Thursday, February 26, 2015

MA DC WATAKIWA KUKAMILISHA MAABARA ZIKAMILIKE MACHI

Na John Gagarini, Kibaha
MKUU wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo amewataka wakuu wa wilaya mkoani humo kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa maabara za sayansi kwenye kata ifikapo Machi mwaka huu.
Ndikilo alitoa agizo hilo jana mjini Kibaha wakati wa kuwakaribisha  wakuu hao wa wilaya ambao waliteuliwa na Rais hivi karibuni na kusema kuwa wanapaswa kufanya jitihada madhubuti ili kufikia malengo hayo.
Alisema kuwa mkoa huo unatakiwa kujenga maabara 327 lakini zilizokamilika ni maabara 144 hivyo kuna upungufu wa maabara 183 ili kukamilisha idadi hiyo inayotakiwa.
“Hizi maabara 183 ziko kwenye hatua mbalimbali ili kukamilika kwake kwa hiyo kila mkuu wa wilaya ahakikishe kuwa ujenzi wa maabara unakamilika ifikapo Machi ambapo anapaswa kuwa amekamilisha,” alisema Ndikilo.
Aidha alisema kuwa ikifika kipindi hicho kila mkuu wa wilaya ahakikishe anamkabidhi maabara hizo kufuatia agizo la Rais la ujenzi huo ukamilike ifikapo Juni mwaka huu.
“Agizo la Rais hali jail kuwa muda muda mfupi katika uongozi wenu kinachotakiwa ni maabara hizo kukamilika kwa wakati uliopangwa hivyo hakutakuwa na kisingizio chochote cha kushindwa kukamilisha ujenzi,” alisema Ndikilo.
Katika hatua nyingine mkuu huyo wa mkoa wa Pwani alisema kuwa wakuu hao wanapaswa kuondoa urasimu katika kuwapatia maeneo wawekezaji kwani fursa za uwekezaji ni nyingi sana.
Alisema wakuu hao watenge maeneo kwa ajili ya uwekezaji baada ya Jiji la Dar es Salaam kujaa hivyo fursa iliyopo ni kwa mkoa wa Pwani hivyo wanapaswa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji.

Mwisho.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akiongea na wakuu wapya wa Wilaya hawapo pichani alipokuwa akiwatambulisha na kuwakaribisha mkoani humo baada ya kuteuliwa na Rais hivi karibuni, hafla ilifanyika leo mjini Kibaha.

 Wakuu wapya wa wilaya kuanzia kushoto kwenda kulia ni Subira Mgalu wilaya ya Kisarawe, Majid Mwanga wilaya ya Bagamoyo, Dk Hassan Mohamed wilaya ya Mafia na Abdala Kihato wilaya ya Mkuranga hafla ilifanyika leo mjini Kibaha.

 Baadhi ya wakuu wapya wa wilaya kuanzia kushoto Dk Hassan Mohamed wilaya ya Mafia, Abdala Kihato wilaya ya Mkuranga, Majid Mwanga wilaya ya Bagamoyo na Nurdin Babu wilaya ya Rufiji ambaye hakubadilishwa hafla ilifanyika leo mjini Kibaha. 


 Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Pwani wakimsikiliza mkuu wa mkoa huo hayupo pichani Mahandisi Evarist Ndikilo, wakati wa kuwakaribisha na kuwatambulisha wakuu wa wilaya wapya waliohamishiwa mkoa huo kutoka mikoa mbalimbali hafla ilifanyika leo mjini Kibaha.

 Moja ya kiongozi wa dini ambaye alihudhuria sherehe za kukaribishwa na kutambulishwa kwa wakuu wa wilaya wapya leo mjini Kibaha.

 Baadhi ya watumishi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Pwani wakimsikiliza mkuu wa mkoa huo Evarist Ndikilo hayupo pichani wakati wa kukaribishwa na kutambulishwa kwa wakuu wapya wa wilaya waliohamishiwa mkoani hapo wakitokea mikoa mbalimbali hafla ilifanyika leo mjini Kibaha. 

No comments:

Post a Comment