
Thursday, May 29, 2025
MWANASHERIA MATATANI AKITUHUMIWA KUGHUSHI AKAUNTI YA KIJIJI NA KUJIPATIA FEDHA

Saturday, May 24, 2025
DIWANI MTAMBO AWASILISHA TAARIFA UTEKELEZAJI WA ILANI YA MIAKA 5
GRACE JUNGULU AONGOZA KIKAO UTEKELEZAJI ILANI KATA YA PICHA YA NDEGE
Wednesday, May 21, 2025
ATAKA SIMBA IUNGWE MKONO KUCHUKUA KOMBE LA SHIRIKISHO DHIDI YA BERKANE
WACHEZAJI viongozi na benchi la ufundi la timu ya Simba wametakiwa kupambana kuhakikisha wanatwaa kombe la Shirikisho.
Aidha washabiki na wapenzi wa soka nchini wametakiwa kuwa na mshikamano na kuacha tofauti zao za ushabiki na kuungana ili kuisadia timu ya Simba kwenye mchezo wao wa fainali dhidi ya Berkane mchezo utakaochezwa uwanja wa Amani Zanzibar.
Akizungumza na Brailo Media aliyewahi kuwa mlezi wa Tawi la Simba Tishio Kibaha Fahim Lardhi amesema kuwa Watanzania wanapaswa kuungana kwenye mchezo huo kwani ni wa heshima kwa nchi.
Lardhi amesema kuwa licha ya Simba kufungwa kwenye hatua ya kwanza kwa magoli 2-0 lakini wanaimani kuwa Simba itapindua matokeo na kuwa mabingwa.
"Tuenzi maneno ya Rais Hayati Dk John Magufuli aliyoitoa kwenye uwanja wa Mkapa wa kutaka Simba au timu nyingine ya Tanzania kuleta kombe la Afrika,"amesema Lardhi.
Amesema kuwa itakuwa ni fedhaha kwa Simba kuchukua kombe hilo ambalo litakuwa kwenye ardhi ya Tanzania ambapo mwaka 1993 walifungwa kwenye fainali na Stella Abidjan ya Ivory Coast.
"Mwaka huu kwa uzalendo wetu tuhakikishe tunalipigania Taifa letu kama kila mtu atatimiza wajibu wake kuanzia wachezaji hadi kwa mashabiki,"amesema Lardhi.
Amewaomba Watanzania kuwa na mshikamano kwa wakati wa maandalizi na wakati wa mchezo kwa kuungana na kuacha tofauti kwani hiyo ni mechi ya heshima kwa nchi.
Monday, May 19, 2025
WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA WARIPOTI HABARI ZA UCHAGUZI KWA UMAKINI
VYOMBO vya Habari nchini vimetakiwa kutoa taarifa za vyama vyote vya siasa kwenye kampeni wakati wa uchaguzi wa mwaka huu ili wananchi waweze kujua sera za vyama na kuchagua viongozi bora.
SERIKALI IDHIBITI FEDHA HARAMU
Friday, May 16, 2025
WATAKIWA KUWATIA MOYO VIONGOZI
Tuesday, May 13, 2025
WAFANYABIASHARA SOKO LA LOLIONDO WARIDHIA KUJENGWA UPYA
KUFUATIA mpango wa Halmashauri ya Mji Kibaha kulibomoa na kujenga upya soko la Loliondo liwe a kisasa uongozi wa soko hilo umeridhia lakini umetoa maombi kwa Halmashauri hiyo.
Sunday, May 11, 2025
ALIYE OKOLEWA NA MKUNGU WA NDIZI AJALI YA MV BUKOBA MIAKA 29 ILIYOPITA ASIMULIA MKASA MZIMA
ILIKUWA mwaka 1996 majira ya asubuhi nilisikia wimbo wa Taifa kupitia Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) wakati huo kwa sasa ni TBC Taifa jambo ambalo si la kawaida kwani unapopigwa wimbo huo basi kuna tukio kubwa la kitaifa ambapo Rais wa Awamu ya Tatu Benjamini Mkapa alitangaza kutokea tukio la ajali ya Mv Bukoba iliyotokea Mkoani Mwanza.
Thursday, May 8, 2025
WANACHAMA WA CCM NYANG'WALE WATAKA KUHARAKISHWA UJENZI WA OFISI.
WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Nyang'hwale Mkoani Geita wametaka ujenzi wa ofisi ya chama ufanyike kwani tayari baadhi ya wadau wamechangia fedha za ujenzi huo.
Wamesema moja ya wadau waliochangia fedha kwa ajili ya ujenzi huo ni Naibu Waziri Mkuu Dotto Biteko ambaye alichangia kiasi cha shilingi milioni 50.
Wamesema kuwa fedha hizo zilikabidhiwa kwa Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Hussein Amar hivyo kutaka fedha hizo zifanye ujenzi huo ili kupata ofisi kwa kazi za chama.
"Tunataka ujenzi ufanyike kwani kama ni fedha zipo hakuna sababu ya kuchelewesha ujenzi huo wa ofisi ya chama ambapo endapo itajengwa itakuwa ya kisasa,"wamesema wanachama hao.
Waliongeza kuwa wanataka fedha hizo zijenge na kukamilisha ofisi ya chama na kwamba wao wanachotaka ni kuona CCM Wilaya ya Nyang'hwale inaendelea kama Wilaya nyingine zilivyoendelea.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Hussein Amar akizungumza kwa njia ya simu ameeleza kusitikishwa na malalamiko ya wananchama hao huku akisema jambo hilo halina usiri wowote.
Amar amesema kuwa yeye ndiye iliyemuomba awasaidie na sio mara moja amekuwa akisaidia na bahati nzuri alipokuja yeye mwenyewe alimkumbushia ombi hilo na akakubali kusaidia lakini hakutamka kiwango.
Aidha amesema kuwa fedha hizo zilivyoingia alimpa taarifa Mkuu wa Wilaya, Mwenyekiti wa Chama, Mwenezi, kamati ya Siasa na kamati ya ujenzi na yeye ndiye aliyetafuta fundi na kuwashauri kuwa kuna fundi kwa hiyo ni vyema akatumika kwakuwa yupo vizuri.
Mbunge huyo ameongeza kuwa yeye binafsi amekuwa na mchango mkubwa sana katika ujenzi wa ofisi hiyo ya Chama maana alishawai kutoa mashine zake na magari yake (Tipa) kufanyakazi katika ujenzi huo.
"Fedha zipo mikono salama na Mei 3 niliongea na Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi kumweleza juu ya fedha kwani zinatakiwa kufanyakazi iliyokusudiwa kwa kuwa mimi sitaki kukaa nazo nipeni akaunti niwahamishie lakini alinijibu kuwa watakaa na kamati yake ya ujenzi na akasema wakati huu aendelee kukaa nazo na wakihitaji kununua vifaa watamjulisha ili atoe hizo fedha",amesema Amar.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nyang'hwale Adam Mtore amesema kuwa kama kuna malalamiko ndani ya Chama kuuna utaratibu wake na mara nyingi huanzia ngazi ya chini ya tawi lakini kwakuwa suala hilo linagusa ngazi ya Wilaya ilitakiwa wapeleke malalamiko yao kwa Katibu wa Chama Wilaya.