Sunday, November 26, 2017
KIFO MTOTO KUUWAWA SERIKALI KUFANYA UCHUNGUZI
![]() |
Mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumter Mshama akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Lukenge kwenye mkutano maalumu |
![]() |
Mke wa mtuhumiwa Zena Manoza |
![]() |
Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Lukenge waliohudhuria mkutano mkuu maalumu wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Kibaha hayupo pichani |
![]() |
Mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumter Mshama akiangalia nyumba lilipotokea tukio la mtoto kuuwawa kwa kupigwa risasi,kushoto ni matundu ya risasi |
Na John
Gagarini, Magindu
WAKAZI wa
Kijiji cha Lukenge kata ya Magindu wilayani Kibaha wametakiwa kuendelea na
shughuli zao na kuishi kwa amani huku serikali ikiendelea na uchunguzi juu ya
tukio la mtoto kuuwawa kwa kupigwa na bunduki na baba yake mdogo Ally Sakalawe
(43) wakati akijibizana na polisi walipokwenda kukagua silaha.
Akizungumza
kwenye mkutano mkuu maalumu wa Kijiji hicho mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumter
Mshama alisema kuwa serikali inaendelea na uchunguzi na itatoa taarifa ili
kuondoa utata ambao umegubika tukio hilo kwa baadhi ya ndugu na wakazi wa
kijiji hicho kudai kuwa polisi ndiyo walimwua mtoto huyo aitwaye Mark Joel
Modest (15).
Mshama
alisema kuwa anajua kuwa tukio hilo limewaumiza sana wakazi hao pamoja na
familia husika lakini hawana budi kuwa na subira juu ya uchunguzi ili kubaini
ukweili juu ya tukio hilo.
“Nawaomba
muishi kwa amani na msiwe na wasiwasi serikali inaendelea na uchunguzi na
mtapewa majibu mara uchunguzi huo utakapokamilika watu wanaosema kuwa hawaishi
majumbani kuhofia kukamatwa wasiogope kama si wahalifu hawana haja ya kuogopa,”
alisema Mshama.
Alisema kuwa
vyombo vyote vya ulinzi na usalama vinafanya kazi zake na haki itatolewa kwani
jambo hili linasikitisha sana kwani mtoto kapoteza uhai na alikuwa hausiki kwa
lolote.
“Tunamasikitiko
makubwa ya kumpotez amtoto huyu ambaye hakuwa na hatia lakini ninachowaomba
muwe na imani na serikali kwani inalifanyia kazi suala hili ili kuweza kujua
ukweli hivyo nanyi mnapaswa kuwa na imani na endeleeni na shughuli zenu za
uzalishaji mali msiishi kwa hofu,” alisema Mshama.
Aidha alisema
kuwa wananchi hao pia wawe makini katika kumiliki silaha ambapo mtuhumiwa licha
ya kutokea kwa tukio hilo la mauaji pia alibainika kuwa alikuwa akimiliki gobore
bila ya kibali pia alikutwa na vitu mbalimbali ambavyo vinaleta maswali mengi
juu ya matumizi ya silaha hiyo.
“Lazima
tujiulize licha ya kifo cha mtoto huyo lakini mtuhumiwa ambaye anashikiliwa na
polisi alikutwa na bunduki mbili aina ya gobore, risasi ya mark 4, vipande vya
nondo na gololi vyote vikitumika kama risasi hivyo lazima tujiulize matumizi ya
silaha hizi,” alisema Mshama.
Awali
akielezea juu ya tukio hilo mke wa mtuhumiwa Zaina Manoza alisema kuwa siku ya
tukio hilo walikuwa wamelala ndani majira ya saa 8 kwenda saa 9 usiku askari
walifika na kuanza kupiga bunduki na wao kuanza kupiga kelele wakiomba msaada
kwa majirani.
Manoza
alisema kuwa walitakiwa kutoka nje na kuambiwa watoke nje na kujitambulisha kwa
majina lakini yeye akawaambia katika hao mtoto mmoja hayupo wakamwambia
akamwangalie chumba kingine ambapo alipokwenda alimkuta mtoto huyo akiwa
anavuja damu ubavuni.
“Baada ya
hapo walinitaka nikamwite mwenyekiti wa kitongoji na alipofika wakawaambia
wampeleke mtoto akapate tiba na kunitaka niongozane na huyo mtoto na mwanangu
mwingine tukiwa tumembeba nikaona kama hali ni mbaya nikajua tayari kafa,”
alisema Manoza.
Kwa upande
wake kamanda wa Polisi wa wilaya Caster Ngonyani alisema kuwa wananchi
wanapaswa kuishi kwa amani na hawatakiwi kuwa na woga na hawakwenda kwa ajili
ya kuwatisha wananchi na wanafanya kazi kwa kufuata sheria.
Ngonyani
alisema kuwa ripoti aliyopewa juu ya tukio hilo ilisema kuwa polisi walikwenda
kwenye nyumba hiyo baada ya kupata taarifa kuwa kuna silaha aina ya gobore bila
ya kibali ambapo taarifa hizo walizipata kutoka kwa wakazi wa kijiji hicho
ndipo walipokwenda kwa ajili ya kuzikamata.
“Kulikuwa na
wamiliki wawili wa hizo silaha ambao ni Ally Sakalawe na Robinus Almas na
hawakutoa taarifa kwa uongozi kwa hofu taarifa kuvuja na walipofika waligonga
na kushindwa kuingia ndani baada ya mtuhumiwa kukataa kufungua mlango na kuanza
kurusha hewani,” alisema Ngonyani.
Alisema kuwa
mwili wa marehemu ulifanyiwa uchunguzi kwenye Hospitali ya Rufaa ya mkoa ya
Tumbi mbele ya baba Mzazi Modest na Anna Raphael mama mzazi
“Ndani ya
tumbo walikuta kipande cha chuma ambacho ni kipande cha nondo kwenye tumbo la
marehemu hali ambayo inaonyesh silaha iliyotumika ni gobore na silaha ya polisi
haitumii chuma inatumia risasi na zingekutwa tungejua kuwa polisi walihusika,”
alisema Ngonyani.
Aidha alisema
kwa mujibu wa ripoti hiyo ni dhahiri kuwa mtoto huyo alipigwa na mtuhumiwa
kwani tumboni kilikutwa kipande cha nondo ambazo zimekatwa na hutumika kama
risasi kwenye magobore hayo ambapo vipande vingine 10 vilikutwa nyumbani kwa
mtuhumiwa.
Tukio hilo
lilitokea Oktoba 28 mwaka huu wakati polisi walipokwenda kufanya upekuzi juu ya
uwepo wa silaha hizo aina ya magobore ambaye yalikuwa yakitumika kwa uhalifu na
uwindaji haramu ambapo licha ya mtuhumiwa wa kwanza kukutwa na silaha hizo pia
walimkamata Robson Almas naye akiwa na magobore mawili yakiwa hayana vibali vya
umiliki.
Mwisho.
UJUMBE WA WAWEKEZAJI TOKA NCHI YA CHINA WATUA PWANI
Baadhi ya wawekezaji toka nchini China wakiwa wanamsikiliza mkuu wa mkoa wa Pwani hayuko pichani walipomtembelea ofisini kwake Mjini Kibaha |
Mkuu wa mkoa katikati waliokaa akiwa na ugeni toka nchi ya China walipomtembelea ofisini kwake mjini Kibaha |
Mkuu wa mkoa wa Pwani na mgeni wake na katibu tawala wa mkoa wakiwa wanafuatialia mazungumzo |
Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akimkabidhi zawadi mwakilishi wa wawekezaji toka nchi ya China |
Wataalamu wa mkoa |
Wataalamu wa mkoa |
Mkuu wa mkoa wa Pwani akimkabidhi zawadi moja ya wawakilishi wa wawekezaji toka nchi ya China Na John Gagarini, Kibaha |
WAWAKILISHI wa makampuni toka nchi ya China wameonyesha nia ya kuwekeza kwenye sekta mbalimbali mkoani Pwani baada ya kuonyeshwa fursa za uwekezaji kwenye mkoa huo.
Wakizungumza baada ya kumtembelea mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo wawakilishi hao baada ya kuonyeshwa maeneo hayo ya uwekezaji kwa njia ya video waliahidi kuwatuma wataalamu ili waone wawekeze kwenye masuala gani.
Mwakilishi wa wawekezaji hao Liv Ming alisema kuwa wamefurahishwa na nchi ya Tanzania na kikubwa ni uhusiano mzuri uliokuwepo tangu enzi za marais Julius Nyerere na Mao Tse Sung.
“Tumeona fursa nyingi za uwekezaji na tunatarajia kuwatuma wataalamu wetu kujua kuangalia na kutupa ushauri lakini baadhi ya vitu ni uwekezaji kwenye sekta ya umeme, vipuri vya magari na uhifadhi wa mazao,” alisema Ming.
Alisema kuwa wameona maeneo mbalimbali kwa njia ya video ambayo wanaweza kuwekeza na wataendelea kufanya mawasiliano na mkoa kwa ajili ya masuala ya uwekezaji kwenye sekta mbalimbali.
“Tumevutiwa na mambo mengi pia kuna baadhi ya makampuni ya wenzetu kutoka China wamewekeza viwanda mengine yanazaidi ya miaka 20 hivyo tutaendelea kuhamasisha wenzetu nao waje kuwekeza,” alisema Ming.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alisema kuwa ujio wa wageni hao ni faraja kwa mkoa pamoja na nchi kwa ujumla kwani itasaidia azma ya serikali ya kuwa nchi ya viwanda.
Ndikilo alisema kuwa mkoa utaendelea kuhamasisha wawekezaji wa nje na ndani ya nchi ili wawekeze kwenye sekta mbalimbali ikiwemo viwanda ili kufikia malengo ya serikali ya awamu ya tano ya nchi ya viwanda na uchumi wa kati.
Ujio wa wawekezaji hao ni kufuatia ziara ya wiki mbili iliyofanywa na timu ya mkoa wa Pwani ya Viongozi pamoja na wataalamu walioifanya mwezi Oktoba mwaka huu ambapo waliweza kuzungumza na makampuni 106 na 30 kukubali kuja mkoani Pwani kwa ajili ya kuja kuangalia maeneo ya uwekezaji.
Mwisho.
Wednesday, November 22, 2017
TANESCO WATAKIWA WATUMIE NGUZO ZA ZEGE
![]() |
Mkurugenzi wa kiwanda cha kutengeneza nguzo kwa kutumia zege cha East Africa Infrastructure Engineering Ltd kilichopo Kidomole kata ya Fukayosi wilayani Bagamoyo |
![]() |
Waziri wa Nishati Dk Merdard Kalemani katikati akipata maelezo juu ya uzalishaji wa nguzo kutumia zege |
![]() Baadhi ya nguzo zinazozalishwa na kiwanda chaEast Africa Infrastructure Engineering Ltd kilichopo Kidomole kata ya Fukayosi wilayani Bagamoyo |
Na John Gagarini, Bagamoyo
SERIKALI imelitaka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuanza kutumia nguzo za umeme za zege kwenye miradi yake mikubwa ukiwemo ule wa Stieglers Gorge wilayani Rufiji mkoani Pwani ambao mara utakapokamilika utazalisha megawati 2,100 ikiwa ni uzalishaji wa megawati nyingi tangu mwaka 1930 uzalishaji ni megawati 1,451 hadi hivi sasa.
Aidha ifikapo Agosti mwakani nchi itaweza kuzalisha megawati 240 kutoka kwenye mradi wa chanzo cha umeme cha Kinyerezi namba mbili ambapo kuanzia Desemba mwaka huu megawati 30 zitakuwa zinaunganishwa kwenye greti ya Taifa kupitia mradi huo na kutosheleza kwa ajili ya viwanda vilivyopo.
Hayo yalisemwa wilayani Bagamoyo na Waziri wa Nishati Dk Merdard Kalemani alipotembelea kiwanda cha kutengeneza nguzo za zege cha East Africa Infrastructure Engineering Ltd kilichopo Kidomole kata ya Fukayosi wilayani Bagamoyo kujionea uzalishaji wa nguzo hizo.
Dk Kalemani alisema kuwa baada ya serikali kupiga marufuku uingizwaji wa nguzo za umeme toka nje na kuruhusu wawekezaji kutengeneza umefika wakati shirika hilo lianze kutumia nguzo za zege kuanzia Desemba mwaka huu kwa kuanzia kewenye mradi huo wa Stiglers Gorge.
“Mradi huo unatarajia kutumia nguzo kati ya 500 hadi 600 na kutokana na ukubwa wa mradi huo lazima tutumie nguzo imara ambazo zinauwezo wa kudumu kwa miaka 70 kuliko kutumia nguzo za miti ambazo zinadumu kwa miaka mitatu kwani ni gharama kubwa ukilinganisha na nguzo za zege,” alisema Dk Kalemani.
“Huwezi kuimarisha uchumi wa viwanda kwa kutegemea malighafi toka nje ya nchi lazima tutegemee vitu vionavyotengenezwa hapa nchini na mmetekeleza agizo la serikali la awamu ya tano kuanzisha viwanda vyetu kwa kutengeneza malighafi wenywe hakuna sababu ya kuagiza vifaa toka nje manufaa yameanza kuonekana tulipozuia wananchi wengi waliomba kuunganishiwa umeme wengine miaka miwili kisa kukosekana nguzo lakini kwa sasa shida hiyo haipo,” alisema Dk Kalemani.
Alisema kuwa walipozuia nguzo zisitoke nje kulikuwa na watu 29,000 walikuhawajaunganishiwa lakioni baada ya hapo watu 20,000 waliunganishiwa umeme na kama kuna mteja hajaunganishiwa umeme zaidi ya mwezi meneja hajafanya hivyo atachukuliwa hatua changamoto kuchelewesha kuunganishiwa hilo ni tatizo la meneja na atachukuliwa hatua kwani hilo ni tatizo lake.
“Utumiaji wa nguzo zinazotumia miti madhara ni kuharibu vyanzo vya maji na mazingira hivyo kaeni na kamapuni hii mshirikiane ili mradi wa Rufiji utakapoanza kutekelezwa zitumike nguzo za zege ambapo kilometa 36 zitatumia nguzo hizo kwani maeneo ya mbugani huwezi kutumia nguzo za miti au kupitisha umeme chini ya ardhi kwani lengo langu ni kuhakikisha kila mwananchi anapata umeme,” alisema Dk Kalemani.
Awali akielezea juu ya kiwanda hicho mmiliki wake Otieno Igogo ambaye anashirikiana na Wachina katika uzalishaji wa nguzo hizo alisema teknolojia hiyo ni ya kisasa kwa umeme na mawasiliano ambayo inadumu kwa zaidi ya miaka 70 hivyo kupunguza gharama za kuweka nyingine kama ilivyo kwa zile za miti.
Igogo alisema kuwa gharama za ujenzi wa kiwanda hicho ni kiasi cha shilingi ni bilioni 13 ambapo changamoto inayowakabili ni kukosa soko kwenye sekta za umma na binafsi na kuiomba serikali kuwaunga mkono kwa kutumia nguzo hizo kwenye miradi mbalimbali ya mawasiliano na umeme.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga kwaniaba ya mkuu wa mkoa wa Pwani alimshukuru Waziri wa Nishati kwa kuendelea kufanikisha upatikanaji wa umeme hasa ikizingatiwa mkoa huo ni moja ya mikoa yenye viwanda vingi hapa nchini.
Mwanga alisema kuwa wilaya ya Bagamoyo na mkoa una mahitaji makubwa ya umeme kutokana na kuwa na uwekezaji mkubwa hasa kwenye sekta ya viwanda ambayo ina mahitaji makubwa ya umeme na kusema mipango mbalimbali ya uzalishaji umeme itasaidia kuondoa tatizo la upungufu wa umeme.
Akishukuru kwa niaba ya wananchi wa Bagamoyo Mbunge wa Jimbo hilo Dk Shukuru Kawambwa alisema kuwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme ukiwemo ule wa REA ni miradi muhimu sana ambayo inakwenda kuondoa kabisa tataizo la umeme.
Dk Kawambwa alisema kuwa anampongeza Rais wa awamu ya tano Dk John Magufuli kwa kuanzisha miradi ya uzalishaji wa umeme ambapo kwa miaka mingi kumekuwa na tataizo la upungufu wa umeme na baadhi ya maeneo kutokuwa na huduma hiyo.
Mwisho.
PWANI WATAKA WATAALAMU WA UWEKEZAJI
Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Zuberi Samataba ambaye aliongoza ujumbe wa viongozi na wataalamu waliotembelea nchi ya China akiongea |
Katibu Tawala wa mkoa wa Pwani Zuberi Samataba akielezea jambo kulia ni mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo |
Baadhi ya washiriki wakijadili baada ya kupokea taarifa ya baadhi ya viongozi na wataalamu waliotembelea nchi ya China |
Na John Gagarini, Kibaha
WATAKA kuwekwa wataalamu wa uwekezaji kwenye kila Halmashauri mkoani humo ili kuwawekea mazingira mazuri ya mawasiliano na wawekezaji.
Ushauri huo ulitolewa mjini Kibaha na baadhi ya wakuu wa wilaya za mkoa huo wakati wa kupokea taarifa toka kwa timu ya wataalamu na viongozi wa mkoa na Halmasahuri ya wilaya ya Kibaha waliokwenda nchini China.
Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga alisema kuwa wataalamu hao wakiajiriwa itasaidia kurahisisha wawekezaji kuwa na mtu maalumu ambaye atakuwa anawajibika kwa wawekezaji wanaokuja mkoani humo.
“Kukiwa na dawati maalumu kwa ajili ya wawekezaji itasaidia kupunguza usumbufu wa mwekezaji kuzungushwa wakati wa kupata vibali mbalimbali vya uwekezaji,” alisema Sanga.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kisarawe Happynes Seneda alisema kuwa mtaalamu huyo atakuwa akiwajibika na suala la wawekezaji kwani kwa sasa nchi imehamasisha ujengwaji wa viwanda hivyo kutakuwa na wageni wengi toka nje ya nchi kwa ajili ya uwekezaji.
Seneda alisema kuwa mtaalamu atajua masuala mbalimbali yanayohusiana na uwekezaji kuanzia masuala ya ardhi, upatikanaji wa vibali mbalimbali na kuwa na mawasiliano na sekta wezeshi kwa ajili ya kutatua changamoto kwa wawekezaji.
Naye mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alisema kuwa madawati ya wataalamu wa uwekezaji kwenye Halmashauri pia sekta wezeshi zinapaswa kuwa na wtu watakaokuwa wanahusika na wawekezaji.
Ndikilo alisema kuwa sekta wezeshi kama vile TANESCO, CHALIWASA, DAWASCO, TARURA, TRA, Polisi na Uhamiaji lazima inakuwa na watu wanaofanya kazi ya kushughulikia wageni.
“Tukiwa na wataalamu wa kudili na wageni itakuwa rahisi kutoa huduma kwa haraka na kwa wakati pia itasaidia kuondoa urasimu wakati wa kuwahudumia wawekezaji ili waweze kutekeleza majukumu yao,” alisema Ndikilo.
Mwisho.
|
Thursday, November 16, 2017
WENGI WAMWAGA ALBERT NGWADA
![]() |
Katibu wa CCM Mkoa wa Pwani Anastazia Amas akizungumza wakati wa kuaga mwili wa Albert Ngwada kwenye ofisi za CCM Kibaha Mjini. |
![]() |
Baadhi ya waombolezaji wakiaga mwili wa Ngwada |
![]() |
Baadhi ya waombolezaji wakiangua vilo baada ya kuuaga mwili wa Ngwada |
![]() |
Vijana wa CCM wakiwa wamebeba jeneza lililokuwa na mwili wa Ngwada |
![]() |
Mama wa Marehemu katikati akiwa anabembelezwa wakati wa kuaga mwili wa mwanae kwenda mkoani Iringa kwa ajaili ya mazishi. |
UINGIZAJI MIFUGO TOKA NJE YA NCHI SERIKALI YASHAURIWA
Na John Gagarini, Kibaha
SERIKALI imetakiwa iendee kudhibiti uingizaji mifugo kutoka nje ya nchi ili kuepuka magonjwa ambayo yakiingia yataathiri soko la nje ambalo linapato kubwa.
Hayo yalisemwa wilayani Kibaha na Mwenyekiti wa Chama Cha Waganga Wasaidizi wa Mifugo Tanzania (TAVEPA) Salim Mselem wakati wa mkutano wa kamati kuu ya chama hicho na kusema kuwa lazima kuwe na udhibiti wa magonjwa.
Mselem alisema kuwa suala la udhibiti wa magonjwa ni mgumu sana lakini serikali kwa kushirirkrana na wataalamu wake wanapaswa kudhibiti uingizwaji wa mifugo hapa nchini.
“Hivi karibuni serikali ilivichoma moto vifaranga ambavyo viliingizwa kwenye mpaka wa Namanga ambapo wahusika hawakufuata taratibu za uingizaji mifugo na hizo ndiyo sheria hata kwenye mataifa mengine,” alisema Mselem.
Alisema kuwa ili kudhibiti magonjwa lazima mifugo inayoingia nchini lazima ikaguliwe ili kuangalia kama imepata chanjo na kama haijapata chanjo lazima uharibiwe.
“Magonjwa mengine ni ya hatari sana licha ya kuathiri soko la nje ambapo endapo itabainika mifugo yetu ina maganjwa haitaruhusiwa kwenye nchi za nje hata kwa afya za walaji pia ni hatari sana na hatutakubali nchi yetu kuwa sehemu ya kuuzwa vitu vibaya,” alisema Mselem.
Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa TAVEPA Ephrahim Masawe alisema kuwa kitengo cha ukaguzi wa uingizwaji mifugo kinapaswa kuwa makini ili kuepuka uingizwaji wa mifugo ambayo haijachanjwa.
Masawe alisema kuwa mifugo inayo ingizwa bila ya kuchanjwa ina hatari ya kuingiza magonjwa ambayo ni ya hatari kwa mifugo pamoja na afya za walaji.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)