Hayo yamesemwa na ofisa uendeshaji na matengenezo Mhandisi Charles Stephen wa Dawasa Kibaha akitoa taarifa ya mradi wa kisima kirefu cha maji kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ismail Ussi amesema mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 45.9.
Stephen amesema kuwa mradi huo umefadhiliwa na taasisi ya Direct Aid Society na lengo la mradi huo ni kupata chanzo mbadala cha maji ili kusaidia kupata huduma ya maji ya uhakika inapotokea changamoto.
"Hospitali inatumia lita 110,000 kwa siku ambapo awali ilikuwa inategemea chanzo kimoja tu cha Dawasa hivyo kwa sasa maji yatakuwa ya uhakika mara inapotokea changamoto Dawasa,"amesema Stephen.
Amesema mradi huo ulianza Julai mwaka 2024 na kukamilika Agosti 2024.
No comments:
Post a Comment