Na John Gagarini, Kibaha
Akizungumza na waandishi wa habari katibu wa chama cha mchezo
huo mkoani Pwani (COREVA) Lonjin Mzava alisema kuwa wanatarajia mafunzo hayo
yatawahusisha walimu wa mchezo huo kwa shule za msingi walimu wanne , sekondari
walimu wanne , vyuo pamoja na wadau wengine wanaopenda kujifunza mchezo huo.
Mzava alisema kuwa washiriki watatoka wilaya zote za mkoa wa
Pwani ambapo kwa walimu tayari barua za kuomba ushiriki wao zimepelekwa kwa
wakurugenzi wa Halmashauri ili kuwpaatia ruhusa ya kushiriki mafunzo hayo.
“Wanafunzi wa mchezo huo watajifunza masomo ya darasani
pamoja nay a vitendo ili kuwajengea uwezo wa kuujua mchezo huo hata
watakapokwenda kuwafundisha wengine wawe na maarifa ya kutosha na mafunzo haya yameandaliwa
kwa pamoja na chama cha mchezo huo nchini (TAVA) alisema Mzava.
Alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwapa ujuzi wa kutosha
walimu wa mchezo huo ili waweze kujua sheria na namna mchezo unavyochezwa na
kuusimamia kama sheria za mchezo huo zinavyoonyesha na kupitishwa na chama cha
mchezo huo cha kimataifa FIVB.
“Hadi sasa walimu kutoka Hlamashauri za Bagamoyo, Mkuranga,
Rufiji na Kibaha Mji tayari wamethibitisha kushiriki mafunzo hayo na waliobaki
wanapaswa kuthibitisha kabla ya tarehe 22 Machi ili waweze kuwekewa utaratibu
wa kushiriki mafunzo hayo,” alisema Mzava.
Aidha alisema kuwa walimu watakaofanya vizuri kwenye mafunzo
hayo watapata nafasi ya kushiriki mafunzo ya Kimataifa ya Beach yatakayofanyika
Aprili mwaka huu Jijini Dar es Salaam hivyo itasaidia kuutangaza mkoa kupitia
mchezo huo.
“Tunaomba wadau mbalimbali wajitokeze kudhamini mafunzo haya
kwani hata wakitoa maji au kitu chochote itasaidia kupunguza gharama za
kuendesha mafunzo hayo kwani hadi sasa hakuna wadhamini waliojitokeza kuzamini
mafunzo hayo,” alisema Mzava.
Alibainisha kuwa matarajio ni kuzalisha walimu wengi wa
mchezo huo hasa mashuleni na itasaidia kupunguza gharama za kuwalipa walimu
toka nje hawa wakati wa mashindano ya Umoja wa Shule za Msingi na Utamaduni
Tanzania( UMITASHUMTA) na Umoja wa Shule za Sekondari na Sanaa Tanzania
(UMISSETA).
Mwisho.