MTAA wa Bamba Kata ya Kongowe Wilayani Kibaha imesafisha eneo kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari kwa wanafunzi wanaotoka Mtaa huo ambapo hutembea umbali wa kilometa 16 kwenda Shule ya Sekondari Mwambisi.
Friday, February 3, 2023
MTAA WA BAMBA KUJENGA SEKONDARI
RC ATAKA WANAOSUBIRIA MABADILIKO KUCHAPA KAZI
MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amewataka Wakurugenzi na viongozi ambao nafasi zao zinatokana na uteuzi wa Rais kutofanya kazi zao kwa hofu ya kutochaguliwa kwani hiyo ni mipango ya Mungu.
Kunenge aliyasema hayo Mjini Kibaha alipokuwa akiwaapisha wakuu wapya wa Wilaya na kuwakaribisha waleo waliohamishiwa vituo vyao vya kazi na kuja kwenye mkoa huo.
Alisema kuwa hakuna sababu kwa viongozi hao kutofanya kazi kwa ufanisi kuhofia uteuzi kwani hiyo itasababisha shughuli za maendeleo kutofanyika kikamilifu.
"Wakurugenzi na wale ambao nafasi zao bado hazijafanyiwa mabadiliko na Rais fanyeni kazi mambo mengine mwachieni Mungu mbona mimi nafanya kazi zangu kama taratibu zilivyo mengine tumuachie Mungu yeye ndiye anayejua,"alisema Kunenge.
Aidha alisema kuwa kuchaguliwa hiyo ni mipango ya Mungu hivyo kila mtu afanye kazi kwa mujibu wa sheria msihofie uteuzi kwani kazi za mtu ndiye zitakazomfanya achaguliwe tena.
"Yawezekana unaangaliwa hivyo ukifanya kazi chini ya kiwango unaweza ukajiharibia ni vema ukaendekea kuwajibika bila kujali mbele kutakuwa na nini kwani hayo ni majaaliwa,"alisema Kunenge.
Aliwataka viongozi hao ambao nafasi zao zinatokana na uteuzi wa Rais kutatua changamoto za wananchi kwani ndiyo wajibu wao na wamewekwa hapo kutokana na uwezo wao.
"NIKI WA PILI" AKABIDHIWA KIJITI NA SARA MSAFIRI KUONGOZA WILAYA YA KIBAHA BAADA YA MABADILIKO YA WAKUU WA WILAYA.
MKUU mpya wa Wilaya ya Kibaha Nickson John ambaye amehamishiwa hapa kutoka Wilaya ya Kisarawe amesema kuwa ili kufikia ndoto za Rais DK Samia Suluhu Hassan na matarajio ya wananchi ni kujenga timu ya pamoja.
John aliyasema hayo alipokuwa akikaribishwa Wilayani hapo na viongozi na watendaji wa taasisi na wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha na Halmashauri ya Mji Kibaha na kumuaga aliyekuwa mkuu wa Wilaya hiyo Sara Msafiri.
Alisema kuwa wananchi wana matarajio makubwa ya kupata maendeleo kutoka kwa viongozi hivyo anachohitaji ni ushirikiano ili kuwa na timu itakayofanya kazi kwa pamoja.
"Ndoto yangu ni kuhakikisha tunashirikiana na Rais ili ndoto za kuleta maendeleo zitimie kwa ushirikiano wetu sisi tukiwa ni viongozi,"alisema John.
Aidha alisema kuwa wananchi wanamatumaini makubwa makubwa na viongozi hivyo watazingatia vipaumbele vya Rais na vya wananchi ili kuleta maendeleo.
"Ili tufanye kazi vizuri napenda uwazi na utu ambacho ni kitu kikubwa pamoja na nidhamu na uwajibikaji haya yatatusaidia katika kufikia malengo tuliyojiwekea,"alisema John.
Kwa upande wake mkuu wa zamani wa Wilaya ya Kibaha Sara Msafiri aliwashukuru viongozi na watendaji wa Wilaya hiyo kwa ushirikiano waliompa alipokuwa hapo na kuwatakia heri wanaoendelea na utumishi kushirikiana.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Erasto Makala alisema kuwa watahakikisha wanashirikiana na Mkuu wa Wilaya ili kutoa huduma bora kwa wananchi.
Makala alisema kuwa kwa kushirikiana na Mkuu huyo wa Wilaya wanaamini watakuwa na ushirikiano kufikia ndoto za wananchi.
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Musa Ndomba alisema kuwa watamapa ushirikiano mkuu mpya wa Wilaya ili kuwatumikia wananchi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mhandisi Mshamu Munde alisema kuwa watashirikiana naye ili kufikia pale wanapopataka.
WAKAMATWA NA SILAHA MMOJA ATUHUMIWA MAUAJI
JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani linamshikilia mtu mmoja mwanaume (53) ambaye jina limehifadhiwa mkulima mkazi wa Kijiji cha Ruvu Stesheni Wilaya ya Kibaha akiwa na silaha aina ya Shortgun Greener yenye namba za usajli 729 na maganda sita ya Risasi za Shortgun na unga wa baruti.
Thursday, February 2, 2023
WATAKIWA KUPIMA VIWANJA VIWANJA
MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge ametoa mwezi mmoja kwa wananchi wa mitaa ya Lumumba na Mkombozi Kata ya Pangani Wilayani Kibaha kupima viwanja vyao ambavyo serikali ilitoa baada ya kuvamia eneo lililokuwa la Kituo cha Mitamba Kibaha.
Tuesday, January 31, 2023
HESHIMUNI VIAPO VYENU
VIONGOZI WATAKIWA KUHESHIMU VIAPO VYAO.
Sunday, January 29, 2023
SHULE BORA KUINUA KIWANGO CHA UBORA WA ELIMU AWALI NA MSINGI
Na Wellu Mtaki, Dodoma