Thursday, April 3, 2025

MWENGE WAZINDUA MRADI WA KISIMA CHA MAJI HOSPITALI YA TUMBI KUTOA LITA 10,000 KWA SAA

HOSPITALI ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani ya Tumbi imepata mradi wa kisima kirefu kinachohudumia watu 920 kwa siku ambapo kwa siku kina uwezo wa kuzalisha lita 10,000 kwa saa.

Hayo yamesemwa na ofisa uendeshaji na matengenezo Mhandisi Charles Stephen wa Dawasa Kibaha akitoa taarifa ya mradi wa kisima kirefu cha maji kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ismail Ussi amesema mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 45.9.

Stephen amesema kuwa mradi huo umefadhiliwa na taasisi ya Direct Aid Society  na lengo la mradi huo ni kupata chanzo mbadala cha maji ili kusaidia kupata huduma ya maji ya uhakika inapotokea changamoto.

"Hospitali inatumia lita 110,000 kwa siku ambapo awali ilikuwa inategemea chanzo kimoja tu cha Dawasa hivyo kwa sasa maji yatakuwa ya uhakika mara inapotokea changamoto Dawasa,"amesema Stephen.

Amesema mradi huo ulianza Julai mwaka 2024 na kukamilika Agosti 2024.

No comments:

Post a Comment