Jeshi la Polisi Mkoani Pwani linamshikilia Zaina Selemani umri miaka 14 mkazi wa Kitongoji cha Janga tarafa ya Mlandizi Wilaya ya Kibaha kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wake aitwaye Mariam Stamili mwenye miezi tisa.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina Msaidizi Ulrich Matei amethibitisha kutokea
kwa tukio hilo na ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo tarehe
21/10/2013 majira ya saa 00:00 usiku kwa kumnywesha vitu vinavyosadikiwa kuwa
ni sumu ya panya huko Kata ya Janga mtoto wake huyo.
Kamanda
Matei ameongeza kuwa kifo cha mtoto huyo hapo awali ilidaiwa kuwa kilitokana na
kusumbuliwa na maradhi ya degedege hali iliyopelekea familia yake na majirani
kuamini hivyo na kupelekea taratibu zingine za mazishi kufanyika.
Kamanda
Matei ameongeza kuwa siku ya tukio, baada ya mzazi wa mtoto huyo kununua sumu
hiyo alimnyeshwa mtoto wake na baada ya kuona hali yake imebadilika na kuwa
mbaya alimpigia simu mume wake Stamili Shabani umri miaka 21 na kumweleza kuwa mtoto
wao anasumbuliwa na ugonjwa wa degedege hivyo wampeleke kwa mganga wa kienyeji.
Ameongeza
kuwa baada ya mume wake kurejea nyumbani walimchukua motto huyo na kumpeleka
kwa mganga huko Kijiji cha Disunyara ambapo marehemu alianza kupatiwa matibabu
lakini hata hivyo kutokana na hali yake kuzidi kuwa mbaya walimchukua mtoto
huyo na kwenda nae kituo cha afya Mlandizi ambapo alipoteza maisha siku ya
tarehe 21/102013 majira ya saa 00:00 usiku.
Baada
ya kutokea kwa kifo hicho mwili wa marehemu ulichukuliwa na ndugu zake na
kuzikwa majira ya saa 17:00 jioni huko Kijiji cha Kilangalanga, lakini hata
hivyo baada ya kumalizika kwa mazishi hayo mtuhumiwa wa mauaji hayo usiku wa
kuamkia tarehe 23/10/2013 alianza kulia
na kumwambia mume wake huyo kuwa mtoto wao hakufa kwa ugonjwa wa degedege ila
alikuwa amemnywesha sumu hivyo kumuomba amsamehe.
Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi
yake mara baada ya upelelezi kukamilika.
Katika
tukio jingine mnamo tarehe 03/11/2013, majira ya saa za 6.30 usiku huko Kijiji
cha Mindutulieni Kata ya Talawanda Tarafa ya Chalinze (W) Bagamoyo (M) Pwani. Said Mbena miaka 30, mbena, mkulima
mkazi wa Kijiji cha Mindutulieni aliuawa kwa kupigwa na fimbo sehemu mbalimbali
za mwili na Machocho Matei miaka 35, mmasai, mfugaji, mkazi wa Kijiji cha
Mindutulieni baada ya kutokea ugomvi kati yao wakiwa kwenye sherehe za ngoma za
kienyeji nyumbani kwa Asha Rashid. Mtuhumiwa baada ya kukamatwa akiwa njiani
kupelekwa katika ofisi ya Kijiji cha Mindutulieni kabla ya kufikishwa katika
ofisi hiyo aliuawa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi. Miili ya
marehemu ya marehemu imehifadhiwa katika ofisi ya Kijiji hicho ikisubiri
kufanyiwa uchunguzi na Daktari.
Aidha
mnamo tarehe 02/11/2013, majira ya saa za 9.00 usiku huko Kitongoji cha
Mlandizi Kati Kata ya Mlandizi Tarafa ya Mlandizi Wilaya ya Kibaha (M) Pwani. Mtu mmoja aliyefahamika kwa
jina moja la Kingstone umri kati ya miaka 30-35, mkulima mkazi wa Mlandizi
aliuawa na mtu / watu wasiofahamika kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali
sehemu ya mguu wa kushoto kwenye maungio ya goti, hali iliyosababisha damu
nyingi kuvuja na kusababisha kifo chake. Mwili wa marehemu umehifadhiwa chumba
cha maiti Hospitali ya Tumbi Kibaha ukisubiri kufanyiwa uchunguzi na Daktari /
kutambuliwa na ndugu.
Kadhalika
Kamanda Matei ameeleza kuwa mnamo tarehe
02/11/2013, majira ya saa za 4.00 asubuhi huko Kijiji cha Kazimzumbwi Kata ya
Kisarawe Tarafa ya Sungwi barabara ya Dar es Salaam - Kisarawe (W) Kisarawe (M) Pwani. Gari Na. T.762 BSB
aina ya Noah likiendeshwa na Dereva asiyefahamika akitokea Dar es Salaam kwenda
Msanga aligongana uso kwa uso na pikipiki Na. T.219 BUM aina Fekon iliyokuwa
ikiendeshwa na Sixbert Ngatunga miaka 36, mkazi wa Kazimzumbwi akitokea Kisanga
kwenda Kazimzumbwi. Katika ajali hiyo dereva wa pikipiki alifariki dunia papo
hapo. Mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi na Daktari na kukabidhiwa ndugu
kwa mazishi. Chanzo cha ajali ni mwendo kasi wa dereva wa Gari Na. T.762 BSB
aina ya Noah.
No comments:
Post a Comment