Maji huku akitaja umegarimu  Shilingi Milioni Tisa na Laki Tatu na Elfu Hamsini hivyo akatoa wito zaidi kwa Wanakisarawe hasa Mzenga kuitunza miundombinu ya Mradi ili idumu na Kuendelea Kutoa huduma kwa Muda mrefu,

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Wilaya kisarawe katika ufunguzi wa mradi wa Maji Ndg Nancy Kasamala Alisisitiza kuhifadhi miundombinu ya Mradi pamoja na Kutoa wito kwa Jamii Kuendelea kuzitumia vyema Kamati za maji za Vijiji katika kusimamia  Mradi,

*"Ndugu zangu tuliopo hapa naomba niwakushe  jambo Moja kuna bodi ya maji Vijijini Hivyo nashauri mshirikiane na Uwongozi wa kituo Cha Afya Mzenga kwa kuendesha Mradi huu ambao umejengwa hapa kituoni badala ya Kijijini alishauri Ndugu Kasamala*"

Mradi Huu wa maji katika Tarafa ya Mzenga kata ya Mzenga Kijiji Cha Mzenga umefadhiliwa na Taasisi ya Afrika Relief umegarimu  dhamani ya Milioni Tisa na Laki Tatu na Elfu Hamsini unategemea kuwahudumia watu Elfu Moja  mia Nne na Sitini na Tatu pamoja watu mbalimbali wanaofika kituo Cha Afya Mzenga,

Aidha Mradi huo pia Unategemea kwa Raia kuchangia Bei ya Maji kwa Ndoo  Moja ya  lita Ishirini kwa  Shilingi Arobaini Tu kwa Mujibu wa muongozo ili uweze kuendesha Miundombinu mbalimbali pamoja na Kukarabati.

WATOTO ZAIDI YA LAKI 4 KUPATA CHANJO YA POLIO MKOA WA SONGWE

 

Na. WAF - Songwe

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amebainisha kuwa zaidi ya watoto laki Nne wanatarajia kupata chanjo dhidi ya ugonjwa wa Polio katika Mkoa wa Songwe. 

Waziri Ummy ameyasema hayo Septemba 11, 2023 wakati akianza ziara yake ya kukagua huduma zinazotolewa katika Halmashauri ya Wilaya ya Songwe ambapo ameanza kutembelea katika Hospitali ya Wilaya hiyo, Zahanati ya Mbala pamoja na Kituo cha Afya Mbuyuni kilichopo katika Wilaya hiyo.

“Baada ya kupatikana kwa mtoto Mmoja mwenye ugonjwa wa Polio tumeamua kutoa chanjo ya ugonjwa huo ambapo kwa Mkoa wa Songwe tunatarajia kuchanja watoto takribani Laki Nne ambao wana umri chini ya Miaka Nane”. Amesema Waziri Ummy 

Amesema, Mwaka 2015 Shirika la Afya Duniani (WHO) iliitangaza Tanzania kuwa ni nchi ambayo imetokomeza ugonjwa Polio, Mwaka huu 2023 Tanzania imepata Mtoto mwenye ugonjwa huo katika Manispaa ya Sumbawanga Mkaoni Rukwa. 

“Baada ya Miaka 8 toka WHO iitangaze Tanzania kumalizika kwa ugonjwa wa Polio, Mwaka huu 2023 tumepata mtoto mmoja kutoka Mkoa wa Rukwa ambaye ana virusi vya ugonjwa wa Polio (aina ya Pili)”. Amesema Waziri Ummy 

Aidha, Waziri Ummy amesema kutokana na hatari iliyopo, Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais TAMISEMI imeamua kuendesha kampeni maalumu ya kutoa chanjo ya kuwakinga watoto dhidi ya ugonjwa wa Polio. 

Amesisitiza kuwa, chanjo hiyo itatolewa katika Mikoa Sita iliyopo mipakani ambayo ni Mkoa wa Songwe, Kigoma, Rukwa, Katavi, Mbeya pamoja na Kagera. 

“Mikoa Sita itafikiwa na zoezi hili na lengo ni kuwafikia zaidi ya watoto Mil. 3.5 ambao wana umri chini ya Miaka Nane kwa sababu watoto wote waliozaliwa kuanzia Mwaka 2016 walipata chanjo ya Polio ya kukinga kirusi aina ya kwanza”. Amesema Waziri Ummy 

Pia, Waziri Ummy amesema zoezi hilo la utolewaji wa chanjo litaendeshwa kwenye vituo vya kutoa huduma za Afya, mashuleni, nyumba kwa nyumba, sehemu za ibada na vilabuni.

“Wakati wa zoezi hili tutawatumia watu Watatu Watatu katika kila timu ambao watapita kama ni mashambani, mashuleni au masokoni kwa ajili ya kuwapa watoto chanjo hiyo dhidi ya ugonjwa wa Polio ili tuwakinge watoto wetu na ugonjwa huo”. Amesema Waziri Ummy

KIBITI WAKABIDHIWA VIFAA VYA MICHEZO NYERERE SUPER CUP


Picha ya matukio ya Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ikiwakirishwa na Ndugu Omary Punzi Katibu wa Taasisi hiyo wakikabidhi Tshirt na Mipira ya zawadi ya mashindano ya NYERERE SUPER CUP 2023 Kwa Mhe Kanali Joseph kolombo Mkuu wa wilaya ya Kibiti Mashindano hayo yanatarajiwa kuanza Tarehe 23.9.2023 na kutamatisha 12.10.2023 yakishirikisha Timu 12 Timu 6 kutoka Kibiti na Timu 6 kutoka Rufiji wadhamini wa mashindano ni NSSf,NBC BANK na  TANGANYIKA ORGANIC Kauli mbiu ya mashindano AMANI NA UMOJA VITAWALE MITANO TENA

Saturday, September 9, 2023

NYERERE SUPER CUP TIMU ZAKABIDHIWA VIFAA



Katika kuelekea kumbukizi ya Miaka 24 ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ikiwakirishwa na Ndugu Omary Abdull Katibu wa Taasisi hiyo Mkoa wa Pwani Leo Tarehe 9.9.2023 imekabidhi Vifaa vya michezo ya mashindano ya NYERERE SUPER CUP Jezi seti Moja na Mpira Mmoja Kwa Kila Timu, Tshirt za maandalizi ya Ufunguzi, Zawadi za Mashindano na Mpira Kwa Chama Cha Mpira Rufiji Kwa Mkuu wa wilaya ya Rufiji Mhe Meja Edward Gowele ili akabidhi Kwa Timu sita hizo zitakazoshiriki kwa upande wa Rufiji 1. NGORONGO 2.UTETE,3.MGOMBA, 4.MUHORO 5.UMWE na 6.MKONGO yatakayoshirikisha Wilaya Mbili KIBITI na RUFIJI yatanza kutimua vumbi kuanzia tarehe 23.9.2023 na kutamatika 12.10.2023 Wadhamini wa mashindano hayo NBC bank, NSSF, TANGANYIKA ORGANIC na UNGA AFYA LISHE kauli mbiu ya Mashindano UMOJA NA AMANI VITAWALE MITANO TENA

MTANZANIA ALICE GYUNDA AOMBA APIGIWE KURA MRS/MISS AFRICA UK 2023




MSHIRIKI wa shindano la Miss/Mrs Africa UK 2023 kutoka Tanania Alice Gyunda amesema kuwa endapo atafanikiwa kushinda taji hilo atajenga studio kwenye baadhi ya shule a msingi a Jijini Dar es Salaam ili kuzalisha vipaji vingi vya waimbaji waweze kuitangaa nchi kupitia muziki.

Aidha alisema kuwa ndoto yake nyingine ni kusaidia jamii ya watu wenye ulemavu hususani wanawake na watoto ili waweze kupata haki zao za msingi ili nao waweze kufikia malengo waliojiwekea katika maisha yao.

Gyunda ambaye ni mwalimu na mwimbaji akizungumza kwa njia ya simu kutokea nchini Uingereza anakoishi alisema kuwa endapo Watanania watampigia kura kwa wingi atakuwa na uwezo wa kushinda kwani hadi sasa bado yuko kwenye nafasi nzuri ya kufanya vema.

“Namewaomba Watanzania wanipigie kura ili nishinde ambapo vigezo ni kuonyesha utashi jinsi unavyo ongea na watu na namna unavyofanya mambo yako uwe mtu mwenye ushawishi na nikiwa mshindi nitakuwa balozi wa Kiswahili duniani na malengo yangu kuacha alama kwenye jamii kwa kusaidia watu wasiojiweza huko nyumbani japo niko mbali,”alisema Gyunda.

Alisema kuwa endapo atashinda atahakikisha anajenga studio kwenye baadhi ya shule za Msingi Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya wanafunzi ambao wana vipaji lakini hawana uwezo wa kurekodi itakuwa bure bure au kama kutakuwa na malipo yatakuwa ni madogo sana kwani muziki Tanzania uko chini sana licha ya kuwa na vipaji vingi kwani wengi hawawezi kurekodi kutokana na gharama kuwa kubwa.

“Nia ni kuinua muziki ambapo tutawekea kwa wanafunzi na vijana ambao wana vipaji vikubwa lakini kutokana na mazingira magumu ya uwezo wanashindwa kutimiza ndoto zao na wakipatikana vijana wenye vipaji wataenda kwenye matamasha ya American Good Talent au UK Good Talent ambapo vijana wa nchi za Uganda na Kenya huwa wanakwenda kwenye matamasha hayo ambapo atashirikiana na serikali ili nao washiriki wakirudi wawe chachu kwa wengine,”alisema Gyunda.

Aliongeza kuwa aliingia kwenye shindano hilo baada ya kuona tangazo na walipewa maswali 10 kuchujwa ambapo walikuwa 30 wakachujwa tena wakabaki 20 wakachujwa na kubaki 15 na baadaye mchujo mwingine ulifanyika na kubaki 13 ambapo wanatoka nchi za Afrika na Asia na kuwaomba Watanania wampigie kura ambapo hadi wakati anaongea alikuwa ameshapigiwa kura 1,800 kupitia https://africaukpageants.co.uk/poll/mrs-miss-africa-finalist-2023/

MTANZANIA ALICE GYUNDA AOMBA APIGIWE KURA MRS/MISS AFRICA UK 2023

MSHIRIKI wa shindano la Miss/Mrs Africa UK 2023 kutoka Tanania Alice Gyunda amesema kuwa endapo atafanikiwa kushinda taji hilo atajenga studio kwenye baadhi ya shule a msingi a Jijini Dar es Salaam ili kuzalisha vipaji vingi vya waimbaji waweze kuitangaa nchi kupitia muziki.

Aidha alisema kuwa ndoto yake nyingine ni kusaidia jamii ya watu wenye ulemavu hususani wanawake na watoto ili waweze kupata haki zao za msingi ili nao waweze kufikia malengo waliojiwekea katika maisha yao.

Gyunda ambaye ni mwalimu na mwimbaji akizungumza kwa njia ya simu kutokea nchini Uingereza anakoishi alisema kuwa endapo Watanania watampigia kura kwa wingi atakuwa na uwezo wa kushinda kwani hadi sasa bado yuko kwenye nafasi nzuri ya kufanya vema.

“Namewaomba Watanzania wanipigie kura ili nishinde ambapo vigezo ni kuonyesha utashi jinsi unavyo ongea na watu na namna unavyofanya mambo yako uwe mtu mwenye ushawishi na nikiwa mshindi nitakuwa balozi wa Kiswahili duniani na malengo yangu kuacha alama kwenye jamii kwa kusaidia watu wasiojiweza huko nyumbani japo niko mbali,”alisema Gyunda.

Alisema kuwa endapo atashinda atahakikisha anajenga studio kwenye baadhi ya shule za Msingi Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya wanafunzi ambao wana vipaji lakini hawana uwezo wa kurekodi itakuwa bure bure au kama kutakuwa na malipo yatakuwa ni madogo sana kwani muziki Tanzania uko chini sana licha ya kuwa na vipaji vingi kwani wengi hawawezi kurekodi kutokana na gharama kuwa kubwa.

“Nia ni kuinua muziki ambapo tutawekea kwa wanafunzi na vijana ambao wana vipaji vikubwa lakini kutokana na mazingira magumu ya uwezo wanashindwa kutimiza ndoto zao na wakipatikana vijana wenye vipaji wataenda kwenye matamasha ya American Good Talent au UK Good Talent ambapo vijana wa nchi za Uganda na Kenya huwa wanakwenda kwenye matamasha hayo ambapo atashirikiana na serikali ili nao washiriki wakirudi wawe chachu kwa wengine,”alisema Gyunda.

Aliongeza kuwa aliingia kwenye shindano hilo baada ya kuona tangazo na walipewa maswali 10 kuchujwa ambapo walikuwa 30 wakachujwa tena wakabaki 20 wakachujwa na kubaki 15 na baadaye mchujo mwingine ulifanyika na kubaki 13 ambapo wanatoka nchi za Afrika na Asia na kuwaomba Watanania wampigie kura ambapo hadi wakati anaongea alikuwa ameshapigiwa kura 1,800 kupitia https://africaukpageants.co.uk/poll/mrs-miss-africa-finalist-2023/