Thursday, April 3, 2025

MWENGE WAWEKA JIWE LA MSINGI MRADI SHULE YA AWALI MSINGI YA MCHEPUO WA KIINGEREZA KATA YA SOFU

HALMASHAURI ya Mji Kibaha imetoa kiasi cha shilingi milioni 458.4 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya awali na msingi ya Nyerere ya muundo wa Kiingereza iliyopo Mtaa wa Sofu na Kata ya Sofu.

Aidha hadi mradi huo utakapokamilika utatumia kiasi cha shilingi milioni 704.6 ikiwa ni mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akisoma taarifa mbele ya kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ismail Ussi, ofisa elimu awali na msingi Theresia Kyara amesema kuwa ujenzi huo uko hatua ta umaliziaji.

Kyara amesema kuwa ujenzi huo umehusisha vyumba tisa vya madarasa, matundu 17 ta vyoo, kichomea taka, jengo la utawala, ununuzi wa samani na madawati.

Amesema kuwa hadi sasa zimetumika kiasi cha shilingi milioni 297.7 kwa awamu ya kwanza huku awamu ya pili ikitumia milioni 157.1 na awamu ya tatu zitatumika kiasi cha shilingi milioni 89 na ujenzi umefikia asilimia 64.5

Kwa upande wake kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa shule za msingi za mchepuo wa Kiingereza za serikali ni nzuri katika kuendeleza elimu kwa watoto.

Ussi amesema kuwa shule hizo ni nzuri kwani gharama zake ni nafuu hivyo mradi huo ni mkombozi kwa wanafnzi walioko kwenye maeneo jirani na shule hiyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ambaye pia Diwani wa kata ya Sofu Mussa Ndomba amesema kuwa wananchi waliomba mradi huo ambapo na kupelekwa kwenye baraza la madiwani na kupitishwa.

Ndomba amesema hilo lilikuwa hitaji kubwa la wananchi wa Mtaa na Kata hiyo hivyo utakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi kwa watoto wao.

No comments:

Post a Comment