Monday, March 20, 2017

MLANDIZI QUEENS YAPONGEZWA KWA KUWA MABINGWA NCHINI

Na John Gagarini, Kibaha

SHIRIKISHO la Soka Nchini (TFF) limeombwa kuhamasisha uanzishwaji wa mashindano ya soka kwa wanawake kwa ukanda wa Afrika Mashariki ili kuendeleza vipaji vya wanawake kimataifa.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mratibu wa timu ya Mlandizi Queens Florence Ambonisye wakati wa sherehe za kuipongeza timu hiyo kwa kutwaa ubingwa huo na kuwa mabingwa wa kihistoria wa kwanza kwa soka la Wanawake Tanzania.

Ambonisye alisema kuwa kwa kuwa kuna mashindano ya soka la wanawake ngazi ya nchi na nchi kuna haja ya kuwa na mashindano ya vilabu kama ilivyo kwa wanaume.

“Imefika wakati TFF kuhamasisha kuanzishwa mashindano ya vilabu vya soka la wanawake ili kuinua soka la wanawake hapa nchini kwani itasaidia kuwa na timu bora kutokana na kushindana na wenzao wa nchi zingine,” alisema Ambonisye.

Ambonisye ambaye pia ni katibu wa chama cha soka la wanawake mkoa wa Pwani alisema kuwa mashindano hayo pia yatasaidia kuimarisha timu ya soka ya Taifa ya wanawake Twiga Stars.

“Tukianzisha mashindano ya nchi za Afrika Mashariki tutakuwa na timu ya Taifa ya wanawake imara kwani watapata uzoefu mkubwa hivyo nchi itaweza kufika mbali kwenye mashindano ya Kimataifa,” alisema Ambonisye.

Aidha alisema kuwa washindi wa mashindano hayo watakuwa hawana mashindano yoyote hadi mwakani lakini wangekuwa na mashindano ya vilabu vya nchi nyingine ingewasaidia sana kuendeleza vipaji vyao ambapo kwa sasa watakaa muda mrefu bila ya kucheza.

Naye mgeni rasmi kwenye sherehe hizo Ivan Chenga ambaye ni katibu msaidizi wa chama cha soka wilayani Kibaha Ivan Chenga alisema kuwa timu hiyo haitakiwi kubweteka kwa kutwaa ubingwa huo.

Chenga alisema kuwa katika kipindi hichi wanapaswa kuendelea na mazoezi na kuachana na vitendo ambavyo vitasababisha kushusha viwango vyao.

Kwa upande wake mwakilishi wa chama cha soka mkoa wa Pwani COREFA Simon Mbelwa alisema kuwa timu hiyo imeleta mafanikio makubwa kwa kuweka historia kwa kuitoa Pwani kimasomaso kwa kutwaa ubingwa huo.

Mbelwa alisema kuwa timu za soka za wanaume za mkoa wa Pwani zimekuwa zikifanya vizuri kwenye ligi Kuu lakini hazijawahi kutwaa ubingwa lakini hii ya wanawake imeweza kuleta kombe na kuonyesha mfano mzuri.

Mwisho.

 Diwani wa Kata ya Mlandizi Ephrasia Kadala akibusu kombe la soka la Wanawake lililotwaliwa na timu ya soka ya wanawake ya Mlandizi Queens wakati wa sherehe za kuipongeza timu hiyo zilizofanyika Mlandizi hivi karibuni.

 Baadhi ya wachezaji wa timu ya Mlandizi Queens wakiwa wamepozi wakati wa sherehe za kuwapongeza baada ya kufanikiwa kuwa mabingwa wa soka la wananwake nchini.

 Baadhi ya viongozi wa timu ya Mlandizi Queens wakiwa wametulia wakifuatilia wakati wa sherehe za kuipongeza timu hiyo kwa kutwaa ubingwa wa soka la wanawake nchini hivi karibuni.

 Wachezaji wa timu ya Mlandizi Queens wakicheza wakati wa sherehe ya kuwapongeza kwa kuwa mabingwa wa soka la wanawake nchini.

 Wachezaji wa Mlandizi Queens wakicheza.

 Wachezaji wa Mlandizi Queens wakicheza pamoja na viongozi wao wakati wa sherehe ya kuwapongeza iliyofanyika Mlandizi hivi karibuni.

 Katibu Msaidizi wa Chama cha soka wilaya ya Kibaha Ivan Chenga akipokea kombe toka kwa kepteni wa Mlandizi Queens Mwanahamis Gaucho katikati ni diwani wa kata ya Mlandizi Ephrasia Kadala akishuhudia. 

 Katibu Msaidizi wa Chama cha soka wilaya ya Kibaha KIBAFA Ivan Chenga akiongea wakati wa sherehe ya kuipongeza timu ya Mlandizi Queens kwa kuwa mabingwa wa soka la wanawake nchini

 Katibu Msaidizi wa Chama cha soka wilaya ya Kibaha KIBAFA Ivan Chenga akinyanyua kombe kama ishara ya pongezi kwa timu ya soka ya wanawake ya Mlandizi Queens kulia ni mjumbe wa Chama caha Soka mkoa wa Pwani COREFA Simon Mbelwa na wakwanza kulia ni Mwanahimis Gaucho Kapteni wa timu hiyo  


Tuesday, March 14, 2017

MUHONGO AZINDUA REA AWAMU YA TATU PWANI



Kushoto katibu Tawala mkoa wa Pwani Zuberi Samataba akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kulia ni mkurugenzi wa REA Injinia Gisima Nyamo-Hanga na kushoto nyuma ni mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo  wakati wa uzinduzi wa REA awamu ya tatu mkoa wa Pwani uliofanyika kwenye Kitongoji cha Msufini wilaya ya Kibaha

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisalimiana na kiongozi wa timu ya kampuni ya Steg International Services ya Tunisia ambayo imepewa zabuni ya mradi wa Umeme Vijijini REA awamu ya tatu mkoani Pwani
Wabunge Abou Jumaa kushoto na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete wakiwa wanasikiliza jambo wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini REA Mkoa wa Pwani awamu ya tatu   



Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo aliyebeba udongo kwa ajili ya kuweka kwenye nguzo ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa REA awamu ya tatu mkoa wa Pwani kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete


Mkurugenzi wa REA Injinia Gisima Nyamo-Hanga akizungumza wakati wa uzinduzi huo 

Kushoto mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo akiongea huku Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akimsikiliza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Umememe Vijijini REA awamu ya tatu mkoani Pwani kwenye kitongoji cha Msufini wilayani Kibaha 


Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akisisitiza jambo mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo wa kwanza kushoto mbele ya mafundi wa kampuni ya Tunisia ya Steg International Services ambao ndiyo watakaoendesha mradi huo.

 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akiongea mbele ya mafundi wa kampuni ya Steg International Services ya Tuniasia waliopewa kazi ya kusimamia mradi wa REA awamu ya tatu mkoani Pwani, katikati ni Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete na kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Abou Jumaa.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria uzinduzi wa mradi wa umeme vijijini  

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo aliyeshika mkasi kwa ajili ya kukata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa REA mkoa wa Pwani kushoto ni mkuu wa mkoa wa Pwani injinia Evarist Ndikilo na kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijijini Abou Jumaa akifuatiwa na Mkurugenzi wa REA Injinia Gisima Nyamo-Hanga  

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akifunua kitambaa kuashiria uzinduzi wa mradi wa Umeme Vijijini REA mkoa wa Pwani kulia ni Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete na kushoto Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Abou Jumaa 

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa mradi wa REA mkoa wa Pwani kulia ni mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo kushoto mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Abou Jumaa anayefuatia ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete 

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo katikati akikabidhiwa mbuzi na baaadhi ya wakazi wa mkoa wa Pwani, kulia ni mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo na kushoto ni mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Abou Jumaa 

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI WAANDISHI WACHAGIZA


 Mratibu wa Chama Cha Waandishi wa Habari Tanzania TAMWA akizungumza wakati wa sherehe za siku ya mwanamke duniani zilizofanyika Maili Moja Kibaha mkoani Pwani zilizoandaliwa na Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Mkoa wa Pwani PWMO.


Mwakilishi wa Mahakama ya Mkoa wa Pwani Herieth Mwailolo akizungumza wakati wa sherehe za siku ya mwanamke zilizofanyika Maili Moja wilayani Kibaha.
Mwenyekiti wa Kituo cha Msaada wilaya ya Kibaha KPC Catherine Mlenga akizungumza wakati wa maadhimisho hayo



Mwanasheria wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Isihaka Ibrahimu akizungumza.
  

Gladys Munuo katikati ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe hizo akizungumza kushoto ni mwenyekiti wa chama cha waandishi wa Habari wanawake mkoa wa Pwani PWMO Mwamvua Mwinyi


Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari wanawake mkoa wa Pwani PWMO Mwamvua Mwinyi akizungumza wakati wa sherehe za siku ya mwanamke duniani iliyofanyika Maili Moja wilayani Kibaha kushoto ni Herieth Mwailolo mwakilishi wa Mahakam ya mkoa wa Pwani na kulia ni Gladys Munuo mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA.


Mratibu wa Chama cha waanidhi wa habari mkoa wa Pwani PWMO Selina Wilson akisoma risala ya chama hicho wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani iliyofanyika Maili Moja wilayani Kibaha.   

Na John Gagarini, Kibaha

CHAMA cha waandishi wa Habari wanawake mkoani Pwani (PWMO) kimeviomba vyombo vya sheria ikiwa ni pamoja na Mahakama polisi na mawakili kufanya kazi wa kuzingatia haki na kumaliza kesi zinazohusisha wabakaji na wanaofanya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Chama hicho Mwamvua Mwinyi wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyoandaliwa na (PWMO) na kusema kuwa watoto na wanawake wengi wamekuwa wakinyimwa haki zao baada ya kufanyiwa vitendo hivyo.

Mwinyi alisema kuwa kuna haja ya vyombo vinavyohusika na utoaji haki kuwajibika bila ya upendeleo au rushwa ili kusababisha haki za wahanga kupotea kutokana na sherian kupindishwa.

“Endapo vyombo hivyo vya kutoa haki vingezingatia haki hakika walengwa wanaohusika na matukio hayo wangepewa adhabu kubwa ambazo zingewafanya wasiendeleze vitendo hivyo,” alisema Mwinyi.

Alisema kuwa haki za wahanga zinapotea kutokana na mashauri hayo kuchukua muda mrefu na hatimaye haki kupotea kabisa kwani ucheleweshaji wa makausudi mashauri hayo hupoteza haki.

“Wanaume wanaofanya unyanyasaji wa kijinsia,kubaka na kulawiti tatizo kubwa ni tamaa pamoja na kujihusisha na vitendo vya kishirikina vinavyo sababisha matukio hayo inayosababisha kukua kwa vitendo hivyo naomba kila mmoja awe mlinzi wa mwenzake na jamii irudishe majukumu yake kwa kulinda watoto kwenye maadili mema,” alisema Mwinyi.

Akizungumzia kauli mbiu ya siku ya wanawake mwaka huu,Tanzania ya viwanda wanawake ni msingi wa mabadiliko ya kiuchumi,alieleza,mkoa wa Pwani umedhamiria kuwa ukanda wa viwanda na uwekezaji.

“Kutokana na hilo utakuwa mkoa wa ajabu kuwa na ufahari wa kuwa na viwanda vingi huku ukiacha kutoa ajira kwa wazawa, akinamama ,wasichana na wengine huku vijana wetu wakiwa wanaongoza kukaa vijiweni kwa kukosa ajira,”alisisitiza Mwinyi.

Naye Mwenykiti Kituo cha Msaada wa Kisheria cha Kibaha (KPC) Catherine Mlenga alisema kuwa wananchi wa Wilaya hiyo wanapaswa kutembelea kito hicho ili waweze kusaidiwa masuala mbalimbali ya kisheria kabla ya kwenda mahakamani.

Mlenga alisema kuwa wao kama watoa msaada wa kisheria wamapewa mafunzo na wanauwezo wa kutatua masuala hivyo kupunguza mzigo kwa mahakama kwa kuyamaliza mashauri kituoni kwao.  

Chama cha wanahabari wanawake Pwani kilianzishwa mwaka 2013 kikiwa na wanachama 15 huku kikikabiliwa na ubaha wa fedha kufika maeneo ya vijijini kuibua vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na changamoto nyingine za kijamii.

Mwisho.

Saturday, March 4, 2017

HABITAT FOR HUMANITY TANZANIA YAKARABATI VYOO KIBWEGERE

 Ofisa Elimu Vifaa na Takwimu Halmashauri ya Ubungo Hussein Masoud akiongea wakati wakukabidhi vyoo vya shule ya Msingi ya Kibwegere kata ya Kibamba wilaya ya Ubungo Jijini Dar es Salaam vilivyokarabatiwa na Shirika la Habitat For Humanity Tanzania, kushoto ni mkurugenzi wa shirika hilo Danny Mpogole na kulia ofisa elimu kata ya Ubungo.  

 Ofisa Elimu kata ya Ubungo Jijini Dar es Salaam katikati akiongea kushoto ni ofisa elimu vifaa na Takwimu Halmashauri ya Ubungo Hussein Masoud na kulia mwalimu mkuu shule ya Msingi Kibwegere kata ya Kibamba wilaya ya Ubungo  Maragareth Mkwekwe wakati wa kukabidhi vyoo vilivyokarabatiwa na shirika la Habitat for Humanity Tanzania.

 Mwenyekiti wa Mtaa wa Kibwegere Edson Nyingi akiongea wakati wa kukabidhi vyoo vilivyokarabatiwa na shirika la Habitat for Humanit Tanzania

 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kibwegere kata ya Kibamba Halmashauri ya Ubungo wakishangilia baada ya kufanyika zoezi la kukabidhi vyoo vilivyokarabatiwa na shirika la Habitat for Humanity Tanzania

 Mkurugenzi wa Shirika la Habitat for Humanity Tanzania Danny Mpogole akiongea wakati wa zoezi la kukabidhi vyoo vilivyokarabatiwa na shirika hilo kwa shule ya Msingi Kibwegere kulia ni mgeni rasmi Ofisa elimu Vifaa na Takwimu wa Halmashauri ya Ubungo Hussein Masoud

 Mwanafunzi wa darasa la nne shule ya Msingi KibwegereWitnes Hamaro akisoma risala ya shule wakati wa kukabidhiwa vyoo vilivyokarabatiwa na shirika la Habitat for Humanity Tanzania   

 Kushoto ni Ofisa elimu Vifaa na Takwimu Hussein Masoud akikata utepe kuashiria kukukabidhiwa vyoo hivyo vilivyojengwa na Habitat for Humanity Tanzania ambapo kulia ni mkurugenzi wa shirika hilo Danny Mpogole

 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Kibwegere
Na John Gagarini
JAMII imetakiwa kutoitumia vibaya dhana ya elimu bure na kuacha uchangiaji kwenye sekta ya elimu kwa kutotoa mchango wake kwa madai kuwa elimu inatolewa bure.
Hayo yalisemwa na ofisa Elimu Vifaa na Takwimu wa Manispaa ya Ubungo Hussein Masoud wakati wa kupokea msaada wa ukarabati wa choo uliofanywa na Shirika lisilo la Kiserikali la Habitat for Humanity Tanzania kwenye shule ya Msingi Kibwegere kata ya Kibamba wilaya ya Ubungo.
Masoud alisema kuwa katika kuwaondolea kero serikali iliondoa baadhi ya michango iliyokuwa ikichangwa na wazazi ikiwemo ada lakini haijakataza wadau kuchangia changamoto mbalimbali kwenye shule za msingi na sekonadri.
“Serikali haijafunga milango kwa jamii kuchangia shule zetu kwani haiwezi ikafanya kila kitu kutokana na uwezo wake bali inasaidiana na wadau wake kuchangia ili kuzikabili changamoto mbalimbali zilizopo kwenye shule,” alisema Masoud.
Alisema kuwa shule zina changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na upungufu wa madawati, upungufu wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo, vitabu na mambo mengine ya kitaaluma.
“Tunaomba wadau kama hawa waendelee kujitokeza na kuchangia pale wanapoona kuna hitaji msaada ili watoto wetu waweze kusoma kwenye mazingira mazuri yatakayowafanya wapate elimu bora,” alisema Masoud.
Naye mkurugenzi wa Habitat For Humanity Tanzania Danny Mpogole alisema kuwa baada ya kupokea changamoto hiyo wao kama wafanyakazi wa shirika hilo na wajumbe wa bodi walijichangisha na kufanikisha ujenzi wa matundu matatu na sehemu ya kunawia na kugharimu kiasi cha shilingi milioni 3.3.
Mpogole alisema kuwa kufanikiwa ukarabati huo kutasaidia mazingira ya wanafunzi kufanya vizuri na kuongeza ufaulu kwani itaongeza hamasa ya wanafunzi kusoma kwani mazingira yao yatakuwa mazuri.
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Margareth Lukwekwe alilishukuru shirika hilo na kusema kuwa limewapunguzia wanafunzi kero ya choo ambapo shule hiyo ina wanafunzi 1,268.
Mwisho.

   

MAPAMBANO DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA WATANZANIA WATAKIWA KUUNGA MKONO MAPMBANO



Na John Gagarini
WATANZANIA wametkiwa kuunga na serikali ya awamu ya tano katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya na matumizi ya pombe za viroba kwa kutowajengea chuki wale wanaokabili suala hilo.
Hayo yalisemwa na Kuhani mkuu wa Kituo cha Maombi na Maombezi cha Gombo Gambusi Alista Albano kilichopo Kibamba Jijini Dar es Salaam na kusema kuwa vita hiyo ni ya wananchi wote ili kuwanusuru Watanzania.
Albano alisema kuwa dawa hizo na pombe hiyo imewafanya watumiaji kudhurika na kushindwa kufanya kazi zao kikamilifu ambapo baadhi wamejikuta wakiwa wagonjwa na wengine kufikia hatua ya kupoteza maisha.
“Tumuunge mkono Rais wetu Dk John Magufuli katika vita hii ambayo imepewa nguvu na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda lakini kuna abaadhi ya watu wameonekana kupingana na mapambano hayo jambo ambalo linashangaza,” alisema Albano.
Alisema kuwa athari ya matumizi ya dawa na pombe hizo ni makubwa tofauti na watu wanavyofikiria ambapo nguvu kazi kubwa imeathirika na kushindwa kuzalisha kutokana na matumizi hayo.
“Sisi kama kaanisa tunapaswa kuliombea Taifa ikiwa ni pamoja na viongozi wetu ambao wanajaribu kuhakikisha wanatuletea maendeleo lakini kwanza wanaondoa vikwazo vilivyokuwa vinazuia nchi ishindwe kupiga hatua ikiwemo dawa na pombe hizo,” alisema Albano.
Aidha alisema Magufuli ni moja ya viongozi ambao ni bora na wataleta mabadiliko makubwa ya nchi na kuifanya Tanzania kuwa nchi ambayo itazalisha na kutoa misaada tofauti na ilivyo sasa imekuwa nchi ya kuomba wahisani.
“Hamasa yake ya kuifanya Tanzinia kuwa nchi ya viwanda itafanya nchi kuwa na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali hivyo itasababisha uchumi kukua na kuwa moja ya nchi zitakazokuwa zinatoa misaada kwa nchi nyingine,” alisema Albano.
Alibainisha kuwa nchi kwa sasa inapita kwenye kipindi cha mpito lakini baadaye kila mwananchi atafurahia maisha kwani anarejesha vile ambavyo viliporwa na watu wachache ili viweze kutumiwa na watu wengi.
“Ninachowaomb Watanzania wenzangu tuache kulalamika kwani tumebakia kulalamika badala ya kufanya kazi kwani malamiko hayataweza kutusaidia badala yake yatatufanya tusiwajibike,” alisema Albano.
Alisisitiza kuwa Rais Magufuli ni mkombozi wa Taifa hili hivyo watu wamwombee katika kuirekebisha nchi na kuiweka katika mazingira mazuri ya kutoa huduma nzuri kwa wananchi wake.
Mwisho.

   

Friday, February 24, 2017

MWIJAGE AWEKA JIWE LA MSINGI KIWANDA CHA VIGAE PWANI










Na John Gagarini,Chalinze

WIZARA ya Biashara Viwanda na Uwekezaji imesema kuwa imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji na kuzitaka taasisi zinazohusika na uwekezaji kutokuwa na ukiritimba.
Hayo yalisemwa na Waziri wa Biashara Viwanda na Uwekezaji Charles Mwijage kwenye Kitongoji cha Pingo Chalinze wakati akiweka jiwe la Msingi kwenye kiwanda cha Vigae cha Twyford Ceramics Ltd.
Mwijage alisema kuwa uwekezaji kama huu unaendana na dhana ya Rais Dk John Magufuli wa kuifanya nchi kuwa ya Viwanda ambapo itaongeza pato la nchi na itazalisha ajira kwa wingi.
“Baadhi ya idara ambazo zinafanikisha uwekezaji ikiwa ni pamoja na brela, idara ya uhamiaji, idara ya kazi, mamlaka ya mapato TRA, wizara ya ardhi, shirika la viwango TBS, Baraza la Mazingira NEMC na nyinginezo zinapaswa kufanya kazi kwa wepesi ili kufanikisha uwekezaji,” alisema Mwijage.
Alisema kuwa kati ya idara hizo baadhi zimekuwa zikifanya vizuri lakini nyingine zimekuwa zikiwapa usumbufu mkubwa wawekezaji hali ambayo inawakatisha tamaa.
“Kwa upande wa wizara yangu hakuna tatizo lolote lakini kuna baadhi ya idara zimekuwa kero kubwa kwa wawekezaji kwa kuwa na ukiritimba usio na sababu naomba kama kuna idara zinakuwa kikwazo niambieni ili tuwachukulie hatua,” alisema Mwijage.
“Viwanda vikiwa vingi nchi itapata mapato makubwa kupitia kodi ambazo zitalipwa kutokana na uuzwaji wa bidhaa zitakazokuwa zinazalishwa viwandani,” alisema Mwijage.
Alisema kuwa nchi zilizofanikiwa kukuza uchumi wake kupitia viwanda zimeweza kutoa ajira nyingi hasa kwa vijana kupitia sekta rasmi na isiyo rasmi.
Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa kiwanda hicho Jack Feng alisema kuwa kiwanda hicho asilimia 95 ya malighafi itakuwa inatoka hapa nchini ambapo kigae kinatumia maligahafi zaidi ya 10.
Feng alisema kuwa mara kiwanda hicho kitakapokamilika Agosti mwaka huu kitaweza kupunguza asilimia 30 ya uagizaji wa vigae toka nje ya nchi.
“Tunatarajia kuajiri wafanyakazi 2,000 moja kwa moja na 4,000 kazi za muda na gharama ya mradi huu ni dola milioni 56 sawa na bilioni 120 ambapo tunatarajia kuuza hadi nje ya nchi kama vile Zambia, Uganda, Rwanda na Burundi,” alisema Feng.
Alisema kuwa wanaunga mkono nchi ya Tanzania kuwa na mpango wa kuwa nchi ya viwanda na wao wanapenda kuwa mfano kwa wawekezaji.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa kituo cha uwekezaji Cliford Tandari alisema kuwa uwekezaji wa kiwanda hicho ni wa mfano kwani utavutia makampuni mengi.
Tandari alisema kuwa hadi sasa kituo chake kimeweza kutoa wigo mkubwa katika kuandikisha miradi mbalimbali toka china na kufikia miradi 667 ambayo itazalisha ajira 83,141 kwa watanzania ambapo miradi 452 ni miradi inayohusiana na sekta ya uzalishaji viwandani.
Naye mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo alisema kuwa kwa sasa mkoa huo umeweza kuwa na viwanda 264 huku vikubwa vikiwa ni viwili.
Ndikilo alisema kuwa uwekezaji huo ni mkubwa na unatarajia kukuza ajira kwa vijana wa mkoa wa Pwani na Tanzania kwa ujumla.
Alisema kuwa mkoa wa Pwani bado una maeneo makubwa ya uwekezaji na tayari kuna eneo lenye bukubwa wa hekari 5,000 linahitaji mwekezaji na wameamua mkoa huo kuwa kituo cha uwekezaji.
Naye Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete aliwapongeza wawekezaji hao kutoka nchi ya China na kusema kuwa Chalinze nayo imejipanga kuwa sehemu ya uwekezaji ambapo kuna ujenzi wa viwanda mbalimbali.
Ridhiwani alisema kuwa changamoto kubwa inayokabiliwa wananchi na wawekezaji ni ukosefu wa maji ambapo wamekuwa wakijitahidi kuikabili lakini bado hawajafanikiwa kuidhibiti aliomba wawekezaji hao kutoa ajira bila ya kuwabagua wenyeji.
Mwisho.









Ramani ya kiwanda cha vigae cha Twyford kilichopo Pingo Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani 


Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage akiongea wakati wa uwekeji jiwe la msingi kiwanda cha vigae cha Twyford kilichopo Pingo Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.




Mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo wa pili kulia akiwa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kulia wakifuatilia jambo wakati wa uwekaji jiwe la msingi kwenye kiwanda cha vigae cha Twyford kilichopo Pingo Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.




Katikati Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage akifunua kitambaa kuashiria uwekeji jiwe la msingi kwenye kiwanda cha vigae cha Twyford kilichopo Pingo Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani kushoto mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo kulia kwa waziri ni Jack Feng mkurugenzi wa kiwanda hicho na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Riziwani Kikwete.


  


Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo kushoto Magid Mwanga akifuatiwa na mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo, mkurugenzi wa kiwanda cha vigae cha Twyford Jack Feng na mbunge wa Jimbo la Chalinze Riziwani Kikwete wakiweka udongo kwenye jiwe la msingi.



Friday, February 3, 2017

VIJANA JKT WALIOJITOLEA UJENZI MABWENI WAPONGEZWA

 Mkuu wa mkoa wa Pwani mwenye shati jeupe Injinia Evarist Ndikilo akionyeshwa ramani ya majengo ya mabweni ya shule ya sekondari ya Nasibugani na moja ya wasimamizi wa ujenzi huo yanayaojengwa na vijana toka Jeshi la Kujenga Taifa JKT Ruvu Mlandizi wilayani Kibaha, kushoto ni katibu tawala wa mkoa Zuber Samataba  
Na John Gagarini, Mkuranga
MKUU wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo emelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kambi ya Ruvu Mlandizi wilayani Kibaha kwa kujitolea kujenga mabweni ya shule ya Sekondari ya Nasibugani iliyopo kata ya Msonga Tarafa ya Kisiju wilayani Mkuranga.
Alitoa pongezi hizo alipotembelea shule hiyo ili kujionea maenedeleo ya ujenzi huo wa mabweni matano na nyumba tano za walimu za shule hiyo ambapo wanafunzi wanalala kwenye baadhi ya vyumba vya madarasa.
Ndikilo alisema kuwa kambi hiyo ilitoa vijana zaidi ya 100 ambao wanaenedelea na ujenzi huo ambao umefikia hatua ya linta na kwa sasa wana miezi mitatu.
“Jeshi limeonyesha uzalendo wa hali ya juu kwa kujitolea kujenga bure mabweni hayo lengo ni kuhakikisha wanafunzi wa shule hiyo wanaishi kwenye mazingira mazuri kuliko ilivyo sasa,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa jeshi hilo limeunga mkono serikali kwa kujitolea kujenga mabweni hayo hivyo kuokoa fedha nyingi endapo wamengepewa wakandarasi.
“Hadi sasa wametumia fedha kidogo sana kiasi cha zaidi ya milioni 120 lakini endapo wangewapa wakandarasi fedha ambazo zingetumika zingekuwa ni nyingi zaidi,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa watu wanaojitolea wanaisadia serikali kwa kuiunga mkono kwa mambo mambo ya kimaendeleo inayoyafanya hali ambayo inapunguza gharama na fedha hizo zinazookolewa zinatumika kwenye mipango mingine.
“Kwa kuwa ujenzi unaendelea tunawaomba wadau mbalimbali waendelee kujitokeza kusaidia ujenzi huo ili ukamilike mapema na wanafunzi waweze kuishi kwenye mazingira mazuri na mnachotakiwa kukifanya kwa sasa ni kufanya upembuzi kujua mahitaji ya vitu vinavyotakiwa ili kukamilisha zoezi hili,” alisema Ndikilo.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mkuranga Gilbert Sanga alisema kuwa anawashukuru wadau mbalimbali ambao wamejitolea kujenga mabweni hayo na kufikia hatua hiyo.
Sanga alisema kuwa Waziri wa elimu Profesa Joyce Ndalichako alitoa kiasi cha shilingi milioni 250 ambazo zianaendelea kutumika katika ujenzi wa mabweni hayo hadi sasa   
Alisema kuwa kazi ya kupanua ilianza kwa wananchi kuchangia zaidi ya milioni nne na kuwataka wanaochangisha wawasilishe fedha walizochangisha ili zifanye kazi husika
“Halmashauri walisema wametenga fedha kiasi cha shilingi milioni 32 kwa bweni moja wanafunzi 48 tu tuliungana na kamati ya ulinzi na usalama nao walikubali kuongeza mabweni zaidi na mkoa nao ukakubali na kambi ya wazalendo ambao walipiga kambi na walifyetua tofali 45,000 na ni kazi ambayo haina bajeti,” alisema Sanga.
Kwa upande wake msimamizi wa ujenzi toka kikosi cha Ruvu JKT Mohamed Boko alimwomba mkuu wa mkoa wa Pwani kufanya jitihada ili ujenzi huo uweze kukamilika ambapo kazi hiyo ilipangwa kufanyika kwa miezi miwili lakini imekuwa kubwa na muda kuongezeka.
Mwis