Tuesday, November 18, 2014

KLABU YA JOGGING YAZINDULIWA MKE WA MBUNGE ASAIDIA FEDHA

Na John Gagarini, Kibaha
WANANCHI wa Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kujiunga na klabu za mazoezi kwa ajili ya kuboresha afya zao pamoja na kuinua vipaji vya michezo.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Selina Koka alipokuwa akizindua klabu ya mazoezi ya Makapalo Jogging Club ya Maili Moja Shuleni chini ya chama cha msalaba Mwekundu.
Koka alisema kuwa mazoezi ni sehemu ya kujenga afya bora kukabiliana na maradhi yanayotokana na kutofanya mazoezi.
“Ufanayaji wa mazoezi unasaidia kukabiliana na magonjwa ambayo endapo mtu akifanya mzaoezi anaweza kuyaepuka kama vile kisukari, uzito na homa,” alisema Koka.
Alisema kuwa baadhi ya watu wamekuwa hawana utamaduni wa kufanya mazoezi lakini mazoezi ni dawa ya kukabiliana na magonjwa ambayo wanaweza kuyamudu kama watafanya mazoezi.
“Mazoezi kwa sasa ni kila kitu hivyo watu wakijiunga na vilabu hivi vya mazoezi itasaidia kukabiliana na maradhi pia tutawajengea vijana kupenda michezo na kuinua vipaji,” alisema Koka.
Aidha aliwataka wananchi kujijengea utamaduni wa kufanya mazoezi kila wakati hasa nyakati za asubuhi na jioni.
Awali akimkaribisha Koka mwenyekiti wa klabu hiyo Tekla Clemence alisema kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni vifaa vya mazoezi ambapo walipatiwa kiasi cha shilingi 150,000 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa.

Mwisho. 

No comments:

Post a Comment