Na John Gagarini, Kibaha
WANACHAMA
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kibaha Mjini wametakiwa kuacha tabia ya
kukumbatia makundi mara baada ya uchaguzi wa ndani kumalizika kwani
yanasababisha chama kushinda kwa tochi.
Hayo
yalisemwa juzi na mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini Maulid Bundala wakati
akiwanadi watia nia waliojitokeza kuwania kuchaguliwa na chama hicho
kupeperusha bendera kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba
mwaka huu.
Bundala
alisema kuwa makundi hayo yanachangia kwa kiasi kikubwa chama kushindwa
kutokana na mshikamano na ushirikiano kutokuwepo kwenye chaguzi mbalimbali
ambazo zinahusisha vyama vingi vya siasa.
“Kipindi
hichi ni kigumu sana kuwa na kundi siyo tatizo lakini mara atakapopatikana
mgombea mmoja wa ubunge makundi yanatakiwa kwisha na kubakia kundi moja tu la
CCM ambalo linatakiwa lipambane na wapinzani,” alisema Bundala.
Alisema
kuwa kwanini chama kishindwe kwa mbinde kwa ushindi wa tochi wakati kina
wanachama wengi ukilinganisha na vyama vya upinzani lakini inaonekana kushindwa
kunatokana na kukumbatiwa kwa makundi hayo.
“Makundi
yanatakiwa yaishe mara uteuzi wa mwanachama mmoja ambaye atawakilisha chama
kwenye uchaguzi tatizo linguine ni wanachama kumpenda mtu badala ya kukipenda
chama na kuachana na tabia ya kuwasema vibaya wagombea kwani wote ni Wanaccm,”
alisema Bundala.
Aliwataka
wanaccm ambao wanasifa ya kupiga kura za maoni za kuchagua mbunge kwenye kura
za maoni wanapaswa kuwa hai kwa kulipia kadi za chama, wawe wameorodheshwa
kwenye daftari la tawi na wawe na kadi ya kupigia kura.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment