Na John Gagarini, Bagamoyo
KATIKA kukabiliana na
changamoto ya huduma ya afya kwa wananchi wa kijiji cha Kidomole Kata ya
Fukayosi, wilaya ya Bagamoyo, mkoa wa Pwani, wamejenga zahanati kwa thamani ya 58.7
Akizungumzia kuhusu ujenzi huo
ofisa mtendaji wa Kijiji hicho Sef Mayala alisema kuwa ujenzi wa zahanati hiyo
unaondoa adha ya kufuata huduma ya afya nje ya kijiji hicho.
Mayala alisema
kuwa katika kufanikisha ujenzi huo kila mwananchi wa Kijiji hicho alitoa kiasi
cha shilingi 5,000 kabla ya kuungwa mkono na wadau wengine na kufanikiwa
kukamilisha ujenzi huo.
“Mradi huu wa ujenzi wa zahanati
uliibuliwa na wananchi kupitia mkutano ulioitishwa na uongozi wa serikali ya
kijiji ambao ulianza mwaka 2009 na kukamilika mwaka huu 2015,” alisema Mayala.
Alisema
kuwa kuwa katika kuhakikisha ujenzi wa zahanati hiyo unakamilika kwa wakati Halmashauri
kupitia ruzuku ya maendeleo ya serikali ilichangia pia kwenye ujenzi huo.
“Ujenzi
wa zahanati hii umetokana na utekelezaji wa sera ya afya ya kijiji kuwa na
zahanati na pia kuwepo kwa ongezeko la watu katika kijiji cha Kidomole na
uhitaji mkubwa wa huduma za afya,,” alisema Mayala.
Aidha
alisema kwenye ujenzi huo nguvu za wananchi wamechangia kiasi cha shilingi
milioni 45.9, wadau mbalimbali shilingi. milioni 2.8, ruzuku ya serikali
shilingi milioni 10 huku Mbunge jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akichangia
bati 129.
Diwani wa
kata ya Fukayosi Ally Issa aliwashukuiru wananchi wa kijiji hicho na Kata kwa
ujumla kwa kuwa na mwamko wa kimaendeleo kwa kuchangia ujenzi wa zahanati hiyo
hadi kukamilika.
Issa alisema
kuwa anawashukuru wananchi kwa kujitolea pia kwani niaba ya viongozi ngazi
mbalimbali anawashukuru kwa michango yao ya hali na mali kwa kujitolea kwa
ajili ya shughuli za maendeleo kwenye Kijiji na kata kwani zahanati hiyo ni
faida kwa wanancho wote.
Mwisho
Na John Gagarini, Kibaha
WAUMINI wa Kanisa la Angikana na Watanzania kwa ujumla wametakiwa
kutunza vitambulisho vyao vya kupigia kura ili waweze kushiriki kikamilifu
zoezi la upigaji kura kwa ajili ya kuwapata viongozi mbalimbali akiwemo Rais
atakayeongoza Taifa letu kwa amani na utulivu.
Aidha kanisa linaamini kuwa kutokana na baadhi ya watu kufunga kwa ajili
ya kuombea uchaguzi huo kuwa wa amani ni dhahiri Watanzania wasiwe na wasiwasi
wakati wa uchaguzi kikubwa ni kuepukana na watu wanaohamasisha uvunjifu wa
amani.
Hayo yalisemwa na Mchungaji wa Kanisa
la Anglikana Tumbi wilayani Kibaha
Mkoani Pwani Methew Mwela kwenye baraza la Halmashauri kuu ya
kanisa hilo lililoketi kwaajili ya kujadili maswala ya maendeleo ya Kanisa hilo
na waumini wake ambapo alisema kuwa kinachotakiwa kufanywa na waumini hao
ni kutunza vitambulisho vyao vya mpiga kura na kushiriki zoezi hilo
kikamilifu siku itakapofika.
"Nawakumbusheni waumini na Watanzania kwamba dhambi ya manung'uniko
ni mbaya sana na hata kwenye vitabu vitakatifu imeandikwa kuwa iliwatafuna wana
wa Israel hivyo kama mtakaa bila kwenda kupiga kura kisha akachaguliwa
kiongozi ambaye hamkupenda achaguliwe na mkaanza kunung'unika mtakuwa
mnajitafutia dhambi,"alisema Mch Mwela.
Mch Mwela alisema kuwa wanachopaswa kufanya hivi sasa waumini hao ni
kutunza vitambulisho vyao vya mpiga kura na siku ikifika wafike mapema kwaajili
ya kupiga kura na kwamba ili kuwawezesha waumini wake kushiriki kikamilifu
ibada ya siku hiyo itaanza mapema na kuisha mapema .
"Ili kuhakikisha wote mnapata haki yenu
ya msingi ya kupiga kura ibada ya tarehe hiyo ya siku ya uchaguzi itaanza
mapema hapa kanisani kwetu ili waumini wangu wote wenye kadi ya mpiga kura
aende akapige kura ili kuchagua viongozi anaowapenda kadri Mungu
atakavyomuonyesha,”alisema Mch Mwela.
Aliwashauri waleambao kwa bahati mbaya ama kwa sababu mbalimbali walishindwa kufanikiwa kupata kadi za mpiga kura kuwa watulivu na wanayopaswa kufanya ni kumuomba Mungu ili viongozi watakaochaguliwa waiongoze nchi kwa haki na kweli pasipo na upendeleo wa aina yoyote ili taifa liendelee kuwa na amani.
“Nawaomba Watanzania kuondoa hofu na mashaka juu ya kuwepo na uwezekano wa kuzuka vurugu kabla na baada ya uchaguzi huo mkuu nchini kwani wanachopaswa kutambua ni kuwa mungu amesha mchagua Rais atakayewaongoza watu wake,” alisema Mch Mwela.
MWISHO
Aliwashauri waleambao kwa bahati mbaya ama kwa sababu mbalimbali walishindwa kufanikiwa kupata kadi za mpiga kura kuwa watulivu na wanayopaswa kufanya ni kumuomba Mungu ili viongozi watakaochaguliwa waiongoze nchi kwa haki na kweli pasipo na upendeleo wa aina yoyote ili taifa liendelee kuwa na amani.
“Nawaomba Watanzania kuondoa hofu na mashaka juu ya kuwepo na uwezekano wa kuzuka vurugu kabla na baada ya uchaguzi huo mkuu nchini kwani wanachopaswa kutambua ni kuwa mungu amesha mchagua Rais atakayewaongoza watu wake,” alisema Mch Mwela.
MWISHO
Na John Gagarini, Kibaha
ABIRIA wanaosafiri kutumia
vyombo mbalimbali vya vya moto mkoani Pwani wametakiwa kuacha tabia kuwashabikia
madereva wanaoendesha mwendo wa kasi wakati wakisafiri kwani ni hatari kwa
maisha ya wasafiri.
Wito huo ulitolewa mwishoni mwa wiki na
mgeni rasmi kwenye kilele cha wiki nenda kwa usalama barabarani kimkoaFlorence
Mwenda iliyofanyika mjini Kibaha na kusema kuwa kuwa pamoja na juhudi
zinazofanywa na Jeshi hilo kuhakikisha ajali za barabarani zinapungua bado kuna
changamoto mbalimbali hususa kwa upande wa abiria ikiwemo
kuhamasisha madereva kwenda na mwendo kasi wakiwa safarini.
Mwenda ambaye ni ofisa wa jeshi la
polisi alisema kuwa kikosi cha usalama barabarani kimeendelea kutoa
elimu kwa watumiaji wa barabara juu ya matumizi sahihi ya barabara lakini
kumekuwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na baadhi ya abiria
kushangilia mwendo wa kasi.
“Vitendo kama hivi na vingine
havipaswi kufumbiwa macho kwani vinahatarisha usalama wa abiria pamoja na
uharibifu wa mali lakini endapo madereva watazingatia matumizi sahihi ya
barabara itasaidia kupunguza ajali ambazo zimekuwa ni moja ya vyanzo vikuu vya
vifo pamoja na ulemavu,” alisema Mwenda.
Aidha alisema kuwa kikosi cha
usalama barabarani kimetoa elimu ya matumizi sahihi ya barabara kwa
wanafunzi wa shule za msingi na sekondari mkoani humo wapatao
1,568 lengo likiwa ni kuielimisha jamii na makundi mbalimbali juu
ya matumizi salama ya barabara ili kupunguza ajali zisizokuwa za lazima.
“Makundi mbalimbali yamepatiwa elimu
hiyo ikiwa ni pamoja na madereva wa magari wapatao 905,waendesha pikipiki1,220
na abiria 16,802 wa magari ya aina mbalimbali ambapo zoezi hilo
litakuwa endelevu hali itakayosaidia kupunguza ajali
ambazo zimekuwa zikigharimu maisha na mali,” alisema Mwenda.
Alibainisha kuwa kamati ya usalama
barabarani ya Mkoa huo pia ilifanya mambo mbalimbali ikiwa ni
pamoja na huduma ya upimaji wa macho bure kwa wananchi wa kawaida na
madereva wa vyombo vya moto.
MWISHO
No comments:
Post a Comment