Tuesday, January 6, 2015

MBUNGE WA JIMBO LA CHALINZE RIDHIWANI KIKWETE AENDELEA NA ZIARA JIMBONI

Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo Ridhiwani Kikwete akiwahutubia wakazi wa Kijiji cha Pera kweny kata ya Kibindu wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wakati wa ziara ya kutembela shughuli za maendeleo

 Ridhiwani Kikwete Mbunge wa Jimbo la Chalinze akikabidhi mpira kwa moja ya Wazee kwenye Kijiji cha Pera Kata Kibindu wakati wa zaiara yake kwenye jimbo hilo

 Hili ni darasa la shule ya msingi ya Kibindu ambayo iliezuliwa paa baada ya kutokea mvua kubwa iliyonyesha mwishoni mwa mwaka jana

 Diwani wa Kata ya Kibindu Mawazo Mkufya akiongea na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete mwenye kofia alipotembelea shule hiyo kuangalia uharibifu uliotokana na mvua kubw ailiyonyesha na kuharibu baadhi ya madarasa na ofisi ya mwalimu mkuu wa shule hiyo

 Moja ya Madarasa ya shule ya Msingi Kibindu yaliyoharibiwa na mvua kubw ailiyonyesha mwaishoni mwa mwaka jana 

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kulia akiongea na waandishi wa habari hawapo kushoto ni diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya. 

 Baadhi ya akinamama wa Kijiji cha Kibindu wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete hayupo pichani wakati wa ziara yake kwenye jimbo hilo

 Choo cha shule ya Msingi Maluiwi kikiwa kimebomoka hali ambayo inawafanya wanafunzi wa shule hiyo kujisaidia porini kwa zaidi ya miaka miwili sasa.

 Hichi ni choo cha nyasi ambacho kinatumiwa na walimu wa shule ya Msingi Maluiwi

 Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete akiongea na wananchi wa Kitongoji cha Mdaula alipotembelea kwenye ziara yake ya kuangalia shughuli za maendeleo kwenye jimbo hilo.

Monday, January 5, 2015

MCHAKATO WA MAMLAKA YA MJI MDOGO CHALINZE CHANGAMOTO KUBWA, MAJAMBAZI WATUMIA MSITU WA MWIDU

Na John Gagarini, Ubena
MCHAKATO wa kuifanya Chalinze kuwa mamlaka ya Mji Mdogo umekumbwa na changamoto kubwa baada ya makundi mawili ya wakulima na wafugaji kupinga mpango huo.
Makundi hayo ambayo ndiyo makubwa katika Jimbo la Chalinze yameonekana kutoupokea mpango huo kwa madai kuwa utawasababisha kushindwa kufanya shughuli za ambazo ndizo zinazowafanya waweze kuishi.
Changamoto za kupinga mchakato huo zimebainika wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete kutembelea shughuli za maendeleo.
Akizungumzia changamoto hizo Ridhiwani alisema Jimbo hilo lilitenga maeneo kwa ajili ya wafugaji na wakulima katika mpango bora wa matumizi ya ardhi ambapo kila kundi linakaa kwenye eneo lake.
“Changamoto hizi zinakuja kutokana na hali halisi kuwa endapo mamlaka hiyo itakubalika ina maana kutakuwa na sheria ya kuzuia ufugaji wa mifugo pamoja na kuzuia kilimo huku makundi hayo yakitegemea shughuli hizo kuendeshea maisha yao,” alisema Ridhiwani.
Ridhiwani alitoa mfano kwenye maeneo ya wafugaji ya Vijiji vya Chamakweza ambao wana mifugo zaidi ya 18,000, Lukenge wana mifugo zaidi ya 10,000 na Matuli mifugo zaidi ya 8,000.
“Wafugaji wamesema kuwa endapo Mamlaka hiyo itapitishwa mifugo yao wataipeleka wapi na wao ufugaji ndiyo maisha yao kwa ajili ya chakula pamoja na uchumi,” alisema Ridhiwani.
Alisema pia kwa wakulima nao hawataruhusiwa kulima je wataishije wakati kilimo ndiyo shughuli yao ya kuendeshea maisha yao ikiwa ni pamoja na uchumi wao na hawana kitu kingine wanachoweza kukifanya.
“Changamoto hizi katika kueleka Mji Mdogo zimekuwa ni kubwa na ukiangalia zina uzito hivyo mchakato huu umesitishwa huku serikali ikiwa inaangalia namna bora ya kufanya ili kutoathiri maisha ya wananchi,” alisema Ridhiwani.
Aliongeza hata hivyo wananchi wanapaswa kujiandaa na mabadiliko kwani kila jambo lina wakati wake ambapo mipango kama hiyo ina lengo la kuwasogezea huduma karibu wananchi.
Mwisho.
Na John Gagarini, Ubena
WANANCHI wa Kata ya Ubena Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani wameuomba uongozi wa Gereza la Ubena kuwaruhusu kulitumia eneo la pori la Mwidu kwenye barabara ya Morogoro Chalinze ambalo limekuwa likitumiwa na majambazi kujificha kwa ajili ya kuteka magari nyakati za usiku.
Ombi hilo lilitolewa na diwani wa kata hiyo Mrisho Choka mbele ya Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ambaye yuko kwenye ziara kutembelea Jimbo hilo kukagua shughuli za maendeleo.
Choka alisema kuwa kuwa pori hilo limekuwa likitumiwa na majambazi ambao hujificha kisha kutega magogo barabarani na kusababisha ajali kisha kufanya uhalifu kwa kutumia silaha mbalimbali.
“Eneo hili limekuwa hatarishi kwa magari hasa nyakati za usiku ambapo kumekuwa na matukio mengi ya utekwaji wa magari ambayo kabla ya kutekwa husababishiwa ajali kwa kuwekewa magogo hivyo tunauomba uongozi wa gereza kuturuhusu tutumie eneo hilo ili kuzuia vitendo hivyo,” alisema Choka.
Alisema kuwa endapo wananchi watalitumia eneo hilo itasaidia kupunguza vitendo hivyo kwani kwa ambapo kwa sasa majambazi hao wanafanya wanavyotaka kutokana na eneo hilo kuwa pori.
Aidha alisema kuwa wiki iliyopita magari manne yalitekwa na katika kukabiliana na uhalifu katika eneo hilo wamekuwa wakifanya doria na askari polisi lakini hata hivyo majambazi hao wamekuwa wakiwategea na kutekeleza uhalifu.
Kwa upande wake Ridhiwani Kikwete alisema kuwa ombi lao atalipeleka kwenye vyombo husika ili lifanyiwe kazi ili kuondokana na vitendo hivyo ambavyo vimekithiri katika eneo hilo.

Mwisho.

Sunday, January 4, 2015

WALILIA WODI YA WAZAZI

Na John Gagarini, Chalinze
WANANCHI wa Kijiji cha Kwaruhombo kwenye Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wametoa kilio cha kujengewa wodi ya wazazi kwenye kituo cha afya cha Kwaruhombo ili wanawake wajawazito wasijifungue kwenye wodi za kawaida.
Akizungumza kijijini hapo wakati wa ziara ya maendeleo ya mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete, Hadija Stambuli alisema kuwa akinamama wamekuwa wakijifungulia kwenye wodi hivyo kutokuwa na usiri.
Stambuli alisema kuwa hiyo imekuwa changamoto kubwa kwa akinamama wanapokwenda kujifungua wamekuwa wanashindwa kusitiriwa wakati wa uzazi.
“Tunakuomba Mbunge wetu utusaidie wakinamama ili tunapokwenda kujifungua kwani hakuna usiri hivyo tungepata jengo maalumu kwa ajili ya kujifungungulia ingekuwa vizuri,” alisema Stambuli
Akijibu malalamiko hayo mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kuwa kujifungua ni jambo jema na linahitaji usiri.
Ridhiwani alisema kuwa kwa kushirikiana na halmashauri ili kuhakikisha kunakuwa na jengo kwa ajili ya kinamama kujifungulia.
“Tutakaa na uongozi wa Halmashauri ili kuhakikisha kunakuwa na jengo maalumu kwa ajili ya kujifungulia ili kuwaondolea fadhaa akinamama wakati wakijifungua,” alisema Ridhiwani.
Aidha alisikitishwa na matumizi mabaya ya mafuta kwa ajili ya gari la wagonjwa wanaopata rufaa na kuutaka uongozi wa kituo hicho kuhakikisha kinadhibiti matumizi hayo.

Mwisho.

WANANCHI WAMLALAMIKIA MWEKEZAJI

Na John Gagarini, Chalinze
WAWEKEZAJI kwenye Kijiji cha Changarikwa wametakiwa kufuata taratibu za kisheria ili kuondoa migogoro baina yao na wananchi.
Hayo yalisemwa na mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete, wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji hicho kwenye ziara yake ya maendeleo jimboni humo.
Ridhiwani alitoa ushauri huo kufuatia wananchi hao kulalamika dhidi ya moja ya wawekezaji kwenye kijiji hicho kuchukua eneo lenye ukubwa wa hekari 500 na kutotimiza ahadi za kuwasaidia kwenye huduma za kijamii.
Moja ya wananchi wa Kijiji hicho Bakary Hatibu alisema kuwa mwekezaji huyo wakati anaomba ardhi hiyo moja ya masharti waliyokubaliana naye ni kuwajengea shule, zahanati na trekta lakini sasa ni miaka 15 hakuna hata kimoja alichotekeleza.
“Tumekuwa tukipata tabu kwani wakati mwingine tnazuiwa kupita kwenye maeneo amabayo yanamilikiwa na mwekezaji,” alisema Hatibu.
Kwa upande wake Mbunge huyo alisema kuwa kumekuwa na malalamiko mengi dhidi ya wawekezaji kujipatia maeneo pasipo kutimiza masharti ya maombi ya ardhi.
“Jambo la kushangaza ni mwekezaji kupewa hekari 500 na kijiji jambo ambalo ni kinyume cha sheria ya ardhi namba 5 ya mwaka 1999 inayosema kuwa kijiji kinauwezo wa kumpa mwekezaji si zaidi ya hekari 50,” alisema Ridhiwani.
Alisema kuwa kama wameona mwekezaji hafai kwani wao ndiyo waliompa ardhi wanauwezo wa kumnyanganya kwa kufuata taratibu za kisheria endapo wataona ameshindwa kutekeleza ahadi wakati anaomba ardhi.
“Mnauwezo wa kumuondolea umiliki endapo atakiuka masharti kwani huo ni mkataba na endapo atakiuka masharti unaweza kuvunjika na ardhi ikarudishwa kwa wanakijiji,” alisema Ridhiwani.
Alisema ni vema wawekezaji wakatekeleza tatatibu ili kuwa na ushirikiano na wananchi ambao wanatoa ardhi yao ili nao wanufaike nayo.
Mwisho.


Saturday, January 3, 2015

SHULE HATARIN I KUWAANGUKIA WANAFUNZI

 Baadhi ya wananchi na wafanyabiashara wa Kijiji cha Kibindu wilayani Bagamoyo wakimsikiliza Mbunge wao wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete alipotembelea Kijiji hicho wakati wa ziara yake ya kushukuru wananchi baada ya kumchagua kuwa mbunge miezi kadhaa iliyopita

 Akinamama wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete hayupo pichani baada ya kutembelea kijiji cha Kibindu kutoa shukrani kwa wananchi kumchagua kwenye nafasi hiyo miezi kadhaa iliyopita.

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kibindu wilayani Bagamoyo mkoani Pwani

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akizungumza na waandishi wa Habari mbele ya jengo la shule ya Msingi Kibindu ambalo lilianguka kufuatia mvua kubwa ziulizonyesha mwishoni mwa mwaka jana kushoto ni diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya.


 Moja ya madarasa ya shule ya msingi Kibindu likiwa limebomoka kufuatia mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa mwaka jana.

 Diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya aliyenyanyua mikono juu akitoa maelezo kwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kulia aliyevaa kofia ya kijani kufuatia mvua kubwa kubomoa madarasa ya shule ya Msingi Kibindu

 Moja ya Madarasa ya shule ya Msingi Kibindu likiwa limeezuliwa paa kufuatia mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa mwaka jana na kusababisha madarasa mawili na ofisi ya mwalimu mkuu kuharibika.

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete akikabidhi mpira kwa baadhi ya viongozi wa timu za soka za Kijiji cha Kibindu

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akionge na wananchi wa Kijiji cha Kibindu alipofanya ziara ya kushukuru wananchi wa Jimbo hilo kwa kumchagua kushika nafasi hiyo miezi kadhaa iliyopita.

Wednesday, December 31, 2014

WAZEE ZAIDI YA 300 WAPATIWA MATIBABU MAALUMU

Na John Gagarini, Kibaha
JUMLA ya Wazee zaidi ya 300 kati ya wazee 2,500 kwenye kata ya Kibaha katika halmashauri ya mji wa Kibaha mkoani Pwani wamepatiwa matibabu ya maradhi mbalimbali.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Msamaria Mwema Huduma za Jamii (GSSST), Elisha Sibale alipozungumza na waandishi wa habari juu ya huduma walizotoa kwa wazee.
Sibale alisema kuwa wazee hao ambao wanahudumiwa na shirika lake ni wale wenye umri kuanzia miaka 60 walitibiwa magonjwa mbalimbali kama vile Kisukari, Macho, Wingi wa damu, Uoni hafifu na ugonjwa wa Ukimwi.
“Lengo la mradi huu ni kuwawezesha wazee kupata matibabu kwa wakati kwani wengi wao wamekuwa hawapati huduma hizo kutokana na jamii kutowathamini hivyo kujikuta wakiwa na changamoto za kuumwa maradhi mengi,” alisema Sibale.
Naye mtaalamu wa maabara kwenye zahanati ya Mwendapole Hans Amon alisema kuwa wazee hao wameanza kujiamini kwenda kupata matibabu ambapo awali walikuwa na woga kutokana na jamii kutowapeleka hospitali na kuwaacha.  
Kwa upande wake moja ya wazee walionufaika na mradi huo Hadija Mbwambo alisema kuwa wameweza kujua afya zao na kujitambua na kuona umuhimu wa kuwahi kupata matibabu.
 Mradi huo wa miaka miwili unatekelezwa kwenye mitaa ya Kwa Mfipa, Simbani, Mwendapole A na B kwa Kibaha Mjini na Kibaha Vijijini Mwanabwito na Kikongo na matibabu hayo yalifadhiliwa na shirika hilo kwa kushirikiana na Help Age International na Pfizer Pharmaceuticals kuanzia Oktoba Mosi siku ya wazee duniani hadi Desemba mwaka jana na litakuwa endelevu.

Mwisho.  

AFA KWA KUJINYONGA KISA KUUGUA MUDA MREFU

Na John Gagarini, Kibaha
HUKU leo ikiwa ndiyo siku ya kwanza ya mwaka mpya wa 2015 ikiwa imeanza fundi wa kuchomelea Michael Mpondo (36) mkazi wa Machinjioni wilayani Kibaha mkoani Pwani ameamua kukatisha uhai kwa kujinyonga.
Imeelezwa kuwa chanzo cha fundi huyo kuamua kuchukua maamuzi hayo magumu ya kuamua kujiua kunatokana na kuugua kwa muda mrefu.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha mwenyekiti wa mtaa wa Machinjioni Evarist Kamugisha alisema kuwa marehemu alijinyonga jirani na nyumba laiyokuwa akiishi.
Akielezea kwa kina tukio hilo Kamugisha alisema kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 30 mwaka huu majaira ya saa 4:30 asubuhi baada ya mwili wake kukutwa ukininginia kwenye mti umbali wa mita 60 na alipokuwa akiishi.
“Marehemu usiku wa majira ya saa 2:30 kabla ya kifo chake alikula chakula na ndugu zake lakini aliondoka na jitihada za kumtafuta zilifanyika bila ya mafanikio lakini asubuhi yake ndipo watu walipouona mwili wake ukinginginia,” alisema Kamugisha.
Kamugisha alisema kuwa marahemu alikuwa akiumwa ambapo baada ya chumba chake kupelkuliwa kulikutwa dawa aina ya Panadoli pamoja na Amoxilini ambazo inasemekana alikuwa akizitumia.
“Marehemu alijinyonga kwa kutumia kamba ya nguo ya jeshi ambayo aliikata na kuwa kama kamba na kujinyonga nayo na hakuacha ujumbe wowote juu ya kifo chake,” alisema Kamugisha.
Kwa upande wake kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alithibitisha kutokea tukio hilo na kusema kuwa chanzo cha kifo hicho ni marehemu kuugua muda mrefu na kukata tamaa ya maisha.

Mwisho.