Friday, February 3, 2017

VIJANA JKT WALIOJITOLEA UJENZI MABWENI WAPONGEZWA

 Mkuu wa mkoa wa Pwani mwenye shati jeupe Injinia Evarist Ndikilo akionyeshwa ramani ya majengo ya mabweni ya shule ya sekondari ya Nasibugani na moja ya wasimamizi wa ujenzi huo yanayaojengwa na vijana toka Jeshi la Kujenga Taifa JKT Ruvu Mlandizi wilayani Kibaha, kushoto ni katibu tawala wa mkoa Zuber Samataba  
Na John Gagarini, Mkuranga
MKUU wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo emelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kambi ya Ruvu Mlandizi wilayani Kibaha kwa kujitolea kujenga mabweni ya shule ya Sekondari ya Nasibugani iliyopo kata ya Msonga Tarafa ya Kisiju wilayani Mkuranga.
Alitoa pongezi hizo alipotembelea shule hiyo ili kujionea maenedeleo ya ujenzi huo wa mabweni matano na nyumba tano za walimu za shule hiyo ambapo wanafunzi wanalala kwenye baadhi ya vyumba vya madarasa.
Ndikilo alisema kuwa kambi hiyo ilitoa vijana zaidi ya 100 ambao wanaenedelea na ujenzi huo ambao umefikia hatua ya linta na kwa sasa wana miezi mitatu.
“Jeshi limeonyesha uzalendo wa hali ya juu kwa kujitolea kujenga bure mabweni hayo lengo ni kuhakikisha wanafunzi wa shule hiyo wanaishi kwenye mazingira mazuri kuliko ilivyo sasa,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa jeshi hilo limeunga mkono serikali kwa kujitolea kujenga mabweni hayo hivyo kuokoa fedha nyingi endapo wamengepewa wakandarasi.
“Hadi sasa wametumia fedha kidogo sana kiasi cha zaidi ya milioni 120 lakini endapo wangewapa wakandarasi fedha ambazo zingetumika zingekuwa ni nyingi zaidi,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa watu wanaojitolea wanaisadia serikali kwa kuiunga mkono kwa mambo mambo ya kimaendeleo inayoyafanya hali ambayo inapunguza gharama na fedha hizo zinazookolewa zinatumika kwenye mipango mingine.
“Kwa kuwa ujenzi unaendelea tunawaomba wadau mbalimbali waendelee kujitokeza kusaidia ujenzi huo ili ukamilike mapema na wanafunzi waweze kuishi kwenye mazingira mazuri na mnachotakiwa kukifanya kwa sasa ni kufanya upembuzi kujua mahitaji ya vitu vinavyotakiwa ili kukamilisha zoezi hili,” alisema Ndikilo.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mkuranga Gilbert Sanga alisema kuwa anawashukuru wadau mbalimbali ambao wamejitolea kujenga mabweni hayo na kufikia hatua hiyo.
Sanga alisema kuwa Waziri wa elimu Profesa Joyce Ndalichako alitoa kiasi cha shilingi milioni 250 ambazo zianaendelea kutumika katika ujenzi wa mabweni hayo hadi sasa   
Alisema kuwa kazi ya kupanua ilianza kwa wananchi kuchangia zaidi ya milioni nne na kuwataka wanaochangisha wawasilishe fedha walizochangisha ili zifanye kazi husika
“Halmashauri walisema wametenga fedha kiasi cha shilingi milioni 32 kwa bweni moja wanafunzi 48 tu tuliungana na kamati ya ulinzi na usalama nao walikubali kuongeza mabweni zaidi na mkoa nao ukakubali na kambi ya wazalendo ambao walipiga kambi na walifyetua tofali 45,000 na ni kazi ambayo haina bajeti,” alisema Sanga.
Kwa upande wake msimamizi wa ujenzi toka kikosi cha Ruvu JKT Mohamed Boko alimwomba mkuu wa mkoa wa Pwani kufanya jitihada ili ujenzi huo uweze kukamilika ambapo kazi hiyo ilipangwa kufanyika kwa miezi miwili lakini imekuwa kubwa na muda kuongezeka.
Mwis

No comments:

Post a Comment