
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa ujenzi huo ni azma ya Rais anayoitaka ya kuwaondolea adha wananchi ya kupata huduma za afya mbali.
Ussi amesema kuwa anaipongeza Halmashauri na wananchi kwa kufanikisha ujenzi huo ambapo hadi kukamilika kwake unatarajia kutumia kiasi cha shilingi milioni 234.3.
"Tumeambiwa mara itakapokamilika wananchi hawatapata usumbufu kwenda mbali kupata huduma za afya watapata karibu hivyo kupata muda kufanya shughuli za maendeleo,"amesema Ussi
Akisoma taarifa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Catherine Saguti amesema kuwa ujenzi wa Zahanati hiyo kwa sasa umefikia asilimia 61 ya ujenzi na mradi huo unatarajiwa kukamilika mwaka wa fedha wa 2025/2026.
Saguti amesema kuwa manufaa ni kwa Kata tatu za Tangini, Maili Moja na Pangani zenye jumla ya mitaa 16 ambapo wananchi wataondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.
Aidha amesema kuwa hadi sasa mradi huo umetumia kiasi cha shilingi milioni 108.3 huku wananchi wakichangia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni moja kwa kujaza kifusi.
Naye Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka amesema anaishukuru serikali kuwapatia eneo hilo ambalo lilikuwa mali ya Wizara ya Mifugo na kupangiwa matumizi ya jamii.
Koka amesema kuwa afya ni kipaumbele kikubwa kwa wananchi kwani wakiwa na afya njema wataweza kujiletea maendeleo.
No comments:
Post a Comment